Aelezea ziara ya Rais Samia nchini Urusi Na MWANDISHI WETU SAME - Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema ziara ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi inathibitisha dhamira ya Tanzania kutofungamana na upande wowote. Akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wilayani Same mkoani Kilimanjaro Juni 9, 2026 wakati wa kuhitimisha ziara ya kukagua uhai wa Chama na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, Wasira alisema waasisi wa Taifa wakiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere waliitaka Tanzania kukaa katikati pale pande mbili zinapogombana. “Tulitaka tuwe huru na uhuru uwe wa kudumu. Kazi yetu ni kudumisha uhuru na kudumisha uhuru ni kutupa haki ya kuamua mambo tunayoona yanatufaa sisi, sio kutegemea wengine wakuambie mfanye nini,” alisema. Akizungumzia maswali kuhusu ziara ya Rais Samia Urusi, Wasira alidai: “Na juzi Rais wetu ameenda Urusi wengine wanauliza ameenda kufanya nini. Mbona alivyoenda China hamkuuliza, mbona alipoenda Marekani hamkuuliza. Akienda Urusi...
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, wamekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji ili kuongeza manufaa kwa wananchi wa mataifa hayo mawili kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. Kupitia makubaliano hayo, yalitofanyika mapema hii leo June 9, Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais samia ameeleza kuwa licha ya ukuaji wa biashara kati ya Tanzania na Singapore, kiwango cha sasa cha dola milioni 299 za Marekani bado hakijafikia matarajio ya pande zote. Kwa sasa Singapore imewekeza katika miradi 36 nchini Tanzania, huku makubaliano yaliyofikiwa yakilenga kuongeza uwekezaji, biashara na fursa mpya za ushirikiano katika sekta mbalimbali za uchumi. Tanzania pia imeiomba Singapore kufungua ubalozi wake nchini ili kuimarisha zaidi mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi, pamoja na kuanzisha mfumo wa mashauriano ya mara kwa mara kwa ajili ya kuratibu maeneo ya ushirikiano. Katika sekta ya kilimo, nchi hizo zimeonyesha nia ya k...