Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Mawakili na Maafisa Sheria wa Serikali kuhakikisha sheria, mikataba na maamuzi ya Serikali vinalinda uhuru, usalama, rasilimali na maslahi ya Taifa. Rais Dkt. Samia ametoa agizo hilo leo jijini Arusha wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA). Amesema ushindani wa kiuchumi na kisiasa duniani unaitaka Tanzania kuwa na mfumo imara wa sheria unaolinda mamlaka ya nchi, uchumi wake na rasilimali za Taifa. Aidha, amewataka Mawakili wa Serikali kutambua vihatarishi vya kisheria mapema na kutoa ushauri kabla ya Serikali kuingia mikataba, kuanza miradi au kufanya maamuzi makubwa ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na maamuzi hayo. "Ni wajibu wenu kugundua vihatarishi mapema, kushauri kwa wakati na kuhakikisha nchi inalindwa kwa misingi imara ya kisheria," amesema Rais Dkt. Samia. Halikadhalika, amesisitiza ushirikishwaji wa Mawakili na Maa...
MBUNGE wa Jimbo la Tarime Mjini, Mhe. Esther Matiko, amekabidhi mifuko 120 ya saruji kwa shule za msingi zilizopo katika kata za Sabasaba na Nyamisangura, Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara, ikiwa ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuboresha miundombinu ya elimu na kuweka mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mhe. Matiko amesema ofisi yake imekuwa ikipokea maombi mengi kutoka kwa shule, taasisi mbalimbali pamoja na wananchi wanaohitaji msaada wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Alisema pamoja na mahitaji kuwa makubwa kuliko uwezo uliopo, ataendelea kushirikiana na Serikali, viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha changamoto zinazokabili sekta ya elimu zinapatiwa ufumbuzi. "Tumekuwa tukipokea maombi mengi kutoka shule na taasisi mbalimbali. Mahitaji ni mengi sana, lakini kwa ushirikiano wetu na wadau wa maendeleo tutaendelea kuyashughulikia hatua kwa hatua ili kuboresha mazingira ya wato...