Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MAHAKAMA KUU YAPANGA KIKAO CHA AWALI CHA SHAURI LA UHAINI LA LISSU

 Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imepanga kufanya kikao cha awali cha maandalizi ya usikilizwaji wa Shauri la Uhaini Na. 19605/2025 linalomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antiphas Lissu. Kwa mujibu wa waraka rasmi uliotolewa Julai 31, 2026 na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, H. S. Mushi, kikao hicho cha awali (Pre-Session Meeting) kitafanyika Agosti 5, 2026 kuanzia saa nane kamili mchana kwa njia ya mtandao kupitia Masjala Ndogo ya Mahakama Kuu, Dar es Salaam. Mahakama imeeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kujadili maandalizi muhimu yatakayowezesha usikilizwaji wa shauri hilo kufanyika kwa ufanisi kabla ya kuanza rasmi kwa mwenendo wa kesi. Aidha, usikilizwaji wa shauri hilo umepangwa kuanza Agosti 10, 2026 na unatarajiwa kuendelea hadi Septemba 7, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Mahakama. Waraka huo umeelekezwa kwa Mkuu wa Mashtaka wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Gereza Kuu la Ukonga na ...
Recent posts

RAIS SAMIA APATA MAPOKEZI MAKUBWA NCHINI ANGOLA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.

TIB YANADI DIRA 2050 MKUTANO WA VIWANDA WA SADC DURBAN

 Na Benny Mwaipaja, Durban Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Tanzania (TIB), Bw. Deogratius Kwiyukwa, amesema kuwa uunganishaji nguvu ya pamoja ya Taasisi za kifedha katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC, utachochea ujenzi wa viwanda vitakavyokuwa chachu ya kukuza maendeleo ya nchi wanachama wa Jumuiya hiyo kiuchumi na kijamii. Bw. Kwiyukwa, amesema hayo kando ya Mkutano wa 9 wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week) unaoendelea katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (ICC), jijini Durban, nchini Afrika Kusini. Alisema kuwa TIB ambayo ni Taasisi ya Serikali imeshiriki katika mkutano huo kutafuta fursa za kushirikiana na taasisi nyingine za kifedha ndani ya ukanda wa SADC ili kuunganisha mitaji kwa ajili ya kufadhili miradi mikubwa ya maendeleo itakayo changia kufikia lengo la utekelezaji wa DIRA ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayotaka uchumi wa Tanzania ufikie thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka huo. Bw. Kwiyukwa alisisit...

PAUL CHACHA AAGA TABORA KWA HISIA, AAHIDI KUTUMIKIA DHAMANA MPYA KWA UAMINIFU

 Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Paul Chacha, ameaga rasmi wananchi wa mkoa huo kwa ujumbe wenye hisia na shukrani, akisema anaondoka akiwa na kumbukumbu nyingi nzuri za ushirikiano alioupata katika kipindi chote cha utumishi wake. Katika ujumbe wake, Chacha amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa imani aliyomuonesha kwa kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Machi 9, 2024, akieleza kuwa ilikuwa heshima kubwa kulitumikia Taifa kupitia mkoa huo. Pia amewashukuru watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, viongozi wa taasisi mbalimbali na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kwa ushirikiano wao katika kusimamia amani, usalama na maendeleo ya Tabora. Chacha alisema wananchi wa Tabora watabaki sehemu muhimu ya maisha yake kutokana na ushirikiano waliompa kupitia mikutano, mawasiliano ya simu, ujumbe mfupi na hata waliomtembelea ofisini kwake. "Kutoka kwenu nimejifu...

BODI YA STAKABADHI ZA GHALA YAONGEZA MAZAO MAPYA,YAWAPA WAKULIMA FURSA ZA MASOKO

 BODI ya Stakabadhi za Ghala (WRRB) imesema imejipanga kupanua wigo wa mfumo wa stakabadhi za ghala kwa kusajili mazao mapya yakiwemo mazao ya viungo na mifugo, hatua inayotarajiwa kuongeza fursa za masoko, kuwawezesha wakulima kupata huduma za kifedha na kuimarisha biashara ya mazao nchini. Akizungumza leo jul 31,2026 jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na mwelekeo wa mwaka wa fedha 2026/2027, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Asangye Bangu, amesema taasisi hiyo imepata uzoefu wa kutosha katika usimamizi wa mfumo wa stakabadhi za ghala na sasa imejielekeza kuongeza mazao yatakayohudumiwa ili kuwafikia wazalishaji wengi zaidi. Amesema katika hatua za awali, Bodi inalenga kuingiza mazao ya viungo kama iliki, tangawizi, kitunguu saumu na pilipili manga (black pepper), huku ikiendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi zinazoratibu maendeleo ya mazao hayo ili kuhakikisha yanaingizwa rasmi kwenye mfumo wa stak...

TARI YAADHIMISHA MIAKA 10 KWA MARATHON NA MAONESHO YA TEKNOLOJIA ZA KILIMO

 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki Marathon ya TARI itakayofanyika Agosti 2, 2026, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI). Mhe. Senyamule ameyasema hayo mara baada ya kutembelea banda la TARI na kukabidhiwa jezi za marathon hiyo, ambapo alieleza kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo. Amesema marathon hiyo inalenga kuhamasisha afya, kuunganisha wadau wa sekta ya kilimo na kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu mchango wa TARI katika utafiti na maendeleo ya kilimo nchini. Amesema hadi sasa zaidi ya washiriki 1,000 wamekwishajisajili, huku akiwahimiza wananchi wengine kuendelea kujisajili ili kushiriki mbio hizo zitakazoanzia eneo la Nzuguni saa 2:00 asubuhi. Marathon hiyo itakuwa na mbio za kilomita 5, 10 na 21, ili kutoa nafasi kwa makundi mbalimbali ya washiriki. K...