Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 03 Septemba, 2026, amezindua rasmi Jengo la Ramani la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lililopo katika Mji wa Serikali, Mtumba, Jijini Dodoma. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo hilo ambalo ni sehemu ya miundombinu ya kimkakati ya Jeshi, Dkt. Nyansaho amelipongeza JWTZ kwa kukamilisha mradi huo na kupata jengo la kisasa lililowekewa vifaa na teknolojia za kisasa zitakazowezesha utoaji wa huduma kwa ufanisi na weledi zaidi. Waziri Nyansaho amesema kukamilika kwa mradi huo ni kielelezo cha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuendelea kuliwezesha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kulinda uhuru, mamlaka na usalama wa nchi. “Kukamilika kwa mradi huu wa kimkakati ni alama ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuendelea kuliwezesha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kutimiza majukumu yake ya ulinzi na usal...
MARATO TV
Marato tv - Sauti ya Jamii