Na Angela Sebastian; Bukoba Mwenge wa Uhuru Kuzindua na Kukagua Miradi 54 ya Sh. Bilioni 23 Kagera Mwenge wa Uhuru mwaka huu unatarajiwa kuzindua, kufungua, kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi 54 ya maendeleo yenye thamani ya Sh. bilioni 23 mkoani Kagera. Akizungumza na waandishi wa habari leo, Agosti 26, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahya Kido, amesema Mwenge huo utapokelewa wilayani Muleba ukitokea mkoani Geita tarehe Agosti 30, 2026, kabla ya kuanza kukimbizwa katika halmashauri nane za mkoa huo. Kwa mujibu wa Kanali Kido, Mwenge wa Uhuru utatembea umbali wa takribani kilomita 1,230 ndani ya Kagera, huku ukiifikia miradi 54 katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo,katika miradi hiyo, 25 itawekewa mawe ya msingi, mitano itafunguliwa, 11 itazinduliwa na 13 itakaguliwa ili kujiridhisha na utekelezaji wake pamoja na manufaa yake kwa wananchi. Miradi hiyo inahusisha sekta muhimu za maendeleo, ikiwemo maji, ...
Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mamlaka za kiserikali zimetakiwa kutoa elimu zaidi kwa jamii ili kuepusha uharibifu wa miundombinu ya serikali ikiwemo reli,mabomba ya maji na umeme. Hayo yamesemwa na mkurungenzi wa kampuni ya Migungani company limited inayojishughulisha na ukusanyaji taka rejeleshi (chuma chakavu,oil chafu na chupa za maji) Bwana. Johannes Alexander Chacha iliyopo jijini Tanga. Chacha ametoa kauli hiyo kufuatia changamoto wanazopitia kutokana na biashara wanayofanya ya chuma chakavu,wao ambao wanafata Sheria zote na kuwa na vibali pia hujikuta wanatiwa matatizoni. "Niiombe serikali kusimamia vema sheria zilizowekwa katika biashara hii ya taka rejeleshi kwani itasaidia kuwatambua hata wale wanaofanya biashara hii kinyume cha Sheria",alisema Chacha Aidha chacha pia ameishukuru serikali Kwa kuwaona na kuwapa kipaumbele pale inapokuja miradi ya kimkakati kama ujio wa Bomba la mafuta ghafi linaloendelea kujengwa huko chongoleani,kwani wao ni wadau wa kubwa wa mae...