Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WILAYA YA MUSOMA YAVUKA LENGO WATOTO 222,076 WAPATIWA CHANJO YA POLIO.

 Na Mwandishi wetu Jovina Massano Musoma  Mwitikio mzuri wa wazazi na walezi kwa kushiriki na kuhakikisha watoto wanapata chanjo ya Polio yapaisha lengo watoto 222,076 Wilaya ya Musoma mkoani Mara wafikiwa. Wilaya mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amewapongeza wazazi na walezi kwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la utoaji Chanjo kwa watoto. Amesema katika halmashauri ya Manispaa ya Musoma idadi tarajiwa ilikuwa ni Walengwa 66,176 kutokana na mwitikio mkubwa imepelekea waliopata chanjo hiyo kufikia 77,104 sawa na 120% huku halmashauri ya Musoma Vijijini walengwa walikuwa ni 118,760 na kufikia waliochanjwa 144,972 sawa na 157%. Nae Mratibu wa Halmashauri ya Musoma DC Joseph Chacha amesema zoezi hilo limefanyika vizuri kutokana na elimu na hamasa iliyotolewa kwa wakati kwa jamii kupitia wenyeviti wa mitaa,vitongoji na vijiji na makundi mbalimbali ya kijamii. "Ushirikiano katika ngazi zote umeleta matokeo na mwitikio mkubwa kwa jamii na kupata Idadi kubwa ya watoto kupata...
Recent posts

CHINA, TANZANIA MINISTERS HOLD TALKS ON MINING MODERNIZATION

By Prosper Makenea The United Republic of Tanzania and the People's Republic of China have agreed to deepen cooperation in the mining sector, with a focus on modernizing operations, expanding geological research, and building local capacity. The agreement was reached today during bilateral talks between Tanzania's Minister of Minerals, Hon. Anthony Mavunde, MP, and China's Deputy Minister of Natural Resources, Hon. Dr. Xu Dachun, held at the Government Conference Center in Tianjin. Speaking after the meeting, Hon. Mavunde said the two governments will work together to apply modern mining technology and improve systems for the issuance and management of mineral licenses. He noted that China, through the China Geological Survey, has committed to build the capacity of Tanzanian professionals in geology and in the interpretation of mineral exploration data. "The vision of our President, Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, is to see the mining sector grow and make a gre...

KATIBU TAWALA MKOA WA MARA AONGOZA HAFLA YA KUMPONGEZA MKUU WA MKOA BRIGEDIA JENERALI EVANS MTAMBI.

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Kusaya, leo tarehe 11,septemba 2026, ameongoza hafla ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Brigedia Jenerali Evans Alfred Mtambi, kufuatia kupandishwa cheo chake cha kijeshi kutoka Kanali hadi Brigedia Jenerali. Hafla hiyo imefanyika katika viunga vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali, watumishi wa umma, viongozi wa dini pamoja na wadau wengine wa mkoa. Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Kusaya, ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara na kuwaamini viongozi wenye uwezo na uadilifu. Amesema kupandishwa cheo kwa Mkuu wa Mkoa ni ishara ya kutambua weledi, uhodari, utii na utumishi wake uliotukuka katika kulitumikia taifa. “Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara. Kupandishwa cheo kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ni heshima kubw...

TANZANIA, MISRI ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KATIKA ULINZI NA TEKNOLOJIA ZA ANGA

 Tanzania na Misri zimejadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika sekta ya ulinzi na teknolojia za anga, ikiwemo kubadilishana uzoefu, maarifa na teknolojia kwa manufaa ya pande zote. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji wa Kijeshi na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Luteni Jenerali Ashraf Salem Zaher, jijini El Alamein, Misri. Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 10, Septemba 2026, wakati Tanzania ikishiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Anga na Teknolojia za Anga za Juu ya El Alamein (ELIAS). Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamejadili fursa za kuendeleza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Misri katika maeneo ya ulinzi na teknolojia za anga, pamoja na umuhimu wa kubadilishana uzoefu, maarifa na teknolojia katika maeneo yenye maslahi ya pamoja. Ushiriki wa Tanzania katika Maonesho ya ELIAS unalenga pia kujenga na kuimarisha mahusi...

WAZIRI WA ULINZI NA JKT ZIARANI MISRI, AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA ULINZI NA AMIRI JESHI MKUU WA MISRI

 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 10 Septemba 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji wa Kijeshi na Amiri  Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mheshimiwa Luteni Jenerali Ashraf Salem Zaher, jijini El Alamein, Misri. Mazungumzo hayo ya viongozi hao waandamizi yalilenga kujadili na kuimarisha maeneo mbalimbali ya ushirikiano baina ya Wizara za Ulinzi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, ambazo ni nchi rafiki zenye uhusiano wa muda mrefu na wa kihistoria. Aidha, viongozi hao walijadili masuala mbalimbali ya kiulinzi na usalama, pamoja na utekelezaji wa mambo yaliyojadiliwa wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mheshimiwa Abdel Fattah el-Sisi, nchini Tanzania mnamo  Julai 18, 2026, ambapo alifanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mazungumzo hayo yalisisitiza umuhi...

WAITARA:JKT NI MUHIMU KUWAANDA VIJANA KUKABILIANA NA MAISHA

  Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini na mzazi wa mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mwita Waitara, amelipongeza Jeshi hilo kwa kuendelea kuwajenga vijana katika misingi ya uzalendo, nidhamu, uwajibikaji na kujitegemea, akisema mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa katika kuwaandaa vijana kukabiliana na changamoto za maisha. Waitara ameyasema hayo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, Operesheni Linda Amani na vijana waliojitolea, iliyofanyika katika Kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mlandizi, mkoani Pwani, ambapo amesema vijana wanaomaliza mafunzo hayo wanapaswa kutumia ipasavyo maarifa na stadi walizopata ili kujiajiri, kushiriki katika shughuli za maendeleo na kuwa raia wema wenye mchango kwa Taifa. Aidha, Waitara amehimiza matumizi sahihi ya teknolojia ya Akili Bandia (AI) katika kuwaandaa vijana kwa mazingira ya sasa, akisema teknolojia hiyo inaweza kutumika kuwaongezea maarifa na stadi mbalimbali zitakazowasaidia kukabiliana na mahit...