Skip to main content

Posts

Showing posts from December 27, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka Siku tatu baada ya Ukaguzi Kubaini haina hitilafu-Sebukoto

Kampuni ya Meli Tanzania(TASHICO)imetoa taarifa kwa umma kuhusu tukio la kupinduka kwa meli ya Mv.Serengeti lililotokea usiku wa kuamkia Desemba 26 mwaka huu katika Bandari ya Mwanza Kusini. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Mwanza,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Paul Sebukoto amesema kuwa Meli hiyo imelalia upande wa nyuma baada ya maji kuingia ndani. ‘’Meli hii ilikuwa kwenye eneo la Maegesho,Maji yameingia ndani zikiwa zimepita kama siku mbili au tatu baada ya kufanyiwa ukaguzi uliobaini iko sawa,kwa hiyo ni lazima kutakuwa na chanzo ambacho kimesababisha maji kuingia ndani ya meli na kuipeleka chini upande wa nyuma’’alisema Sebukoto na Kuongeza kuwa ‘’Sasa tofauti na Tafsiri kuwa meli imepinduka au imezama ni kwamba meli hii haijapinduka wala haijazama isipokuwa tunasema imeegemea upande wa nyuma baada ya kulemewa na maji yaliyoingia ndani’’ Sebukoto amesema kuwa shughuli zinazofanyika kwa sasa ni kuinyanyua Meli hiyo kwa nyuma ili iweze kurudi kwenye hali yake ya...

Mnadhimu wa Jwtz aongoza Maafisa,Askari na wananchi kuaga mwili wa Meja Jenerali Mstaafu Busungu

  Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Luteni Jenerali Salum Haji Othman, ameongoza Maafisa, Askari na Waombolezaji kuaga mwili wa marehemu Meja Jenerali Martin Busungu, katika hospitali kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.  Marehemu Meja Jenerali Martin Busungu, enzi za uhai wake alishika nafasi mbalimbali ikiwemo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kuanzia mwaka 2018 hadi 2019. Marehemu Meja Jenerali Martin Busungu, alifariki dunia tarehe 24 Desemba 2024, katika hospitali ya Taifa ya Rufaa Muhimbili Dar es Salaam na kuagwa leo tarehe 27 Desemba 2024 na kusafarishwa kuelekea Mkoani Mwanza kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika Nyegezi, Mwanza tarehe 28 Desemba 2024.

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa afanya tukio kubwa Arusha.

  Aongoza msafara mkubwa wa bodaboda kwenda ukumbi wa AICC  Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi na mjumbe wa kamati kuu ya CCM Mohammed Ali Kawaida (MCC) ameongoza maelfu ya maafisa usafirishaji (bodaboda) wa jiji la Arusha kuelekea Ukumbi wa AICC kunakofanika Mkutano wa Maafisa usafirishaji Arusha.  Mwenyekiti UVCCM taifa ndio atakuwa mgeni rasmi wa Mkutano huo.

Taasisi ya Saratani ya Babuu kutoa elimu ya Saratani Jijini Mwanza

  Taasisi ya Saratani ya Babuu(BCF) ya Jijini Dar es salaam imeandaa Kampeni ya Saratani kitaa inayolenga kutoa elimu ya saratani kwa Jamii ya Mkoa wa mwanza pamoja na maeneo Jirani. Mandingo amesema kuwa, kampeni hiyo itakayofanyika kesho Desemba 28 mwaka huu kwenye uwanja wa michezo wa Nyamagana Jijini Mwanza ambayo itatanguliwa na matembezi ya furaha ya umbali wa kilometa tano.  Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Jijini Mwanza,Mwenyekiti wa Taasisi ya BCF, Cedou Mandingo ‘BABUU WA KITAA amesema, kuwa matembezi hayo yatawaleta pamoja wananchi ili kuunga mkono mapambano ya saratani, kupata elimu, kukutana na wataalamu na watoa huduma za afya sanjari na kuzifikia familia za wagonjwa wa saratani. Kwa upande wake, Daktari bingwa wa saratani Dokta Frank rutachunzibwa amesema kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa saratani nchini wanatokea mikoa ya kanda ya ziwa ambapo tafiti zinaendelea kufanyika ili kubaini sababu zinazochangia kuwepo kwa tatizo hilo. Amesema kuwa elimu itakayotolewa ...