Musoma. Serikali mkoani Mara imiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuanzisha Mamlaka ya Uhifadhi wa ziwa Victoria hatua ambayo itasaidia uhifadhi na uendelevu wa ziwa hilo ambalo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa mkoa na watu wake. Ombi hilo limetolewa mjii Musoma leo Jumanne Agosti 11 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Bashiru Ally ambaye yupo mkoani Mara kwa ziara ya siku nne. Kanali Mtambi amesema kutokana na shughuli za kiuchumi na kijamii zinazofanywa ndani ya ziwa hilo ipo haja ya kuwa na mamlaka maalumu itakayokuwa inasimamia ziwa hilo ili shughuli hizo ziweze kufanyika kwa ufanisi na kuleta tija zaidi bila kuathiri uhai wake. Ametolea mfano suala la ufugaji wa vizimba ambalo limepata mapokeo makubwa mkoani Mara baada ya Serikali kuanza kuwezesha wavuvi ambapo amesema vijana wengi hivi sasa wameamua kujiajiri kupitia ufugaji huo ndani ya ziwa hilo hivyo ipo haja ya kuwa na mamlaka rasmi itakayosimamia rasilimali hiyo muhimu. "Kuhus...
NA: MWANDISHI WETU Kodi ni chanzo muhimu cha mapato kinachoiwezesha serikali kufanikisha mipango na mikakati yake ya kimaendeleo kwa wananchi wake. Wananchi wanahitaji huduma nzuri za kijamii kama elimu, afya, maji, umeme, barabara na masoko. Aidha, wanahitaji pia kuwezeshwa kiuchumi kwa kupatiwa mikopo nafuu ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha shughuli za kibiashara na za kiujasiriamali. Ni kwamba, mambo haya mazuri na mengine mengi, hayawezi kufanikiwa endapo serikali haitakuwa na fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wao. Hapa ndipo umuhimu wa ulipaji kodi unapoonekana. Kimsingi, pamoja na umuhimu wa ulipaji kodi kwa maendeleo, walipakodi wanazo changamoto ambazo wanahitaji kuziwasilisha serikalini kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili ziweze kufanyiwa kazi. Iko hivi: Ulipaji kodi unahusisha wadau wawili yaani TRA na walipakodi. Kutokana na hili, haitawezekana ulipaji kodi ukawa na ufanisi endapo walipakodi hawatatatuliwa changamoto...