Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

KISHINDO CHA NGORONGORO SCHOLARSHIP FUND

 Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) kwa kushirikiana na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu  (HESLB) imetoa elimu kwa jamii ya Ngorongoro kuhusu  mfuko wa  Ngorongoro Scholarship Fund  unaolenga kuwezesha wanafunzi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kupata fursa ya masomo ya elimu ya juu kupitia ufadhili Ngorongoro Fund.   Elimu hiyo iliyotolewa katika ofisi za Ngorongoro ilijumuisha wadau muhimu wanaoguswa na mpango huo ambao ni viongozi wa jamii, wanafunzi pamoja na wadau mbalimbali ambao wamepewa uelewa kuhusu vigezo vya mkopo, sifa za waombaji pamoja na kupitia na kujadili mwongozo wa programu ya Ngorongoro Scholarship Fund. Katika kikao hicho, viongozi wa jamii wamepongeza hatua ya Mamlaka ya kushirikiana na HESLB katika kuandaa na kuboresha mwongozo wa mfuko huo, wakieleza kuwa utasaidia kuweka utaratibu unaozingatia usawa, uwazi na mahitaji ya wakati katika kuwawezesha wanafunzi wenyeji kupata fursa za elimu ya juu. Mw...
Recent posts

CDICD YAONGEZA THAMANI YA BLACK GRANITE

 🔸Uchakataji wa kisasa waongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la ndani na nje 🔸Uwekezaji wa kampuni wafungua ajira kwa vijana na kuchochea maendeleo ya viwanda 📍Dodoma Kampuni ya CDICD Group Limited imeendelea kuimarisha mnyororo wa thamani katika Sekta ya Madini kwa kuchakata madini ya black granite na kuzalisha bidhaa mbalimbali za ujenzi zinazouzwa katika soko la ndani na nje ya nchi, hatua inayochochea ukuaji wa viwanda, kuongeza ajira na kukuza mauzo ya bidhaa zenye thamani. Akizungumza jijini Dodoma kwenye Maonesho ya Nane Nane, Meneja wa CDICD, Shija Shimba, amesema kampuni hiyo imewekeza katika kiwanda cha kisasa cha uchakataji wa black granite kinachobadilisha mawe ghafi kuwa bidhaa mbalimbali zikiwemo countertops za majiko, paving stones, slabs za ujenzi na headstones zinazotumika katika makaburi. Amesema shughuli za uchimbaji na uchakataji zinafanyika katika kijiji cha Manyemba, wilayani Chamwino mkoani Dodoma, ambapo kampuni imejikita katika kuonge...

TAASISI 54 ZA UMMA KUWASILISHA TAARIFA ZA UTENDAJI WA UWEKEZAJI BUNGENI

  Dodoma.  Jumla ya taasisi za umma 54 zinatarajiwa kuwasilisha taarifa za utendaji wa uwekezaji mbele ya Kamati za Kudumu za Bunge kwa muda wa wiki tatu, katika mchakato unaolenga kuwezesha uchambuzi wa thamani na utendaji wa mitaji ya umma pamoja na utekelezaji wa mipango ya kimkakati ya taasisi husika. Katika awamu hii iliyoanza Jumatatu, Agosti 3, 2026, taasisi hizo zimepangwa kuwasilisha taarifa zao mbele ya Kamati mbili za Kudumu za Bunge, ambapo 27 zitawasilisha mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) na nyingine 27 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Umma (PAC). Hadi Jumatano, Agosti 5, 2026, taasisi nne zilikuwa tayari zimewasilisha taarifa zao mbele ya Kamati.  Taasisi hizo ni Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) na Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA), huku Kamati zikionesha kuridhishwa na utendaji wa taasisi husika. Uwa...

WAGENI WAMIMINIKA BANDA LA MALIASILI MAONESHO YA NANE NANE*

 📌 Wamo Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala  📌 Wanafunzi kutoka shule mbalimbali wapatiwa elimu ya uhifadhi, malikale, wanyamapori, misitu na nyuki 📌' Kasongoyeye' apata umaarufu mkubwa Banda la Maliasili *Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma* WAGENI mbalimbali wameendelea kumiminika kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye Maonesho ya Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani (NANE NANE), kujionea shughuli mbalimbali za uhifadhi na wanyamapori zinazofanywa na Wizara. Miongoni mwa wageni waliotembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii ni pamoja na Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala mbalimbali ambapo waliipongeza Wizara kwa ushiriki wa Maonesho hayo ya NANE NANE kwani wamekuwa wakichagiza uwepo wa wananchi wengi wanaokuja kufanya utalii wa ndani wa kuona wanyamapori. Makatibu Tawala hao ni pamoja na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kongwa Sozi Ngate, Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma Mjini Sakina Mbugi, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kondoa Christina Kalekezi na Wakuu  wa W...

54 PUBLIC ENTITIES SET TO PRESENT INVESTMENT PERFORMANCE REPORTS TO PARLIAMENT

 Dodoma. A total of 54 public institutions are set to present their investment performance reports before Parliamentary Standing Committees over a three-week period, in a process aimed at enabling Parliament to assess the value and performance of public capital as well as the implementation of the institutions’ strategic plans. The exercise, which began on Monday, August 3, 2026, involves presentations before two Parliamentary Standing Committees, with 27 institutions scheduled to appear before the Parliamentary Standing Committee on Public Investments (PIC) and another 27 before the Parliamentary Standing Committee on Public Accounts (PAC). As of Wednesday, August 5, 2026, four institutions had already presented their reports before the Committees.  They are Air Tanzania Company Limited (ATCL), Tanzania Agricultural Development Bank (TADB), Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA) and Government Procurement Services Agency (GPSA), with the Comm...

TAASISI 54 ZA UMMA KUWASILISHA TAARIFA ZA UTENDAJI WA UWEKEZAJI BUNGENI

 Dodoma.  Jumla ya taasisi za umma 54 zinatarajiwa kuwasilisha taarifa za utendaji wa uwekezaji mbele ya Kamati za Kudumu za Bunge kwa muda wa wiki tatu, katika mchakato unaolenga kuwezesha uchambuzi wa thamani na utendaji wa mitaji ya umma pamoja na utekelezaji wa mipango ya kimkakati ya taasisi husika. Katika awamu hii iliyoanza Jumatatu, Agosti 3, 2026, taasisi hizo zimepangwa kuwasilisha taarifa zao mbele ya Kamati mbili za Kudumu za Bunge, ambapo 27 zitawasilisha mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) na nyingine 27 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Umma (PAC). Hadi Jumatano, Agosti 5, 2026, taasisi nne zilikuwa tayari zimewasilisha taarifa zao mbele ya Kamati.  Taasisi hizo ni Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) na Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA), huku Kamati zikionesha kuridhishwa na utendaji wa taasisi husika. Uwas...