Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MATAIFA 50 KUSHIRIKI MKUTANO MKUBWA WA MADINI NCHINI TANZANIA

 _Rais Samia Suluhu Hassan kufungua mkutano huo mkubwa mwezi Novemba 2026 -▪️Ni Mkutano mkubwa wa Madini na Uwekezaji ▪️Washiriki 2000 kutoka kushiriki mkutano huo ▪️Kauli Mbiu ya Mkutano inalenga kuongeza thamani madini kwa maendelezo ya Viwanda ▪️Serikali na Sekta Binafsi kushirikiana kuandaa mkutano huo ▪️Waziri Mavunde azindua rasmi maandalizi ya mkutano huo 📍 DAR ES SALAAM.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia S. Hassan anatarajiwa kufungua rasmi Mkutano wa Saba wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIC 2026) utakaofanyika Novemba 19 hadi 21, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Akizungumza leo Juni 27, 2026 wakati wa uzinduzi wa TMIC 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imeamua kujenga uchumi wa viwanda unaotokana na madini kwa kuwekeza katika uchakataji na uyeyushaji wa madini badala ya kuendelea kuuza malighafi. Amesema kaulimbiu ya mkutano huo, "Madini Yaliyoongezwa Thamani: Chach...
Recent posts

DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI LA JENGO LA TAALUMA TIA SINGIDA

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya juu kwa kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia ili kuandaa rasilimali watu yenye ujuzi na uwezo wa kuchangia maendeleo ya Taifa. Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipoweka jiwe la msingi la Jengo la Taaluma la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani Singida. Waziri Mkuu amesema ujenzi wa jengo hilo unaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuboresha mazingira ya elimu ya juu na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi. "Leo hii jengo hili la chuo chetu liko Singida. Hii ni hatua kubwa sana. Hongereni bodi, hongereni chuo, hongereni wanafunzi. Tunawatakia kila la heri," amesema. Aidha, amewapongeza wahandisi, washauri na wakandarasi wazawa wanaotekeleza mradi huo akisema ushiriki wao unaonesha uwezo wa Watanzania katika kutekeleza m...

DKT. MWIGULU: HATUTAFANYA MZAHA NA ANAYETAKA KUVURUGA AMANI YA NCHI

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kulinda amani, usalama wa wananchi na rasilimali za Taifa na haitamvumilia mtu yeyote atakayejihusisha na vitendo vinavyohatarisha usalama wa nchi. Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipowasalimia wananchi wa Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo. Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kufuatilia taarifa kuhusu watu wanaodaiwa kupanga au kufadhili vitendo vinavyoweza kuvuruga amani ya nchi na kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vitaendelea kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo. "Hatutafanya mzaha na mtu wa aina hiyo. Tumepewa jukumu la kuilinda nchi yetu na watu wake, na hatutafanya mchezo kwenye jambo hilo." Amesema Serikali haina mgogoro na chama chochote cha siasa kwa kuwa vyama hivyo vinatambuliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kulinda a...

MIAKA 30 YA TRA: MAKUSANYO YAPAISHWA HADI TRILIONI 32, TANGA YAVUKA LENGO KWA KUKUSANYA BILIONI 495

 📍Wafanyabiashara wakiri kumalizika kwa uhasama wa 'Paka na Chui', taasisi za fedha zaahidi ushirikiano NA Mashaka Mhando, Tanga MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imepata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, ambapo makusanyo ya kodi yamepanda kutoka Shilingi Bilioni 531 mwaka 1996/1997 hadi kufikia Shilingi Trilioni 32 kwa mwaka uliopita. Hayo yamebainishwa leo wakati wa matembezi maalum ya hisani na mazoezi yaliyoanzia katika ofisi za TRA Mkoa wa Tanga hadi viwanja vya Usagara, yakiwa ni sehemu ya kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 30 ya mamlaka hiyo na maandalizi ya Tuzo ya Rais kwa Mlipakodi Bora. Akizungumza baada ya kuongoza matembezi hayo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, aliipongeza TRA kwa hatua kubwa iliyopigwa na kueleza kuwa Mkoa wa Tanga umefanya vizuri kwa kuvuka malengo ya makusanyo kwa asilimia 100. Balozi Batilda alieleza kuwa kukua kwa shughuli za Bandari ya Tanga, mipaka ya Horohoro, na wilayani kumeufan...

KARAMAGI AONGOZA KAMATI SIASA MKOA WA KAGERA KUKAGUA MIRADI

 Na Angela Sebastian ;Bukoba  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Kagera,Nazir Karamagi, ameongoza Kamati ya Siasa ya Mkoa huo kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ikiwa ni utaratibu wa chama hicho kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM ili kuhakikisha miradi inanufaisha wananchi. Katika ziara hiyo, kamati ilitembelea mradi wa ghala la kuhifadhia dagaa uliopo katika Mwalo wa Rukojo, Kata ya Kaagya uliogharimi zaidi ya shilingi milioni 100 pia, ilikagua ujenzi wa shule ya msingi Kamagoba ambao umegharimu zaidi ya shl mil. 300 ambapo Karamagi amemshukuru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kiasi hicho cha pesa ili kufanikisha miradi hiyo yenye manufaa kwa jamii. Pia ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo sambamba na kutenga fedha ya mapato ya ndani kutekeleza miradi mbalimbali kwa ufanisi wa hari ya kulidhisha huku, akisisitiza umuhimu ...

WAFANYABIASHARA MKOANI TANGA WATAKIWA KUWA WAZALENDO KWA KODI KWA UAMINIFU.

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewataka wananchi wanaoanzisha kampuni binafsi kusajili ndani ya mkoa ili kuongeza mapato  ya mkoa Kwa mafunufaa ya mkoa na taifa Kwa ujumla . Hayo ameyasema alipokuwa  akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika katika uwanja wa usagara baada ya matembezi ya furaha ikiwa ni muendelezo wa shughuli  maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya mapato Tanzania TRA yaliyoanza tangu tarehe 22 Juni mwaka huu na  kilele chake ni tarehe 1 julai mwaka huu. Aidha Batilda alisema kuwa kufanya hivyo serikali ya mkoa itafikia malengo inayojiwekea Kila mwaka kwani mkoa wa Tanga una fursa nyingi ya kujipatia Kodi ikiwemo bandari,uvuvi,madini pamoja na mipakani. Sambamba na hayo aliwataka wafanya biashara wote kuweza kutoa risiti  na Kwa wale ambao wanapunguza gharama kwenye risiti waache mara moja tabia ya kuiibia serikali hivyo wafanya biashara hususanabwafanya biashara wa madini kuwa makini katika kuan...