Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WIZARA YA MALIASILI NA TAASISI ZAKE ZAJIPANGA UJIO WA MAONESHO YA NANENANE

 📌Kamati ya kitaifa yakutana kwa ajili ya maandalizi na kutoa mwelekeo wa ushirikiano wa Wizara 📌Maliasili yajipanga kuleta wanyama hai na kutangaza vivutio vya Utalii Dodoma  📌Taasisi zajipanga kutoa huduma bora kwa wananchi Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma KAMATI ya kitaifa ya Kuratibu maandalizi ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) kwa Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake imekutana leo Julai 21,2026 Jijini Dodoma na kuazimia kutoa huduma bora kwa wananchi ili watambue kazi na majukumu ya Wizara na taasisi zake. Akizungumza na kutoa maelekezo ya namna ya kuboresha ushiriki wa Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake kwenye maonesho ya nanenane, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utalii, Richard Wandwi amesema, ushiriki wa Wizara kwa mwaka huu unapaswa kuwa wa kiubunifu na kutangaza maeneo ya vivutio vya utalii kwa Mkoa wa Dodoma kama ilivyoainishwa kwenye mkakati wa uendelezaji utalii kwa mkoa wa Dodoma uliozinduliwa na Waziri Mkuu, Mhe Dkt Mwigulu Nchemba. ‘’ Naomb...
Recent posts

RAIS SAMIA AONDOKA NCHINI KUELEKEA NCHINI GHANA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiondoka nchini kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Julai, 2026 kuelekea Accra, Ghana ambapo atashiriki katika Mkutano Mkuu Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu afya, utakaofanyika tarehe 22 Julai, 2026 jijini Accra.

MAPINDUZI YA UMWAGILIAJI: SERIKALI YASAMBAZA PAMPU 2,000, YACHIMBA VISIMA 390 KUINUA KILIMO

Njedengwa, Dodoma Serikali imeongeza kasi ya mapinduzi ya sekta ya kilimo kwa kuanza kusambaza pampu za umwagiliaji na kuchimba visima 390 katika mikoa 15, hatua inayolenga kuwawezesha wakulima kulima mwaka mzima, kuongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha usalama wa chakula nchini. Mpango huo unatarajiwa kunufaisha wakulima 15,022 waliounganishwa katika vikundi 769, huku ekari 13,518.75 zikiingizwa kwenye kilimo cha umwagiliaji ili kupunguza utegemezi wa mvua. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa, alisema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuwainua wakulima wadogo, hususan wanawake na vijana, kwa kuwapatia uhakika wa maji kwa ajili ya uzalishaji. Alisema pamoja na kuendelea na ujenzi wa miradi mikubwa na ya kimkakati ya umwagiliaji, Serikali imeamua kuwekeza pia katika uchimbaji wa visima na usambazaji wa pampu kwa vikundi vya wakulima ili kuongeza tija mashambani. "Tumeelekezwa kutaf...

_DKT MWIGULU: AFRIKA IGEUZE MABADILIKO YA DUNIA KUWA FURSA ZA MAENDELEO_*

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Afrika inapaswa kutumia mabadiliko yanayoendelea katika siasa, uchumi na usalama duniani kama fursa ya kuharakisha maendeleo yake. Amesema inapaswa kufanya hivyo kwa kuimarisha uongozi wa kimkakati, kuongeza thamani ya rasilimali zake na kujenga taasisi imara zitakazolinda maslahi ya wananchi wake na kuharakisha maendeleo ya Bara la Afrika. "Afrika isiendelee kuwa uwanja wa ushindani wa mataifa makubwa. Tunapaswa kutumia nafasi yetu ya kimkakati, rasilimali tulizonazo na nguvu ya watu wetu kujiletea maendeleo yenye manufaa kwa wananchi wetu," amesema. Waziri Mkuu alisema hayo leo (Jumanne, Julai 21, 2026) alipokuwa Mzungumzaji Mkuu katika Mkutano wa Pili wa Wahitimu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania (National Defence College – Tanzania) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam. Alisema dunia inaendelea kushuhudia mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kiusalama yanayo...

SERIKALI NA TARI VYASHIRIKIANA KATIKA KUPAMBANA NA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU

 Na AngelaSebastian, Bukoba Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Tanzania Relief Initiative (TARI) pamoja na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi imefanikiwa kuwaokoa jumla ya wahanga 160 wa usafirishaji haramu wa binadamu katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026. Kati ya wahanga hao, 126 waliokolewa ndani ya mipaka ya Tanzania, huku 34 wakiokolewa kutoka nje ya nchi, hatua inayodhihirisha kuimarika kwa ushirikiano wa kitaifa na kimataifa katika kupambana na uhalifu huo. Takwimu hizo zimetolewa na Afisa kutoka Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Joseph, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wasimamizi wa sheria mkoani Kagera. Mafunzo hayo yamewakutanisha askari wa Polisi, Maafisa Uhamiaji, Waendesha Mashtaka wa Serikali na Mahakimu, yakilenga kuwaongezea uelewa wa namna ya kutambua, kuchunguza na kushughulikia kesi za usafirishaji haramu wa binadamu...

DKT. NUMBI: LCCF 2026 NI JUKWAA MUHIMU KUPANUA FURSA ZA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI*

 📍MWANZA Mwenyekiti wa Kamati ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini kutoka Tume ya Madini, Dkt. Theresia Numbi, amesema Jukwaa la Tano la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini (LCCF 2026) ni jukwaa muhimu la kuwawezesha Watanzania kuongeza ushiriki wao katika uchumi wa madini kwa kuwajengea uelewa kuhusu fursa, sheria na taratibu za utoaji wa bidhaa na huduma migodini. Dkt. Numbi ameyasema hayo leo, Julai 21, 2026, alipokuwa akizungumza mubashara kupitia kipindi cha Tuongee Asubuhi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star TV, akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, CPA Venance Kasiki. Amesema LCCF 2026 inatoa nafasi kwa wadau kujifunza, kujenga mitandao na kuchangamkia fursa zinazopatikana katika sekta ya madini, hususan katika eneo la ushirikishwaji wa Watanzania katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo. Dkt. Numbi amesema utekelezaji wa sera ya ushirikishwaji wa Watanzania ni muhimu katika kuhakikish...