Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Salome Kessy, amewataka wanamichezo wanaoiwakilisha Wizara katika Michezo ya SHIMIWI 2026 mjini Moshi kuzingatia nidhamu, uwajibikaji na maadili ya Utumishi wa Umma, akisisitiza kuwa kila mmoja abebe taswira ya Wizara katika kipindi chote cha mashindano. Bi. Kessy ameyasema hayo Septemba 18, 2026 jijini Dodom akizungumza na wanamichezo watakaoshiriki michezo inayotarajiwa kufanyika mkoani Kikimanjaro kuanzia Septemba 20 hadi Oktoba 7, 2026. Ameongeza kuwa, mafanikio katika michezo hayawezi kutenganishwa na nidhamu, akiwataka wanamichezo kutunza utimamu wa miili yao, kuzingatia ushauri wa madaktari, kula vizuri na kupumzika kwa wakati badala ya kutumia muda wa mapumziko kuzurura. Aidha, amewataka viongozi na walimu wa timu kuhakikisha kila mchezaji anatumika ipasavyo kulingana na uwezo wake, huku akisisitiza kuwa vitendo vya utovu wa nidhamu havitavumiliwa na hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaokiuka ta...
Marato tv - Sauti ya Jamii