Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imepanga kufanya kikao cha awali cha maandalizi ya usikilizwaji wa Shauri la Uhaini Na. 19605/2025 linalomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antiphas Lissu. Kwa mujibu wa waraka rasmi uliotolewa Julai 31, 2026 na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, H. S. Mushi, kikao hicho cha awali (Pre-Session Meeting) kitafanyika Agosti 5, 2026 kuanzia saa nane kamili mchana kwa njia ya mtandao kupitia Masjala Ndogo ya Mahakama Kuu, Dar es Salaam. Mahakama imeeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kujadili maandalizi muhimu yatakayowezesha usikilizwaji wa shauri hilo kufanyika kwa ufanisi kabla ya kuanza rasmi kwa mwenendo wa kesi. Aidha, usikilizwaji wa shauri hilo umepangwa kuanza Agosti 10, 2026 na unatarajiwa kuendelea hadi Septemba 7, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Mahakama. Waraka huo umeelekezwa kwa Mkuu wa Mashtaka wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Gereza Kuu la Ukonga na ...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.