Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RAIS SAMIA AIPA TADB NGUVU,MTAJI WAPAA HADI BILLIONI 452.16

 Jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha sekta ya kilimo zimeendelea kuzaa matunda baada ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuongeza mtaji wake kutoka Shilingi bilioni 60 hadi kufikia Shilingi bilioni 452.16, hatua inayoongeza uwezo wa benki hiyo kufadhili kilimo, mifugo na uvuvi kwa kiwango kikubwa zaidi. Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 30, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari  MAELEZO jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya kilimo Tanzania TADB, Frank Nyabundege, amesema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa wa Serikali pamoja na ushirikiano na taasisi mbalimbali za maendeleo. Amesema kabla ya Serikali ya Awamu ya Sita, mtaji wa TADB ulikuwa Shilingi bilioni 60 pekee, lakini sasa umefikia Shilingi bilioni 452.16, jambo linaloifanya benki hiyo kuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kuwafikia wakulima, wafugaji na wavuvi nchini. "Kabla ya Serikali ya Awamu ya Sita, mtaj...
Recent posts

MKURUGENZI MKUU WA REA AZUNGUMZA NA WADAU KATIKA KUWEKA MIKAKATI YA USAMBAZAJI WA NISHATI YA UMEME VIJIJINI

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy leo Julai 30, 2026 amezungumza na Wajumbe wa Rural Energy Working Group, ambalo ni Jukwaa lililoundwa na REA likishirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali ambao ni Wadau muhimu katika kusambaza Nishati Bora Vijijini. Mhandisi Saidy amesema kuwa Jukwaa hilo ni muhimu sana katika kuratibu, kubadilishana taarifa na kuwa na mipango ya pamoja katika kusaidia utekelezaji wa miradi ya Wakala na kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya nishati bora vijijini kwa wakati.  Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Utafiti wa REA, Mhandisi Jensen Mahavile amesema kuwa kundi hilo pia ni jukwaa muhimu kwa sababu linatoa ushauri pamoja na kutoa ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazotokea wakati wa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati bora vijijini.

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA NA MKURUGENZI MTENDAJI MUHIMBILI WAWEKA MIKAKATI MADHUBUTI KUBORESHA MFUMO WA MALIPO YA HUDUMA ZA AFYA

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Dellilah Kimambo, kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za afya na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha mfumo wa malipo ya huduma ili kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa urahisi, haraka, kwa ufanisi na kuondoa malalamiko ya wananchi. Katika kikao hicho, Dkt. Magembe amesisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma za afya, akimtaka Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha mifumo ya TEHAMA ya hospitali inaendelea kuimarishwa ili kurahisisha mchakato wa malipo ya huduma, kuongeza uwazi kwa wananchi, kupunguza usumbufu na muda wa kusubiri kwa wagonjwa, pamoja na kuondoa udanganyifu. “Mwananchi apate taarifa za malipo anayotakiwa kufanya kiganjani mwake kupitia simu ili kabla ya kulipa ajihakikishie kama malipo hayo ni sahihi au hapana”, amesema Dr Grace.  Amemwelekeza Mkurugenzi wa Muhimbili kuimarisha usimamizi wa hu...

CHATANDA SASA MLEZI WA CCM MKOA WA MARA

 NA: MWANDISHI WETU Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu (MCC), Mary Chatanda, amebadilishwa mkoa wa ulezi wa kichama na sasa ni mlezi wa CCM mkoa wa Mara. Mabadiliko hayo yamefanyika Julai 29, 2026, Zanzibar, kufuatia vikao vya Chama vinavyoendelea. Kabla ya mabadiliko hayo, Chatanda alikuwa mlezi wa mikoa ya Mjini na Magharibi, Zanzibar. Akizungumzia mabadiliko hayo, Chatanda amekishukuru Chama chake kwa kuendelea kumuamini kutekeleza majukumu mbalimbali ya kichama. "Nimepokea taarifa hii ya mabadiliko ya ulezi wa Chama mkoa kwa moyo wa unyeyekevu. Nakishukuru Chama changu kwa kuniamini. Niwaombe wanachama wenzangu na wananchi kwa ujumla tushirikiane kuhakikisha tunasukuma mbele gurudumu la maendeleo na Chama chetu". Ameongeza kuwa "Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imepeleka fedha nyingi za miradi ya maendeleo mkoani Mara, ni wajibu wetu kuhakikisha fedha hizo zina...

VISIMA 67,000: NGUVU MPYA YA KUONGEZA CHAKULA NA KIPATO CHA MKULIMA

 Arusha.  Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imeanza utekelezaji wa mpango wa kuchimba visima 67,000 kwa wakulima wadogo nchini, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kufungua maelfu ya ajira kwa vijana. Akizungumza katika Kongamano la 10 la Ununuzi wa Umma mwaka 2026 jijini Arusha, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa, amesema mpango huo unatekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa wakati wa uzinduzi wa mradi wa uchimbaji wa visima kwa wakulima wadogo katika Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Mbeya mwaka 2023. «"Lengo letu ni kumkomboa mkulima mdogo kutokana na utegemezi wa mvua kwa kuhakikisha anapata maji ya uhakika kwa ajili ya uzalishaji wa mwaka mzima. Hii itachochea uzalishaji, kuongeza kipato cha wakulima na kuimarisha usalama wa chakula nchini," amesema Mndolwa.» Amesema mpango huo pia unalenga kufikisha huduma za umwagiliaji kwa wakulima walio nje ya skimu ra...

KINGOBA: UHURU WA KUTOA MAONI UENDE SAMBAMBA NA UWAJIBIKAJI

 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mjumbe wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) na Kaimu Meneja wa Huduma za Kiswahili wa Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN), Mgaya Kingoba, amesema uhuru wa kutoa maoni una mipaka ya kisheria na kimaadili, hivyo haupaswi kutumiwa kutoa matusi, kudhalilisha wengine, kuchochea chuki au kusambaza taarifa zisizo sahihi. Kingoba amesema hayo leo, Julai 30, 2026, alipowasilisha mada kuhusu “Kuimarisha Uzalendo katika Uandishi wa Habari ili Kulinda Amani, Umoja na Mshikamano” katika siku ya pili ya mafunzo kwa watumishi wa Bongo FM, redio dada ya TBC (Shirika la Utangazaji Tanzania), yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 29, 2026. Amesema ukosoaji ni sehemu muhimu ya uhuru wa kujieleza, lakini unapaswa kulenga kuonesha kasoro na kuchochea maboresho badala ya kushambulia watu, kutumia lugha ya kejeli au kubomoa imani ya jamii kwa taasisi. “Mkosoaji mzalendo hafichi makosa, lakini pia hatumii matusi, kejeli au upot...