Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MIKOPO YA TADB INAVYOCHOCHEA MAPINDUZI YA KILIMO NA UKUAJI WA UCHUMI

*Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO* Sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania. Inatoa ajira kwa mamilioni ya Watanzania, inachangia usalama wa chakula na ni chanzo kikuu cha malighafi kwa viwanda. Hata hivyo, kwa miaka mingi sekta hii ilikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mitaji, hali iliyowafanya wakulima wengi kuendelea na kilimo cha kujikimu badala ya kilimo cha biashara. Katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita , hali hiyo imeanza kubadilika kufuatia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Kupitia ongezeko la mtaji na upanuzi wa utoaji wa mikopo, benki hiyo imekuwa nyenzo muhimu ya kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa. Serikali imeendelea kuiongezea mtaji TADB ili iweze kuwafikia wakulima wengi zaidi kwa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo kuu ni kuongeza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula, kupunguza umaskini na kukuza kilimo cha kisasa kinachozalisha kwa tija. Mwa...
Recent posts

WAZIRI MAVUNDE AAGIZA MASOKO YA MADINI KUWA WAZI MPAKA USIKU

 ▪️ Lengo ni kurahisisha huduma kwa wateja *▪️ Kamati ya Bunge yaishauri Serikali kupunguza tozo zinazowaumiza wachimbaji wadogo *▪️ Dhahabu tani 67.8 zenye thamani ya Sh trilioni 18.4 zazalishwa kwenye viwanda vya usafishaji ▪️Waziri Mavunde aeleza mkakati wa kukuza biashara ya Tanzanite DODOMA. Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameiagiza Tume ya Madini kuongeza muda wa uendeshaji wa masoko ya madini mpaka saa 3:00 usiku, hatua inayolenga kuongeza fursa za biashara na kuwahudumia wafanyabiashara na wauzaji wa madini kwa muda mrefu zaidi ili kuendana na mahitaji ya wadau na kuongeza ufanisi katika biashara ya madini. Mavunde ametoa agizo hilo Agosti 11, 2026, wakati akijibu maswali ya Wabunge katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini jijini Dodoma, ambapo Wizara imewasilisha taarifa kuhusu hali halisi na maendeleo ya sekta ya madini nchini. Mavunde amesema Serikali pia inaendelea kuimarisha udhibiti wa biashara ya madini na utoroshaji, huku ikisisitiza u...

NCHIMBI AWASILI ZANZIBAR, KIZIMKAZI FESTIVAL 2026 YAPAMBA MOTO

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili Zanzibar, leo tarehe 11 Agosti 2026. Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Ufunguzi wa Jengo la Dakhalia katika Skuli ya Sekondari ya Husnuu Makame – Kibuteni Unguja, ikiwa ni shamrashamra ya Tamasha la Kizimkazi. (Kizimkazi Festival 2026)

DKT. SAMIA: UMOJA NA MSHIKAMANO WENU NDIO NGUVU YA CCM

  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewashukuru wanachama wa CCM kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, hatimaye kukiwezesha Chama Cha Mapinduzi kupata ushindi wa kishindo na kuendelea kuongoza dola Tanzania Bara na Zanzibar. Dkt. Samia ameyasema hayo mara baada ya kukaribishwa na kuzungumza na wananchi pamoja na wanachama wa CCM katika Maskani Kaka Kisonge, Zanzibar. Amesema jitihada zinazofanywa na wanachama katika kujenga umoja na mshikamano ndani ya maskani ni miongoni mwa mambo yanayomtia moyo, kwani zinaonesha kuwa wanachama wa CCM wako pamoja na wana dhamira ya kuendelea kukiimarisha chama kwa ajili ya maendeleo endelevu. Aidha, Dkt. Samia amesema Mapinduzi ni urithi walioachiwa na viongozi na wazee waliotangulia, hivyo kuna wajibu kwa kizazi cha sasa kuulinda, kuutunza na kuuendeleza ili uweze kudumu kwa muda mrefu na kuendelea kuwa na tija kwa ...

DKT. SAMIA: UMOJA NA MSHIKAMANO WENU NDIO NGUVU YA CCM

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewashukuru wanachama wa CCM kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, hatimaye kukiwezesha Chama Cha Mapinduzi kupata ushindi wa kishindo na kuendelea kuongoza dola Tanzania Bara na Zanzibar. Dkt. Samia ameyasema hayo mara baada ya kukaribishwa na kuzungumza na wananchi pamoja na wanachama wa CCM katika Maskani Kaka Kisonge, Zanzibar. Amesema jitihada zinazofanywa na wanachama katika kujenga umoja na mshikamano ndani ya maskani ni miongoni mwa mambo yanayomtia moyo, kwani zinaonesha kuwa wanachama wa CCM wako pamoja na wana dhamira ya kuendelea kukiimarisha chama kwa ajili ya maendeleo endelevu. Aidha, Dkt. Samia amesema Mapinduzi ni urithi walioachiwa na viongozi na wazee waliotangulia, hivyo kuna wajibu kwa kizazi cha sasa kuulinda, kuutunza na kuuendeleza ili uweze kudumu kwa muda mrefu na kuendelea kuwa na tija kwa vizazi...