Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MWEMBENI SEKONDARI YAPATA MSUKUMO MPYA KUPITIA AGNES MARWA

 SHULE ya Sekondari Mwembeni mkoani Mara imepata msukumo mpya wa kuinua kiwango cha taaluma baada ya Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Agnes Marwa, kukabidhi projector ya kufundishia pamoja na taulo za kike kwa wanafunzi wa shule hiyo, huku akiwataka wanafunzi kujituma katika masomo na kuwa walinzi wa amani ya Taifa. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi Projector ya kufundishia pamoja na Taulo za Kike katika shule ya sekondari Mwembeni, Mhe. Agnes Marwa Mbunge viti Maalumu Mkoa wa Mara, amesema ndoto yake ni kuona Shule ya Sekondari Mwembeni ikitajwa miongoni mwa shule zinazofanya vizuri kitaifa, akisisitiza kuwa mafanikio hayo yatapatikana kupitia nidhamu, juhudi na kujituma kwa wanafunzi. "Natamani sana kuisikia Mwembeni iking'ara kitaifa. Ninyi ndiyo mtakaolibeba na kulipandisha jina la shule yenu. Kumbukeni kuwa elimu mnayoipata ni uwekezaji wa maisha yenu wenyewe, hivyo jitumeni kwa bidii ili kutimiza ndoto zenu," amesema Mhe. Agnes. Mhe. Agnes amesema msaad...
Recent posts

TANZANIA KINARA WA HIFADHI YA GRAPHITE AFRIKA, MAHITAJI YA LITHIUM YAENDELEA KUONGEZEKA DUNIANI

 📍_Dar es Salaam_ Mjiolojia kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Njombe, Abbas Mruma, amesema Tanzania inaendelea kujijengea nafasi muhimu duniani kutokana na kuwa na hifadhi kubwa ya madini muhimu ya kimkakati, yakiwemo graphite, lithium na rare earth elements, ambayo ni nguzo muhimu katika maendeleo ya teknolojia za kisasa na nishati safi. Mruma ameyasema hayo wakati akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Richard Stanslaus Muyungi, alipotembelea banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba). Amesema mahitaji ya madini ya lithium yanaendelea kuongezeka kwa kasi duniani kutokana na matumizi yake katika utengenezaji wa betri za magari ya umeme, simu za mkononi, kompyuta mpakato (laptops) na vifaa vingine vya kisasa vya kielektroniki. Amefafanua kuwa nchini Tanzania, madini ya lithium yanapatikana zaidi katika maeneo ya Dodoma na Ikungi, mkoani Singida. Akizungumzia madini ...

HISTORIA MPYA MAFINGA: SHULE YA SEKONDARI NDOLEZI YAANZA KUPOKEA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO

  Na Mwandishi Wetu, Mafinga SHULE ya Sekondari Ndolezi iliyopo Halmashauri ya Mji Mafinga, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, imeandika historia mpya baada ya kuanza rasmi kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano kwa mara ya kwanza. Hatua hii inatajwa kuwa ukombozi mkubwa utakaopanua fursa za elimu ya sekondari ya juu (A-Level) katika eneo hilo. Akizungumza na wanafunzi wa kwanza waliowasili shuleni hapo, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Mwalimu Stephen Shemdoe, amesema lengo kuu la Halmashauri ni kuhakikisha wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini wanapata elimu bora itakayowezesha kupata matokeo mazuri na kuchangia maendeleo ya Taifa. Mwalimu Shemdoe amebainisha kuwa Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika ujenzi wa miundombinu na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. Kutokana na uwekezaji huo, amewataka wanafunzi kutumia fursa hiyo adhimu kusoma kwa bidii, kutunza mali za shule, na kuzingatia nidhamu ya hali ya juu. "Matamanio ya Serikali ni kuona...

JAKAYA KIKWETE,BAN KI-MOIN WAIBUA DIRA MPYA YA KUINUA ELIMU DUNIANI

 Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya mazungumzo ya ngazi ya juu na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, yaliyolenga kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuboresha elimu ya awali na msingi kwa mamilioni ya watoto duniani. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Seoul, Korea Kusini, ambapo Dkt. Kikwete yupo katika ziara ya kikazi kama Mwenyekiti wa Bodi ya Global Partnership for Education (GPE), taasisi ya kimataifa inayoratibu juhudi za kuongeza fursa za elimu katika zaidi ya nchi 90 duniani. Katika mkutano huo, Dkt. Kikwete alimpongeza Ban Ki-moon kwa kuendelea kuwa kinara wa kuhamasisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hususan kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bora bila kujali mazingira anayokulia. Aidha, alimshukuru kwa mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na Serikali ya Korea Kusini, ambayo imeendelea kuwa miongoni mwa wadau muhimu wanaofadhili miradi ya elimu duniani. Ak...

WAKULIMA WA MARA WAHIMIZWA KUFUATA KALENDA ZA MAZAO YA BIASHARA KUONGEZA TIJA

 Adeladius Makwega – Serengeti, Mara, Tanzania Wakulima wa Mkoa wa Mara wametakiwa kuzingatia kalenda za mazao ya biashara, hususan zao la tumbaku, ili kuongeza tija, kuboresha kipato chao na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Wito huo umetolewa Julai 10, 2026, wilayani Serengeti na Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Mheshimiwa Alfa Haule, alipokuwa akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi, katika mkutano wa WAMACU unaowakutanisha wadau wa zao la tumbaku mkoani hapa. Akizungumza katika mkutano huo, mheshimiwa Haule alisisitiza kuwa sekta ya kilimo ni mhimili muhimu wa uchumi, unaogusa moja kwa moja maisha ya wananchi kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja hadi taifa. “Sekta ya kilimo ni chanzo kikubwa cha mapato. Ina uwezo wa kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja, kaya, kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla. Ni wajibu wa wananchi kuongeza juhudi katika sekta hii huku serikali ikiendelea kuwapa ushirikiano,” alisema Haule. Aidha, aliwataka wakulima kuzingatia mi...

KITABU CHA FALSAFA YA SHERIA YA MAMA SAMIA KUBORESHA MAGEUZI YA KIUCHUMI NA KIJAMII

 SERIKALI imesema, Sheria zinapaswa kutumika kama nyenzo ya maendeleo ya taifa kwakuwa ubora wa Sheria hupimwa kwa matokeo yake katika kuboresha maisha ya wananchi, kuvutia uwekezaji, kuimarisha utawala bora na kuchochea ukuaji wa uchumi. Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Hemed Suleiman Abdullah alipomuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika Uzinduzi wa Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia uliofanyika katika Ukumbi wa Maktaba mpya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), tarehe 10 Julai, 2026.  Aidha, Mhe. Abdulla,amempongeza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari kwa kutoa wazo la kuandikwa kwa Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia (Mama Samia Doctrine of Law): Utekelezaji Wake katika Mageuzi ya Kiuchumi na Kijamii.  “Nitoe pongezi za dhati kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Said Johari, kwa kuja na wazo hili muhimu la kuandaa Kitabu hiki...