Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua meli nne mpya za mizigo katika Ziwa Tanganyika na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Tabora hadi Kigoma, yenye urefu wa kilomita 506. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua meli hizo leo Jul 20,2026 Mkoani kigoma ambapo amesema kuwa Serikali inaendelea kujenga mfumo jumuishi wa uchukuzi nchini unaounganisha reli, bandari, barabara na viwanja vya ndege ili kupunguza gharama za usafirishaji, kuongeza ushindani wa biashara na kufungua masoko mapya. "Kigoma haitakuwa tena mwisho wa reli. Itakuwa mwanzo wa kufunguka kwa fursa za biashara na uwekezaji," amesema Rais Dkt. Samia. Ameongeza kuwa, reli ya Tabora-Kigoma, itakapokamilika, itaunganisha mkoa huo na Bandari ya Dar es Salaam pamoja na mtandao wa bandari za kisasa katika Ziwa Tanganyika, hivyo kurahisisha usafirishaji wa mizigo ndani na nje ya nchi. Rais Dkt. Samia amesema uwekezaji unaoendelea kufany...
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amekutana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS), Mhe. Moussa Saleh Batraki, katika mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na OACPS pamoja na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya mageuzi ndani ya Jumuiya. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 20 Julai 2026, Waziri Kombo amesisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuunga mkono mageuzi yanayolenga kuifanya OACPS kuwa taasisi yenye ufanisi, uwajibikaji na uwezo mkubwa wa kuhudumia nchi wanachama. Aidha, Waziri Kombo ameeleza umuhimu wa OACPS kuwa daraja na kiungo muhimu cha kuimarisha ushirikiano kati ya nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki, pamoja na kuwa na usimamizi bora wa rasilimali na utekelezaji wenye matokeo wa programu za Jumuiya ili kuongeza imani ya nchi wanachama na washirika wa maendeleo. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa OACPS, Mhe.Batraki...