Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

Waziri Mkuu Avitaka Vyombo Vya Ulinzi na Usalama Kuwa Macho Dhidi ya Wavunja Amani

Recent posts

Tutazifanya Mbio za Siku ya Afrika kuwa za Kimataifa - Makonda

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali inafikiria kuzifanya Mbio za Siku ya Afrika kuwa za kimataifa ili kufanikisha lengo la kuleta maendeleo ya pamoja kwa bara la Afrika.  Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mbio hizo jijini Dar es Salaam Mei 23, 2026, Mhe. Makonda alisema mbio hizo zimeendelea kuwa alama ya umoja, mshikamano na maendeleo ya Waafrika. Alisema Serikali inalenga kukuza mbio za Siku ya Afrika ili ziwe jukwaa la kimataifa litakalokutanisha Waafrika kutoka mataifa mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano na diplomasia kupitia michezo. Akizungumzia mshikamano na uwajibikaji wa Waafrika, Waziri Makonda alisema hakuna Mtu atakayekuja kutupa hela ili kuijenga au kuilinda Tanzania na Afrika isipokuwa Waafrika wenyewe na kusisitiza kuwa ni wajibu wa Watanzania na Waafrika kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha wanailinda na kuiendeleza Afrika kwa kutumia nguvu, umoja na rasilimali walizonazo.  “Sisi ni Waafrika, tunapas...

Elimu Ugonjwa wa Ebola Yatolewa Funguni Sekondari

NA: MWANDISHI WETU, PANGANI Walimu na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga wamenufaika na elimu kuhusiana na ugonjwa wa Ebola. Elimu hiyo imetolewa Mei 22, 2026, na Jackline Mjema ambaye ni Afisa Afya kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa wilaya hiyo alipozungumza na walimu na wanafunzi hao. Katika maelezo yake, Mjema ameeleza kuwa ugonjwa huo huambukizwa na virusi vya Ebola ambapo chimbuko lake lilianzia kwa wanyama wa porini aina ya sokwe na nyani nchini Kongo.  Vilevile, alieleza dalili za ugonjwa huo kuwa ni homa kali, macho kuwa mekundu, maumivu ya kichwa, koo na misuli, kutoka damu puani, masikioni au mdomoni. "Ni vyema mkanawa mikono yenu kwa sabuni na maji tiririka muwapo shuleni na nyumbani, kuepuka kushika matapishi, mate au majimaji kutoka kwa mgonjwa," alisisitiza Mjema. Vilevile, alishauri kuepuka kula nyama mbichi au ambazo hazijaiva vizuri, huku akisisitiza chakula kipikwe na kuiva vizuri ndipo kiliwe.  Njia nyingine za kujikinga ni...

Mawakili Tuwe Watetezi wa Serikali

Mawakili wa Serikali wametakiwa kuendelea kuwa watetezi wa Serikali katika uendeshaji wa mashauri ya madai na usuluhishi kwa niaba ya Serikali na taasisi zake. Hayo yameelezwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali uliofanyika jijini Arusha. “Mawakili wa Serikali wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mtambue mna jukumu la kuendelea kuitetea Ofisi na Serikali mahakamani katika uendeshaji wa mashauri ili tulinde maslahi ya taifa letu,” amesema Dkt. Possi. Pia, amewataka watumishi wa Ofisi hiyo kuendelea kudumisha umoja, mshikamano na upendo ndani ya taasisi kwa kuwa hii ni afya kwa taasisi na nchi yetu na hili liwe mpaka chini kwa watumishi wote. Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo aliwapongeza watumishi wa Ofisi hiyo kwa ushirikiano wa pamoja na mwenendo huu unaendelea kuijengea heshima Ofisi na ina akisi ukomavu wa Ofisi. “Kila kiungo ni muhimu, mchango wa kila mtumishi ni muhimu ili k...

