NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), umepongeza uamuzi wa wabunge kumthibitisha Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais kwa kura 324, sawa na ushindi wa asilimia 100. Akisoma tamko la UWT, Agosti 28, 2026, Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Umoja huo Taifa, Mary Chatanda, amesema ushindi wa asilimia 100 unadhihirisha imani kubwa waliyonayo wabunge kuwa Makamu wa Rais mteule, atatimiza kikamilifu majukumu yake katika kumsaidia Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. "UWT tunawapongeza wabunge kwa kupiga kura za kishindo kwa asilimia 100 na hivyo kufanikisha hatua muhimu iliyokuwa mbele ya kuthibitishwa bungeni," amesema Chatanda. Ameongeza kuwa, UWT inaiunga mkono Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kupitisha jina la Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais kwani ni kiongozi mzalendo, mchapakazi na muadilifu katika utekelezaji wa majukumu. "Halmashauri Kuu haikufanya makosa kupitisha jina hili kwani kote alipofanya kazi, Ndejembi ameonyesha uwezo mkubw...
MWENYEKITI wa Bunge Bonanza, Festo Sanga, amesema maandalizi yote yamekamilika kwa ajili ya Bonanza la Bunge–NMB litakalofanyika kesho, Agosti 29, 2026, katika Viwanja vya John Meling, jijini Dodoma. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Sanga amesema bonanza hilo litaanza saa 12:00 asubuhi, likiwa na ushiriki wa taasisi na wizara mbalimbali za Serikali, huku washiriki wakitarajiwa kuwa wengi zaidi ikilinganishwa na mabonanza yaliyopita. Amesema bonanza hilo ni sehemu ya jitihada za Bunge kuendeleza michezo miongoni mwa watumishi, pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge na taasisi mbalimbali za Serikali na wadau wake. “Mheshimiwa Spika ametoa msisitizo kwamba Bunge lazima lijishirikishe katika shughuli za michezo, kwa sababu michezo ni muhimu katika kuimarisha afya na kujenga ushirikiano,” amesema Sanga. Takribani wizara 14 pamoja na taasisi nyingine zaidi ya 10 zimealikwa kushiriki bonanza hilo, hivyo kufanya idadi ya taasisi zinazotarajiwa kushiriki kufiki...