Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mwenge wa Uhuru unatarajia kuwasili mkoani Tanga June 17 mwaka huu katika kijiji cha Mtoro Kata ya Tunguri wilaya ya Kilindi ukitokea mkoani Morogoro. Ukiwa mkoani hapa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri 11 kwa umbali wa kilometa 1340 ukikagua, kuzindua, kufungua na kuweka mawe ya misingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 27 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Burian amesema baada ya kukamilisha mbio zake mkoani hapa Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa mkoani mkoani Kilimanjaro June 28 mwaka huu. "Mwenge huu wa Uhuru utaweka mawe ya misingi jumla ya miradi 34, utafungua na kuzindua jumla ya miradi 26, utatembelea na kukagua jumla ya miradi 11 ya shughuli za vijana na miradi miwili ya maendeleo ya sekta ya maji, miradi hii yote ina jumla ya thamani ya shilingi bilioni 27, milioni 764, laki 390 na 480.01" Amesema Batilda. "Ujumbe wa mwenge kwa mwaka huu wa ...
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, amewataka Waheshimiwa Wabunge kutumia majukwaa yao kuhamasisha wananchi, hususani waliojiajiri, kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ili waweze kunufaika na huduma na mafao mbalimbali yanayotolewa na mifuko hiyo. Amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza wigo wa hifadhi ya jamii kwa makundi ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakishiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa, lakini bado hayajafikiwa ipasavyo na huduma za hifadhi ya jamii. Bw. Mshomba ameeleza kuwa kuongezeka kwa wanachama katika mifuko ya hifadhi ya jamii kutasaidia juhudi za Serikali za kupunguza umaskini wa kipato, kuongeza tija katika uzalishaji mali, kukuza uchumi wa nchi na kuimarisha ustawi wa wananchi. Kauli hiyo ameitoa leo Juni 15, 2026, katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, wakati wa mafunzo maalumu kwa Waheshimiwa Wabunge yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana...