KONGO: Kamanda wa Brigedi ya kujibu ya mashambulizi (FIB) inayohudumu chini ya Mwamvuli wa Umoja wa Mataifa (MONUSCO) nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Brigedia Jenerali Alexandar Masangura amewatembelea Walinda amani wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wa Kikundi Cha Utayari (TANZQRF-05) kilichokalia eneo la Kiteule cha Mambasa kilichopo katika Jimbo la Ituri, Mashariki mwa nchi hiyo tarehe 25 Julai 2026. Lengo la ziara hiyo ni kujionea mazingira halisi ya kiutendaji wakati Kikundi hicho kikiendelea kutekeleza jukumu la ulinzi wa amani. Brigedia Jenerali Masangura amewapongeza walinda amani hao kwa namna wanavyotekeleza majukumu kwa weledi licha ya kuwa na changamoto kadhaa za kimazingira. Brigedia Jenerali Masangula wa Tanzania anaongoza Brigedi hiyo inayoundwa na vikundi kutoka nchi za Tanzania, Malawi, Kenya na Nepal ambavyo vinaendelea kuwajibika Mashariki ya Kongo kwa kulinda raia dhidi ya mashambulizi kutoka kwa makundi ya watu wenye silaha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Uwanja wa Arusha, utakaotumika katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027), unaojengwa Jijini Arusha. Makamu wa Rais amepongeza maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, ambapo amesema ni faraja kuona ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa ili kuvutia michuano hiyo kufanyika nchini Tanzania, inatakelezwa kikamilifu. Amemshukuru Mhe. Rais kwa kuendelea kutoa fedha ili kuhakikisha uwanja huo unakamilika kwa wakati. Aidha, Makamu wa Rais ameishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na mkoa wa Arusha, Wakandarasi na Mshauri Elekezi kwa kazi kubwa waliyofanya katika Uwanja huo. Makamu wa Rais amewataka Viongozi wa Wizara pamoja na Mkoa wa Arusha kusimamia vema agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha barabara zinazotumika katika kufika uwanjani hapo zinakamilika ...