Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MASHINDANO YA UJUZI YA WORLD SKILLS TANZANIA 2026 YAANZA TANGA

Mashindano ya Kitaifa ya Ujuzi ya WorldSkills Tanzania 2026 yameanza leo, Agosti 20, 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea mkoani humo. Mashindano hayo yanawakutanisha jumla ya vijana 46 wenye ujuzi mbalimbali wakionesha uwezo wao katika fani tofauti za ufundi na ubunifu, huku yakilenga kutambua, kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana pamoja na kuwaandaa kushindana katika viwango vya kimataifa.  Tanzania inashiriki mashindano hayo ikiwa ni sehemu ya hatua za kuimarisha mafunzo ya ujuzi na kuwaunganisha vijana na fursa za ajira na kujiajiri, ambapo mashindano hayo yanatarajiwa pia kuwa jukwaa la kuonesha namna ujuzi na ubunifu wa vijana unavyoweza kubadilishwa kuwa bidhaa na huduma zenye thamani, kuongeza uzalishaji wa ndani na kuchangia uchumi wa taifa. ‎Mashindano hayo yanaratibiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kwa kushirikiana na W...
Recent posts

MBUNGE TULIA ATEMBELEA KUKAGUA MIUNDOMBINU YA SHULE YA MSINGI IGANJO

  Agosti 18, 2026. Mbunge wa Jimbo la Uyole na Rais wa IPU Mhe. Dkt. Tulia Ackson ametembelea na kukagua miundombinu ya shule ya msingi Iganjo kata ya Igawilo Jimbo la Uyole na kuangalia hali ya wanafunzi ambapo ametoa ahadi ya kuiomba serikali kuweza kusaidia kuboresha miundombinu ya shule hiyo pamoja na kuongezwa kwa matundu ya vyoo katika shule hiyo. Wakati huohuo Dkt. Tulia ametoa ahadi kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo kuchangia kompyuta, mashine ya kutolea nakala (printer mashine) hivi karibuni ili kuweza kurahisisha shughuli za elimu katika shule hiyo.

DKT. MSEMO: SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KWA WANAWAKE INAONGOZA TANZANIA

MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, amesema saratani ya shingo ya kizazi ndiyo inayoongoza kwa wanawake nchini Tanzania, ikiwa pia miongoni mwa saratani zinazochangia vifo kwa kiwango kikubwa. Dkt. Msemo amesema takribani asilimia 34 ya saratani zinazowapata wanawake nchini ni saratani ya shingo ya kizazi, akisisitiza kuwa hali hiyo inapaswa kuchukuliwa kwa uzito kutokana na ukweli kwamba ugonjwa huo unaweza kuzuilika na kugundulika mapema. Amesema saratani ya shingo ya kizazi inaweza kuzuilika kupitia chanjo, huku uchunguzi wa mara kwa mara ukisaidia kugundua mabadiliko ya awali na kutoa matibabu kabla ugonjwa haujawa mkubwa. “Ni saratani ambayo inaweza kuzuilika kwa chanjo, inaweza kugundulika mapema kupitia uchunguzi na inapogundulika katika hatua za awali, uwezekano wa kupona huwa mkubwa sana,” amesema Dkt. Msemo. Amesema hali hiyo inapaswa kuwa changamoto kwa jamii, kwa kuwa kuna wanawake wanaopoteza maisha kutokana na ugonjwa ambao kwa...

DKT. MSEMO: SARATANI INATIBIKA, HASA INAPOGUNDULIKA MAPEMA

  WANANCHI wametakiwa kujenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara na kutafuta huduma za kitabibu mapema, kwa kuwa saratani inaweza kutibiwa kwa ufanisi zaidi inapogundulika katika hatua za awali. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, wakati akizungumza na waandishi wa habari leo, Agosti 19, 2026, jijini Dodoma, akisisitiza umuhimu wa wananchi kuondokana na dhana potofu kuhusu saratani na kuchukua hatua za mapema katika afya zao. Dkt. Msemo amesema wananchi wanapaswa kufahamu kuwa saratani si ugonjwa usiotibika, hasa pale inapogundulika mapema, huku akiviomba vyombo vya habari kuendelea kushirikiana na ORCI kutoa elimu sahihi kwa umma kuhusu kinga, uchunguzi na matibabu ya saratani. Katika hatua nyingine, Serikali imeongeza uwekezaji mkubwa katika huduma za saratani kupitia ORCI, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza uwezo wa uchunguzi na matibabu, kupunguza muda wa wagonjwa kusubiri huduma na kuimarisha nafasi ya ...

WIKI YA ELIMU YAZINDULIWA TANGA: SERIKALI YAMWAGA TRILIONI 2.8, BUNGE LATAKA BUNIFU ZIZALISHE PESA

Na MASHAKA MHANDO,Tanga Serikali imetangaza dhamira yake thabiti ya kuleta mapinduzi ya elimu ya ujuzi na ubunifu nchini, huku ikibainisha kuwa imetenga kiasi cha Shilingi Trilioni 2.8 kwenye bajeti ya Wizara ya Elimu ili kutekeleza kwa vitendo maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuandaa vijana kwa soko la ajira la ndani na nje ya nchi. Hayo yamebainishwa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, wakati akizindua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika viwanja vya Usagara jijini Tanga, yakishirikisha zaidi ya taasisi na vyuo vikuu 90. Waziri Mkenda amesema mabadiliko makubwa yanayoendelea katika mitaala ikiwemo ujenzi wa shule za sekondari za amali na vyuo vya VETA kila wilaya, ni matokeo ya maelekezo ya Rais Samia ambaye tangu aingie madarakani aliweka mkazo kwenye elimu inayojenga ujuzi. "Hiki mnachokiona kwa vijana wa Tanga Tech ni matokeo ya utekelezaji wa maono ya Rais. Hapo baadaye vizazi vijavyo vi...

SERIKALI KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

Na. Mwandishi Wetu - Shinyanga SERIKALI imesema itaendelea kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU), kwa kuboresha vituo vya huduma, kuwezesha vikundi na kuimarisha ushirikiano na wadau, ili kuhakikisha Tanzania inafikia lengo la kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dk. Jim Yonazi, wakati wa ziara yake mkoani Shinyanga, ambapo alitembelea vikundi mbalimbali vya vijana vinaoishi na Maambukizi ya VVU pamoja na Kituo cha Maarifa Kahama kilichopo Kagongwa mkoani humo. Dk. Yonazi amesema juhudi zinazofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wadau zimeanza kuzaa matunda, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi katika utoaji wa elimu, upimaji, ushauri nasaha, pamoja na huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU. “Lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma karibu nao, lakini vilevile wanapata elimu inayowasaidia katika ma...