Mabalozi wa mataifa mbalimbali wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania leo, Juni 19, 2026, wameanza safari kuelekea Jijini Dodoma kwa kutumia Treni ya Kisasa ya Mwendokasi (SGR) kushiriki Grand Bunge Bonanza litakalofanyika Juni 20, 2026 katika Uwanja wa Jamhuri. Bonanza hilo linatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kuimarisha umoja, ushirikiano na uhusiano wa kimataifa kupitia michezo, huku likiwa sehemu ya maandalizi na hamasa kuelekea mashindano ya AFCON 2027, ambayo Tanzania itaandaa kwa ushirikiano na Kenya na Uganda. Mabalozi waliosafiri ni wa nchi za Comoro, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Afrika Kusini, Sudan, Zimbabwe, Msumbiji na Angola. Ushiriki wa mabalozi hao unaonesha namna michezo inavyoendelea kuwa chombo muhimu cha kuunganisha mataifa, kuimarisha diplomasia na kujenga mahusiano imara kati ya Tanzania na jumuiya ya kimataifa. Grand Bunge Bonanza linatarajiwa kukutanisha viongozi wa Serikali, wabunge, mabalozi na wadau mbalimbali wa mich...
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Ghati Zephania Chomete, ameendelea kushiriki Mkutano wa 19 wa Maspika wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika unaoendelea jijini Johannesburg, Afrika Kusini, ukiwaleta pamoja viongozi wa mabunge kujadili masuala muhimu yanayogusa maendeleo ya bara la Afrika. Katika siku ya pili ya mkutano huo, Mwakilishi wa Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Cecilia Paresso, aliwasilisha mada iliyojikita katika nafasi ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola katika kuwawezesha vijana wa Afrika kushiriki kikamilifu katika kufanikisha maendeleo endelevu. Akiwasilisha mada hiyo, Mhe. Paresso alisisitiza kuwa mabunge yana wajibu mkubwa wa kutunga sheria, kupitisha sera na kuimarisha mifumo inayowapa vijana mazingira rafiki ya kushiriki katika uchumi jumuishi, uongozi na ubunifu. Alibainisha kuwa zaidi ya asilimia 65 ya wakazi wa Afrika ni vijana wenye umri chini ya miaka 30, jambo linaloifanya rasilimali hiyo kuwa nguvu muhimu katika maendeleo ya bara. Aidha, alie...