Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

PROF. KABUDI:TANI 29.52 ZA DAWA MPYA YA KULEVYA AINA YA KRATOM ILIKAMATWA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Profesa Palamagamba Kabudi, amesema Serikali imeendelea kupata mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya kupitia operesheni maalumu za ufuatiliaji na udhibiti nchini. Akiwasilisha taarifa kuhusu hali ya dawa za kulevya kwa waandishi wa habari leoei 29,2026 jijini Dodoma, Profesa Kabudi amesema mwaka 2025 jumla ya tani 26.36 za mirungi zilikamatwa, ikiwa ni ongezeko la asilimia 42.88 ikilinganishwa na mwaka 2024. Amesema ongezeko hilo linaonyesha kuimarika kwa ufanisi wa operesheni za ufuatiliaji na udhibiti, hususan katika maeneo ya mipaka na njia zinazotumika kusafirisha dawa hizo nchini. Kwa upande wa dawa za kulevya za viwandani, Profesa Kabudi amesema Serikali ilikamata kilogramu 907.18 za methamphetamine, kilogramu 672.23 za heroin, kilogramu 4.89 za cocaine, pamoja na gramu 178 za MDMA na gramu 7.82 za MDA. Aidha, amebainisha kuwa kwa mara ya kwanza mwaka 2025, Serikali ...
Recent posts

SERIKALI YAZIDISHA MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA, YATIBU ZAIDI YA WATU 85,000

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Profesa Palamagamba Kabudi, amesema Serikali imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kuhakikisha waathirika wanapata huduma za tiba na marekebisho ya tabia. Profesa Kabudi ameyasema hayo leo Mei 29,2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2025. Amesema katika mwaka huo, jumla ya watu 85,425 wenye uraibu wa dawa za kulevya walipatiwa huduma za tiba kupitia vitengo vya afya ya akili vilivyopo katika hospitali za rufaa za mikoa na kanda, kliniki za MAT pamoja na nyumba za upataji nafuu nchini. Ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuhakikisha waathirika wanapata huduma stahiki zinazowasaidia kurejea katika maisha ya kawaida na kuwa sehemu ya kuchangia maendeleo ya taifa. Aidha, Profesa Kabudi amesema Serikali pia imeendelea kuimarisha elimu kwa umma kuhusu madhara ya dawa...

SERIKALI YASISITIZA KUHARAKISHWA UJENZI WA OFISI ZA MIKOA ILI KUONGEZA NGUVU ZA UDHIBITI DAWA ZA KULEVYA

 SERIKALI imesisitiza kuharakishwa kwa ujenzi na uanzishwaji wa ofisi za Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya katika mikoa yote inayotajwa kuwa njia kuu za mapito ya dawa za kulevya, ili kuongeza kasi ya udhibiti na kuimarisha mapambano dhidi ya biashara hiyo haramu. Akizungumza leo Mei 29,2026 Jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa kuhusu hali ya dawa za kulevya nchini, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Palamagamba Kabudi amesema ni muhimu kuharakisha ujenzi na uanzishwaji wa ofisi katika mikoa yote inayotumika kama njia za mapito ya dawa za kulevya ili kuongeza ufanisi wa udhibiti na operesheni. Amesema kuwa ujenzi wa ofisi hizo lazima uendane na kuimarishwa kwa uwezo wa kiutendaji wa mamlaka hiyo. “Tumeamua pia kuimarisha uwezo wa kiutendaji ikiwemo kununua magari 17 yatakayosaidia kuongeza nguvu za operesheni za udhibiti, ufuatiliaji na ukamataji wa mitandao ya dawa za kulevya,” amesema. Prof. Kabudi ...

MAKAMU WA RAIS AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA MAREHEMU BI SUZANA MAGUFULI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli, ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, yaliyofanyika Kilimani, Chato mkoani Geita. Akitoa salamu za rambirambi mara baada ya kumalizika kwa Ibada ya kumuombea Marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli, Makamu wa Rais amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameguswa na msiba huo na anatoa salamu za pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki na wote walioguswa na msiba huo. Makamu wa Rais amewasihi Watanzania kumtumia marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli kama kielelezo cha malezi ya watoto, malezi ya maadili na uzalendo kwa kuwafanya watoto kutanguliza maslahi ya Taifa mbele na kuwa tayari kutumikia Taifa kwa nafasi yeyote wanayopewa. Ameongeza kwamba namna bora ya kumuenzi marehemu Bi. Suzana Ngolo Mag...

MWANAFA ACHIMBA KISIMA KWABASTOLA SEKONDARI

📍Wanafunzi wafurahia, wampongeza mbunge  Na Mwandishi Wetu, Muheza MBUNGE wa Muheza, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), amekagua mradi wa kisima cha maji matamu katika Shule ya Sekondari ya Kwabastola. Shule hiyo iliopo Kata ya Makole wilayani hapa, kisima kimegharimu Shilingi milioni 12 kupitia kampuni ya Mo Maji, ikiwa ni mwendelezo wa mikakati yake ya kusogeza huduma za kijamii karibu na wapiga kura wake tangu aingie madarakani mwaka 2020. Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Leo Mei 29, 2026, Mhe. Mwinjuma alionyesha kufurahishwa na kukamilika kwake, hasa baada ya kubainika kuwa maji hayo ni matamu na hayana chumvi, jambo linaloyafanya yafae kwa matumizi ya shule na wananchi wa jirani. "Wakati wa kampeni zangu, miongoni mwa ahadi kubwa nilizotoa ni kuhakikisha natatua kero ya dharura ya maji katika maeneo mbalimbali ya jimbo letu. Kupatikana kwa maji haya matamu hapa Kwabastola ni ushahidi kuwa tunatekeleza Ilani kwa vitendo ili kuwasaidia watoto wetu wasome kwa utulivu,...

MATIVILA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA TACTICS MUSOMA, AISISITIZA KUKAMILIKA KWA WAKATI

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amesema ameridhishwa na kiwango cha utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Manispaa ya Musoma kupitia Mradi wa Kuboresha Miundombinu ya Miji kwa Njia ya Ushindani Tanzania (TACTICS). Amesisitiza juuu ya umuhimu wa miradi hiyo kukamilika kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazolengwa. Mhandisi Mativila amesema hayo leo baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa chini ya mpango huo katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara. Katika ziara hiyo, alikagua utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara za Shaaban, Mkendo pamoja na Musoma Bus–Saa Nane, sambamba na miradi ya ujenzi wa jengo la ofisi, stendi ya mabasi ya Bweri na soko la Nyasho. Akiwa kwenye ukaguzi huo, Mhandisi Mativila pia alishuhudia zoezi la upimaji wa tofali katika maabara maalumu kwa ajili ya kuhak...