Na Shomari Binda-Rorya MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Bara Stephine Wasira amesema wanaelewa tatizo la ki bajeti kukamilisha ujenzi wa barabara za mkoa wa Mara. Kauli hiyo ameitoa wilayani Rorya wakati wa ziara yake inayoendelea mkoani Mara baada ya kusikiliza maelezo ya meneja wa Wakala wa Barabara ( TANROADS) mkoa wa Mara Vedastus Maribe. Amesema kazi ya CCM ni kuwasemea watu na suala la ukamilishwaji wa ujenzi wa barabara zikiwemo za Wilaya ya Rorya watafikisha taarifa Wizara ya Ujenzi ili zifanyiwe kazi. Wasira amesema mkoa wa Mara una barabara kubwa 4 ambazo zipo kwenye hatua mbalimbali za ujenzi katika kuunganisha mkoa wa Mara nazo zitafikishiwa taarifa. Amesema ipo barabara ya Mika-Utegi-Shirati-Kirongwe yenye urefu wa kilomita 56.8,Tarime-Serengeti-Sanzate-Serengeti na Musoma-Busekera ambazo zikikamilika zitafungua zaidi mkoa wa Mara kiuchumi. Wasira amesema TANROADS mkoa wa Mara inafanya kazi nzuri na msukumo wa kusaidiwa masuala ya bajeti ya miradi yao ndio i...
Marato tv - Sauti ya Jamii