WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, ametoa onyo kali kwa watu wanaovamia maeneo ya hifadhi nchini, akisisitiza kuwa serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote watakaobainika kuhusika na uharibifu wa maliasili. Waziri Kijaji ameyasema hayo leo Juni 25, 2026 jijini Dodoma Katika Mkutano wa Mwaka wa Wahifadhi Wanyamapori, unaofanyika chini ya kauli mbiu isemayo “Uhifadhi Endelevu kwa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Taifa katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.” Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Kijaji amesema sekta ya uhifadhi inaendelea kukabiliwa na changamoto kubwa zinazohitaji ushirikiano wa wadau wote ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho. Amesema moja ya changamoto kubwa ni ongezeko la migongano kati ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu, hali inayosababisha uharibifu wa mashamba, makazi na mifugo, hususan katika maeneo ya vijijini. Ameeleza kuwa hali hiyo inachangiwa zaidi ...
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YATEMBELEA HOSPITALI KUU YA JWTZ MSALATO
Kamati ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), tarehe 23 Juni 2026, ilifanya ziara katika Hospitali Kuu ya Kanda ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Msalato, jijini Dodoma, kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi wa hospitali hiyo. Katika ziara hiyo, Kamati ya NUU ilipokelewa na uongozi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ukiongozwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho. Ziara hiyo ni sehemu ya jukumu la Kamati la kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyo chini ya sekta ya ulinzi, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya afya inayolenga kuboresha huduma za matibabu kwa wanajeshi, familia zao na wananchi kwa ujumla. Kamati hiyo, ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Mheshimiwa Pascal Chinyele, ilitembelea maeneo mbalimbali ya hospitali na kujionea hatua za utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mheshimiwa Pascal Chinyele...