Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MWANAFA ANOGESHA 'AWESO CUP' PANGANI, AAHIDI SKAUTI KUSAKA VIPAJI

 * Ampongeza Aweso kwa kuandaa timu 80, ashangaa kuizidi Ligi Kuu. *Na Mashaka Mhando, Pangani NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu 'MwanaFA', amekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mashindano makubwa ya soka ya 'Aweso Cup' yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Sakura, wilayani Pangani. Akizindua mashindano hayo kwa kupiga penalti ya kifundi, MwanaFA alimmwagia sifa Mbunge wa Pangani ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, kwa kuwekeza kwenye michezo na kufanikiwa kukusanya timu takribani 80 kutoka kata 14 za jimbo hilo. "Hongera Mheshimiwa, timu 80 siyo mchezo! Umeishinda hata Ligi Kuu yetu yenye timu 16 tu. Hili ulilolifanya si jambo dogo," alisema MwanaFA kwa mshangao. MwanaFA alibainisha kuwa Serikali imeweka mpango madhubuti wa kuhakikisha kila yanapofanyika mashindano ya mpira wa miguu, haijalishi yana udogo gani, inapeleka skauti kutoka Shirikisho la Soka Nchini (TFF) kusaka vipaji ili kuvilea kama inavyofanya kwa timu za...
Recent posts

KIONGOZI MWENGE WA UHURU AIPONGEZA ALLIANCE ONE KWA KUPANDA MITI KWA GHARAMA YA SH.BILIONI 1.2 WILAYANI BUHIGWE

 Na Mwandishi Wetu,Kigoma Kampuni ya tumbaku ya Alliance One Tanzania Tobacco Limited imepongezwa kwa kutoa mchango mkubwa katika kuhifadhi mazingira mkoani Kigoma kupitia katika miradi ya kurejesha uoto wa miti katika maeneo yaliyoathiriwa na shughuli za binadamu na mabadiliko ya tabia nchi. Pongezi hizo zimetolewa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2026 Bw.Wazo Mwang’onda, baada ya kukagua mradi wa shamba la miti katika shule ya sekondari Munagana  linalofadhiliwa na kampuni hiyo kwa kupanda miti ekari 414 ambapo mpaka sasa gharama za uendeshaji kwenye shamba hilo ni Shilingi 1,264,723,200. Bw. Mwang’onda amebainisha kuwa kitendo cha kampuni ya Alliance One kuamua kuwekeza katika upandaji wa miti ni cha kizalendo na chenye nia ya kuunga mkono juhudi za serikali katika kuhifadhi mazingira na kukuza Uchumi wa wananchi kupitia kilimo cha tumbaku na miti. Mwang’onda ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa Alliance One kuendelea kutoa usaidizi wa ujuzi kwa halmshauri za wi...

TANZANIA NA DRC CONGO WAFUNGUA UKURASA MPYA WA USHIRIKIANO KWENYE MADINI*

▪️Waziri Mavunde na Waziri Kabamba wakubaliana msingi wa ushirikiano, ▪️Ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia na Rais Tshisekedi ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili, ▪️Ushirikiano walenga kurahisisha usafirishaji na biashara ya madini, ▪️Wakubaliana kuweka mikakati ya pamoja kuimarisha ufuatiliaji wa uzalishaji wa madini (traceability), *TIANJIN, CHINA* Pembezoni mwa Mkutano wa Madini wa China uliofanyika Jijini Tianjin, Waziri wa Madini *Mhe. Anthony Mavunde* amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), *Mheshimiwa Louis Watum Kabamba* yaliyolenga kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano kwenye sekta ya madini. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika tarehe 11 Septemba, 2026 Waziri Mavunde na mwenzake Mhe. Kabamba walijadiliana kwa kina namna ya kuendeleza sekta ya madini baina ya Nchi zao na hatimaye kuweka msingi ambao utakuwa ni mwanzo wa kuimarisha ushirikiano utakaoleta tija kwa pande zote mbili. "Leo tumekutana hapa si kwa...

