Skip to main content

Posts

Showing posts from March 4, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Hakuna wa Kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Meaka 2025-Makala

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), *CPA Amos Makalla* amesema uchaguzi mkuu mwaka wa huu 2025 utafanyika kwa mujibu wa katiba na sheria kwani mabadiliko yameshafanyika, hivyo hakuna atakayezuia uchaguzi. CPA. Makalla ameeleza hayo wakati akizungumza katika Mkutano wa Viongozi wa Chama na Jumuiya ngazi ya Shina, Tawi, Kata na Wilaya katika Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es salaam, ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya siku tano katika mkoa huo. “Uchaguzi utafanyika kwa mujibu wa katiba kwa mujibu wa sheria, nimeona kwenye magroup yao wanaambiana wachangiane tone kwa tone tuchangiane tuende kwenye nguvu ya umma kuzuia uchaguzi, hela zitaliwa kwa sabaau uchaguzi utafanyika,” Amesema Makalla. Akizungumza na Viongozi hao CPA. Makalla ameongeza kuwa kama watabaki na msimamo wao wa kutoshiriki uchaguzi ni dhahiri baada ya uchaguzi mkuu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakitokuwa na nguvu ya kuendelea kuwa chama kikuu cha upi...

Meneja Tanroads Mara Aitaja Bunda Vinara Wizi wa Taa za Barabarani

Na Shomari Binda-Musoma  MENEJA wa Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Mara mhandisi Vedastus Maribe ameitaja Wilaya Bunda kama vinara wa wizi wa taa za barabarani Hayo ameyasema kwenye kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika kwenye ukumbi wa uwekezaji.  Amesema matukio ya wizi huo yamekuwa mengi kwenye Wilaya hiyo na kuomba vyombo vya dola kufatili wezi hao na kuwakamata. Maribe amesema wamekuwa wakiunganisha miundombinu ya taa lakini kwa Wilaya ya Bunda kumekuwa na tatizo kubwa la wizi wa taa hizo zinazowasaidia wananchi. Akizungumza kwenye kikao hicho mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi ameagiza kusakwa na kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria wezi wa taa za barabarani. Amesema haikubaliki kuona wizi huo unaendelea kwa masrahi ya watu binafsi wasiopenda maendeleo. Amesema serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za maendeleo lakini wapo wachache wanaotaka kukwamisha ambao hawawezi kuvumiliwa. Mtambi amesema wizi ulioripotiwa hauwezi kuvumilika na ku...

Ccm Wameanza Kucheza Ngoma ya Chadema?

  George Michael Uledi. Leo karibu Social Media platforms zote za Kitanzania zilikuwa zimebeba kauli,Maoni na MSIMAMO wa Chama cha Mapinduzi kuhusu kauli ya Chadema ya No Reforms No Election kupitia Katibu wa NEC, Itikadi Uenezi na mafunzo,ndugu Amos Makalla! Sijajua kwanini CCM wameingizwa"king"(Provocation Trap)kirahisi MNO na Chadema this time na ni kama kauli hiyo ya Chadema inawasumbua sana CCM bila uwepo wa sababu za msingi!Bado sijaona "suppression maneuver" ambayo strategists wa Chama wameshafanya! Matokeo yake badala ya watu wa CCM kufanya "suppression" wanajikuta wanaifanyia "promotion" slogan ya "no reforms no election"mbele ya Watanzania!Machadema huko yaliko yatakuwa yanacheka kweli kweli! Wakati nawaza haya niliamua kufanya "mchezo" mdogo wa "brain arrest" huku nikiamua "kuingia na kukaa" ndani ya vichwa vya Mwenyekiti wa Chadema Taifa ndugu Tundu Lissu,Makamu Mwenyekiti Ndugu John Heche na Mz...

