Skip to main content

Posts

Showing posts from September 21, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Sumve Iheshimishe Ccm Kwa Kura Nyingi - Dkt. Biteko

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM, Taifa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe, Ndugu Doto Mashaka Biteko amewahimiza wananchi wa Jimbo la Sumve, wilaya ya Kwimba Mkoani  Mwanza kuwapigia kura wagombea wa CCM kwa kuwa Chama hicho kimefanya jitihada kubwa ya kuwaletea maendeleo. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 21, 2025 Kwimba - Mwanza wakati akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Sumve kwa tiketi ya CCM, Moses Bujaga ikiwa ni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Amesema Serikali ya CCM imeendelea na jitihada zake za  kujenga Kituo cha Reli ya Kisasa ya SGR kwa ajili ya kupokea mizigo itakayosafirishwa kwenda maeneo mbalimbali pamoja na kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Mwanza ili kufungua uchumi wa mkoa huo kwa ujumla. Aidha, imehakikisha wananchi wa vijiji vyote katika Jimbo hilo wanapata umeme ikiwa ni pamoja na usambazaji umeme katika vitongoji. Dkt. Biteko ameendelea kusema Dkt. Samia Suluhu Hass...

Katibu Mkuu wa Madini Atembelea Banda la Tume ya Madini Kwenye Maonesho ya Madini Geita

Geita, Septemba 22, 2025 Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, ametembelea Banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea kwenye Viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili, Manispaa ya Geita. Katika ziara hiyo, Mhandisi Samamba ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo pamoja na viongozi waandamizi wa Tume ya Madini wakiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Dkt. Janet Lekashingo, pamoja na Makamishna wa Tume, Mhandisi Theonestina Mwasha na Dkt. Theresia Numbi. Ziara hiyo imelenga kukagua na kujionea ubunifu na teknolojia mbalimbali zinazotumika katika sekta ya madini, huku Tume ya Madini ikiendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau kuhusu fursa na wajibu wao katika maendeleo ya sekta hiyo.

Mpina Wa Act Wazalendo Yupo "ICU"

 Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesisitiza kuwa, Chama cha ACT-Wazalendo, hakina mgombea urais wala makamu wa urais. Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ramadhan Kailima imeeleza hivi: “Katika tovuti rasmi ya Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT -Wazalendo) taarifa iliyotolewa tarehe 21 Septemba, 2025, imeonesha uwepo wa Mkutano wa Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya ACT- Wazalendo katika Makao Makuu ya Chama hicho na kufuatiwa na Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Ubunge katika Jimbo la Segerea.  Taarifa hiyo imebainisha kuwa, shughuli zote mbili zitahudhuriwa na waliotajwa kama wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Luhaga Joelson Mpina na Ndugu Fatma Abdulhabib Ferej. Tunasisitiza kwamba, chama cha ACT-Wazalendo hakina wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa kuzingatia uamuzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wa tarehe 1...

Chege Alia na Neno "Mamlaka"Linavyopandisha Gharama za Maisha Kwa Wananchi wa Shirati

MGOMBEA Ubunge wa jimbo la Rorya mkoani Mara Jafari Wambura Chage ameonesha kusikitishwa na kitendo cha wananchi wa Shirati jimboni humo kupandishiwa gharama za huduma kwa madai kuwa eneo hilo linastahili kuwa mji mdogo wakati mchakato wake haujakamika. Chege ametoa kilio hicho mbele ya mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi Fadhili Maganya wakati akiomba kura kwa maelfu ya wananchi wa Michire eneo la Shirati. Amesema wananchi hao wanekuwa katika mateso makubwa ya kupandishiwa huduma mbalimbali zikiwemo za nishati ya umeme,maji na viwanja kwa kutumia jina la "Mamlaka"huku wahusika wakijua wazi kuwa  mchakato huo haujakamilika.  "Maji katika Mji wa Shirati na Vitongoji vyake haijakidhi huitaji wa huduma kwa Jamii. *Lazima tupambanie hii,Gharama za Maisha Kwa jamii ya Shirati na Raranya,yamfanya kushtuka na Neno Mamlaka ya Mji"alisema Chege huku akishangikiwa na maelefu ya wananchi wa eneo hilo.  "Amesema pamoja na Mamlaka hakuna,lakini uendeshaji...

Majaliwa Asema Ccm Imejipanga Kuendelea Kuleta Maendeleo

*_Asema Rais Dkt. Samia na Dkt. Mwinyi ni Madaktari wa Maendeleo*_ *_Asisitiza kuichagua CCM ni kuchagua Maendeleo._* *_Awaomba wananchi kumchagua Mhe. Hemed kwa kishindo_* Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Chama cha Mapinduzi kimejipanga kuendelea kuleta maendeleo katika sekta zote nchini. Amesema kuwa Chama hicho mara zote kimekuwa kikigusa maendeleo kwa watanzania katika sekta zote hivyo kukichagua katika uchaguzi wa mwezi Oktoba 2025 ni uamuzi wa kuchagua maendeleo. Amesema hayo leo Jumapili (Septemba 21, 2025) alipozindua kampeni za uchaguzi katika Jimbo la Kiwani, katika viwanja vya Kwareni, Pemba Zanzibar. Mgombea Uwakilishi wa Jimbo hilo ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla. "Wote ni mashahidi, Pemba ya leo, Zanzibar ya leo ni tofauti na tulipotoka, hatua za kimaendeleo katika maeneo haya ni mkubwa na yanaonekana kila sekta imeguswa...

Wasira : Mchagueni Dk.Samia yupo tayari kutumia juhudi binafsi kuleta maendeleo ya Watanzania

Na Mwandishi Wetu,  Songwe Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira miongoni mwa sababu za Watanzania kymchagua Mgombea urai wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan ni pamoja na uwezo wake kutumia juhudi binafsi kuleta maendeleo ya Watanzania. Aidha, kupitia CCM chini ya Dk. Samia, Watanzania wataendelwa kuwa salama huku fursa za uchumi zikiendelea kufunguka kupitia sekta mbalimbali ukiwemo uwekezaji. Aliyaeleza hayo  alipozungumza na wana CCM katika mji wa Vwawa, wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe alipokuwa akimtafutia kura Dk. Samia na wagombea ubunge na udiwani waliosimamishwa na Chama kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu. "Tukiwaambia Watanzania tuchagueni la kwanza tutawathibitishia umoja wa Watanzania utalindwa la pili tutawahakikishia amani ya Tanzania inalindwa na tatu maendeleo ya Tanzania yanapatikana. Mambo matatu; umoja.amani na maendeleo ya kudumu maendeleo ya watu ndio ajenda zetu kuu. "Kwa hiyo tukija hapa ni mwaka wa uchaguzi, tunapo...

Majaliwa kuzindua kampeni za CCM Jimbo la Kiwani

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Septemba 21, 2025 anazindua kampeni za uchaguzi katika Jimbo la Kiwani zinazofanyika katika uwanja wa Kwareni, Pemba, Zanzibar. Mgombea kiti cha Uwakilishi wa Jimbo hilo ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Pili wa Rais  wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla.