MWaziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema Mkoa wa Mbeya na kwa ujumla Nyanda za Juu Kusini una uwezo mkubwa wa kuongeza mchango wake katika uchumi wa Tanzania, akisisitiza umuhimu wa kuongeza uzalishaji, kuchakata mazao na kuimarisha uwekezaji katika viwanda. Mhe. Balozi Omar ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja mkoani Mbeya, ambapo alitembelea Ofisi za Mkoa za Chama cha Mapinduzi (CCM), jijini Mbeya. Amesema Nyanda za Juu Kusini zinachukua takribani asilimia 20 ya eneo lote la Tanzania, lakini mchango wake katika Pato la Taifa bado haujaakisi kikamilifu ukubwa wa eneo hilo na utajiri wa fursa zilizopo. Amesema hali hiyo inatoa nafasi kwa Serikali, sekta binafsi na wadau wengine kuongeza uwekezaji katika kilimo, madini, viwanda na sekta nyingine za uzalishaji ili kuongeza tija na mapato ya wananchi pamoja na Taifa kwa ujumla. “Bado tuna fursa kubwa sana ya kuimarisha mchango wetu katika pato la Taifa uendane na eneo tulilonalo, na si kwa s...
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha-Rose Migiro, amefungua rasmi Tawi la CCM Kibuteni, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja, leo tarehe 12 Agosti 2026. Tawi hili lina historia kubwa tangu nyakati za ASP na TANU, na ni jambo la kujivunia kuona sasa lina sura mpya inayokwenda sambamba na mahitaji na hadhi ya Chama. Dkt. Migiro amewahimiza viongozi na wanachama kuhakikisha Tawi hilo linakuwa kituo cha uhai wa Chama, mshikamano, mafunzo, vikao na utekelezaji wa shughuli za Chama. Pia, Katibu Mkuu amewashukuru wana-CCM wa Kibuteni kwa mapokezi mazuri, upendo na zawadi.