Wakazi wa Mkoa wa Kigoma wameaswa Kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mkoani humo ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Gombe ambayo ina wanyama aina ya sokwe mtu pamoja na maporomoko mazuri ya maji. Wito huo umetolewa na Sheikh Hassan Kabeke wakati wa Tamasha la kwanza la kihistoria na Utamaduni wa Mji Mkongwe wa Kigoma ujiji lililolenga kutangaza mji huo mkongwe pamoja na vivutio kadhaa vya utalii vilivyopo mkoani Kigoma. Sheikh Kabeke ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Tamasha hilo amesema kuwa ni Jukumu la kila mwana Kigoma wakiwemo wa Ujiji,Kasulu,Kibondo,Kakonko,, Buhigwe,Ilagala,Mwamgongo, Mwanga,Bangwe,Gundu,Mwandiga, Kibirizi kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo kwenye mji huo pamoja na Mkoa Kigoma kwa Ujumla. " Mji wa Kigoma Ujiji una zaidi ya miaka 300 na Majengo ya ibada na Misikiti yenye zaidi ya karne tano likiwemo Kanisa lenye umri wa miaka Mia Moja sanjari na visima vilivyo chimbwa wakati wa Utawala wa Waingereza"alisema Sheikh Kabeke kwa nyakati tofauti wakati ak...
Marato tv - Sauti ya Jamii