Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

CCM:TANZANIA INAHITAJI HOJA ZA MAENDELEO SIYO MAANDAMANO

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema Tanzania inahitaji zaidi ujenzi wa hoja za maendeleo kupitia majadiliano ya kidemokrasia na utekelezaji wa mipango ya maendeleo, badala ya maandamano na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jun 13,2026,jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amesema CCM itaendelea kusimamia na kuimarisha siasa za maendeleo zinazolenga moja kwa moja kutatua changamoto za wananchi na kuboresha maisha yao. Amesema chama hicho kinaendelea kutekeleza majukumu yake kwa vitendo kupitia ziara mbalimbali za viongozi wake nchini, ambapo hukutana na wananchi katika mikutano ya hadhara na majukwaa tofauti kwa lengo la kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu kwa kushirikiana na Serikali. Kihongosi ameongeza kuwa CCM inaelewa vipaumbele vya wananchi ambavyo ni pamoja na huduma bora za afya, maji safi na salama, elimu bora, miundombinu imar...
Recent posts

DEGE ZA ABIRIA KUANZA KUTUA MUSOMA JULAI, 2026

 Waziri wa Uchukuzi Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa leo tarehe 12 Juni, 2026 amezindua majaribio ya kuruka na kutua ndege katika Uwanja wa Ndege Musoma na kuahidi kuwa ndege za abiria kuanza kufanya kutua katika uwanja huo mwezi Julai, 2026. Akizungumza katika hafla, Mhe. Mbarawa ambaye alikuwa mgeni rasmi ameliagiza Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuharakisha utaratibu wa kuupanga Uwanja wa Ndege Musoma katika ratiba za ndege za abiria ili wananchi wa Mkoa wa Mara waweze kuanza kutumia usafiri huo.  “Ninaiagiza ATCL kuhakikisha kuwa inauingiza Uwanja wa Ndege Musoma katika ratiba za ndege haraka iwezekanavyo ili huduma za usafiri ziweze kutolewa kwa wananchi” amesema Mhe. Mbarawa.  Mhe. Mbarawa amesema majaribio ya utayari katika viwanja vya ndege vya Musoma na Shinyanga yanaashiria kukamilika kwa sehemu muhimu za miradi ya ukarabati na upanuzi wa viwanja hivyo na kuwa tayari kuanza kutoa huduma kwa wananchi.  Mhe. Mbarawa amezielekeza taasisi zinazohusika na mra...

CGP. KATUNGU AWATAKA MAAFISA USTAWI KUELIMISHA WAFUNGWA HAKI NA WAJIBU WAO

 Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma. Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii wa Jeshi la Magereza kuhakikisha wanawaelimisha wafungwa na mahabusu kuhusu haki na wajibu wao mara wanapopokelewa magerezani pamoja na taratibu zinazopaswa kufuatwa katika kipindi chote wanaposhikiliwa gerezani. CGP Katungu ametoa maelekezo hayo leo Juni 12, 2026 wakati akifunga rasmi Mafunzo ya Maafisa Ustawi wa Jamii kuhusu Mwongozo wa Utekelezaji wa Programu za Urekebishaji yaliyofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Rugimbana, Msalato jijini Dodoma. Amesema mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Jeshi la Magereza za kuendelea kuboresha huduma za urekebishaji kwa wafungwa sambamba na kutekeleza maelekezo ya Serikali na mapendekezo ya Tume ya Kuboresha Vyombo vya Haki Jinai. Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo, CGP Katungu alisema mwongozo huo umebainisha maeneo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa katika utekelezaji wa jukumu la urekebishaji, ikiwemo maadili...

RAIS SAMIA ATOA AGIZO HILI SEKTA YA FEDHA NCHINI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameielekeza Wizara ya Fedha, Benki Kuu na taasisi za fedha nchini kuimarisha mazingira ya upatikanaji wa mikopo, kupunguza gharama za mikopo na kuongeza ushindani ili kunufaisha sekta binafsi, wanawake, vijana, wakulima na wafanyabiashara wadogo. Ametoa agizo hilo leo katika hafla ya maadhimisho ya miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania, yaliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam. Rais Dkt. Samia amesema mafanikio ya mfumo wa fedha hayapaswi kupimwa kwa idadi ya wananchi waliofikiwa na huduma za kifedha pekee, bali kwa matokeo yake katika kipato, biashara, ajira na ustawi wa wananchi wenyewe. "Kipimo chetu kisiwe tu idadi ya wananchi waliofikiwa na huduma za fedha, bali namna huduma hizo zilivyowaongezea kipato, kupanua biashara, kuwawezesha wakulima kupata mitaji kwa wakati, kuwasaidia vijana kuanzisha kampuni, na kujenga akiba za familia," am...

DKT. MWIGULU: SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA SEKTA BINAFSI KATIKA KUINUA UBORA WA ELIMU NCHINI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuthamini na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi katika sekta ya elimu kutokana na mchango wake mkubwa kwenye kuongeza ubora wa elimu na kuandaa rasilimali watu yenye maarifa, ujuzi na maadili yanayohitajika katika maendeleo ya Taifa. Dkt. Mwigulu amesema hayo alipokuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 11 ya wahitimu wa Kidato cha Nne (Year 11–IGCSE) wa mwaka wa masomo 2025/2026 ya Shule ya Kimataifa ya Feza yaliyofanyika Salasala, Dar es Salaam, leo Ijumaa, Juni 12, 2026. "Nimekuja leo kwa kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambua ubia huu muhimu ambao shule yenu imekuwa ikifanya katika sekta ya elimu. Hatuwezi kuyataja mafanikio katika sekta ya elimu bila kutaja mchango wa shule za sekta binafsi, na kwa umuhususi shule za Feza," amesema Dkt. Mwigulu. Amesema Taasisi ya Feza ni miongoni mwa taasisi zilizochangia kwa kiasi kikubwa mageuz...

SERIKALI IMETOA KIPAUMBELE KWA MIRADI YA KIMKAKATI YA UCHUKUZI MARA

 Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 12 Juni, 2026 ameshiriki uzinduzi wa majaribio ya kutua na kuruka kwa ndege katika Uwanja wa Ndege Musoma na kumuomba Waziri wa Uchukuzi Mhe. Profesa Makame Mbarawa kuanza utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya uchukuzi ya Mkoa wa Mara.  Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtambi ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa reli kwa kiwango cha SGR kutoka Tanga hadi Musoma, mradi wa ukarabati na upanuzi wa Bandari ya Musoma na Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Serengeti. “Kasi hii ya ukamilishaji wa Uwanja wa Ndege Musoma ninaomba ije pia katika miradi hii ya kimkakati ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla” amesema Mhe. Mtambi.  Mhe. Mtambi amesema miradi hiyo muhimu katika kukuza uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara na mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa ujumla kwani itafungua fursa nyingi za kiuchumi nchini Tanzania na nchi jirani zinazopakana na Tanza...