KAMPALA, Uganda Serikali ya Uganda imepanga kuanza kuhamisha kwa awamu wizara, idara na taasisi zake kutoka Kampala kwenda Nakasongola , katika mpango wa muda mrefu ambao unaweza kuendelea hadi mwaka 2040 . Mpango huo umetangazwa na Waziri wa Nchi wa Maendeleo ya Miji, Margaret Muhanga , mbele ya Kamati ya Ardhi na Nyumba ya Bunge la Uganda. Muhanga amesema Rais Yoweri Museveni anaunga mkono mpango huo, ambao Serikali inautazama kama sehemu ya utekelezaji wa maono ya maendeleo ya Uganda kuelekea mwaka 2040. KAMPALA YAWA CHANGAMOTO Serikali imesema msongamano mkubwa wa magari na changamoto za upangaji wa mji zimefanya Kampala kuwa na mazingira magumu kwa watu kuishi na kufanya kazi. Muhanga amesema Uganda inapoteza takribani dola bilioni 1.6 kwa mwaka kutokana na foleni za magari, huku baadhi ya wakazi wakilazimika kuamka saa 10 alfajiri (4:00 asubuhi) ili waweze kufika kazini saa 2 asubuhi (8:00) . “Kampala haiwezi kuishiwa, haiwezi kubadilishwa, haiwezi kuendelez...
Na Angela Sebastian ;Kyerwa Mbunge wa Kyerwa, Khalid Nsekela, ameahidi kushirikiana na Halmashauri pamoja na wadau wa elimu kutatua changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama katika Shule ya Sekondari Kimuli, ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda mwingi kujisomea badala ya kutembea hadi saa nne kufuata maji. Ahadi hiyo imekuja wakati wa afla ya utoaji tuzo kwa walimu na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kidato cha sita 2026, licha ya shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma, ambapo katika matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2026 ilishika nafasi ya kwanza wilayani,ya kwanza kwa shule za Serikali kimkoa na ya pili kimkoa kwa shule zote. Kimuli inakabiliwa pia na changamoto ya ukosefu wa ofisi za walimu na mabweni, hali inayowalazimu baadhi ya wanafunzi kulala katika vyumba vya madarasa visivyo na madirisha lakini wanafanya vizuri katika masomo yao. Kwa niaba ya Mbunge, Nekmia Nguma Katibu wa Mbunge-Kitengo cha Mahusiano, amesema Nsekela amewapongeza wanafunzi na...