WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, ameipongeza Idara ya Uhamiaji kwa kufanya vizuri katika utoaji wa huduma na kuiwezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa huduma bora za uhamiaji barani Afrika. Katambi amesema hayo leo, Septemba 6, 2026, akizungumza katika kikao cha viongozi waandamizi wa Idara ya Uhamiaji, ambapo amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuboresha huduma kwa wananchi na wageni wanaoingia nchini. Amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika uboreshaji wa pasipoti, akieleza kuwa pasipoti ya Tanzania imekuwa miongoni mwa pasipoti bora katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, huku ikiwa na mifumo imara ya kiusalama inayoweza kuwa mfano kwa nchi nyingine. “Ni jambo kubwa ambalo Watanzania wanapaswa kujivunia kwamba pasipoti yetu ni nzuri na ina security features ambazo kwa nchi nyingine ni ya mfano,” amesema Katambi. Aidha, Katambi ameipongeza Idara ya Uhamiaji kwa kutambuliwa kutokana na ubora wa huduma zake, akisema hatua hiyo ni ushahi...
KAMISHNA Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maboresho makubwa yaliyofanyika katika Idara ya Uhamiaji, akisema hatua hizo zimeongeza ufanisi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wageni wanaoingia na wanaotoka nchini. Dkt. Makakala amesema maboresho hayo yamekuwa chachu ya kuimarisha utendaji kazi wa Idara ya Uhamiaji na kuiwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi, hususan katika kusimamia shughuli za uhamiaji, udhibiti wa wageni pamoja na utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi na wageni wanaofika nchini. Dkt. Makakala Ameyasema hayo wakati akizungumza katika Kikao Kazi cha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji na Maafisa Uhamiaji wa Mikoa, kilichofanyika mkoani Kilimanjaro, kikao kilicholenga kutathmini utendaji kazi wa Idara ya Uhamiaji katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026, pamoja na kupitia utekelezaji wa mpango na bajeti kwa ...