>>Ni kuhusu barabara ya TANROADS iliyogeuka mashimo NA MWANDISHI WETU, Tarime MAKAMU Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara Mkoa wa Mara, Dkt. Rhimo Nyansaho, amewapa matumani wakazi wa wilaya Tarime kuhusu matenegenezo ya barabara ya Tarime-Mogabiri ambayo imechimbika mashimo kwa muda mrefu sasa. Ni barabara inayotumiwa na maelfu ya wasafiri wakiwemo watalii wanaotembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti na magari ya biashara kati mji wa Tarime, Nyamongo na Serengeti. Barabara hiyo ipo chini ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), lakini imebaki kulalamikiwa na wananchi kwa muda mrefu sasa wakiomba itengenezwe bila mafanikio. “Naona nilisemee jambo hii, uhakika ni kwamba barabara hii imewekwa kweye mpango wa matengenezo na mkandarasi alishapatikana,” Dkt. Nyansaho ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa alisema Jumatatu iliyopita. Dkt. Nyansaho aliyasema hayo mjini Tarime wakati akitoa salamu za pole kwenye mazishi ya Frank Peter Zakaria (41), kijana wa mf...
Marato tv - Sauti ya Jamii