Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WAZIRI MKUU: HATUPASWI KUPUUZIA VIASHIRIA VYA UVUNJIFU WA AMANI

 WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania waendelee kuhimizana kuhusu ulinzi wa Taifa na kamwe wasipuuze viashiria vya uvunjifu wa amani. "Tuendelee kuhimizana kuhusu suala la ulinzi wa Taifa letu. Ulinzi wa Taifa letu ni wa kila Mtanzania na amani yetu ni ya kila Mtanzania." "Sasa hivi hatupaswi kupuuzia viashiria vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Hatutakiwi kuvipuuza kwa sababu vimetuachia doa," amesema. Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 28, 2026) katika ibada maalumu ya kilele cha harambee iliyofanyika kwenye usharika wa Amani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kati, mjini Singida.  Harambee hiyo ambayo ni ya nne kufanyika, ililenga kukusanya sh. bilioni 1.4 kwa ajili ya kuboresha vituo vya huduma za afya, kuimarisha vituo vya huduma za elimu, utumishi na uinjilisti vya Dayosisi hiyo ambavyo vinapaswa kukamilika ifikapo Desemba, mwaka huu. Jumla ya sh. bilioni 1.331 zilikusanywa zikiwa ni fedha taslimu na ...
Recent posts

TRA YAHAMASISHA UPANDAJI MITI JIJINI TANGA

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Leo wamefanikiwa kupanda miti isiopungua 1000 katika shule ya sekondari Ummy Mwalimu iliyopo katika kata ya maweni wilayani na hii ikiwa ni muendelezo wa shughuli za kijamii wanazoshiki katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake. Wakiwa katika zoezi hilo mgeni rasmi Naibu kamishna shughuli za ufundi - Kodi za ndani Ted Frank silkiluwasha amesema TRA pamoja na shughuli ilizonazo lakini pia imekuwa mstari wa mbele katika kushiriki mambo ya kijamii na hii na inadhihisha ushirikiano mzuri uliopo baina ya Mamlaka ya mapato Tanzania na jamii. Aidha Silkiluwasha pia amesisitiza utunzaji wa miti hiyo kwani Kwa kuilinda itasaidia kuilinda ozone laya,leya inayozuia mionzi ya jua kufika katika uso wa dunia ambayo ni hatari sana Kwa afya ya wanadamu na viumbe vingine vilivyopo. Sambamba na hilo amemtaka Meneja wa TRA mkoa wa Tanga kuendelea kutoa elimu ya Kodi kwani elimu hiyo inapaswa kuwa endelevu na ili kuboresha ha...

ELIMU DODOMA YAINGIA HATUA MPYA KUPITIA ZIARA YA WALIMU KOREA KUSINI

 Na Mwandishi Wetu UJUMBE  wa walimu na viongozi wa elimu kutoka Mkoa wa Dodoma wapatao 40 umeondoka kwenda Korea Kusini kujifunza, namna ya kufundisha, kusimamia shule na kutumia teknolojia katika elimu. Ujumbe huo unatarajiwa kushiriki programu ya mafunzo na ziara ya kielimu ya siku nne kamili nchini Korea Kusini, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa walimu walioonesha utendaji bora na kufanikisha ongezeko la ufaulu wa wanafunzi katika Mkoa wa Dodoma. Mratibu wa safari hiyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulmalik Molle  alisema walimu hao waliondoka juzi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, Juni 27, 2026, kuelekea Seoul, Korea Kusini, kupitia Doha, Qatar. Alisema ziara hiyo ya kimasomo itafanyika kwa siku nne, ambapo walimu na viongozi wa elimu wanatarajiwa kushiriki katika mafunzo, kubadilishana uzoefu na kujifunza kuhusu matumizi ya teknolojia, ubunifu, uongozi wa shule na mbinu za kisasa za ufundishaji. Al...

WAZIRI MBARAWA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MATANKI YA KUHIFADHIA MAFUTA KIGAMBONI*

Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, leo Juni 27,2026 ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa matanki ya kuhifadhia mafuta katika eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, ambapo ameridhishwa na kasi na ubora wa utekelezaji wa mradi huo.  Mradi huo unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ukiwa ni sehemu ya uwekezaji mkubwa unaolenga kuimarisha miundombinu ya bandari na sekta ya nishati ili kuongeza ufanisi wa uchumi wa Taifa. Baada ya kukamilika, matanki hayo 15 yatakuwa na uwezo wa kuhifadhi takribani mita za ujazo 378,000 za mafuta, hatua itakayoongeza uwezo wa nchi kuhifadhi mafuta ya akiba, kupunguza muda wa kusubiri kwa meli bandarini, kupunguza gharama za usafirishaji wa mafuta, kuimarisha usalama wa nishati nchini na kuongeza mapato ya Serikali kupitia huduma za bandari. Mradi huo pia unatarajiwa kuifanya Tanzania kuwa kitovu muhimu cha biashara ya mafuta katika ukanda wa Afrika Mash...

DKT. MWIGULU: SERIKALI YAHAKIKISHA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SINGIDA

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo iliyoahidiwa katika Mkoa wa Singida, ikiwemo barabara, reli ya kisasa (SGR), uwanja wa ndege pamoja na miradi ya maji, afya na elimu kwa lengo la kuchochea maendeleo ya wananchi na kukuza uchumi wa Taifa. Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipohutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Maonesho wa Mandewa, wilayani Ikungi, mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo. Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtuma kuwahakikishia wananchi wa Mkoa wa Singida kuwa miradi yote ya maendeleo iliyoahidiwa itaendelea kutekelezwa hatua kwa hatua kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali. "Mheshimiwa Rais amenituma niwahakikishie kwamba mambo ambayo wabunge wenu wamekuwa wakiyasema na ambayo aliwaahidi wananchi wa Singida yatakwenda kutekelezwa," amesema. Amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya barabara ikiwemo Saba...

WAZIRI WA FEDHA AONGOZA MBIO ZA SHUKRANI KWA MLIPAKODI KUELEKEA TUZO YA RAIS KWA MLIPAKODI BORA NA MAADHIMISHO YA MIAKA 30 YA TRA

 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) leo tarehe 27 Juni 2026 imefanya Mbio na Matembezi ya Shukrani kwa Mlipakodi katika mikoa yote nchini ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuelekea Utoaji wa Tuzo ya Rais kwa Mlipakodi Bora na Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026. Katika Mkoa wa Dar es Salaam, mbio hizo zimefanyika katika Viwanja vya Gymkhana na kuhudhuriwa na watumishi wa TRA, wadau mbalimbali, wafanyabiashara na walipakodi. Mgeni rasmi alikuwa Mheshimiwa Balozi Khamis Mussa Omary, Waziri wa Fedha, ambaye aliongoza mbio hizo na kushiriki matembezi ya shukrani pamoja na mamia ya washiriki. Mbio na matembezi hayo yamefanyika kwa lengo la kutoa shukrani kwa walipakodi kwa mchango wao mkubwa katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali na maendeleo ya Taifa, sambamba na kuhamasisha ushiriki wa wadau katika Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA na hafla ya Tuzo ya Rais kwa Mlipakodi Bora.