*Ukosefu wa mawasiliano chanzo cha mgogoro wa wabia katika leseni 33* *Wachimbaji watakiwa kuweka mifumo ya wazi ya ushirikiano na mawasiliano* *Serikali yaonya leseni zisizoendelezwa kufutwa* 📍*Mwanza* Ukosefu wa Mawasiliano na taarifa sahihi miongoni mwa wamiliki wa leseni za uchimbaji madini unaweza kuchochea migogoro isiyo ya lazima na kudhoofisha shughuli za uchimbaji, hasa kwa wachimbaji wadogo. Hayo yamebainishwa leo Septemba 15, 2026 jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, wakati akiongoza kikao cha kutatua mgogoro uliowahusisha wachimbaji wadogo jijini humo. Dkt. Kiruswa amesema mgogoro huo umetokana kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa taarifa sahihi na mawasiliano baina ya wabia wanaomiliki kwa pamoja leseni 33, ambapo upande mmoja uliamini kuwa baadhi ya wabia wanafanya uzalishaji bila kumshirikisha na bila kumpatia stahiki zake, huku upande mwingine ukieleza kuwa katika leseni hizo bado haujaanza uzalishaji. Baada ya kusikiliza pande zote, Dkt. Kirus...
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Jumanne Abdallah Sagini amewataka Wananchi wa Mkoa wa Mbeya hasa Wafanyabiashara kuendelea kulipa kodi stahiki kwa mjibu wa Sheria ikiwemo kutoa risiti na unapotoa huduma na kudai risiti baada ya kununua ili kuendelea kuchochea uchumi utakaosaidia kujenga na kuboresha miradi ya Maendeleo ndani ya Mkoa wa Mbeya. Mhe. Sagini amesema Miradi mbalimbali inayotekelezwa mkoani Mbeya inategemea Uwepo wa Uchumi na ni Makusudio mema ya Serikali kuhakikisha uchumi unaimarika katika viwango vya Nchi na hata Uchumi wa Mtu mmoja mmoja na viwango vyote vinategemea ukusanyaji Mapato. Ameyasema hayo leo wakati wa hotuba yake ya Ufunguzi katika kikao cha Ujirani mwema kati ya Majeshi ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania na Malawi yaliyoketi kwa lengo ya kujadili hali ya Usalama na uimarishwaji wa Amani kati ya Nchi hizi hususani kwa mikoa ya Nyanda za juu kusini inayopakana na Nchi ya Malawi. Aidha Mhe. Sagini amewaomba wananchi Kuchukua tahadhari dhidi ya Mvua za El- nino zi...