Skip to main content

Posts

Showing posts from February 25, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali, Sekta Binafsi Kuimarisha Huduma Za Fedha Nchini

  📌 Dkt. Biteko afungua tawi la Exim Benki Kahama 📌 Exim yachangia vifaa vya matibabu vya shilingi milioni 25 Hospitali ya Wilaya Kahama Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Bank Kahama ni uthibitisho wa ukuaji wa sekta ya benki, ushirikiano wa sekta binafsi na Serikali na dhamira ya kukuza uchumi wa wananchi. Aidha, Serikali imekuwa ikihimiza taasisi za fedha kuipeperusha bendera ya Tanzania nje ya nchi kwa kufanya uwekezaji wa kimkakati.  Hayo yameelezwa leo Februari 25, 2025 Kahama mkoani Shinyanga na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati akizindua tawi la Benki ya Exim. “ Kahama ni kitovu kikubwa cha shughuli za kiuchumi, hasa sekta ya madini ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kwenye pato la Taifa. Zaidi ya madini, mji huu pia ni maarufu katika sekta ya kilimo na biashara. Ni wazi kuwa ufanisi wa sekta hizi unategemea upatikanaji wa huduma za kifedha imara na zinazokidhi mahitaji ya wajasiriamali na wafanyabiashara,” amesema ...

Dkt. Biteko Ahimiza Mshikamano, Upendo Na Umoja Msalala

📌 Awaasa Wanamsalala kuchagua maendeleo badala ya maneno 📌 Rais Samia atakeleza Ilani ya CCM kwa 99% Msalala *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa angependa kuona wananchi wa Kahama wanashirikiana na kuungana kwa pamoja katika shughuli za maendeleo ya Wilaya yao. Aidha, amewaasa kutoacha msingi wa Chama Cha Mapinduzi wa kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba Taifa linategemea CCM iwahudumie na sio kuruhusu mipasuko miongoni mwao. Dkt. Biteko ameyasema hayo Februari 25, 2025 Kahama, mkoani Shinyanga wakati aliposhiriki katika Mkutano Maalum wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Msalala uliolenga kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2020-2025. Akizungumzia fursa za maendeleo zilizopo wilayani humo, Dkt. Biteko amesema  kuwa Kahama ni Wilaya  ya kimkakati ambayo ina bandari kavu iliyopo Isaka ambapo pia kitajengwa kiwanda cha kuchenjua madini pamoja na uwepo wa ba...

Rais Samia Atangaza Kuilea Tanzania Kwa Kuongeza Kasi Zaidi Ya Maendeleo

 Na Mwandishi Wetu , Korogwe RAIS wa Jamhuri ya Muungano, Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa ahadi kwa wananchi kuwa atailea Tanzania kwa kusukuma mbele maendeleo kwa kuanzisha na kuibua miradi mikubwa yenye tija na maendeleo kwa nchi. Rais, aliyasema hayo jana wakati akiweka jiwe la msingi la bwawa la umwagiliaji lililopo Tarafa ya Mkomazi, wilayani Korogwe ambapo alisema kuwa anatoa ahadi kuwa atahakikisha anasukuma mbele maendeleo ya wananchi katika sekta mbalimbali "Ahadi yangu kwenu kama mama nitaendelea kuilea Tanzania kama mtoto wangu, nitaendelea kusukuma miradi ya jamii yote inayotakiwa kuwepo, maji, Umeme, afya, elimu, kilimo nitajitahidi kufanya kazi yangu kama inavyotakiwa hiyo ni ahadi yangu kwenu," alisema Rais Dkt Samia. Alisema bwawa la Mkomazi ambalo awali Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alitamani kulitengeneza lakini hakufanikiwa vivyo hivyo kwa Marais wa awamu tofauti nao hawakujaliwa kutokana na Hali ya uchumi, lakini serikali yake imeweza.  Alisema kuwa Tanz...

Waziri Kombo akutana na Wabunge wa Hungary

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na Wabunge wa Bunge la Hungary wanaounda Chama Rafiki cha Ushirikiano wa Kibunge kati ya Bunge la Tanzania na Bunge la Hungary. Wabunge hao wa Hungary wakiongozwa na Mwenyekiti mwenza wa Chama hicho Bi. Mónika Bartos,wamekutana na Mhe. Waziri na Ujumbe wake katika moja ya Ukumbi wa Mikutano katika Bunge la Hungary. Katika mazungumzo yao Mhe Waziri Kombo na Wabunge hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano wa Kibunge ‘Parliamentary Diplomacy’ kwa kuwa na ziara za viongozi wa mabunge na wabunge ili kubadilishana uzoefu, ujuzi na utalaam kuhusu masuala ya Bunge.  Maeneo mengine waliyokubaliana ni pamoja na kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Hungary kupitia sekta za kipaumbele za elimu, afya, utamaduni, michezo, afya, kilimo, biashara, uwekezaji, usambazaji maji, mazingira, mabadiliko ya tabianchi, na viwanda. Mhe. Waziri Kombo pi...