Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RC SENDIGA AHIMIZA WANANCHI KUTEMBELEA MAONESHO YA NANENANE, KUJIFUNZA TEKNOLOJIA MPYA ZA KILIMO

 Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, leo Agosti 7, 2026, akiwa mgeni rasmi wa zamu, ametembelea mabanda mbalimbali katika Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya Themi-Njiro, jijini Arusha. Katika ziara hiyo, Mhe. Sendiga ametoa wito kwa wananchi wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini kujitokeza kwa wingi kutembelea maonesho hayo ili kujifunza teknolojia mbalimbali za kisasa za kilimo, mifugo na uvuvi zitakazochochea ongezeko la uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi. Amesema maonesho hayo yamekusanya wafanyabiashara, wabunifu na wajasiriamali kutoka ndani na nje ya nchi, jambo linalotoa fursa kwa wananchi kupata maarifa, kujifunza ubunifu na kuanzisha ushirikiano wa kibiashara. Maonesho ya Nanenane ya mwaka 2026 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo: "Tambua Soko, Ongeza Tija kwa Kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050."
Recent posts

TUME YA TAIFA YA UNESCO YAJADILI USHIRIKIANO WA KUENDELEZA JUKWAA LA AMANI KWA VIJANA

 Dar es Salaam, Agosti 7, 2026  Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekutana na ujumbe kutoka African Leadership Initiative for Impact (ALI) kwa lengo la kujadili fursa za ushirikiano katika maandalizi ya Jukwaa la Amani kwa Vijana, linalotarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2026 jijini Dar es Salaam. Majadiliano hayo yalilenga kubaini namna pande hizo mbili zitakavyoshirikiana katika kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika kujenga amani, kukuza uongozi wenye maadili na kuimarisha mshikamano wa kijamii kupitia Elimu ya Uraia wa Dunia (Global Citizenship Education - GCED), ambayo ni moja ya maeneo ya kipaumbele ya UNESCO katika kujenga jamii zenye amani, uvumilivu na maendeleo endelevu. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Profesa Hamisi Malebo, alisema Tume imepokea kwa furaha wazo hilo na kuliona kuwa linaendana na dhamira ya UNESCO ya kujenga amani katika fikra za watu kupitia elimu, sayansi, utamaduni, ma...

Vi AGROFORESTRY YASEMA KILIMO MISITU NI SULUHISHO UHABA WA CHAKULA

 Na Mwandishi Wetu, Dodoma SHIRIKA la Vi Agroforestry Tanzania, kwa kushirikiana na wadau wake akiwemo Tanzania Alliance for Biodiversity (TABIO), limeendelea kutumia Maonesho ya Nanenane kuhamasisha matumizi ya kilimo misitu kama suluhisho la kuongeza uzalishaji wa chakula, kuboresha lishe, kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Akizungumza katika maonesho hayo yanayofanyika katika viwanja vya John Malecelea jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkaazi wa  Vi Agroforestry Tanzania, Martha Olotu, alisema shirika hilo linaendelea kuhamasisha mfumo wa kilimo unaounganisha mazao, miti na mifugo katika eneo moja ili kuongeza tija ya uzalishaji, kuboresha rutuba ya ardhi na kuongeza kipato cha wakulima. Alisema banda la Vi Agroforestry limepokea idadi kubwa ya wakulima, wataalamu na wananchi waliotembelea kujifunza mbinu mbalimbali za kilimo misitu pamoja na kuona bidhaa zinazotokana na mfumo huo, zikiwemo mbegu za asili, unga wa ubuyu, vyakula vya lishe na ma...

BWAWA LA FARKWA TUMAINI JIPYA LA MAJI MKOANI DODOMA

  ▪️Ujenzi Wake Kuanza Oktoba 2026 ▪️Fidia Shilingi bil 8.5 Imeshalipwa kwa Wananchi Waliopisha Mradi *Na Adelina Johnbosco – MAELEZO* Tatizo la uhaba wa maji katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Dodoma linaelekea kupata ufumbuzi wa kudumu kufuatia ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Farkwa utakaoanza kujengwa Oktoba mwaka huu. Bwawa hilo litakalojengwa wilayani Chemba, kata ya Farkwa mkoani Dodoma litakuwa na uwezo wa kuzalisha lita milioni 128 kwa siku na kuhifadhi lita bilioni 390 na linatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 22. Bwawa hili litahudumia hasa wilaya za Chemba, Bahi, Chamwino na maeneo mengine ndani na maeneo ya karibu na mkoa wa Dodoma, lengo ni kutokomeza kabisa upungufu wa maji ndani ya mkoa huo. Ujenzi wa bwawa la Farkwa utatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa gharama ya Shilingi bilioni 163.43 hadi kukamilika kwake. Aidha, jumla ya Shilingi bilioni 8.5 zimelipwa kama fidia kwa wananchi kutoka katika vijiji viwili vya Mombose na B...

FURSA ZA BIASHARA ZA MABILIONI KATIKA MIGODI ZAWAFUNGUKIA WATANZANIA

 Vijana na wanawake wapewa kipaumbele kunufaika na mnyororo wa thamani wa madini 📍DODOMA Serikali kupitia Tume ya Madini imefungua fursa za biashara zenye thamani ya mabilioni ya fedha katika migodi kwa Watanzania, huku vijana na wanawake wakipewa kipaumbele ili kuongeza ushiriki wao katika Sekta ya Madini na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Hatua hiyo inalenga kujenga uchumi shindani na jumuishi unaowezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji, kuongeza thamani ya rasilimali za madini na kunufaika zaidi na fursa zinazotokana na sekta hiyo. Akizungumza katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma, Mjiolojia kutoka Kurugenzi ya Ukaguzi na  Biashara ya Madini ya Tume ya Madini, Hassan Mkumba, amesema Tume imeainisha bidhaa na huduma 20 zitakazotolewa mahsusi na Watanzania ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za migodi. Amezitaja baadhi ya huduma hizo kuwa ni usambazaji wa vilainishi migodini...

RAIS SAMIA AZINDUA TUME MAALUMU KUBAINI CHANZO NA WAHUSIKA WA GHASIA ZA WAKATI NA BAADA YA UCHAGUZI 2025

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua Tume ya Rais ya Uchunguzi ya Wahusika wa Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria Katika Matukio ya Ghasia Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, ikiwa na jukumu la kuchunguza kwa kina chanzo cha matukio hayo, wahusika pamoja na waliowezesha kutokea kwake. Akizungumza leo Ijumaa Agosti 7, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Tume hiyo, Rais Samia amesema ameunda Tume hiyo kwa kuzingatia mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Tume ya Uchunguzi, Sura ya 32, ili kuwezesha uchunguzi wa kina kuhusu matukio ya ghasia na ukiukwaji wa sheria yaliyotokea. Amesema Tume hiyo itaongozwa na Jaji Shabani Ally Lila na itakuwa na jumla ya makamishna sita, ambapo mmoja anatoka Uganda na mwingine Namibia, hatua inayolenga kuongeza mtazamo mpana katika utekelezaji wa jukumu hilo. “Katika Tume hii tumeamua kuwashirikisha wenzetu kutoka nje ya Tanzania ili kupata maono mapana,” amesema Rais Samia. Rais Sami...