Waziri Bashungwa Awataka Uhamiaji Kutanguliza Uzalendo kwa Taifa lao

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amewataka Maafisa na Askari wa Idara ya Uhamiaji kutekeleza majukumu yao kwa uzalendo, uadilifu na kujiepusha na vitendo vya rushwa ambavyo vinaweza kupelekea uingiaji wa wahamiaji haramu nchini. Bashungwa ameeleza hayo, leo Machi 04, 2025 katika kikao kazi na Maafisa na Askari wa Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji, Idara ya Uhamiaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika wilaya ya Karagwe, Mkoa wa Kagera. “Wizara itawasimamia kikamilifu maafisa Uhamiaji katika kutekeleza majukumu yao. Wale ambao watakosa uzalendo na uadilifu, na kuwa sehemu ya chanzo cha kuchochea uingiaji wa wahamiaji haramu kwa lengo la kujipatia fedha au rushwa, tutawachukulia hatua kali za kisheria na za kiutumishi” amesema Bashungwa Bashungwa amesema Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa Mikoa ambayo iko mipakani, ambao umekuwa ukikumbwa na changamoto ya baadhi ya wageni kutoka nchi jirani kuingia kinyume na taratibu kutokana na ukubwa wa mpaka...

Rc Mtambi Aagiza Wezi wa Taa Za Barabarani Kusakwa na Kuchukuliwa hatua za Kisheria

  Na Shomari Binda-Musoma  MKU wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi ameagiza kusakwa na kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria wezi wa taa za barabarani. Kauli hiyo ameitoa leo machi 4 kwenye kikao cha bodi ya baraɓara mkoa wa Mara kilichofanyika kwenye ukumbi wa uwekezaji. Akizungumza mara baada ya kutolewa kwa taarifa ya Wakala wa Barabara ( TANROADS) mkoa wa Mara amesema haikubaliki kuona wizi huo unaendelea kwa masrahi ya watu binafsi wasiopenda maendeleo. Amesema serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za maendeleo lakini wapo wachache wanaotaka kukwamisha ambao hawawezi kuvumiliwa. Mtambi amesema wizi ulioripotiwa hauwezi kuvumilika na kuagiza jeshi la polisi kuwasaka wezi hao na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. " Naagiza kusakwa kwa wezi hawa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili hatua ziweze kuchukuliwa dhidi yao maana huu ni uhujumu uchumi. " Taa hizi zinawasaidia wananchi hata kwenye shughuli zao za uchumi lakini watu wachache kwa masrahi bin...

Mbunge Mathayo Kukamilisha Ujenzi Ofisi Ya Ccm Kata ya Kigera anayotoka Mwenyekiti Wa Wilaya

Na Shomari Binda-Musoma  MBUNGE wa Jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo ameahidi kukamilisha ujenzi wa ofisi ya Chama cha Mapinduzi Kata ya Kigera Ahadi hiyo ameitoa leo machi 4 kwenye viwanja vya ofisi hiyo wakati akielezea utekelezaji wa ilani kwenye Mkutano Mkuu wa Kata hiyo. Amesema viongozi wa chama katika kutekeleza majukumu yao wanapaswa  kukaa na kufanya kazi kwenye mazingira mazuri yakiwemo ya ofisi. Mbunge huyo ambaye anaendelea na ziara yake ya kupita kila Kata kuelezea utekelezaji wa ilani amesema alianza kuijenga ofisi hiyo tangu mwanzo na wanachama kuahidi kuikamilisha lakini kutokana na kukwama ameamua kuikamilisha. Akizungumzia utekelezaji wa ilani amesema kila mwachama wa CCM anapàswa kutembea kifua mbele kutokana na ahadi nyingi kutekelezwa. Amesema Kata ya Kigera imekuwa ya kwanza kwenye manispaa ya Musoma kujengwa shule ya ghorofa kwaajili ya wanafunzi wa sekondari. Mathayo amesema kwenye elimu hakuna tena uhaba wa vyumba vya madarasa na tayari ameleta mb...

