Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RAIS DKT. MWINYI ATEMBELEA VITUO VYA UTAFITI NA UBUNIFU IIT MADRAS-INDIA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea idara, vituo vya utafiti na maabara mbalimbali za Taasisi ya Teknolojia ya IIT Madras, jijini Chennai, nchini India leo tarehe 17 Julai, 2026. Ziara hiyo imetoa fursa ya kujionea maendeleo yaliyofikiwa na Taasisi hiyo katika teknolojia, tiba, ubunifu na utafiti, pamoja na kubadilishana uzoefu kuhusu namna elimu, maarifa na teknolojia vinavyoweza kutumika kutatua changamoto za kiafya na kijamii. Miongoni mwa maeneo aliyotembelea ni Kituo cha Sayansi ya Urithi, Kituo cha Taaluma na Tiba Asili za India, vituo vya utafiti wa sayansi na teknolojia za tiba, pamoja na Kituo cha Utafiti wa Kina wa Ubongo kwa kutumia Mbinu za Kisasa na Jumuishi za Anatomia ya Mfumo wa Neva. Aidha, ametembelea Maabara ya Anatomia na kujionea matumizi ya teknolojia za kisasa katika ufundishaji, uchunguzi na tafiti za afya. Ziara hiyo inatarajiwa kufungua fursa zaidi za kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali ya ...
Recent posts

MWENYEKITI WA ACT WAZALENDO AMTEMBELEA SHEIKH RASHID HOSPITALINI

  MWENYEKITI wa Taifa wa ACT Wazalendo, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, Leo Ijumaa ya Tarehe 17 Julai 2026, akiambatana na mke wake Mama Zainab Kombo Shaib, amefika na kumjulia hali Sheikh Rashid Hamad Othman (kaka yake), anayepatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, Jijini Dar es Salaam. Mheshimiwa Othman yupo Jijini Dar es Salaam kwa ziara Maalum ya Kikazi na kijamii.

WAZIRI MKUU AKAGUA MAANDALIZI YA SIKU YA MASHUJAA

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Julai 17, 2026 amekagua na kupokea taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika Julai 25, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa, Mtumba, jijini Dodoma. Katika ukaguzi huo, Waziri Mkuu ameridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuwataka wote wanaohusika kuendelea kukamilisha maandalizi yaliyobaki kwa wakati ili maadhimisho hayo yafanyike kwa utaratibu na hadhi inayostahili. Maadhimisho hayo yataongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu.

VIJANA 10,000 MAFUNDI WA JIMBO LA MTUMBA WENYE UJUZI KUPATIWA VYETI VYA UFUNDI NA KUTAMBULIWA NA VETA

  ▪️Ni vijana wenye ujuzi lakini hawajapitia mfumo rasmi wa mafunzo ▪️Mbunge Mavunde aahidi kuwafikia Vijana 10,000 wenye ujuzi wa Jimbo la Mtumba ▪️Ni kupitia ya Programu ya Mama Samia ya Utambuzi wa Ujuzi chini ya VETA ▪️Mkurugenzi Mkuu VETA awataka vijana kujiunga pamoja na kuchangamkia fursa Dodoma Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mh. Anthony Mavunde amesema kupitia Programu ya Mama Samia ya Kutambua Ujuzi wa Mafundi chini ya VETA anategemea kutambuliwa kwa zaidi ya Vijana 10,000 wenye ujuzi lakini ambao hawajapitia mfumo rasmi wa mafunzo ifikapo mwaka 2030. Mh. Mavunde ameyasema hayo jana tahere 16 Julai 2026 Jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vyeti vya Ufundi kwa vijana 100 wenye ujuzi waliotambuliwa kupitia Chuo cha VETA. “Tunaishukuru Serikali kupitia programu hii ya Mama Samia ya kutambua ujuzi wa vijana kupitia VETA. Vijana hawa wengi walikuwa na ujuzi lakini hawakupata nafasi ya kupata mafunzo rasmi ya ufundi kupitia vyuo vya Ufundi. Kutambuliwa kwa ujuzi wao bila ...

BRIDGING THE GAP: JAB PARTNERS WITH BLOGGERS NETWORK ON TRAINING

 By TBN Writer The Journalists’ Accreditation Board (JAB) has received a formal request from the Tanzania Bloggers Network (TBN) seeking training for its more than 200 members on the Media Services Act, journalism ethics, and the importance of obtaining professional accreditation. The request was submitted on 16 July 2026, when TBN Chairman Beda Msimbe met with JAB’s Acting Director General, Advocate Patrick Kipangula, during discussions held at the Board’s offices in Dar es Salaam. Speaking after the meeting, Advocate Kipangula said the Board had received the request and was ready to work with the network to help bloggers gain a deeper understanding of the Media Services Act, professional ethics, and the value of accreditation. He said the training would begin with bloggers who are already accredited, aimed at strengthening their professionalism and understanding of their professional responsibilities, before extending to those who have not yet obtained accreditation. “Those witho...

WAZIRI MKUU: TUUNGANE KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania, taasisi za umma na binafsi, mashirika na wadau wa maendeleo waungane na Serikali katika kuwezesha matibabu ya upandikizaji wa figo na uloto kwa wananchi wasiokuwa na uwezo ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma hizo za kibingwa. "Hiki ni kitendo cha kiungwana, cha ibada na kinachogusa maisha ya Watanzania. Nawapongeza Umoja wa Wanawake Tanzania kwa kuitikia wito huu na kuwa sehemu ya kuokoa maisha ya wananchi," amesema. "Tunachokifanya leo ni kurejesha matumaini kwa wagonjwa na familia zao. Kila anayeguswa na jambo hili aendelee kushiriki ili wananchi wengi zaidi wanufaike na huduma hizi muhimu," amesema. Waziri Mkuu ametoa wito huo jana (Alhamisi, Julai 16, 2026) katika hafla ya Okoa Maisha Gala iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa kushirikiana na Hospitali ya Benjamin Mkapa katika Ukumbi wa Mabele Hall, Jenerali Venance Mabeyo Complex, jijini Dodoma. Alisema Serikali ya Awamu ya Sita...