UONGOZI WA JUU IPU WAKUTANA NA SPIKA ZUNGU NEW YORK, WAPOKEA HAKIKISHO LA UENYEJI WA MKUTANO WA 153 JIJINI ARUSHA
Na Prosper Makene New York, Marekani– Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Musa Azzan Zungu, ameuhakikishia Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) kuwa Tanzania imejipanga kikamilifu kuandaa Mkutano wa 153 wa IPU utakaofanyika Oktoba 2026 jijini Arusha. Mhe. Zungu ametoa hakikisho hilo wakati wa kikao na Rais wa IPU, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Mbunge, pamoja na Katibu Mkuu wa IPU, Balozi Anda Filip jijini New York, Marekani. Kikao hicho kililenga kupitia hali ya maandalizi, mipango ya kilojisti na uhakika wa utayari kabla ya mkutano huo mkubwa wa kibunge duniani. Spika ameeleza kuridhishwa na kazi ya Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi inayoratibu tukio hilo. Amesema mipango yote ya kilojisti, kiprotocol na usalama inaendelea kama ilivyopangwa, na Tanzania imejitolea kutoa ukaribisho wa kiwango cha kimataifa. Mhe. Zungu amesisitiza kuwa kuandaa mkutano huo ni jambo la fahari kwa Taifa na ni fursa muhimu ya kuimarisha nafasi ya Tanzania katika diplomasia ya kibunge duniani. Ameongez...