Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

NACTVET: WAPISHI WA WORLDSKILLS WAWE MABALOZI WA UKARIMU AFCON 2027

  Kuelekea fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, washiriki wa fani ya upishi katika Mashindano ya Kitaifa ya Ujuzi WorldSkills Tanzania 2026 wametakiwa kujiandaa kuwa mabalozi wa utalii na ukarimu wa Tanzania kupitia umahiri wao wa kupika. Wito huo umetolewa leo Agosti 22,2026 na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Bi. Bernadetta Ndunguru, alipotembelea mashindano yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga. Ndunguru amesema washiriki hao tayari wameonesha kiwango cha juu cha taaluma na wanapaswa kujiona kama wapishi wakubwa watakaokuwa sehemu ya kuipokea Afrika wakati Tanzania itakapokuwa mwenyeji wa AFCON 2027. Kwa mujibu wa Ndunguru, ubora wa huduma za chakula na ukarimu vinatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya taswira ya Tanzania mbele ya maelfu ya wageni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika. "Niwahimize vijana muendelee kuboresha ujuzi wenu na kutumia fursa ya WorldSkil...
Recent posts

RAIS SAMIA: JNHPP YAKAMILIKA, ATOA AGIZO LA TAHADHARI YA MVUA NA UHIFADHI WA VYANZO VYA MAJI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kila kitu katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) kimekamilika na kinafanya kazi, akieleza kuwa kukamilika kwa mradi huo ni fahari kubwa kwa Taifa na uthibitisho kwamba ndoto ya kuwa na mradi mkubwa wa kuzalisha umeme imetimia. Rais Samia amesema hayo leo Agosti 22, 2026, wakati wa hafla ya uzinduzi wa JNHPP iliyofanyika Rufiji mkoani Pwani, ambapo amezindua Kituo cha Kuzalisha Umeme, kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme, pamoja na kukagua tuta kuu na kituo cha kupokea na kusafirisha umeme kwenda kwenye Gridi ya Taifa. Amesema Desemba 22, 2022 alifika katika eneo hilo kushuhudia kufungwa kwa njia ya kugeuza maji ya Mto Rufiji na kuanzishwa rasmi kwa ujazaji wa maji katika bwawa, wakati huo ujenzi wa mradi huo ukitarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka mitatu. Kwa mujibu wa Rais Samia, kwa neema ya Mungu, bwawa hilo lilijaa ndani ya mwaka mmoja na nusu na kuanza majaribio ya uzalishaji ...

RAIS SAMIA AMPONGEZA HAYATI MWALIMU NYERERE KWA MAONO YA KUTUMIA RUFIJI KUZALISHA UMEME

 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amempongeza na kumshukuru Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa maono yake ya muda mrefu ya kutumia Mto Rufiji kuzalisha umeme wa uhakika kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya Tanzania, akisema utekelezaji wa wazo hilo umefikia hatua ya kihistoria baada ya kukamilika na kuzinduliwa kwa Kituo cha Uzalishaji wa Umeme cha Julius Nyerere chenye uwezo wa MW 2,115. Akizungumza leo Agosti 22, 2026 wakati wa kuzindua kituo hicho, Rais Samia amesema maono ya Mwalimu Nyerere yaliendelezwa na viongozi wa awamu zilizofuata, waliokuwa na dhamira ya kuhakikisha wazo hilo linaendelea kuwa sehemu ya safari ya maendeleo ya taifa. Amesema pamoja na Mwalimu Nyerere, anawashukuru Rais wa Awamu ya Pili, Hayati Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, na Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kuendeleza na kuenzi maono hayo. Rais Samia amesema safari ya mradi huo haikuwa...

NDEJEMBI:JNHPP KUSAMBAA UMEME KOTE NCHINI

 SERIKALI imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha umeme unaozalishwa katika Kituo cha Julius Nyerere (JNHPP) unafika kwa uhakika katika maeneo mbalimbali nchini, baada ya kukamilisha na kuendelea na miradi mikubwa ya njia za kusafirisha umeme. Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema uwekezaji huo ni sehemu muhimu ya kuhakikisha ongezeko la uzalishaji wa umeme linaenda sambamba na uwezo wa gridi ya taifa kupokea na kusafirisha umeme huo kwa ufanisi. Ndejembi ameyasema hayo leo Agosti 22, 2026, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere, kilichozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Amesema Serikali inatambua kuwa kuongeza uzalishaji pekee hakutoshi, kwa kuwa umeme huo unahitaji njia imara za kuusafirisha kutoka kwenye vituo vya uzalishaji hadi maeneo mbalimbali nchini. “Mheshimiwa Rais, hata hivyo, tunatambua kwamba kuongeza uwezo wa uzalishaji pekee haitoshi. Lazima tuwe na mtandao wenye uwezo wa kupo...

MKUU WA MKOA AZINDUA 'INNOIP TANZANIA': WABUNIFU 5,000 NA WANAWAKE KUNUFAIKA

Na MASHAKA MHANDO, Tanga SERIKALI imezindua rasmi programu mpya ya kitaifa ijulikanayo kama InnoIP Tanzania, inayolenga kuwasaidia wabunifu zaidi ya 5,000 nchini kulinda haki zao za miliki bunifu kisheria na kuzigeuza kuwa biashara zinazoingiza fedha na kutengeneza ajira, ili kuepuka wizi wa mawazo unaowaathiri wabunifu wengi wazawa. Uzinduzi huo wa kihistoria umefanywa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian Leo Augosti 22 wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi, na Ubunifu yanayoendelea katika viwanja vya Usagara jijini Tanga, hafla iliyobebwa na kaulimbiu isemayo; "Kutoka Wazo hadi Fursa za Miliki Bunifu: Kulinda Ubunifu, Kujenga Thamani na Kuharakisha Ubiasharishaji". Akihutubia mamia ya wadau wa sekta ya sayansi na ubunifu, Mkuu wa Mkoa alisema Tanzania lazima ihakikishe ubunifu wa ndani unalindwa na kuunganishwa na masoko makubwa, ili kuepuka hasara inayosababishwa na wabunifu kuweka wazi mawazo yao mapema mno kwa umma kabla ya kuyalin...

MAPACHA WALIOUNGANA WALIOGEUZA UPEKEE WAO KUWA NGUVU

 Abigail “Abby” Loraine Hensel na Brittany Lee Hensel ni mapacha walioungana tangu kuzaliwa, waliozaliwa tarehe 7 Machi 1990 katika jimbo la Minnesota, Marekani. Wana hali nadra ya kitabibu inayojulikana kama dicephalic parapagus conjoined twins—wakiwa na vichwa viwili lakini mwili mmoja. Licha ya kushirikiana mwili mmoja, kila mmoja ana utu, fikra na uwezo wake wa kufanya maamuzi. Kila mmoja pia ana moyo, mapafu, tumbo, uti wa mgongo na mfumo wake wa fahamu, huku wakishirikiana sehemu nyingine za mwili. Abby hudhibiti zaidi upande mmoja wa mwili, na Brittany hudhibiti upande mwingine. Kutokana na hali hiyo, walijifunza tangu utotoni kushirikiana kwa kiwango cha hali ya juu katika shughuli za kila siku, ikiwemo kutembea, kukimbia, kuogelea, kuendesha baiskeli, kucheza piano na hata kuendesha gari. Walilelewa katika mji wa New Germany, Minnesota, ambako wazazi wao waliwahimiza kuishi maisha ya kawaida bila kuona hali yao kama kikwazo. Walisoma kama watoto wengine na baadaye wakahiti...