*Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO* Sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania. Inatoa ajira kwa mamilioni ya Watanzania, inachangia usalama wa chakula na ni chanzo kikuu cha malighafi kwa viwanda. Hata hivyo, kwa miaka mingi sekta hii ilikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mitaji, hali iliyowafanya wakulima wengi kuendelea na kilimo cha kujikimu badala ya kilimo cha biashara. Katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita , hali hiyo imeanza kubadilika kufuatia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Kupitia ongezeko la mtaji na upanuzi wa utoaji wa mikopo, benki hiyo imekuwa nyenzo muhimu ya kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa. Serikali imeendelea kuiongezea mtaji TADB ili iweze kuwafikia wakulima wengi zaidi kwa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo kuu ni kuongeza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula, kupunguza umaskini na kukuza kilimo cha kisasa kinachozalisha kwa tija. Mwa...
▪️ Lengo ni kurahisisha huduma kwa wateja *▪️ Kamati ya Bunge yaishauri Serikali kupunguza tozo zinazowaumiza wachimbaji wadogo *▪️ Dhahabu tani 67.8 zenye thamani ya Sh trilioni 18.4 zazalishwa kwenye viwanda vya usafishaji ▪️Waziri Mavunde aeleza mkakati wa kukuza biashara ya Tanzanite DODOMA. Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameiagiza Tume ya Madini kuongeza muda wa uendeshaji wa masoko ya madini mpaka saa 3:00 usiku, hatua inayolenga kuongeza fursa za biashara na kuwahudumia wafanyabiashara na wauzaji wa madini kwa muda mrefu zaidi ili kuendana na mahitaji ya wadau na kuongeza ufanisi katika biashara ya madini. Mavunde ametoa agizo hilo Agosti 11, 2026, wakati akijibu maswali ya Wabunge katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini jijini Dodoma, ambapo Wizara imewasilisha taarifa kuhusu hali halisi na maendeleo ya sekta ya madini nchini. Mavunde amesema Serikali pia inaendelea kuimarisha udhibiti wa biashara ya madini na utoroshaji, huku ikisisitiza u...