Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao Cha Kamati Kuu ya Halamshauri Kuu ya CCM Taifa tarehe 29 Julai 2026 Zanzibar
MBUNGE wa Jimbo la Serengeti, Mhe. Mary Daniel Surati (MB), amepata heshima kubwa baada ya kuchaguliwa kuwa miongoni mwa washiriki 40 wa kundi la kwanza la waanzilishi (Founding Fellows) wa programu ya African Academy for Women in Political Leadership, inayotekelezwa kupitia African School of Governance (ASG). Uteuzi huo umefanyika baada ya mchakato wa ushindani uliowashirikisha waombaji 1,334 kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, jambo linaloonyesha kiwango cha juu cha ushindani na ubora wa washiriki waliochaguliwa kujiunga na programu hiyo ya kimataifa inayolenga kuwaandaa wanawake viongozi wa kizazi kipya barani Afrika. Akizungumzia mafanikio hayo, Mhe. Surati amesema anajivunia kuwa sehemu ya kundi la kwanza la waanzilishi wa programu hiyo, akieleza kuwa ni fursa muhimu ya kujifunza, kukuza uwezo wake wa uongozi na kujenga mtandao wa ushirikiano na wanawake viongozi kutoka nchi mbalimbali za Afrika. Amesema mafunzo hayo yatamwezesha kupata maarifa mapya kuhusu uongozi wa kisias...