Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema China imekuwa ikiisaidia Zanzibar katika mambo mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya hospitali. Rais Dk. Mwinyi Amesifu ukarabati mkubwa wa Hospitali ya Abdalla Mzee Pemba, utoaji wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa sekta ya afya, msaada wa vifaa vya matibabu na dawa, pamoja na udhamini wa masomo kwa madaktari wazalendo. Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 26 Agosti 2024, Ikulu Zanzibar, alipozungumza na timu ya madaktari 29 kutoka kundi la 33, walioongozwa na Kaimu Balozi Mdogo wa China Zanzibar, Chang Ming, chini ya kiongozi wa madaktari hao, Dk. Yuzheng Huang, waliofika kumuaga baada ya kufanya kazi nchini kwa kipindi cha mwaka mmoja. Aidha, Dk. Mwinyi ameishukuru Serikali ya China kwa ushirikiano wake na Zanzibar kupitia sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo sekta ya afya, unaochangiwa na uhusiano wa kidiplomasia uliopo baina Zanzibar na China tangu kuasisiwa ...