KAMPUNI YA BIMA BUMACO YAWAFIKIA WANANCHI WA TANGA

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Kampuni ya bima ya BUMACO imewataka wateja wake kuhakikisha wanauhisha bima zao mara tu zinapoisha muda wake ili kuweza kupata msaada wa haraka pale wanapopata changamoto. Wito huo umetolewa na Afisa Masoko wa kampuni hiyo Mkoa wa Tanga Hosea Urasa wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo amesema kuwa changamoto inaweza kutokea wakati wowote ule hivyo ni vyema wadau wao ikiwemo wamiliki wa vyombo vya moto na nyumba wakawa tayari muda wote. Urasa amesema kwasasa mwitiko ni mkubwa Kwa wakazi wa Tanga tofauti na awali katika kukata bima na hii imechagizwa na elimu wanayoitoa kwa jamii juu ya umuhimu wa kuwa na bima na hasa ukataji wa bima za moto. "Watu wa Tanga ni waelewa wanachohitji ni kupatiwa elimu tu,hata baada ya lile janga la moto lililotokea stendi ya daladala baada ya kutoa elimu muitikio umeongezeka zaidi," alisema urasa Aidha Urasa ameongeza kuwa BUMACO wanatoa bima za maisha,mali, vyombo vya moto (magari,piki...

WATOTO WAINUA SAUTI: “VIBOKO SHULENI, NDOA ZA UTOTONI VIKOME”

WATOTO nchini wametaka Serikali kuimarisha utekelezaji wa sheria na sera zinazolinda haki zao, wakisisitiza kukomeshwa kwa vitendo vya ukatili ikiwemo kupigwa viboko shuleni na ndoa za utotoni, wakieleza kuwa hali hizo zinaweza kuathiri elimu, ustawi na mustakabali wao. Kauli hiyo imetolewa leo Septemba 11, 2026, na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Watoto, Daniel Magembe, kwa niaba ya watoto nchini, katika kikao kilichowakutanisha wadau mbalimbali wanaojihusisha na masuala ya watoto. Magembe amesema pamoja na kuwepo kwa taratibu zinazodhibiti matumizi ya viboko shuleni, bado baadhi ya walimu wanaendelea kutumia adhabu hiyo kwa kiwango kikubwa, wakiamini kuwa ndiyo njia sahihi ya kurekebisha tabia za wanafunzi. Amesema matumizi ya viboko yanaweza kuwafanya baadhi ya wanafunzi kuishi kwa hofu, kupoteza kujiamini na kushindwa kushiriki kikamilifu katika masomo, hivyo Serikali na wadau wanapaswa kutafuta njia mbadala za kujenga nidhamu bila kumuweka mtoto katika mazingira ya ukatili. “Tuna...

WILAYA YA MUSOMA YAVUKA LENGO WATOTO 222,076 WAPATIWA CHANJO YA POLIO.

 Na Mwandishi wetu Jovina Massano Musoma  Mwitikio mzuri wa wazazi na walezi kwa kushiriki na kuhakikisha watoto wanapata chanjo ya Polio yapaisha lengo watoto 222,076 Wilaya ya Musoma mkoani Mara wafikiwa. Wilaya mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amewapongeza wazazi na walezi kwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la utoaji Chanjo kwa watoto. Amesema katika halmashauri ya Manispaa ya Musoma idadi tarajiwa ilikuwa ni Walengwa 66,176 kutokana na mwitikio mkubwa imepelekea waliopata chanjo hiyo kufikia 77,104 sawa na 120% huku halmashauri ya Musoma Vijijini walengwa walikuwa ni 118,760 na kufikia waliochanjwa 144,972 sawa na 157%. Nae Mratibu wa Halmashauri ya Musoma DC Joseph Chacha amesema zoezi hilo limefanyika vizuri kutokana na elimu na hamasa iliyotolewa kwa wakati kwa jamii kupitia wenyeviti wa mitaa,vitongoji na vijiji na makundi mbalimbali ya kijamii. "Ushirikiano katika ngazi zote umeleta matokeo na mwitikio mkubwa kwa jamii na kupata Idadi kubwa ya watoto kupata...