Na Angela Sebastian, Ngara Baadhi ya wakazi wa Kata ya Ngara mjini, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, wameeleza kuwa ujenzi wa barabara ya Magereza–Kabalenzi kwa kiwango cha lami utarahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao kwenda sokoni, hatua wanayoamini itachochea shughuli za kiuchumi na kuongeza kipato cha wananchi pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa. Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 0.55 imejengwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Ngara kwa gharama ya zaidi ya Shilingi milioni 316. Mbali na kuboresha mandhari ya mji, wananchi wameitaja kuwa ni fursa muhimu ya kurahisisha usafirishaji wa bidhaa, ikiwemo mazao yanayopelekwa katika nchi jirani ya Burundi hivyo kuongeza mzunguko wa biashara katika eneo hilo. Meneja wa TARURA Wilaya ya Ngara, Mhandisi Mokoro Magori, akisoma taarifa ya mradi huo kwa kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa 2026a amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Oktoba 2024 na unalenga kuboresha miundombinu ya barabara pamoj...
NA: DK. REUBENI LUMBAGALA Malazi, chakula na mavazi ni mahitaji ya msingi ya binadamu. Mwanadamu anapoyapata mahitaji haya kwa ukamilifu wake, hujenga utulivu wa akili, moyo na ari ya kufanya kazi kwa bidii. Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini kinatekeleza mpango mkakati wake wa kuhakikisha watumishi wa Chama wanajengewa makazi ya kudumu kwani makazi ni hitaji la msingi la binadamu. Kupatikana kwa makazi hayo, kunachochea uwajibikaji na uchapakazi wa watumishi hao, ambao wapo nchi nzima kwa madhumuni ya kuwatumikia wananchi. CCM mkoani Tanga, chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Rajab Abdallah, maarufu "Ustadhi Rajab," ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MCC), umedhamiria kuhakikisha ujenzi wa nyumba 36 unakamilika kwa wakati katika wilaya zote tisa za mkoa wa Tanga. Kila wilaya zitajengwa nyumba nne za makatibu wa Chama wilaya, na za makatibu wa jumuiya ya vijana, wanawake na wazazi. Jumla ya gharama za nyumba zote 36 ni shilingi bilioni 2.5....