Mbunge wa Jimbo la Serengeti, Mhe. Mary Daniel Surati, amewahimiza wanafunzi kuendelea kusoma kwa bidii, kuweka malengo makubwa na kutumia fursa za elimu kujijengea msingi imara wa maisha na maendeleo ya jamii. Mhe. Surati ameyasema hayo aliposhiriki Usiku wa Tuzo kwa Wadau wa Elimu uliofanyika katika Shule ya Sekondari Manga wilayani Tarime, ambapo hafla hiyo iliambatana na utoaji wa tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo. Hafla hiyo imekuwa sehemu ya kutambua na kuenzi juhudi za wanafunzi walioonesha umahiri katika masomo, huku ikiwahamasisha wengine kuongeza bidii ili kufikia mafanikio makubwa zaidi kitaaluma. Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Surati amesema amefurahishwa na jitihada zinazofanywa na wanafunzi, walimu, wazazi pamoja na wadau mbalimbali wa elimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira yanayowawezesha kufanya vizuri na kutimiza ndoto zao. Amesema mafanikio ya mwanafunzi hayajengwi na juhudi za mtu mmoja pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa k...
📌*Mitungi ya gesi ya kilo sita 3,255 kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya Shilingi 17,500* 📍*Mkinga, Tanga* Serikali imeanza kutekeleza kwa vitendo Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia katika Wilaya ya Mkinga, Mkoa wa Tanga, kupitia mradi wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku. Kupitia mradi huo, jumla ya mitungi 3,255 ya gesi ya kilo sita itasambazwa na kuuzwa kwa wananchi wa Mkinga kwa bei ya ruzuku ya Shilingi 17,500 kwa mtungi. Mwananchi anayehitaji kunufaika na mpango huo anatakiwa kuwa na Kitambulisho cha Taifa (NIDA). Mtungi huo utauzwa ukiwa tayari kwa matumizi, ukiwa na gesi pamoja na vifaa muhimu. Mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, unaolenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia. Utekelezaji wa mradi huo unalenga kuongeza upatikanaji na matumizi ya nishati safi, salama na rafiki kwa afya na mazingira, huku ...