Skip to main content

Posts

Showing posts from February 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Katibu Mkuu Luhemeja Aifariji Familia Ya Marehemu Sifael

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cypriana Luhemeja ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kudumisha na kutunza historia ya Muungano kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuwaenzi waasisi wake. Ametoa wito huo wakati akizungumza na waombolezaji eneo la Makongo Juu Jijini Dar es Salaam leo Februari 22, 2025 Jijini Dar es Salaam, alipofika kutoa pole na kuifariji familia ya aliyeshiriki tukio la kuchanganya udongo wa iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar Marehemu Bi. Sifael Mushi ambaye amefariki dunia Februari 20, 2025. Akitoa salamu za Serikali, Mhandisi Luhemeja amesema Marehemu Sifael alikuwa ni mtu muhimu katika historia ya Muungano wakati wa tukio la kuchanganya udongo lililkofanyika Aprili 26, 1965 ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kuasisiwa kwa Muungano Aprili 26, 1964. Akiifariji familia ya marehemu amesema pamoja na majonzi ya kumpoteza mpendwa wao, ina bahati ya kupata mtu aliyeshuhudia Muungano ambao umedumu hadi leo. “Niwaombe tuudumishe Muungano kwani wengi wetu tumezaliwa baa...

Waziri Mkuu Ashiriki Maziko Ya Bi. Asina Omari

WAZIRI MKUU na Mbunge wa Jimbo ya Ruangwa Mheshimiwa Kassim Majaliwa  leo Februari 22, 2025 ameshiriki katika mazishi ya marehemu Bi. Asina Omary Nyimbilile mkazi wa Kata ya Nkowe, Ruangwa mkoani Lindi. Akizungumza na waombolezaji katika mazishi hayo, Mheshimiwa Majaliwa amewataka ndugu, jamaa na marafiki kumuombea Marehemu Bi. Asina pumziko la milele pamoja na  kuyaenzi yote mema aliyofanya wakati wa uhai wake. Bi. Asina amezikwa katika makaburi ya jumuiya yaliyopo katika kata ya Nkowe. Mazishi hayo pia yamehudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Lindi Ndugu Hassan Jarufu, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ruangwa Ndugu Ibrahim Ndoro.

Waziri Mkuu Ashuhudia Makabidhiano Ya Zana Za Kilimo

_▪️Ni mpango wa Serikali wa kukabidhi zana za kilimo kwenye vituo 45 vya zana nchini._   _▪️Trekta tano na majembe yake yakabidhiwa._   _▪️Asisitiza ni mpango wa Rais Dkt. Samia wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini._   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Februari 22, 2025 ameshuhudia makabidhiano ya trekta tano kati ya Wizara ya Kilimo na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ikiwa ni utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango wa Serikali wa kukabidhi zana za kilimo kwenye vituo 45 vya zana nchini.   Akizungumza wakati wa Makabidhiano hayo Mheshimiwa Majaliwa amewataka wananchi watakaopata fursa ya kutumia matrekta hayo ili yaweze kudumu kwa muda mrefu, kuleta tija na kutimiza malengo yaliyokusudiwa "Tunauzoefu wa matrekta tuliyoyaleta kipindi cha nyuma, hayakudumu kwa kuwa baadhi yetu tulikuwa tunayatumia kulima kwenye visiki, hii sio sawa, yatunzeni ili yale malengo tuliyoyakusudia ya kuendeleza sekta ya kilimo yaweze kutimia"   Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa amesema Ser...

Waziri Kikwete : Rais Samia ni Alama ya Maono Sahihi Kwa Wakati Tulionao

Maneno hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Waziri Mkuu anayesimamia Kazi, Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu Ndg. Ridhiwani Kikwete wakati akimkaribisha Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania azungumze na waliojitokeza katika sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Mafunzo ya Wanawake Viongozi na kutoa vyeti kwa wahitimu wa kozi hiyo kwa mwaka 2024/25. Katika Risala yake, Mh. Rais Samia pamoja kuwapongeza wahitimu na alitumia kuwanasaa wahitimu kutambua nafasi zao katika jamii wanayoishi pasi kusahau kuwa kama wanawake ndiyo walezi wa Jamii na hivyo wasije geuka kuwa wavurugaji wa jamii kwa sababu ya ukubwa wa elimu yao na madaraka waliyonayo. Katika sherehe hizo wahitimu zaidi ya 110 walitunukiwa vyeti. Kiongozi wa Wahitimu hao Bi. Adeline Mushi alimshukuru Mh. Rais kwa kushiriki nao na kuwa jicho ya  programu hiyo toka ilivyoanza. Na wahitimu kwa upande mwengine walitoa zawadi kwa mkoa wa Dar Es Salaam kwa kuchangia vifaa vya kusaidia watoto wadogo wan...