Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RAIS WA NAMIBIA KUFANYA ZIARA YA KITAIFA NCHINI

 Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mheshimiwa Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah, anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 19 Juni, 2026 kwa ziara ya kitaifa. Ziara hiyo, ambayo ni ya pili kuifanya nchini Tanzania tangu aingie madarakani, inaendelea kudhihirisha uhusiano wa kindugu na wa kihistoria kati ya Tanzania na Namibia, uliojengwa katika misingi ya harakati za ukombozi wa Afrika, mshikamano na ushirikiano wa maendeleo unaonufaisha wananchi wa pande zote mbili. Tarehe 20 Juni, 2026, Rais Nandi-Ndaitwah atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam, yatakayojikita katika masuala mbalimbali ya ushirikiano wa pande mbili pamoja na masuala ya kikanda na kimataifa katika maeneo yenye maslahi ya pamoja. Baadaye, viongozi hao wawili watazungumza na waandishi wa habari. Akiwa nchini, Rais Nandi-Ndaitwah atatembelea eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam, ambako aliwahi kuishi katika miaka ya...
Recent posts

TVLA YAWATAKA WAFUGAJI KUONGEZA MWITIKIO WA CHANJO ZA MIFUGO

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi, amewataka wafugaji nchini kuongeza mwitikio wa kuchanja mifugo dhidi ya magonjwa mbalimbali ili kuimarisha afya ya mifugo, kuongeza uzalishaji na kupunguza hatari ya maambukizi ya magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Dkt. Bitanyi ametoa wito huo leo, Juni 18, 2026, mjini Morogoro wakati wa kikao cha pamoja kati ya TVLA na timu ya Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) unaotekelezwa chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Kikao hicho kililenga kujadili maeneo ya ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo. Amesema bado kuna mwitikio mdogo wa wafugaji wadogo katika kuchanja mifugo yao licha ya uwepo wa chanjo zinazozalishwa na TVLA, huku wafugaji wakubwa wakionesha ushiriki mkubwa zaidi katika kampeni za chanjo. “Tunaona mwitikio mkubwa zaidi miongoni mwa wafugaji wakubwa, lakini kwa wafugaji wadogo bado ni mdogo. Tunao utaalamu na wataalamu. Kupitia mradi huo,...

OFISI YA WAZIRI MKUU YATHIBITISHA NYENZO MUHIMU ZA KUIMARISHA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

 Na Mwandishi Wetu, Dodoma SERIKALI imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa nchini ili kuongeza uwezo wa kuzuia, kujiandaa, kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa, kufuatia kuongezeka kwa matukio yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi pamoja na vihatarishi vingine vya asili na kijamii. Hayo yameelezwa leo Juni 18, 2026 jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, wakati akifungua Kikao cha Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa kilicholenga kupitia na kuthibitisha Mwongozo wa Urejeshaji Hali Baada ya Maafa, Mwongozo wa Uendeshaji na Uratibu wa Uhawilishaji Fedha kwa Walioathirika wa Maafa, pamoja na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Maafa (DMIS). Brigedia Jenerali Ndagala amesema kuwa katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekumbwa na matukio mbalimbali ya maafa yakiwemo mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, u...

RAIS DKT. MWINYI: TANZANIA ITAENDELEA KULINDA MAZINGIRA YA BAHARI NA KUENDELEZA UCHUMI WA BULUU

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya za kimataifa katika kulinda mazingira ya bahari, kuimarisha usalama baharini na kuendeleza Uchumi wa Buluu wenye tija kwa wananchi. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema  hayo leo, tarehe 18 Juni 2026, jijini Mombasa, Kenya, wakati wa hafla ya kufunga Mkutano wa 11 wa Masuala ya Bahari (Our Ocean Conference), ambapo alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Amesema mkutano huo umeimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kukabiliana na changamoto za bahari, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza uwekezaji, teknolojia na ujenzi wa uwezo wa taasisi ili kutumia kikamilifu fursa za Uchumi wa Buluu kwa maendeleo endelevu. Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Serikali ya Kenya kwa kufanikisha mkutano huo na kusisitiza dhamira ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kulinda bahari na kuendelez...

WAZIRI NYANSAHO ATANGAZA FURSA KWA UWT MARA

 Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa (JKT)Dkt Rhimo Nyansaho ametoa Vizimba vitano  vya ufugaji wa Samaki kwa Umoja wa  Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Mara ili kusaidia jumuiya kujiimarisha kiuchumi.  Vizimba hivyo vitano ambavyo vitatumika kufugia samaki katika ziwa Victoria vina thamani ya shilingi Milioni 125. Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo ya uongozi ya UWT mkoa wa Mara mjini Musoma June 18 mwaka huu 2026 dkt  Nyansaho amesema lazima jumuiya hiyo muhimu ya chama cha Mapinduzi iweze kuimarika kiuchumi.  Waziri Nyansaho amesema kutokana na ukubwa wa Jumuiya hiyo inahitaji kuwa na mapato yake ili waweze kujitegemea katika uendeshaji wa shughuli zake na kujitegemea hasa nyakati za chaguzi.  Amesema Jumuiya hiyo ni miongoni mwa Jumuia kubwa na muhimu ndani ya CCM hivyo wataendelea kutafuta fursa mbalimbali za kiuchumi ili kukuza uchumi wa Jumuia, familia na Taifa kwa ujumla. Sambamba na hilo Waziri huyo pia ameiahidi Jumuia hiyo kuwa ...

KUIBUA,KUKUZA NA KUENDELEZA VIPAJI NI JUKUMU LETU"MGANDI

Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga  Vijana wametakiwa kuchangamkia fursa ilikuweza kutimizandoto zao na kukuza vipaji kwani bila kufanya hivyo watabaki kuona maisha magumu Kila siku. Hayo yamesemwa na mkurungenzi mtendaji wa kituo cha kulea na kukuza vipaji kwa upande wa soka Mohamed Mgandi kilichopo wilayani Korogwe Cha KOROGWE YOUTH SOCCER CENTER ambacho mpaka sasa kina mwaka mmoja. Mgandi amesema lengo la kituo hicho ni kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vilivyopo kwani mpira sasa ni biashara na ili iweze kuuzika ni lazma ipikwe vizuri kuanzia hatua za awali. "Vipaji ni vingi sana ,Kwa kuliona hilo tukaona tuanzishe kituo ambacho kitazalisha wanasoka Bora na wenye ujuzi wa kutosha kwani sisis tuna pokea watoto kuanzia umri wa miaka sita mpaka kumi na sita (6-16),hapa utaona mtoto huyo lazima awe Bora kwani tunaanza kumpika angali bado mchanga kabisa", alisema Mgandi. Aidha kituo hicho pia kimekuwa kikishirikiana na vituo vingine katika kuendeleza vipjia  ikiwemo Azam na mpaka s...