Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

UGANDA KUHAMISHA WIZARA NA TAASISI ZA SERIKALI KUTOKA KAMPALA

  KAMPALA, Uganda   Serikali ya Uganda imepanga kuanza kuhamisha kwa awamu wizara, idara na taasisi zake kutoka Kampala kwenda Nakasongola , katika mpango wa muda mrefu ambao unaweza kuendelea hadi mwaka 2040 . Mpango huo umetangazwa na Waziri wa Nchi wa Maendeleo ya Miji, Margaret Muhanga , mbele ya Kamati ya Ardhi na Nyumba ya Bunge la Uganda. Muhanga amesema Rais Yoweri Museveni anaunga mkono mpango huo, ambao Serikali inautazama kama sehemu ya utekelezaji wa maono ya maendeleo ya Uganda kuelekea mwaka 2040. KAMPALA YAWA CHANGAMOTO Serikali imesema msongamano mkubwa wa magari na changamoto za upangaji wa mji zimefanya Kampala kuwa na mazingira magumu kwa watu kuishi na kufanya kazi. Muhanga amesema Uganda inapoteza takribani dola bilioni 1.6 kwa mwaka kutokana na foleni za magari, huku baadhi ya wakazi wakilazimika kuamka saa 10 alfajiri (4:00 asubuhi) ili waweze kufika kazini saa 2 asubuhi (8:00) . “Kampala haiwezi kuishiwa, haiwezi kubadilishwa, haiwezi kuendelez...
Recent posts

MBUNGE NSEKELA AHAIDI KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI KIMULI

   Na Angela Sebastian ;Kyerwa Mbunge wa Kyerwa, Khalid Nsekela, ameahidi kushirikiana na Halmashauri pamoja na wadau wa elimu kutatua changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama katika Shule ya Sekondari Kimuli, ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda mwingi kujisomea badala ya kutembea hadi saa nne kufuata maji. Ahadi hiyo imekuja wakati wa afla ya utoaji tuzo kwa walimu na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kidato cha sita 2026, licha ya shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma, ambapo katika matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2026 ilishika nafasi ya kwanza wilayani,ya kwanza kwa shule za Serikali kimkoa na ya pili kimkoa kwa shule zote. Kimuli inakabiliwa pia na changamoto ya ukosefu wa ofisi za walimu na mabweni, hali inayowalazimu baadhi ya wanafunzi kulala katika vyumba vya madarasa visivyo na madirisha lakini wanafanya vizuri katika masomo yao. Kwa niaba ya Mbunge, Nekmia Nguma Katibu wa Mbunge-Kitengo cha Mahusiano, amesema Nsekela amewapongeza wanafunzi na...

MBUNGE NSEKELA AHAIDI KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI KIMULI

 Na Angela Sebastian ;Kyerwa Mbunge wa Kyerwa, Khalid Nsekela, ameahidi kushirikiana na Halmashauri pamoja na wadau wa elimu kutatua changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama katika Shule ya Sekondari Kimuli, ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda mwingi kujisomea badala ya kutembea hadi saa nne kufuata maji. Ahadi hiyo imekuja wakati wa afla ya utoaji tuzo kwa walimu na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kidato cha sita 2026, licha ya shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma, ambapo katika matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2026 ilishika nafasi ya kwanza wilayani,ya kwanza kwa shule za Serikali kimkoa na ya pili kimkoa kwa shule zote. Kimuli inakabiliwa pia na changamoto ya ukosefu wa ofisi za walimu na mabweni, hali inayowalazimu baadhi ya wanafunzi kulala katika vyumba vya madarasa visivyo na madirisha lakini wanafanya vizuri katika masomo yao. Kwa niaba ya Mbunge, Nekmia Nguma Katibu wa Mbunge-Kitengo cha Mahusiano, amesema Nsekela amewapongeza wanafun...

NAIBU WAZIRI MAKAMBA AITAKA PBPA KUENDELEA KUTOA ELIMU KWA UMMA

 Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb.), ameitaka Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuendelea kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma ili wananchi wawe na uelewa mpana kuhusu majukumu ya Wakala na mchango wake katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini. Mhe. Makamba ametoa wito huo alipotembelea banda la PBPA katika maonesho yanayofanyika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya Tamasha la Kizimkazi 2026. Amesema ni muhimu wananchi wakaendelea kuelimishwa kuhusu Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja na namna PBPA inavyotekeleza majukumu yake katika kusimamia uagizaji wa bidhaa za mafuta kwa lengo la kuhakikisha nchi inakuwa na uhakika wa upatikanaji wa bidhaa hiyo muhimu. Aidha, Mhe. Makamba ameipongeza PBPA kwa utendaji wake katika kutekeleza majukumu yake na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, amemweleza Naibu Waziri kuwa Wakala unaendelea kutekeleza majuk...

DKT. DOTO BITEKO ANOGESHA MASHINDANO YA NGALAWA TAMASHA LA KIZIMKAZI

 Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko amesema kuwa mashindano ya ngalawa race ni miongoni mwa matukio makubwa ya kiburudani yanayoipamba Kizimkazi Festival 2026. Mashindano hayo yamefanyika Kizimkazi, Kusini Unguja Agosti 12, 2026 yaliyokuwa na ushindani mkubwa ambapo Nassor Pandu wa Mkunguni ameibuka mshindi wa mashindano ya ngalawa ikiwa ni sehemu ya shughuli mbalimbali zinazoendelea katika Tamasha la Kizimkazi. “ Ni dhahiri kwamba mashindano haya yamekuwa muhimu kwa vijana na jamii kwa ujumla. Tukio hili limewaleta pamoja wadau mbalimbali na kuchangia kwa kiasi kikubwa juhudi za kuboresha mazingira ya michezo na burudani,” amesema Dkt. Biteko. Dkt. Biteko ameongeza kuwa mashindano ya Ngalawa race Kizimkazi Festival yameendelea kutoa fursa za kiuchumi kwa vijana mbalimbali katika kushindana hadi kupata timu mbili bora za Mchangamle na Mkunguni ambapo kila timu imehusisha manahodha 10.

TRA TANGA YATOA MAFUNZO MABADILIKO SHERIA ZA KODI KWA WAFANYABIASHARA

 NA: MWANDISHI WETU, TANGA Katika kuhakikisha wafanyabiashara wanakuwa na uelewa wa kutosha kuhusiana na mabadiliko ya sheria za kodi kwa mwaka 2026/2027, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga, imetoa mafunzo kwa wafanyabiashara mkoani humo. Mafunzo hayo yametolewa Agosti 12, 2026, katika Ukumbi wa YDCP Jijini Tanga. Katika mafunzo hayo, wafanyabiashara wamejengewa uwezo juu ya mabadiliko mbalimbali ya sheria za kodi yaliyofanyika ili kuiwezesha TRA kutekeleza majukumu waliyopangiwa na serikali kuu. Akifungua mafunzo hayo, Meneja wa TRA mkoa wa Tanga, CPA. Castro John, amesema sheria zaidi ya 15 za kodi zimefanyiwa mabadiliko, hivyo wanalo jukumu la kutoa elimu kwa wafanyabiashara. "Niwashukuru wafanyabiashara wa Tanga kwa kujitokeza kupata elimu hii muhimu kwani wafanyabiashara wanapokuwa na uelewa wa mabadiliko haya, basi utekelezaji wa ulipaji kodi utakuwa mwepesi," amesema CPA John. Maofisa mbalimbali kutoka TRA Makao Makuu waliwaelimisha wafanyabiashara hao maba...