Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limefanya matendo ya huruma kwa kutoa m saada wa vitu mbalimbali kwa wagonjwa waliopo katika kituo cha afya Ilembo kilichopo Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi. Akikabidhi msaada huo Julai 25, 2026 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Kaster Ngonyani amebainisha kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kama sehemu ya jamii limeona ni vyema kufanya matendo ya huruma na kutoa faraja kwa wagonjwa hao ili wasijione wapweke. Msaada uliotolewa kwa wagonjwa hao ni pamoja na taulo za kina mama, pempasi, sabuni, sukari, unga, mafuta ya kupaka, maji, juice, mafuta ya kupikia, miswaki na dawa za meno pamoja na kuchangia damu. Akipokea msaada huo Mganga Mfawidhi kituo cha afya Ilembo Dr. Veneranda Musati amelishukuru Jeshi la Polisi kwa msaada huo na kutoa wito kwa jamii kuiga mfano huo kwa kuwa na moyo wa kusaidia wahitaji.
*▪️Waziri Mavunde akagua soko na stendi ya kisasa ya Shilingi bilioni 22 Ushirombo* *▪️Mradi wa maji Businda-Buntubili kunufaisha wakazi 9949* *▪️Wachimbaji wamshukuru Rais Samia kwa ugawaji wa Leseni* *▪️Ujenzi wa barabara-Uyovu na kituo cha polisi na zahanati katika eneo la machimbo ya Msasa wapongezwa* Bukombe, Geita Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameendelea na ziara yake ya kukagua na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Geita kwa kutembelea miradi mbalimbali katika Wilaya ya Bukombe, huku akisisitiza umuhimu wa kukamilika kwa miradi hiyo kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotarajiwa. Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara, Waziri Mavunde amesema serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuleta miradi mingi ya maendeleo ili kupeleka huduma za msingi kwa wananchi. Awali, Waziri Mavunde alikagua mradi wa maji katika Kijiji cha Businda, Kata ya Bulangwa, wenye...