Na Mwandishi Wetu - Msumbiji SERIKALI imesema inaendelea kujipanga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utafiti katika kukabiliana na majanga katika ukanda wa Kusini mwa Afrika (SADC) na Afrika Mashariki, hatua itakayosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari na uokoaji. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi, wakati wa ziara ya kubadilishana uzoefu kati ya Tanzania na Msumbiji kuhusu hatua za mapema kabla ya majanga. Ziara hiyo ya siku tano inayofanyika jijini Maputo nchini Msumbiji kuanzia Mei 25 hadi 29, 2026, inalenga kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa, tafiti na mifumo ya utoaji wa taarifa za tahadhari mapema ili kupunguza athari za majanga. Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Yonazi alisema Tanzania imeendelea kujenga uwezo wake katika kukabiliana na majanga kupitia uwekezaji katika tafiti na matumizi ya teknolojia za kisasa ikiwemo mifumo ya kidijitali na aki...
📍Mtwara Mkoa wa Mtwara umeendelea kujidhihirisha kama kitovu muhimu cha uwekezaji wa madini nchini kutokana na uwepo wa rasilimali nyingi za madini ya viwandani, vito na madini mkakati, huku mapato ya Serikali kupitia sekta hiyo yakiongezeka kwa kasi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara, Winnifrida Mrema, amesema mkoa huo unafahamika zaidi kwa uwepo wa madini ya chokaa yanayotumika kuzalisha saruji katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote, jambo linalochangia kukuza uchumi wa mkoa na kuimarisha shughuli za viwanda nchini. Amesema Mkoa wa Mtwara pia una utajiri wa madini mengine ya viwandani yakiwemo chuma, shaba, kinywe, ulanga pamoja na madini ya mchanga mzito (heavy mineral sands), ambayo ni miongoni mwa madini mkakati yanayohitajika kwa kiwango kikubwa duniani katika utengenezaji wa teknolojia mbalimbali ikiwemo magari ya umeme. Aidha, amesema Bandari ya Mtwara imeendelea kuwa kiungo muhimu cha biashara na usafirishaji wa madini na bidhaa za ...