Kashfa za Ufisadi zamwandama Spika wa Bunge la Uganda Anita Anet Among

 Kwa miezi kadhaa sasa, siasa za Uganda zimeendelea kutikiswa na wimbi la tuhuma, uchunguzi wa kifedha na vita ya chini kwa chini ya kuwania madaraka ndani ya Bunge la taifa hilo, huku jina la Spika Anita Among likiendelea kutawala mijadala ya kisiasa nchini humo. Among, ambaye kwa muda mrefu alionekana kuwa mmoja wa wanasiasa wenye nguvu kubwa ndani ya utawala wa Rais Yoweri Museveni, sasa anakabiliwa na presha kubwa kisiasa kufuatia tuhuma za ufisadi, matumizi mabaya ya fedha za umma pamoja na uchunguzi unaodaiwa kuwagusa baadhi ya viongozi waandamizi serikalini. Kupanda kwake kisiasa kulikuwa kwa kasi kubwa. Baada ya kifo cha aliyekuwa Spika Jacob Oulanyah mwaka 2022, Anita Among alichaguliwa kuongoza Bunge na haraka akajijengea ushawishi mkubwa ndani ya chama tawala cha NRM pamoja na miongoni mwa wabunge.  Uwezo wake wa kusimamia mijadala ya Bunge kwa msimamo mkali ulimfanya kuwa mmoja wa watu muhimu zaidi ndani ya mfumo wa utawala wa Museveni. Lakini nyuma ya nguvu hiyo y...

Rais wa Senegal Avunja Serikali Kufuatia Mvutano wa Kisiasa

 Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye amemfuta kazi Waziri Mkuu Ousmane Sonko na kuvunja rasmi serikali yote kufuatia mvutano wa muda mrefu uliokuwa ukiendelea ndani ya uongozi wa nchi hiyo. Hatua hiyo ilitangazwa kupitia televisheni ya taifa usiku wa kuamkia leo, ambapo Ikulu ya Senegal ilieleza kuwa mawaziri wote wameondolewa madarakani huku serikali mpya ikitarajiwa kuundwa katika siku zijazo.  Serikali iliyovunjwa itaendelea kufanya kazi za kawaida za kila siku kwa muda mfupi hadi utawala mpya utakapotangazwa rasmi. Tukio hilo limewashangaza wananchi wengi wa Senegal pamoja na jumuiya ya kimataifa, hasa kutokana na ukweli kwamba Faye na Sonko walionekana kuwa washirika wa karibu kisiasa walioingia madarakani pamoja baada ya ushindi mkubwa wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2024.  Ushindi wao ulipewa taswira ya “mapinduzi ya kisiasa” yaliyomaliza utawala wa muda mrefu wa mfumo wa kisiasa uliokuwa ukitawala nchini humo kwa miaka mingi. Katika uchaguzi huo, Sonko alikuwa mwanasi...

Tawa Yawafikia Waganga wa Tiba Asili na Mbadala Kanda ya Ziwa

Na Mwandishi wetu Jovina Massano. Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA) Kituo Cha Mwanza imekutana na waganga wa tiba za asili na mbadala kwa kuwapatia elimu ya uhifadhi ikiwemo umiliki nyara wanazotumia katika shughuli zao. Akitoa elimu hiyo mbele ya Katibu Mtendaji wa Umoja wa Machifu Tanzania ambae pia ni  Mtemi Nyamilonda wa tatu Harun Mkomangwa  Wilayani  Ilemela mkoani humo mhifadhi wa wanyamapori kutoka TAWA Bw. Omary Mhando amewafafanulia umuhimu wa kutunza maliasili na kufuata taratibu za umiliki wa nyara kwa mujibu wa sheria za uhifadhi. Hakusita kuwambusha namna Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inavyoendelea kuwajali na kuwasikiliza wananchi wake na kutambua umuhimu wao na kuhakikisha inawajengea uelewa mpana kwa kuweka utaratibu wa kutoa elimu ya uhifadhi ambayo itawezesha kuongeza wigo mpana wa kulinda maliasili kwa uhifadhi endelevu wenye misingi thabiti kwa vizazi hata vijavyo. Sanjari na hayo amewaeleza pia umuhimu ...

Jwtz na Majeshi ya EAC Yaimarisha Ushirikiano wa Kiusalama

Na Aron Msigwa, Nairobi – Kenya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Majeshi ya Ulinzi ya nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) yamehitimisha kwa mafanikio zoezi la 14 la pamoja la Vituo vya Uamrishaji vya Kijeshi lijulikanalo kama Ushirikiano Imara 2026 jijini Nairobi, Kenya. Hafla ya kufunga zoezi hilo imehudhuriwa na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Salum Haji Othman, aliyemwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Jacob John Mkunda. Zoezi hilo kubwa la kijeshi limewakutanisha washiriki zaidi ya 400 kutoka Kenya, Tanzania, Uganda, Burundi, Rwanda, Sudan Kusini, Somalia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, likiwa na lengo la kuimarisha utayari, mshikamano na uwezo wa vikosi vya ulinzi na usalama vya nchi wanachama wa EAC katika kukabiliana na changamoto na matishio ya kiusalama yanayolikabili eneo la Afrika Mashariki. Akizungumza wakati wa kufunga zoezi hilo, Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya ...