Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema Tanzania inahitaji zaidi ujenzi wa hoja za maendeleo kupitia majadiliano ya kidemokrasia na utekelezaji wa mipango ya maendeleo, badala ya maandamano na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jun 13,2026,jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amesema CCM itaendelea kusimamia na kuimarisha siasa za maendeleo zinazolenga moja kwa moja kutatua changamoto za wananchi na kuboresha maisha yao. Amesema chama hicho kinaendelea kutekeleza majukumu yake kwa vitendo kupitia ziara mbalimbali za viongozi wake nchini, ambapo hukutana na wananchi katika mikutano ya hadhara na majukwaa tofauti kwa lengo la kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu kwa kushirikiana na Serikali. Kihongosi ameongeza kuwa CCM inaelewa vipaumbele vya wananchi ambavyo ni pamoja na huduma bora za afya, maji safi na salama, elimu bora, miundombinu imar...
Waziri wa Uchukuzi Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa leo tarehe 12 Juni, 2026 amezindua majaribio ya kuruka na kutua ndege katika Uwanja wa Ndege Musoma na kuahidi kuwa ndege za abiria kuanza kufanya kutua katika uwanja huo mwezi Julai, 2026. Akizungumza katika hafla, Mhe. Mbarawa ambaye alikuwa mgeni rasmi ameliagiza Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuharakisha utaratibu wa kuupanga Uwanja wa Ndege Musoma katika ratiba za ndege za abiria ili wananchi wa Mkoa wa Mara waweze kuanza kutumia usafiri huo. “Ninaiagiza ATCL kuhakikisha kuwa inauingiza Uwanja wa Ndege Musoma katika ratiba za ndege haraka iwezekanavyo ili huduma za usafiri ziweze kutolewa kwa wananchi” amesema Mhe. Mbarawa. Mhe. Mbarawa amesema majaribio ya utayari katika viwanja vya ndege vya Musoma na Shinyanga yanaashiria kukamilika kwa sehemu muhimu za miradi ya ukarabati na upanuzi wa viwanja hivyo na kuwa tayari kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Mhe. Mbarawa amezielekeza taasisi zinazohusika na mra...