Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

DK SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKU SHAHADA KWA WATANZANIA ASEMA NI YAO

  Na Beda Msimbe,TBN, Moscow Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) huku akiitoa shahada hiyo kwa Watanzania. Shahada hiyo ilitolewa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni,2026. Rais Mhe. Dk Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania, pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii, Akizungumza baada ya kupewa shahada hiyo Rais Samia alisema kwamba heshima aliyopewa si ya mafanikio yake binafsi bali ni utambuzi wa juhudi na matarajio ya watanzania wote. Alisema shahada hiyo ni ishara ya utambuzi wa dhamira ya pamoja ya Watanzania wote katika kuleta maendeleo,ushirikiano na ustawi wa binadamu. “Nil...
Recent posts

MWANZA KINARA KATIKA USIMAMIZI WA MAAFA

 Na, mwandishi wetu - Mwanza Mkoa wa Mwanza umetajwa kuwa Kinara kwa kuratibu na kusimamia ipasavyo shughuli za kukabiliana na maafa, majanga na mawasiliano ya dharura kutokana na hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya utayari na mwitikio wa dharura. Sifa hizo zimetolewa Juni 4, 2026 na wataalamu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa yanayofanyika mkoani Mwanza kwa siku mbili yakilenga kuongeza uwezo wa kukabiliana na majanga. Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Said Mtanda amesema maafa yameendelea kuwa tishio kubwa duniani kutokana na athari zake kwa maisha ya watu, uchumi na maendeleo ya jamii. Ametaja baadhi ya majanga yanayoikabili Tanzania kuwa ni mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi, mioto ya misitu na magonjwa ya mlipuko. Kutokana na kuongezeka kwa matukio hayo Mhe. Mtanda amezitaka Wilaya zote Mkoani humo kuwa na mipango kazi na mifumo imara ya usimamizi wa maafa ili kuhakikisha maandalizi, mw...

TASAC NA NBS KUFANYA SENSA YA VYOMBO VYA USAFIRI WA MAJINI NCHINI

 SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wanatarajia kufanya sensa ya vyombo vya usafiri wa majini nchini katika hatua inayolenga kupata takwimu sahihi zitakazosaidia kuboresha usimamizi, usalama na maendeleo ya sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa taifa. Akizungumza leo Jun 3,2026 jijini Dodoma wakati wa hafla ya utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili, Mkurugenzi Mkuu wa TASAC, Mohamed Salumu amesema sensa hiyo itasaidia kufanya uhakiki na uboreshaji wa takwimu zilizokusanywa mwaka 2021 ili kuakisi hali halisi ya sasa ya sekta ya usafiri wa majini. Amesema sensa iliyofanyika mwaka 2021 ilibaini kuwepo kwa takribani vyombo 6,000 vya usafiri wa majini, lakini makadirio ya sasa yanaonyesha idadi hiyo inaweza kuwa imeongezeka hadi kufikia vyombo 21,600. Hivyo, sensa mpya itatoa taswira sahihi ya ukubwa wa sekta na kusaidia kupanga mikakati bora ya maendeleo. Kwa upande wake, Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Am...

LUDEWA YAIMARIKA KIMAENDELEO: ELIMU, MAJI, UMEME NA BARABARA ZAPIGWA JIWE KUBWA

 Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Joseph Zacharius Kamonga, amesema Serikali imeendelea kufanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo katika sekta mbalimbali ndani ya jimbo hilo, hali iliyosaidia kuboresha maisha ya wananchi kwa kiasi kikubwa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Kamonga amebainisha mafanikio na changamoto zilizopo katika sekta za elimu, maji, umeme na barabara, akisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo vijijini. Katika Sekta ya Elimu Kamonga amesema sekta ya elimu imepata mafanikio makubwa kupitia ujenzi wa shule mpya za sekondari pamoja na taasisi za mafunzo ya ufundi. Amezitaja baadhi ya shule mpya kuwa ni Rubonde, Mkia, Ugera, Ruhuhu na Chifldasta Masasi, akisema shule hizo zimeongeza fursa kwa watoto wa Ludewa kupata elimu karibu na makazi yao. Aidha, ameeleza kuwa ujenzi wa Chuo cha VETA cha Mkoa pamoja na Baadhi ya vyuo umeongeza fursa kwa vijana kupata mafunzo ya vitendo na ujuzi wa kujiajiri ambapo ...

MAWAZIRI WA EAC WAAZIMIA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI

 Mawaziri wenye dhamana ya sekta za Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wameazimia kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuongeza ushindani wa uchumi wa kikanda, kuimarisha mtangamano wa soko la pamoja na kuchochea maendeleo ya viwanda katika Jumuiya. Azimio hilo limefikiwa katika Mkutano wa 48 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Juni 4, 2026 katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha. Mkutano huo ulitanguliwa na kikao cha wataalamu kilichofanyika kuanzia Mei 29 hadi Juni 1, 2026, na baadaye kufuatiwa na kikao cha Makatibu Wakuu kilichofanyika Juni 2 hadi 3, 2026. Vikao hivyo vilijadili masuala mbalimbali kuhusu biashara na uwekezaji kabla ya kuwasilisha mapendekezo kwa mawaziri kwa ajili ya maamuzi. Katika mkutano huo, mawaziri walipokea, kujadili na kuridhia mapendekezo yaliyowasilishwa na Kamati ya Forod...

TANZANIA YATUMIA JUKWAA LA CISAC KUIMARISHA HAKIMILIKI AFRIKA

Tanzania imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuimarisha mifumo ya hakimiliki na kulinda ubunifu barani Afrika kupitia ushiriki wake katika mkutano wa Kamati ya Kanda ya Afrika ya Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Watunzi na Wasanii (CISAC Regional Committee for Africa - CAF) uliofanyika Juni 1 na 2, 2026 mjini Paris, Ufaransa. Ujumbe wa Tanzania kutoka Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA), ulioongozwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki, Bi. Naomi Mungure, ulikutana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Saidi Othman Yakubu, na kumweleza kuhusu mafanikio na mijadala iliyofanyika katika mkutano huo. Miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa ni maendeleo, fursa na changamoto zinazotokana na matumizi ya Akili Mnemba (Artificial Intelligence - AI) katika sekta ya hakimiliki, mifumo ya usajili na uhakiki wa kazi za ubunifu, ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha, pamoja na njia za kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za hakimiliki barani Afrika...