Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

_DKT. MWIGULU: MFUMO MPYA WA UNUNUZI PAMBA UJULIKANE NDANI YA MWEZI MMOJA_*

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amemuagiza Waziri wa Kilimo kukutana na wadau wa zao la pamba na ndani ya mwezi mmoja kuwasilisha mapendekezo ya mfumo bora wa ununuzi wa pamba utakaowanufaisha wakulima na kuendeleza uzalishaji wa zao hilo. Ametoa agizo hilo leo, Jumatatu Septemba 14, 2026, wakati akizungumza na wananchi wa Itilima, mkoani Simiyu, baada ya Mbunge wa Itilima, Mhe. Njalu Daudi Silanga, kueleza changamoto zinazowakabili wakulima wa pamba, ikiwemo malalamiko kuhusu mfumo wa sasa wa ununuzi. “Leo tarehe 14, mpaka tunapofika tarehe 14 mwezi ujao, niwe nimeshapata taarifa ya utaratibu mzuri ambao tutakubaliana,” amesema Dkt. Mwigulu. Amesema Serikali italinganisha mifumo iliyowahi kutumika na unaotumika sasa ili kupata utaratibu utakaokuwa na manufaa zaidi kwa wakulima bila kuathiri uzalishaji, bei ya pamba na maisha ya wananchi. Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu amesema Serikali imeondoa sheria iliyokuwa ikiruhusu mifugo ya wananchi kutaifishwa na kuelekeza mapitio ya sh...
Recent posts

MKUU WA MKOA WA MARA BRIGEDIA JENERALI EVANS MTAMBI ATOA POLE KWA RAIS SAMIA

 Mkuu wa Mkoa wa Mara Brigedia Jenerali Evans Mtambi hii leo amefika Kizimkazi Zanzibar kutoa salamu za pole kwa Rais Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha mumewe Ameir Hafidh Hassan kilichotokea hivi karibuni. Brigedia Jenerali Mtambi akiwa ameambatana na mkewe alipata fursa ya kutoa salamu za Wananchi wa Mkoa wa Mara pamoja na kufanya Dua ya pamoja na Viongozi wengine waliofika mahali hapo kwa lengo la kutoa salamu zao.

DC ITUNDA AMFARIJI NA KUMPA POLE RAIS DKT. SAMIA KUFUATIA MSIBA MZITO WA MUMEWE

 Na Mwandishi Wetu, Zanzibar MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, ameungana na majonzi ya Watanzania kwa kuwasilisha salamu za pole na rambirambi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia msiba mzito wa kifo cha mume wake mpendwa. Katika kuonesha utu, heshima, na kuguswa kwa dhati na msiba huo, Mhe. Itunda amefika nyumbani kwa Mhe. Rais visiwani Zanzibar kwa ajili ya kumpa pole na kumfariji uso kwa uso katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mwenza wake wa maisha.  Akiwa msibani hapo, Mhe. Itunda alimpa maneno ya faraja Mhe. Rais na familia yake, akimuombea kwa Mwenyezi Mungu awape subira, afya njema, na nguvu ya kiroho ya kustahimili pigo hili kubwa.  "Tupo pamoja nawe katika kipindi hiki cha majonzi mazito, Mheshimiwa Rais. Tunamuomba Mwenyezi Mungu akutie nguvu wewe na familia nzima, na ailaze roho ya mpendwa wetu mahali pema peponi," yalielezwa sehemu ya maombi na salamu za faraja za Mhe. Itunda.

KIWANDA KIKUBWA CHA KUCHAKATA MCHANGA MZITO WA BAHARINI(HMS) BARANI AFRIKA KUJENGWA PANGANI,TANGA*

 ▪️Ni cha Kampuni ya Madini ya Shenghe ambacho ujenzi wake umeanza ▪️Madin ya mchanga mzito kutoka nchi mbalimbali Afrika kuchakatwa Pangani,Tanga ▪️Waziri Mavunde apongeza hatua ya kuifanya Tanzania kitovu cha uongezaji thamani madini Afrika ▪️Awataka wawekezaji kukamilisha ujenzi wa kiwanda mapema ▪️Rais Samia apongezwa kwa mazingira rafiki ya uwekezaji Chengdu,China Kampuni ya Shenghe Resources ya China imeanza ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kuchakata madini madini ya mchanga mzito wa baharini (𝙃𝙚𝙖𝙫𝙮 𝙈𝙞𝙣𝙚𝙧𝙖𝙡 𝙎𝙖𝙣𝙙𝙨) katika eneo la Tajiri,Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga ambapo kampuni hii inatekeleza mradi mkubwa wa uchimbaji wa madini tembo. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Shenghe Ndg. Xie Bing wakati wa ziara ya Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde kutembelea na kujionea shughuli mbalimbali za uongezaji thamani madini zinazofanywa kampuni hiyo. Akizungumza katika ziara hiyo Ndg. Bing amesema kwa Bara la Afrika wana miradi ya madin...

PSPTB YATOA SIKU 30 KWA WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI KULIPA ADA YA MWAKA

 BODI ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imewapa siku 30 wataalamu wote waliosajiliwa ambao wana madeni ya ada ya mwaka kuhakikisha wanalipa, ikionya kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo wanaweza kufutiwa usajili na kuchukuliwa hatua za kisheria. Agizo hilo limetolewa leo Septemba 14, 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB, Godfred Mbanyi wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ulipaji wa ada ya mwaka ya wanachama wa Bodi hiyo. Amesema ulipaji wa ada ya mwaka ni wajibu wa kisheria kwa kila mtaalamu aliyesajiliwa na PSPTB, kwa mujibu wa Sheria ya PSPTB, Sura ya 179 ya Sheria za Tanzania, pamoja na kanuni zinazosimamia taaluma hiyo. Mbanyi amesema kuwa mtaalamu anayeshindwa kulipa ada kwa kipindi cha miezi 24 mfululizo atachukuliwa kuwa amepoteza hadhi ya usajili na jina lake linaweza kuondolewa katika daftari rasmi la wataalamu waliosajiliwa na Bodi. Bodi pia imeonya kuwa mtu ambaye ataendelea kufanya kazi, kujitambulisha au kujihusisha na taaluma ya ununuzi na uga...

MWANAFA ANOGESHA 'AWESO CUP' PANGANI, AAHIDI SKAUTI KUSAKA VIPAJI

 * Ampongeza Aweso kwa kuandaa timu 80, ashangaa kuizidi Ligi Kuu. *Na Mashaka Mhando, Pangani NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu 'MwanaFA', amekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mashindano makubwa ya soka ya 'Aweso Cup' yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Sakura, wilayani Pangani. Akizindua mashindano hayo kwa kupiga penalti ya kifundi, MwanaFA alimmwagia sifa Mbunge wa Pangani ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, kwa kuwekeza kwenye michezo na kufanikiwa kukusanya timu takribani 80 kutoka kata 14 za jimbo hilo. "Hongera Mheshimiwa, timu 80 siyo mchezo! Umeishinda hata Ligi Kuu yetu yenye timu 16 tu. Hili ulilolifanya si jambo dogo," alisema MwanaFA kwa mshangao. MwanaFA alibainisha kuwa Serikali imeweka mpango madhubuti wa kuhakikisha kila yanapofanyika mashindano ya mpira wa miguu, haijalishi yana udogo gani, inapeleka skauti kutoka Shirikisho la Soka Nchini (TFF) kusaka vipaji ili kuvilea kama inavyofanya kwa timu za...