Na Angela Sebastian; Ngara Kikundi cha vijana wapatao nane wa Kata ya Kabanga Wilayani Ngara mkoani Kagera ambao wamejiunga pamoja na kuanzisha kilimo cha matunda aina ya Parachichi wamekuwa kichocheo cha ukuaji wa shughuli za kiuchumi ambapo huwaingizia kipato. Utekelezaji wa Sera ya vijana ya mwaka 2017 hadi 2034 imeisukuma Halmashauri ya Wilaya ya Ngara kutenga shilingi milioni 52.6 na kati ya hizo ml.40 ikiwa ni asilimia 10 itokanayo na mapato ya ndani huku vijana wenyewe kutokana na Sera hiyo wakichangishana fedha taslimu kupitia kikundi chao na kupata shl.mil 200. Mwenyekiti wa kikundi hicho cha Kabanga matunda group,Livingstone Shedrack ametoa taarifa kwa Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi na kusema kuwa lengo la vijana hao kwa kushirikiana na Halmashauri ya Ngara ni kuhakikisha vijana wanajipatia ajira na kipato pia mradi huo hutumika kujinfunza kilimo cha parachichi kutafuta masoko ili kuuza na kupata faida. Shedrack amesema mradi huo weny...
Marato tv - Sauti ya Jamii