📌Aipongeza Wizara kwa kushirikisha wadau wa mazao ya misitu na nyuki 📌Asema kazi ya uhifadhi inafanyika kwa weledi mkubwa *Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma* NAIBU Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi leo Agosti 03, 2026 ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kujionea wadau mbalimbali wanaoshirikiana na wizara kwenye uzalishaji wa bidhaa za misitu na asali na kuipongeza wizara kwa kushirikiana na wadau hao. Brigedia Jenerali Shija amesema wadau hao wamekuwa wakifanya kazi nzuri katika kuhakikisha mazao hayo ya bidhaa za nyuki ikiwemo asali, miche ya miti na mazao ya misitu yanakuwa na soko ndani na nje ya nchi. Brigedia Jenerali Shija alipata wasaa wa kutembelea wanyamapori hai waliopo kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kama njia mojawapo ya kuutangaza utalii wa ndani.
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika nchini ili kuhakikisha vinaendeshwa kwa uwazi, uwajibikaji na uadilifu, akisisitiza kuwa ushirika wenye misingi hiyo ndiyo nguzo muhimu ya kukuza uchumi jumuishi na kuvutia uwekezaji. Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo leo katika Siku Maalum ya Ushirika, iliyofanyika ndani ya Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane 2026 kwenye Viwanja vya John Malecela, Nzuguni mkoani Dodoma, ambapo pia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha sekta ya ushirika ili iwe kichocheo cha maendeleo ya kilimo na uchumi wa Taifa. Amesema Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) linapaswa kuendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyama vya ushirika ili kudhibiti ubadhirifu wa rasilimali, kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na kuongeza uwazi katika uendeshaji wa vyama hivyo. "Ushirika wenye uadilifu unajenga iman...