BAADHI ya manifesto ambazo aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Amolo Odinga alitumia katika kampeni zake za urais zitakuwa sehemu ya masomo katika Chuo cha Uongozi na Utawala cha Raila Amolo Odinga kinachoanzishwa chini ya Chuo cha Serikali Kenya (KSG). Chuo hicho, kilichozinduliwa Jumanne na Rais William Ruto wakati wa maadhimisho ya miaka 100 ya KSG, kinalenga kuhifadhi na kufundisha falsafa za Raila kuhusu utawala bora, demokrasia, huduma kwa umma na maendeleo ya bara Afrika. Mkurugenzi Mkuu wa KSG, Profesa Nura Mohamed, alisema kundi la kwanza la wanafunzi linatarajiwa kuanza masomo mwezi Septemba. Alisema mtaala wa chuo hicho utajengwa juu ya nguzo tano kuu zilizotawala maisha ya kisiasa ya Raila; umoja wa Afrika, uongozi ushirikishi, utawala bora, elimu na ubunifu, pamoja na amani na haki. “Alipokuwa akiwania urais alikuwa na manifesto mbalimbali, na baadhi yake zitajumuishwa katika masomo ya chuo hiki ili maono yake yaweze kutekelezwa,” alisema. Profesa Mohamed alisema walipol...
WANANCHI wa Mkoa wa Mara wanatarajia kupata ahueni ya huduma za afya baada ya Hospitali ya Royal Polyclinic kutangaza kuwa ipo katika hatua za mwisho za kuanza kutoa huduma kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), hatua inayotarajiwa kupunguza usumbufu wa kusafiri nje ya mkoa kutafuta matibabu ya kibingwa. Akizungumza katika Hospital ya Royal Polyclinic Musoma, Mkurugenzi wa Royal Polyclinic, Stella Eyembe, amesema hospitali hiyo imekamilisha taratibu muhimu za kuingia mkataba na NHIF na muda si mrefu wanachama wa mfuko huo wataanza kupata huduma zote za matibabu katika hospitali hiyo. "Kwa muda mrefu wananchi wengi wa Mkoa wa Mara walitamani huduma za NHIF zipatikane Royal Polyclinic. Sasa tupo katika hatua za mwisho za kukamilisha mkataba, na hivi karibuni wanachama wa NHIF wataanza kuhudumiwa hapa kwa urahisi na kwa viwango vya juu," amesema. Ameongeza kuwa mbali na NHIF, hospitali hiyo tayari inapokea wagonjwa kupitia bima nyingine mbalimbali huku ikiendelea kupanu...