Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

DKT. MWIGULU: SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA SEKTA BINAFSI KATIKA KUINUA UBORA WA ELIMU NCHINI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuthamini na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi katika sekta ya elimu kutokana na mchango wake mkubwa kwenye kuongeza ubora wa elimu na kuandaa rasilimali watu yenye maarifa, ujuzi na maadili yanayohitajika katika maendeleo ya Taifa. Dkt. Mwigulu amesema hayo alipokuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 11 ya wahitimu wa Kidato cha Nne (Year 11–IGCSE) wa mwaka wa masomo 2025/2026 ya Shule ya Kimataifa ya Feza yaliyofanyika Salasala, Dar es Salaam, leo Ijumaa, Juni 12, 2026. "Nimekuja leo kwa kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambua ubia huu muhimu ambao shule yenu imekuwa ikifanya katika sekta ya elimu. Hatuwezi kuyataja mafanikio katika sekta ya elimu bila kutaja mchango wa shule za sekta binafsi, na kwa umuhususi shule za Feza," amesema Dkt. Mwigulu. Amesema Taasisi ya Feza ni miongoni mwa taasisi zilizochangia kwa kiasi kikubwa mageuz...
Recent posts

SERIKALI IMETOA KIPAUMBELE KWA MIRADI YA KIMKAKATI YA UCHUKUZI MARA

 Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 12 Juni, 2026 ameshiriki uzinduzi wa majaribio ya kutua na kuruka kwa ndege katika Uwanja wa Ndege Musoma na kumuomba Waziri wa Uchukuzi Mhe. Profesa Makame Mbarawa kuanza utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya uchukuzi ya Mkoa wa Mara.  Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtambi ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa reli kwa kiwango cha SGR kutoka Tanga hadi Musoma, mradi wa ukarabati na upanuzi wa Bandari ya Musoma na Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Serengeti. “Kasi hii ya ukamilishaji wa Uwanja wa Ndege Musoma ninaomba ije pia katika miradi hii ya kimkakati ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla” amesema Mhe. Mtambi.  Mhe. Mtambi amesema miradi hiyo muhimu katika kukuza uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara na mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa ujumla kwani itafungua fursa nyingi za kiuchumi nchini Tanzania na nchi jirani zinazopakana na Tanza...

AGNES MARWA AWAKATIA BIMA YA MAJANGA WAJASIRIAMALI MARA

 MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Agnes Marwa, ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kuwawezesha wananchi kiuchumi baada ya kuwakatia bima ya majanga wajasiriamali wadogo wa mkoa huo kupitia ushirikiano na Benki ya NMB, hatua inayolenga kuwapa kinga dhidi ya athari za majanga mbalimbali yanayoweza kuwakumba katika maisha na shughuli zao za kila siku. Kupitia bima hiyo, wanufaika watapata msaada wa kifedha endapo watakumbwa na majanga yaliyofunikwa na bima husika, ikiwemo ulemavu wa kudumu, vifo pamoja na matukio mengine yaliyoainishwa kwenye masharti ya bima. Katika baadhi ya matukio, mnufaika anaweza kulipwa hadi Shilingi milioni mbili, fedha zitakazomsaidia kukabiliana na changamoto zinazojitokeza baada ya janga kutokea. Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi bima hizo katika Manispaa ya Musoma, Mhe. Marwa amesema lengo la mpango huo ni kuwajengea wajasiriamali wadogo usalama wa kifedha na kuwapa uhakika wa msaada wanapokumbwa na matatizo yanayoweza kuathiri maisha yao n...

NANI KAMA RAIS SAMIA? NDEGE ZA ABIRIA KUANZA KUTUA MUSOMA JULAI 2026

 Wananchi wa Mkoa wa Mara wanatarajiwa kuanza kunufaika na huduma za usafiri wa anga kuanzia mwezi Julai 2026 baada ya Serikali kuzindua rasmi majaribio ya kutua na kuruka kwa ndege katika Uwanja wa Ndege Musoma. Akizindua majaribio hayo leo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema Serikali imekamilisha hatua muhimu za ukarabati na upanuzi wa uwanja huo na sasa imeelekeza Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuharakisha kuuingiza Uwanja wa Ndege Musoma katika ratiba zake za safari za abiria. “Ninaiagiza ATCL kuhakikisha Uwanja wa Ndege Musoma unaingizwa haraka katika ratiba za ndege za abiria ili wananchi waanze kupata huduma za usafiri wa anga,” amesema Prof. Mbarawa. Waziri huyo amesema majaribio yaliyofanyika Musoma pamoja na Uwanja wa Ndege Shinyanga yanaonesha kuwa miradi ya ukarabati wa viwanja hivyo imefikia hatua za mwisho na ipo tayari kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Aidha, amezitaka taasisi zinazotekeleza mradi huo, ikiwemo TANROADS, TAA pamoja na wakandarasi, k...

SERIKALI YASISITIZA UMUHIMU WA UADILIFU KATIKA UTUMISHI WA UMMA

    Na, mwandishi wetu - Arusha. SERIKALI imeendelea kusisitiza umuhimu wa kuzingatia misingi ya uadilifu katika utumishi wa umma ili kuhakikisha utekelezaji wa majukumu na mipango ya maendeleo unafanyika kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi. Hayo yamesemwa hii leo (12 Juni, 2026) na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, wakati akifungua Mafunzo ya Kamati ya Uadilifu yaliyolenga kuwajengea uwezo wajumbe wa Kamati Maalum ya Menejimenti katika kusimamia masuala ya uadilifu katika ofisi hiyo. “Uadilifu ni nguzo muhimu katika ufanikishaji wa majukumu na utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika sehemu za kazi,” amesema Dkt. Yonazi. Dkt. Yonazi amesema kuwa ni wajibu wa kila mtumishi wa umma kuhakikisha anazingatia maadili ya kazi na kulinda misingi ya uadilifu ili kuimarisha utendaji na kuongeza imani ya wananchi kwa Serikali. Aidha, Dkt. Yonazi amesema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha wajumbe kusimamia utekelezaji ...