* Ampongeza Aweso kwa kuandaa timu 80, ashangaa kuizidi Ligi Kuu. *Na Mashaka Mhando, Pangani NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu 'MwanaFA', amekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mashindano makubwa ya soka ya 'Aweso Cup' yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Sakura, wilayani Pangani. Akizindua mashindano hayo kwa kupiga penalti ya kifundi, MwanaFA alimmwagia sifa Mbunge wa Pangani ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, kwa kuwekeza kwenye michezo na kufanikiwa kukusanya timu takribani 80 kutoka kata 14 za jimbo hilo. "Hongera Mheshimiwa, timu 80 siyo mchezo! Umeishinda hata Ligi Kuu yetu yenye timu 16 tu. Hili ulilolifanya si jambo dogo," alisema MwanaFA kwa mshangao. MwanaFA alibainisha kuwa Serikali imeweka mpango madhubuti wa kuhakikisha kila yanapofanyika mashindano ya mpira wa miguu, haijalishi yana udogo gani, inapeleka skauti kutoka Shirikisho la Soka Nchini (TFF) kusaka vipaji ili kuvilea kama inavyofanya kwa timu za...
KIONGOZI MWENGE WA UHURU AIPONGEZA ALLIANCE ONE KWA KUPANDA MITI KWA GHARAMA YA SH.BILIONI 1.2 WILAYANI BUHIGWE
Na Mwandishi Wetu,Kigoma Kampuni ya tumbaku ya Alliance One Tanzania Tobacco Limited imepongezwa kwa kutoa mchango mkubwa katika kuhifadhi mazingira mkoani Kigoma kupitia katika miradi ya kurejesha uoto wa miti katika maeneo yaliyoathiriwa na shughuli za binadamu na mabadiliko ya tabia nchi. Pongezi hizo zimetolewa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2026 Bw.Wazo Mwang’onda, baada ya kukagua mradi wa shamba la miti katika shule ya sekondari Munagana linalofadhiliwa na kampuni hiyo kwa kupanda miti ekari 414 ambapo mpaka sasa gharama za uendeshaji kwenye shamba hilo ni Shilingi 1,264,723,200. Bw. Mwang’onda amebainisha kuwa kitendo cha kampuni ya Alliance One kuamua kuwekeza katika upandaji wa miti ni cha kizalendo na chenye nia ya kuunga mkono juhudi za serikali katika kuhifadhi mazingira na kukuza Uchumi wa wananchi kupitia kilimo cha tumbaku na miti. Mwang’onda ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa Alliance One kuendelea kutoa usaidizi wa ujuzi kwa halmshauri za wi...