SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limetangaza kuwa baadhi ya mikoa nchini itakumbwa na kukosekana kwa huduma ya umeme kwa muda katika kipindi cha kuanzia Julai 30 hadi Agosti 17, 2026, ili kupisha utekelezaji wa hatua za mwisho za Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma. Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Irene Gowele, amesema mradi huo umefikia asilimia 94 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika rasmi Agosti 21, 2026. Amesema hatua zilizobaki zinahusisha kazi ya kuvuta nyaya za umeme katika maeneo ya Mkambalani mkoani Morogoro na Kikombo mkoani Dodoma, kazi inayohitaji baadhi ya njia za kusafirisha umeme kuzimwa kwa muda ili kuhakikisha usalama wa wafanyakazi, wananchi pamoja na miundombinu ya umeme wakati wa utekelezaji wa mradi huo. "Kazi hizi ni muhimu kwa ajili ya kukamilisha mradi huu wa kimkakati, hivyo kutakuwa na ulazima wa kusitisha huduma ya umeme katika...
Na Dawati la Habari Polisi Mwanza Jeshi la Polisi Wilaya ya Nyamagana limewataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani na usalama wa jamii kwa kushirikiana kwa karibu na vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na serikali za mitaa katika kuwabaini na kuwafichua wahalifu wanaojificha kwenye maeneo yao. Wito huo umetolewa Julai 26, 2026 na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Nyamagana, SSP Virginia Sodoka, wakati wa fainali za mashindano ya Polisi Jamii Cup zilizofanyika katika Kata ya Mirongo, ambapo Mashi FC ilitwaa ubingwa baada ya kuifunga Mirongo FC mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mirongo. Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi na mashabiki wa soka waliojitokeza kushuhudia fainali hizo, SSP Sodoka alisema vijana ni nguvu kazi ya taifa na nguzo muhimu katika kuhakikisha mfumo wa Polisi Jamii unafanikiwa. "Vijana wana nafasi kubwa ya kuwa walinzi wa amani katika jamii. Mkiamua kushirikiana na Jeshi la Polisi mtasaidia kuzuia uhalifu kabla haujatokea. Lakini pia msipo...