NAIROBI, Kenya. Mustakabali wa kisiasa wa Naibu Rais wa zamani wa Kenya,Rigathi Gachagua umeendelea kugubikwa na sintofahamu huku macho ya Wakenya yakielekezwa mahakamani kusubiri hukumu muhimu inayotarajiwa kutolewa Jumatatu kuhusu uhalali wa mchakato uliomwondoa madarakani. Uamuzi huo unatarajiwa kuwa wa kihistoria kwa kiongozi huyo ambaye kwa miaka ya hivi karibuni amekuwa mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi mkubwa nchini Kenya, hasa katika eneo la Mlima Kenya ambalo lina uzito mkubwa wa kisiasa. Gachagua aliingia madarakani mwaka 2022 akiwa Naibu Rais chini ya utawala wa Rais . Hata hivyo, baada ya kipindi cha mvutano wa kisiasa ndani ya serikali, alikumbwa na mchakato wa impeachment uliopitishwa na Bunge la Taifa mwezi Oktoba 2024 na baadaye kuridhiwa na Seneti, hatua iliyomwondoa rasmi katika nafasi hiyo. Tangu kuondolewa madarakani, Gachagua ameendelea kuwa sauti muhimu katika siasa za Kenya, akifanya mikutano ya kisiasa na kukosoa baadhi ya sera za serikali huku akijijenga ...
*Asema uaminifu unazidi kupungua WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka viongozi nchini wawaelimishe wananchi umuhimu wa kuandikishana mikataba wanapopeana ardhi badala ya kuendelea kufanya hivyo kwa kuaminiana. "Viongozi mliopo hapa waambieni wananchi hivi sasa masuala ya ardhi wasifanye kwa kuaminiana, wawe wanaandikishana kwa mikataba na tena katika ofisi za kijiji ili watambulike," amesema. Ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 7, 2026) wakati akizungumza na viongozi wa kada mbalimbali wa mkoa wa Iringa katika kikao cha majumuisho ya ziara zake kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, mjini Iringa. "Ninawasihi wananchi tusiogope kurasmisha mambo yetu kwa sababu uaminifu unaenda unapungua. Tunaporasmisha, tunaepusha migogoro siku za usoni," amesisitiza. Waziri Mkuu ametoa rai hiyo kutokana na wingi wa kero zinazojitokeza kwenye mikutano aliyoishaifanya na hasa kwenye sekta ya ardhi. Amewataka viongozi wanapotaka kufanya uendele...