Na MASHAKA MHANDO, Tanga MATUMIZI ya mitandao ya kijamii jijini Tanga yamechukua sura mpya ya kiuchumi, baada ya vijana zaidi ya 150 kunufaika na mradi maalum wa ujuzi wa kidijitali uliowatoa mitaani na kuwafanya kuwa watengeneza maudhui (Content Creators) wanaojitegemea na kujingizia kipato. Mradi huo umewasaidia vijana kuachana na dhana potofu kuwa mitandao ya kijamii haina faida, na badala yake wamepewa ujuzi wa kuandaa maudhui, kupiga picha, na kuhariri kazi zenye viwango vinavyokidhi masoko ya mtandaoni. Miongoni mwa shuhuda za kusisimua za mradi huu ni ya Peter Msuya, kijana ambaye awali alikuwa fundi stadi wa kutengeneza vitanda na makochi (Sofa). Peter anasema maisha yake yamebadilika kabisa baada ya kujiunga na mafunzo hayo ya kidijitali. "Nashukuru sana mafunzo niliyopata. Leo hii ukurasa wangu unafuatiliwa na watu milioni mbili! Kama siyo mradi wa 'Tanga Yetu', saa hii ningekuwa nagombana na wateja ambao sijawatengenezea vitanda vyao kwa wakati. Sasa naweza ku...
Na MASHAKA MHANDO, Tanga SERIKALI imeshauriwa kuanza kuingia mikataba ya kununua na kuwekeza kwenye teknolojia na bidhaa zinazobuniwa na vyuo vya elimu ya juu nchini, badala ya kutegemea zaidi kuagiza bidhaa hizo kutoka nje ya nchi. Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Husna Sekiboko, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua mabanda mbalimbali katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu yanayofanyika mkoani Tanga. Mhe. Sekiboko amesema hatua ya Serikali kutumia bunifu za ndani itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza utegemezi wa kiteknolojia, kujenga uwezo wa wataalamu wa ndani, kuchochea ajira kwa vijana, na kukuza mapato ya Taifa kupitia bidhaa zenye nembo ya "Made in Tanzania". Akithibitisha uwezo wa vyuo vya ndani kufanya mapinduzi, Mhe. Sekiboko alisema amevutiwa sana na kiwango cha tafiti zinazofanywa, akitolea mfano ubunifu uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Chuo h...