Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RAIS SAMIA AHIMIZA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA AFYA, BARANI AFRIKA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa nchi za Afrika kuongeza uwekezaji wa ndani katika sekta ya afya ili kujenga mifumo imara, endelevu na inayojitegemea katika usimamizi wa sekta hiyo. Rais Dkt. Samia ametoa wito huo leo, tarehe 22 Julai, 2026 alipohutubia Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya, uliofanyika jijini Accra, nchini Ghana. Mkutano huo umejadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa Ajenda ya Afya ya Afrika kupitia usawa katika upatikanaji wa huduma, afya kwa wote, kutokomeza UKIMWI, kuboresha afya ya mama na mtoto, pamoja na kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza na yasiyopewa kipaumbele. Amesema Tanzania tayari imeanza kutekeleza Ramani ya Afya ya Umoja wa Afrika 2030 kwa kuiingiza katika Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa 2026/2027-2030/2031, huku ikijielekeza kwenye uwekezaji katika uzalishaji wa dawa, kuimarisha mifumo ya afya na kuongeza uwezo wa nchi kujitegem...
Recent posts

KAMATI YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA MAAFA YAIDHINISHA MPANGO WA DHARURA WA TAIFA WA KUKABILIANA NA MADHARA YA EL NIÑO

 Na.Mwandishi wetu - Dar es Salaam Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu ya Usimamizi wa Maafa imeidhinisha Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El Niño na kuzielekeza Wizara, Idara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri kuongeza kasi ya maandalizi ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua za El Niño zinazotabiriwa kudumu hadi mwisho wa mwaka 2026. Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, ameelekeza kila sekta kutenga rasilimali zitakazowezesha hatua za kuzuia, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali katika eneo lake na pia kuandaa mipango ya dharura ya manunuzi. Pia amesisitiza umuhimu wa kutambua mapema maeneo hatarishi, kufanya tathmini za vihatarishi na kuwahamasisha wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kuhamia maeneo salama. Aidha, Dkt. Yonazi ameelekeza wananchi kupewa elimu kuhusu namna ya kupunguza madhara ya mvua hizo kwa kuweka ...

AGIZO LA RC LATEKELEZWA: FAMILIA YA RUHUMBIKA KASANJE YALIPWA FIDIA

Familia ya Ndugu Ruhumbika Machumu Kasanje, mkazi wa Kijiji cha Chirorwe aliyekuwa anaidai fidia Kampuni ya Wakazi Mining Limited imelipwa kufuatia maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi aliyoyatoa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho jana tarehe 21 Julai, 2026.  Akizungumza leo tarehe 22 Julai, 2025 baada ya familia hiyo kulipwa fidia na kuhama katika eneo hilo, Mhe. Mtambi amepongeza hatua hiyo kwa kuwa inamaliza mgogoro uliodumu kwa muda mrefu na kuyaondoa maisha ya familia hiyo katika hatari za kiusalama baada ya baadhi ya watu waliokuwa wamepata ajira kwenye mgodi huo kuifanyia vurugu za kuharibu mazao ya familia hiyo baada ya mgodi huo kufungwa.  “Kulipwa kwa fidia hiyo kunatuwezesha kuufungua tena mgodi huo uendelee na shughuli zake za kawaida za uchimbaji wa madini ambapo watu zaidi ya 400 wamepata ajira na maisha yao yanategemea mgodi huo” amesema Mhe. Mtambi.  Akizungumza katika mkutano wa hadhara, Mhe. Mtambi alit...

WAZIRI MAVUNDE AELEKEZA USIMAMIZI THABITI WA SHERIA ILI ASILIMIA 90 YA BIDHAA NA HUDUMA MIGODINI KUFANYWA NA WATANZANIA

 ▪️Ampongeza Rais Samia kwa kuwa kinara wa ushirikishwaji wa Watanzania migodini ▪️Awataka Watanzania kuunganisha nguvu na kutoa huduma bora ▪️Atoa angalizo kwa wawekezaji kutii sheria za nchi ▪️Ununuzi wa bidhaa na huduma sasa wafikia Shilingi Trilioni 5.1 kwa mwaka MWANZA Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony P. Mavunde, ameelekeza usimamizi madhubuti wa Sheria ya Madini na kanuni zake ili kuhakikisha asilimia 90 ya bidhaa na huduma zinazotumika katika migodi nchini zinatolewa na Watanzania, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa wananchi na kukuza uchumi wa nchi. Waziri Mavunde ametoa maelekezo hayo mapema leo Julai 22, 2026, wakati akizindua Jukwaa la Tano la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini, lililofanyika Mwanza na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo, wakiwemo kampuni za uchimbaji wa madini, watoa huduma migodini, wafanyabiashara wa madini, wawekezaji, taasisi za umma na binafsi pamoja na vyama vya wachimbaji wa madini nchini. Amesema u...

MADHARA YA KUCHEZEA AMANI SIERRA LEONE

 Julai 16, 2026, mwandishi Fern McErlane alichapisha makala maalum inayotukumbusha gharama kubwa na chungu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka 11 nchini Sierra Leone. Pichani, ni mabinti warembo kabisa—sawa na wale tunaowaona hapa kwetu Tanzania—lakini mmoja hana mguu na mwingine hana mkono, na wapo wengi Sierra Leone waliopitia mateso haya. Haya ni majeraha ya moja kwa moja ya ujinga wa wachache waliochezea amani ya nchi yao. Picha nyingine ni timu ya mpira wa miguu ya vijana, wakicheza kwa mguu mmoja #kemeaUjingaTunzaAmani.

MAKONDA: ACHENI KUFUATA TAARIFA ZA MITANDAONI, JIFUNZENI KUTAMBUA FURSA ZA KIUCHUMI

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amewahimiza Watanzania kuacha kuamini taarifa zisizo sahihi zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na badala yake kutumia programu za elimu ya fedha kuongeza maarifa ya biashara na uwekezaji. Akizungumza katika uzinduzi wa Msimu wa Nne wa kipindi cha Elimu ya Fedha “Zogo Mchongo” uliofanyika Makao Makuu ya CRDB Bank jijini Dar es Salaam, Makonda amesema elimu ya fedha haiishii kuwaelekeza wananchi mahali pa kupata huduma za kifedha, bali pia huwafundisha namna ya kufanya biashara, kuendesha biashara kwa ufanisi na kutambua fursa zilizopo katika mazingira yao. Aidha, amesema ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za kifedha unalenga kuwapatia wananchi taarifa sahihi na maarifa yatakayowasaidia kufanya maamuzi bora ya kiuchumi na kujiongezea kipato.