Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

UWT YAPONGEZA NDEJEMBI KUTHIBITISHWA KWA ASILIMIA 100 UMAKAMU WA RAIS

 NA: MWANDISHI WETU, DODOMA  Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), umepongeza uamuzi wa wabunge kumthibitisha Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais kwa kura 324, sawa na ushindi wa asilimia 100. Akisoma tamko la UWT, Agosti 28, 2026, Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Umoja huo Taifa, Mary Chatanda, amesema ushindi wa asilimia 100 unadhihirisha imani kubwa waliyonayo wabunge kuwa Makamu wa Rais mteule, atatimiza kikamilifu majukumu yake katika kumsaidia Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. "UWT tunawapongeza wabunge kwa kupiga kura za kishindo kwa asilimia 100 na hivyo kufanikisha hatua muhimu iliyokuwa mbele ya kuthibitishwa bungeni," amesema Chatanda. Ameongeza kuwa, UWT inaiunga mkono Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kupitisha jina la Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais kwani ni kiongozi mzalendo, mchapakazi na muadilifu katika utekelezaji wa majukumu. "Halmashauri Kuu haikufanya makosa kupitisha jina hili kwani kote alipofanya kazi, Ndejembi ameonyesha uwezo mkubw...
Recent posts

BUNGE NMB BONANZA KUFANYIKA DODOMA KESHO, TAASISI ZA SERIKALI 24 KUSHIRIKI

 MWENYEKITI wa Bunge Bonanza, Festo Sanga, amesema maandalizi yote yamekamilika kwa ajili ya Bonanza la Bunge–NMB litakalofanyika kesho, Agosti 29, 2026, katika Viwanja vya John Meling, jijini Dodoma. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Sanga amesema bonanza hilo litaanza saa 12:00 asubuhi, likiwa na ushiriki wa taasisi na wizara mbalimbali za Serikali, huku washiriki wakitarajiwa kuwa wengi zaidi ikilinganishwa na mabonanza yaliyopita. Amesema bonanza hilo ni sehemu ya jitihada za Bunge kuendeleza michezo miongoni mwa watumishi, pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge na taasisi mbalimbali za Serikali na wadau wake. “Mheshimiwa Spika ametoa msisitizo kwamba Bunge lazima lijishirikishe katika shughuli za michezo, kwa sababu michezo ni muhimu katika kuimarisha afya na kujenga ushirikiano,” amesema Sanga. Takribani wizara 14 pamoja na taasisi nyingine zaidi ya 10 zimealikwa kushiriki bonanza hilo, hivyo kufanya idadi ya taasisi zinazotarajiwa kushiriki kufiki...

UTENDAJI KAZI WA MKUU WA MKOA WA MARA WAMKOSHA RAIS SAMIA

 Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amempandisha Cheo Kanali Evans Alfred Mtambi, Mkuu wa Mkoa wa Mara kuwa Brigedia Jenerali kuanzia Tarehe 21 Agosti 2026. Hafla ya kupewa cheo imefanyika leo Dodoma Makao Makuu ya Jeshi. 

BUNGE LAMTHIBITISHA NDEJEMBI KWA ASILIMIA 100 UMAKAMU WA RAIS

_*Waziri Mkuu asema anatosha, kiti kimempata mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais.*_ BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo (Ijumaa, Agosti 28, 2026) limemthibitisha Mheshimiwa Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mheshimiwa Ndejembi amepitishwa kwa asilimia 100 ya kura zote 324 zilizopigwa na waheshimiwa wabunge, ambapo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani aliyoionesha kwake kwa kumteua kuwa Makamu wa Rais na katika nafasi nyingine mbalimbali za uongozi. Pia Mheshimiwa Ndejembi amelishukuru Bunge kwa imani kubwa waliyompa kiasi cha kumpigia kura kwa asilimia mia moja. Mapema akiwasilisha hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Mheshimiwa Deogratius Ndejembi anatosha na ni mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais katika nafasi ya Makamu wa Rais,  akiitaja kuwa ni nafasi yenye dhamana na majuku...

VIONGOZI WA MANISPAA YA MUSOMA WASHIRIKI ZOEZI LA UTOAJI WA CHANJO YA POLIO AWAMU YA TATU

 Na Mwandishi wetu Jovina Massano Viongozi wa Wilaya na halmashauri ya Manispaa ya Musoma mkoani Mara washiriki zoezi la utoaji chanjo. Zoezi hilo limeanza rasmi Agosti 27,2026 na litahitimishwa Agosti  30,2026 ambapo watoa huduma watafanya zoezi hilo nyumba kwa nyumba,mashuleni kwenye masoko,nyumba za Ibada na kwenye maeneo yenye mkusanyiko. Mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amewatoa hofu na kuwahimiza wazazi na walezi wenye watoto walio chini ya miaka 10 kuwa chanjo hiyo ni salama imekidhi viwango vya kitaifa na kimataifa kwa kuwa imethibitishwa na kuidhinishwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba Tanzania (TMDA) sambamba na Shirika la Afya Duniani (WHO). "Kampeni ya chanjo ya matone inatekelezwa ili kuhakikisha Jamii inakuwa na kinga kamili dhidi ya ugonjwa wa Polio pia inatolewa bure,haina madhara kwa watoto imethibitishwa na wataalam wa kitaifa na kimataifa Polio ni miongoni mwa magonjwa yanayozuilika,"amesema Chikoka. Amesisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha walengwa wote...

SPIKA ZUNGU APOKEA RASMI JINA LA NDEJEMBI KWA AJILI YA KUTHIBITISHWA KUWA MAKAMU WA RAIS

 SPIKA wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), leo Agosti 28, 2026, amepokea rasmi jina la Makamu wa Rais Mteule, Mhe. Deogratius John Ndejembi (Mb), lililopendekezwa na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa ajili ya kuthibitishwa na Bunge. Jina hilo limewasilishwa kwa Spika Zungu na Katibu wa Rais, Bal. Ali Jabir Mwadini, aliyeambatana na Mpambe wa Rais (ADC), Brig. Jen. Nyamburi Mashauri. Mapokezi ya jina hilo yameshuhudiwa na viongozi mbalimbali, akiwemo Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo (Mb), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari (Mb), pamoja na Katibu wa Bunge, Ndugu Baraka Leonard. Viongozi wengine walioshuhudia tukio hilo ni Wenyeviti wa Bunge, Mhe. Deogratius Mwanyika (Mb), Mhe. Najma Giga (Mb) na Mhe. Cecilia Pareso (Mb). Mhe. Ndejembi amependekezwa kushika nafasi hiyo ya Makamu wa Rais na jina lake sasa limewasilishwa rasmi Bungeni kwa hatua ya kuthibitishwa kwa mujibu wa taratibu za kikatiba.