Tanzania Yapokea Faru Weupe 17 Kutoka Afri̇ka Kusini

Na Kassim Nyaki, Ngorongoro Kreta, Arusha. Serikali kupitia wizara ya Maliasili na Utalii kwa mara ya kwanza imepokea Faru weupe 17 kutoka kampuni ya AndBeyond ya nchini Afrika Kusini kwa lengo la kuimarisha shughuli za uhifadhi, utafiti na elimu katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro. Akipokea faru hao katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika kreta ya Ngorongoro tarehe 4 machi, 2025 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amesema mradi wa kuwaleta faru weupe  Tanzania unalenga kuimarisha shughuli za uhifadhi na kupanua wigo wa watafiti ambao kupitia faru hao watasaidia  kutoa elimu kwa  wananchi na hata wageni  wenye lengo la kujifunza kuhusu maisha ya wanyama hao. Waziri Chana amebainisha kuwa faru hao 17 kutoka Afrika kusini ni awamu ya kwanza ambapo awamu ya pili itahusisha faru wengine 19 na kufikisha jumla ya faru 36 ambao watawekwa katika maeneo mengine ya uhifadhi nchini. Kamishna wa Uhifadhi  wa Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro...

Asilimia 69 ya maduhuli yakusanywa ndani ya miezi 8

• Watanzania 19,371 wapata ajira migodini • Thamani ya mauzo migodini yafikia 91.68 Mwandishi Wetu TUME ya Madini imefanikiwa kukusanya Shilingi 690, 763, 401,639.06  ndani ya miezi nane  sawa na asilimia 69.08 ya lengo la mwaka wa fedha 2024/2025. Akielezea mafanikio ya Tume ya Madini kwa kipindi cha miaka minne leo Machi 4, 2025 Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo amesema ukusanyaji wa maduhuli yatokanayo na rasilimali umepanda kutoka Shilingi bilioni 624.61 zilizokusanywa Mwaka wa Fedha 2021/2022 hadi kufikia Shilingi bilioni 753.82 kwa mwaka wa fedha 2023/2024.  Amesema makusanyo hayo ni sawa na ongezeko la asilimia 20.7 ya makusanyo kwa miaka mitatu.  “Aidha katika kipindi cha kuanzia Julai, 2024 hadi Februari, 2025, Tume imefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi 690, 763, 401,639.06 sawa na aslimia 69.08 ya lengo la Mwaka wa Fedha 2024/2025,”amesema Mhandisi Lwamo. Amesema, mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa umeongezeka ku...

Waziri Mavunde Akaribisha Sekta Binafsi Kushirikiana na Serikali Kwenye Utafiti wa Madini

▪️Awasilisha mpango wa Mining Vision 2030 ▪️Serikali yajipanga kuongeza eneo kubwa zaidi lililofanyiea Utafiti wa Madini wa kina ▪️Kampuni za Utafiti Madini zakaribishwa Tanzania ▪️Aelekeza STAMICO kufanikisha upatikanaji wa vifaa ya Utafiti wa awali  kwa ajili ya wachimbaji wadogo 𝐓𝐨𝐫𝐨𝐧𝐭𝐨,𝐂𝐚𝐧𝐚𝐝𝐚 Waziri wa Madini *Mh. Anthony Mavunde* amezikaribisha nchini Tanzania Kampuni za Utafiti wa madini kushirikiana na serikali katika kutimiza malengo ya Mining VISION2030 ambayo imejikita katika kufanya utafiti wa kina wa madini kufikia eneo la ukubwa wa asilimia 50 kufikia mwaka 2030. Mh. Mavunde ameyasema hayo jana Toronto,Canada wakati akihutubia kikao cha Mawaziri wa Madini kutoka nchi mbalimbali duniani,Kampuni za Utafiti na Uendelezaji Migodi na Asasi za kiraia. “Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia S. Hassan imeweka mazingira wezeshi ya kiuwekezaji,hivyo ni fursa kubwa ya Kampuni za Utafiti kuja kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mkakati wake ...