Na Mwandishi Wetu, Geita GEITA Gold Mining Limited (GGML) imetenga takribani Sh bilioni 1.2 kwa kipindi cha miaka mitatu kusaidia matibabu ya watoto 300 wenye magonjwa ya moyo nchini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza upatikanaji wa huduma za kibingwa kwa watoto ambao familia zao zinaweza kushindwa kumudu gharama za matibabu. Kupitia makubaliano yaliyosainiwa leo katika ofisi za makao makuu ya Geita Gold Mining Limited (GGML) mkoani Geita, kati ya GGML na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), kampuni hiyo itatoa takribani Sh milioni 400 kila mwaka kusaidia matibabu ya watoto 100 wenye matatizo ya moyo, hivyo kufikisha jumla ya takribani watoto 300 ndani ya kipindi cha miaka mitatu. Ushirikiano huo umefikiwa kwa uratibu wa Global Medicare ya jijini Dar es Salaam, ambayo imekuwa ikiunganisha wadau na kuhamasisha upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo nchini. Makubaliano hayo yanaongeza nguvu katika juhudi za Serikali na wadau w...
SERIKALI imeweka mkakati wa kupunguza muda ambao meli za mafuta hukaa bandarini, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika upokeaji na usambazaji wa mafuta pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji zinazoweza kuathiri bei kwa watumiaji. Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dk. James Mataragio, amesema hayo wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER), jijini Dar es Salaam. Amesema Serikali inalenga kuhakikisha meli zinazowasili nchini zinashusha mafuta kwa ufanisi na kuondoka bandarini kwa wakati, huku akisisitiza kuwa kila taasisi na mdau anayehusika katika mnyororo wa upokeaji na usambazaji wa mafuta anapaswa kutekeleza wajibu wake kwa wakati. “Ni matarajio ya Serikali kuona meli zikifika, zinashusha mafuta na kuondoka. Kila taasisi inapaswa kufahamu jukumu lake na kujipanga ipasavyo,” amesema Dk. Mataragio. Amesema baadhi ya maghala binafsi yanak...