Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

KATAMBI:TANZANIA KINARA HUDUMA ZA UHAMIAJI AFRICA

 WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, ameipongeza Idara ya Uhamiaji kwa kufanya vizuri katika utoaji wa huduma na kuiwezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa huduma bora za uhamiaji barani Afrika. Katambi amesema hayo leo, Septemba 6, 2026, akizungumza katika kikao cha viongozi waandamizi wa Idara ya Uhamiaji, ambapo amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuboresha huduma kwa wananchi na wageni wanaoingia nchini. Amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika uboreshaji wa pasipoti, akieleza kuwa pasipoti ya Tanzania imekuwa miongoni mwa pasipoti bora katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, huku ikiwa na mifumo imara ya kiusalama inayoweza kuwa mfano kwa nchi nyingine. “Ni jambo kubwa ambalo Watanzania wanapaswa kujivunia kwamba pasipoti yetu ni nzuri na ina security features ambazo kwa nchi nyingine ni ya mfano,” amesema Katambi. Aidha, Katambi ameipongeza Idara ya Uhamiaji kwa kutambuliwa kutokana na ubora wa huduma zake, akisema hatua hiyo ni ushahi...
Recent posts

DKT. MAKAKALA: MABORESHO YA RAIS SAMIA YAIFANYA UHAMIAJI KUIMARIKA

 KAMISHNA Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maboresho makubwa yaliyofanyika katika Idara ya Uhamiaji, akisema hatua hizo zimeongeza ufanisi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wageni wanaoingia na wanaotoka nchini. Dkt. Makakala amesema maboresho hayo yamekuwa chachu ya kuimarisha utendaji kazi wa Idara ya Uhamiaji na kuiwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi, hususan katika kusimamia shughuli za uhamiaji, udhibiti wa wageni pamoja na utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi na wageni wanaofika nchini. Dkt. Makakala Ameyasema hayo wakati akizungumza katika Kikao Kazi cha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji na Maafisa Uhamiaji wa Mikoa, kilichofanyika mkoani Kilimanjaro, kikao kilicholenga kutathmini utendaji kazi wa Idara ya Uhamiaji katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026, pamoja na kupitia utekelezaji wa mpango na bajeti kwa ...

TANZANIA YATAKA KISWAHILI KIPATE NAFASI YAKE UMOJA WA MATAIFA

 Na Prosper Makene Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeiomba jamii ya kimataifa kuipa lugha ya Kiswahili heshima yake kama lugha ya umoja, ujumuishaji na utambulisho wa Kiafrika. Hayo yamesemwa na Mhe. Balozi Dkt. Hoyce Temu, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa na Mashirika mengine ya Kimataifa nchini Uswis, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Asili ya Afrika yaliyofanyika Geneva hivi karibuni. Balozi Dkt. Temu amesema lugha ina mchango mkubwa katika kulinda urithi, utu na haki za watu.  Mkutano huo uliandaliwa na Chuo cha Uma cha Kiafrika Uswisi, UPAF, pamoja na washirika wengine.  Balozi Dkt. Temu amewashukuru UPAF kwa kazi nzuri wanayofanya ya kukuza utamaduni wa Kiafrika kupitia Mradi wa Kiswahili. Amesema kwa Tanzania, Kiswahili ni zaidi ya lugha ya mawasiliano. “Ni lugha ya umoja wa Kiafrika, utambulisho, amani na ushirikiano kati ya nchi. Inaunganisha watu wengi kuvuka mipaka. Leo hii inatumika pia...

TANZANIA YAKABIDHIWA BENDERA KUWA MWENYEJI WA MASHINDANO YA MISS WORLD 27

 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, amekabidhiwa rasmi bendera ikiwa ni ishara ya kupokea kijiti cha kuandaa mashindano ya 74 ya Ulimbwende wa Dunia (Miss World 2027) Amekabidhiwa bendera hiyo Septemba 05, 2026 nchini Vietnam wakati wa mashindano ya Miss World 2026.

TANZANIA HIGHLIGHTS MILESTONES IN KISWAHILI’S GLOBAL RECOGNITION

 By Prosper Makene Geneva, Switzerland – The United Republic of Tanzania has called for the international community to give Kiswahili its rightful place as a global language of unity, inclusion, and cultural identity.  Speaking recently during the commemoration of the International Day for People of African Descent in Geneva, H.E. Ambassador Dr. Hoyce Temu, Deputy Permanent Representative to the United Nations Office and other international organizations in Geneva, emphasized that language is central to preserving African heritage, dignity, and justice. The event was organized by the Université Populaire Africaine en Suisse, UPAF, and other partners and was held within the Second International Decade for People of African Descent, 2025–2034. Ambassador Dr. Temu thanked UPAF for its continued work in promoting African heritage through projects such as the Kiswahili Project. Ambassador Dr. Temu told the gathering that for Tanzania, Kiswahili is more than a means of communication...

RAIS SAMIA KUZINDUA MAJENGO 26 YA WIZARA, TAASISI 11 NA KM 57.1 ZA BARABARA MJI WA SERIKALI MTUMBA

  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua majengo ya Ofisi za Wizara 26, Taasisi za Serikali 11 pamoja na barabara za lami zenye urefu wa kilomita 57.1 katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma. Uzinduzi huo utafanyika Septemba 8, 2026 katika Uwanja wa Mashujaa, Mji wa Serikali Mtumba, ikiwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa azma ya kuifanya Dodoma kuwa kitovu cha shughuli za Serikali. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Sept 6,2026 Jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Profesa Palamagamba Kabudi, amesema uzinduzi huo utahusisha maeneo matatu makubwa ambayo ni majengo ya Wizara, majengo ya Taasisi za Serikali na barabara za lami zilizojengwa katika Mji wa Serikali Mtumba. Ujenzi wa Mji wa Serikali ulianza kutekelezwa kwa awamu, ambapo awamu ya kwanza ilianza Novemba 28, 2018 na kukamilika Machi 22, 2019, ikihusisha ujenzi wa majengo 23 ya ofisi za awali. "Baadhi ya majengo mengi...