Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

TUMIENI TAALUMA ZENU KULINDA UHURU NA MASLAHI YA TAIFA," RAIS SAMIA AWAASA MAWAKILI WA SERIKALI

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Mawakili na Maafisa Sheria wa Serikali kuhakikisha sheria, mikataba na maamuzi ya Serikali vinalinda uhuru, usalama, rasilimali na maslahi ya Taifa. Rais Dkt. Samia ametoa agizo hilo leo jijini Arusha wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA). Amesema ushindani wa kiuchumi na kisiasa duniani unaitaka Tanzania kuwa na mfumo imara wa sheria unaolinda mamlaka ya nchi, uchumi wake na rasilimali za Taifa. Aidha, amewataka Mawakili wa Serikali kutambua vihatarishi vya kisheria mapema na kutoa ushauri kabla ya Serikali kuingia mikataba, kuanza miradi au kufanya maamuzi makubwa ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na maamuzi hayo. "Ni wajibu wenu kugundua vihatarishi mapema, kushauri kwa wakati na kuhakikisha nchi inalindwa kwa misingi imara ya kisheria," amesema Rais Dkt. Samia. Halikadhalika, amesisitiza ushirikishwaji wa Mawakili na Maa...
Recent posts

ESTHER MATIKO AKABIDHI MIFUKO 120 YA SARUJI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE TARIME MJINI

 MBUNGE wa Jimbo la Tarime Mjini, Mhe. Esther Matiko, amekabidhi mifuko 120 ya saruji kwa shule za msingi zilizopo katika kata za Sabasaba na Nyamisangura, Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara, ikiwa ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuboresha miundombinu ya elimu na kuweka mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mhe. Matiko amesema ofisi yake imekuwa ikipokea maombi mengi kutoka kwa shule, taasisi mbalimbali pamoja na wananchi wanaohitaji msaada wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Alisema pamoja na mahitaji kuwa makubwa kuliko uwezo uliopo, ataendelea kushirikiana na Serikali, viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha changamoto zinazokabili sekta ya elimu zinapatiwa ufumbuzi. "Tumekuwa tukipokea maombi mengi kutoka shule na taasisi mbalimbali. Mahitaji ni mengi sana, lakini kwa ushirikiano wetu na wadau wa maendeleo tutaendelea kuyashughulikia hatua kwa hatua ili kuboresha mazingira ya wato...

TUMIENI TAALUMA ZENU KULINDA UHURU NA MASLAHI YA TAIFA," RAIS SAMIA AWAASA MAWAKILI WA SERIKALI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Mawakili na Maafisa Sheria wa Serikali kuhakikisha sheria, mikataba na maamuzi ya Serikali vinalinda uhuru, usalama, rasilimali na maslahi ya Taifa. Rais Dkt. Samia ametoa agizo hilo leo jijini Arusha wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA). Amesema ushindani wa kiuchumi na kisiasa duniani unaitaka Tanzania kuwa na mfumo imara wa sheria unaolinda mamlaka ya nchi, uchumi wake na rasilimali za Taifa. Aidha, amewataka Mawakili wa Serikali kutambua vihatarishi vya kisheria mapema na kutoa ushauri kabla ya Serikali kuingia mikataba, kuanza miradi au kufanya maamuzi makubwa ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na maamuzi hayo. "Ni wajibu wenu kugundua vihatarishi mapema, kushauri kwa wakati na kuhakikisha nchi inalindwa kwa misingi imara ya kisheria," amesema Rais Dkt. Samia. Halikadhalika, amesisitiza ushirikishwaji wa Mawakili na Maaf...

KAMBARAHE WASIRA ASHIRIKI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA MAWAKILI WA SERIKALI JIJINI ARUSHA

 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Mhe. Kambarage Masato Wasira, leo Julai 13, 2026, ameungana na viongozi mbalimbali wa Serikali kushiriki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha. Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na umehudhuriwa na viongozi wa Serikali, mawakili wa Serikali kutoka taasisi mbalimbali, pamoja na wadau wa sekta ya sheria na haki. Ushiriki wa Mhe. Kambarage Wasira katika mkutano huo unaonyesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za Serikali na wadau wa sekta ya sheria katika kukuza utawala bora, kuimarisha misingi ya haki na kuendeleza maendeleo ya taifa kupitia mifumo imara ya kisheria. Mkutano Mkuu wa TPBA hufanyika kila mwaka ukiwa jukwaa la kujadili masuala ya taaluma ya sheria, kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati ya kuimarisha utendaji wa mawakil...

SERIKALI YAAHIDI KUTUMIA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI YA JUWATA KUTENGENEZA BIDHAA MBALIMBALI

 Serikali imeahidi kuhakikisha washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali yanayotolewa na Jukwaa Huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) wanayafanyia kazi kwa vitendo kwa kuwawezesha katika mikopo inayotolewa na Halmashauri kupitia utengenezaji wa bidhaa mbalimbali zitakazochangia ukuaji wa uchumi. Kauli hiyo imetolewa mkoani Morogoro na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Beatrice Njawa, wakati akifungua mafunzo hayo kwa wananchi. Bi.Njawa ambaye katika semina hiyo alimwakilisha Mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Adam Malima amesema Serikali inataka kuona mafunzo hayo yanazaa matokeo ya moja kwa moja kwa washiriki kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo, kusindika mazao ya kilimo na kutengeneza bidhaa zenye ubora wa kushindana sokoni. Mafunzo hayo ya siku tatu yanayoratibiwa na Jukwaa huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) na kutolewa na wakufunzi wa taasisi ya MAMO ENTREPRNEURSHIP yanalenga kuwajengea wananchi mbalimbali uwezo wa kubuni miradi ya ujasiriamali itaka...

ESTHER MATIKO AWAHIMIZA WANAFUNZI KUSOMA KWA BIDII, ATOA GUNIA 16 ZA MAHINDI KWA SHULE

 MBUNGE wa Jimbo la Tarime Mjini, Mhe. Esther Matiko, amewahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kuwa na ndoto kubwa maishani, huku akisisitiza kuwa elimu ndiyo msingi wa mafanikio yao ya baadaye. Akizungumza na wanafunzi wakati wa ziara yake katika shule mbalimbali za jimbo hilo, ikiwemo shule ya Msingi Nyamisangura, Magufuli, shule ya msingi Tarime, Mhe. Matiko amesema awali alifika kuzungumza na walimu na kukabidhi saruji kwa ajili ya kuboresha sakafu za madarasa, lakini alipokutana na wanafunzi aliamua kuwasalimia na kuzungumza nao. "Nimefurahi sana kuwaona na kuwasalimia.Nawapenda sana. Leo nimetembelea shule tano na katika shule zote mmeonyesha nidhamu na ari kubwa ya kujifunza," amesema. Kutokana na kufurahishwa na mapokezi aliyoyapata, Matiko alitangaza kutoa gunia 16 za mahindi kwa shule mbalimbali ili kuunga mkono mpango wa chakula shuleni, akieleza kuwa lishe bora itawasaidia wanafunzi kujifunza kwa umakini na kufanya vizuri zaidi katika masomo yao. Pia aliwahimiza ...