Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MAKAMU WA RAIS AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUMUOMBEA RAIS SAMIA ILI AWEZE KUTEKELEZA MAJUKUMU VEMA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasalimu Wananchi wa Mbuyuni, Wilayani Moshi waliokusanyika kumlaki akiwa katika ziara binafsi mkoani Kilimanjaro leo tarehe 01 Septemba 2026. Akiwasalimu wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Amesema kwa imani ya maombi ataweza kumsaidia kwa hekima na utii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Makamu wa Rais amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi. Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema: “Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,” kauli ambayo aliitoa pia mkoani Dodoma, kwa wananchi wa Chamwino, mara baada ya kuapishwa. Awali, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo alipokelewa na v...
Recent posts

MAVUNDE, BALOZI WA UINGEREZA WAZUNGUMZIA FURSA ZA UWEKEZAJI MADINI

 Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde, amekutana na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mheshimiwa Marianne Young, jijini Dodoma, ambapo wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya madini na kuongeza fursa za uwekezaji kati ya Tanzania na Uingereza. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamejadili kwa kina maeneo ya uwekezaji katika sekta ya madini, uongezaji wa thamani ya madini nchini, pamoja na namna ya kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuwa chachu ya ukuaji wa uchumi jumuishi na wenye manufaa kwa wananchi. Mkutano huo pia umeangazia umuhimu wa kuendeleza mazingira yatakayowezesha ushirikiano na uwekezaji wenye tija katika sekta ya madini, huku Tanzania ikiendelea kutumia rasilimali zake za madini kama fursa ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi. Tanzania na Uingereza zimeeleza dhamira ya kuendelea kushirikiana katika maeneo yenye manufaa kwa pande zote mbili, kwa lengo la kuimarisha mahusiano ya nchi hizo na kukuza ustawi na maendeleo ya wananchi wa ma...

TMA YATOA ANGALIZO, WANANCHI WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI MWELEKEO WA MVUA ZA VULI

 Na Mwanamkuu Mwandoro,Tanga.  Wananchi mkoani Tanga wametakiwa kuchukua tahadhari kubwa kufuatia mvua zinazotarajiwa kunyesha na kutopuuzia utabiri wa hali ya hewa kwani kuna uwezekano wa kunyesha kwa mvua kubwa katika msimu ujao wa mvua, huku kukiwa na dalili za kuwepo kwa hali ya hewa ya El Niño. Angalizo hilo limetolewa na Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa mkoa wa Tanga Kurwa Mbwambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo alizitaka pia kamati za maafa kuzingatia taarifa za hali ya hewa na kuchukua tahadhari mapema. Aidha Mbwambo aliongeza kuwa viashiria vya hali ya hewa vinaonesha uwepo wa hali ya El Niño ambayo inaweza kuathiri mwendo wa mvua katika maeneo mbalimbali nchini na kwamba utabiri wa sasa unaonesha kuwepo kwa mvua za vipindi vifupi,na huku mvua za vuli zikitarajiwa kuanza kunyesha katika juma la kwanza/pili la mwezi oktoba 2026 hadi Januari 2027. “Wananchi wasipuuze taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa sababu zinatolewa ili kuwaweze...

STANDI YA MABASI RASMI KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA 8.

 Na Mwanamkuu Mwandoro,Tanga  Serikali mkoani Tanga imetoa agizo Kwa wamiliki wote wa Mabasi yanayosafirisha abiria kwenda nje ya mkoa,nchi jirani na maeneo mbalimbali ya nchi kuhakikisha kuwa ifikapo September 8,2026 Magari yote yanaanza na kumaliza safari zake katika kituo kikuu cha Mabasi kilichopo Kange. Agizo hilo linatokana na maadhimio yaliyotolewa na ofisi ya Waziri mkuu, Kamati ya Bunge inayoshughulika na Ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 'TAMISEMI' pamoja na wamiliki na wadau wa usafirishaji kwa lengo la kuhakikisha huduma ya usafirishaji inaimarika pamoja na kuchangia maendeleo ya mkoa huo hususani kwa Halmashauri ya jiji la Tanga kupitia kituo hicho ambacho kinatarajia kuwa kitovu cha uchumi. Akizungumza katika kikao cha pamoja na wadau wa usafirishaji wakiwemo wamiliki wa Mabasi Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani amesema kuwa utekelezaji wa agizo hilo umezingatia utekelezaji wa Sheria ndogo ya Halmashauri 'by laws' ya mwa...

SHABIBY AWAKABIDHI VIJANA PIKIPIKI 370, ATOA WITO WA UAMINIFU NA BIDII

 Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby, amekabidhi pikipiki 370 kwa vijana wa Jimbo la Gairo kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kujenga vyanzo vyao vya kipato. Akizungumza katika hafla ya kiwakabidhi pikipiki hizo 370, Mbunge huyo wa Jimbo la Gairo Shabiby amesema pikipiki hizo zimetolewa kwa kuzingatia zaidi vijana wenye uhitaji na wasio na uwezo wa kuanzia, akisisitiza kuwa umaskini ni miongoni mwa vigezo vilivyozingatiwa katika kuwafikia wanufaika. Amesema mpango huo utaendelea, ambapo kila mwisho wa mwezi vikundi vitano vitapatiwa pikipiki 50 kwa mfumo wa mkopo, huku akieleza kuwa mpango huo unalenga kuwafikia vijana wengi zaidi ndani na nje ya Gairo. Shabiby amewataka vijana waliopatiwa pikipiki hizo kuzitumia kwa uangalifu, kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanarejesha mikopo kwa wakati, akisema uaminifu wao ndio utakaowezesha vijana wengine kupata fursa hiyo. “Ninyi mliochukua pikipiki si kwamba ndiyo mwisho kupata pikipiki. Ninyi sasa ni mabalozi wazuri. Mtakapoli...

MOI YAZIDI KUBORESHA UPASUAJI KWA TEKNOLOJIA ZA KISASA

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, amesema taasisi hiyo imeendelea kutumia teknolojia za kisasa na akili unde katika kuboresha huduma za upasuaji, uchunguzi na matibabu kwa wagonjwa. Akizungumza leo, Septemba 1, 2026, Dkt. Ulisubisya amesema MOI inatumia teknolojia inayochakata taarifa za mgonjwa na kutengeneza ramani maalum inayomwongoza daktari wakati wa upasuaji, hivyo kumwezesha kufika kwa usahihi katika eneo lenye tatizo na kupunguza hatari wakati wa matibabu. Amesema teknolojia hiyo pia imeanza kutumika katika uchukuaji wa sampuli za uvimbe kwa ajili ya uchunguzi wa maabara, ambapo vifaa vidogo humsaidia daktari kufikia eneo lenye tatizo na kuchukua sampuli bila kulazimika kufanya upasuaji mkubwa kama ilivyokuwa awali. Kwa mujibu wa Dkt. Ulisubisya, matumizi ya teknolojia hiyo yamewezesha kupunguza ukubwa wa afua, muda wa mgonjwa kukaa hospitalini na kuongeza ufanisi wa huduma za uchunguzi na matibab...