Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Tanzania inatarajiwa kupokea ujumbe mkubwa wa viongozi wa elimu ya juu kutoka Malaysia, wakiwemo viongozi kutoka Wizara ya Elimu ya Malaysia, Education Malaysia Global Services (EMGS), pamoja na wawakilishi wa vyuo vikuu tisa vitakavyoshiriki Maonesho ya Elimu ya Malaysia yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 1 hadi 3, 2026 katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam. Ujumbe huo wa watu 19 kutoka Malaysia unatarajiwa kuwasili nchini tarehe ikiwa ni maandalizi ya kushiriki maonesho hayo pamoja na kufanya vikao vya kimkakati na wadau mbalimbali wa elimu nchini, ikiwemo Wizara ya Elimu, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), vyuo vikuu vya Tanzania, shule, wazazi, walezi na wanafunzi. Maonesho hayo, yanayoratibiwa kwa ushirikiano wa Global Education Link (GEL) na wadau wa elimu kutoka Malaysia, yanalenga kufungua fursa za udahili, ufadhili wa masomo, ushirikiano wa kitaaluma, pamoja na kuimarisha mahusiano ya elimu ya juu kati ya Tanzania na Malaysia. Akizungu...
MARATO TV
Marato tv - Sauti ya Jamii