Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

TANESCO: BAADHI YA MIKOA KUKOSA UMEME KWA MUDA KUPISHA UKAMILISHAJI WA MRADI WA 400KV CHALINZE–DODOMA

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limetangaza kuwa baadhi ya mikoa nchini itakumbwa na kukosekana kwa huduma ya umeme kwa muda katika kipindi cha kuanzia Julai 30 hadi Agosti 17, 2026, ili kupisha utekelezaji wa hatua za mwisho za Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma. Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Irene Gowele, amesema mradi huo umefikia asilimia 94 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika rasmi Agosti 21, 2026. Amesema hatua zilizobaki zinahusisha kazi ya kuvuta nyaya za umeme katika maeneo ya Mkambalani mkoani Morogoro na Kikombo mkoani Dodoma, kazi inayohitaji baadhi ya njia za kusafirisha umeme kuzimwa kwa muda ili kuhakikisha usalama wa wafanyakazi, wananchi pamoja na miundombinu ya umeme wakati wa utekelezaji wa mradi huo. "Kazi hizi ni muhimu kwa ajili ya kukamilisha mradi huu wa kimkakati, hivyo kutakuwa na ulazima wa kusitisha huduma ya umeme katika...
Recent posts

SSP SODOKA: VIJANA WAWE MSTARI WA MBELE KULINDA AMANI

  Na Dawati la Habari Polisi Mwanza Jeshi la Polisi Wilaya ya Nyamagana limewataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani na usalama wa jamii kwa kushirikiana kwa karibu na vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na serikali za mitaa katika kuwabaini na kuwafichua wahalifu wanaojificha kwenye maeneo yao. Wito huo umetolewa Julai 26, 2026 na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Nyamagana, SSP Virginia Sodoka, wakati wa fainali za mashindano ya Polisi Jamii Cup zilizofanyika katika Kata ya Mirongo, ambapo Mashi FC ilitwaa ubingwa baada ya kuifunga Mirongo FC mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mirongo. Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi na mashabiki wa soka waliojitokeza kushuhudia fainali hizo, SSP Sodoka alisema vijana ni nguvu kazi ya taifa na nguzo muhimu katika kuhakikisha mfumo wa Polisi Jamii unafanikiwa. "Vijana wana nafasi kubwa ya kuwa walinzi wa amani katika jamii. Mkiamua kushirikiana na Jeshi la Polisi mtasaidia kuzuia uhalifu kabla haujatokea. Lakini pia msipo...

POLISI, TRC WAHAMASISHA WANANCHI KULINDA MIUNDOMBINU YA RELI

Wananchi wa Kata ya Mwabomba, hususan Kijiji cha Mhulula wilayani Kwimba, mkoani Mwanza, wamehimizwa kuwa walinzi wa kwanza wa miundombinu ya reli kwa kutambua kuwa uwekezaji huo ni mali ya Watanzania wote na una mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa. Rai hiyo imetolewa Julai 27, 2026 na Mkuu wa Kituo cha Polisi Reli Mkoa wa Mwanza wakati wa mkutano wa hadhara uliowakutanisha viongozi wa serikali za vijiji na kata, wataalamu kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) pamoja na Jeshi la Polisi. Mkutano huo ulilenga kutoa elimu kuhusu ulinzi wa miundombinu ya reli, usalama wa jamii, kuzuia ukatili wa kijinsia na utatuzi wa migogoro ya ardhi. Akizungumza na wananchi, Mkuu wa Kituo cha Polisi Reli Mkoa wa Mwanza, ASP Jovitha Tibangayuka, alisema ziara hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya jamii na Jeshi la Polisi katika kulinda miundombinu ya reli na rasilimali nyingine za taifa. "Jukumu la kulinda miundombinu ya reli ni la kila mwananchi. Si la Kikosi cha Polisi Reli au Shirika ...

POLISI WANAMAJI WASISITIZA USHIRIKIANO KUZUIA VIFO VYA KUZAMA MAJI

  Na: Dawati la Habari Polisi Mwanza Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza (MPC) kimeshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Kuzuia Kuzama Maji Duniani, ambayo kimkoa yamefanyika katika Ufukwe wa Bismarck Rock, Capri Point jijini humo. ​Akizungumza kwenye maadhimisho hayo, Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza, SSP Abduhaj Mkombe kwa niaba ya Mkuu wa Chuo, amesema chuo hicho ni mdau mkuu katika kuhakikisha kinapunguza vifo vitokanavyo na ajali za majini katika Ziwa Victoria na maeneo mengine nchini. ​"Sisi kama Polisi tuna dhamana ya kusimamia usalama majini na kuhakikisha raia na mali zao wanakuwa salama. Tumeona ipo haja ya kushiriki kwenye tukio hili ili kuonyesha mchango wetu katika kupunguza vifo vinavyotokana na kuzama maji," amesema Mkombe. ​Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Christopher Ngubiagai, amelipongeza Jeshi la Polisi pamoja na vyombo vingine vya usalama kwa kufanya kazi kwa ushirik...

POLISI WANAMAJI WASISITIZA USHIRIKIANO KUZUIA VIFO VYA KUZAMA MAJI

Na: Dawati la Habari Polisi Mwanza Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza (MPC) kimeshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Kuzuia Kuzama Maji Duniani, ambayo kimkoa yamefanyika katika Ufukwe wa Bismarck Rock, Capri Point jijini humo. ​Akizungumza kwenye maadhimisho hayo, Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza, SSP Abduhaj Mkombe kwa niaba ya Mkuu wa Chuo, amesema chuo hicho ni mdau mkuu katika kuhakikisha kinapunguza vifo vitokanavyo na ajali za majini katika Ziwa Victoria na maeneo mengine nchini. ​"Sisi kama Polisi tuna dhamana ya kusimamia usalama majini na kuhakikisha raia na mali zao wanakuwa salama. Tumeona ipo haja ya kushiriki kwenye tukio hili ili kuonyesha mchango wetu katika kupunguza vifo vinavyotokana na kuzama maji," amesema Mkombe. ​Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Christopher Ngubiagai, amelipongeza Jeshi la Polisi pamoja na vyombo vingine vya usalama kwa kufanya kazi kwa ushirikia...