Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

HII HAPA MIKOA 14 NCHINI ITAKAYOKUMBANA NA EL NIÑO

 WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Prof. Palamagamba Kabudi, ameitaka mikoa 13 iliyopewa tahadhari kujiandaa mapema kukabiliana na madhara yanayoweza kusababishwa na mvua za El Niño. Akizungumza kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El Niño, Prof. Kabudi amesema mikoa hiyo inapaswa kuhakikisha maandalizi yanafanyika kwa wakati ili kupunguza madhara kwa wananchi na mali zao. Mikoa iliyotajwa ni Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu,Morogoro, Kigoma, Tanga, Pwani, Ruvuma, Mara, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Dar es Salaam. Prof. Kabudi pia amesisitiza umuhimu wa wananchi kupata na kuzingatia taarifa za tahadhari zinazotolewa na mamlaka husika, huku akivitaka vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa maandalizi na hatua za kuchukua. Amesema Serikali, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, inaendelea kuratibu maandalizi kwa kushirikisha serikali za mikoa, serikali za mitaa na jamii ili kuhak...
Recent posts

SERIKALI YAFAFANUA SHILINGI BILIONI 730 ZA MPANGO WA KUKABILI EL-NIÑO

 SERIKALI imefafanua kuwa makadirio ya Shilingi bilioni 730 yanayotajwa katika Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El-Niño si fedha zilizotengwa na Serikali kwa matumizi ya moja kwa moja, bali ni makadirio ya rasilimali zinazohitajika kutekeleza mpango huo kwa kushirikisha Serikali, taasisi, sekta binafsi, mashirika ya kitaifa na kimataifa pamoja na wadau wengine.  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Prof. Palamagamba Kabudi, amesema mpango huo umeandaliwa kufuatia utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wa Agosti 18, 2026, uliotabiri uwepo wa El-Niño yenye nguvu inayoweza kusababisha mvua kubwa, mafuriko, maporomoko ya ardhi, magonjwa ya mlipuko kwa binadamu na wanyama pamoja na madhara kwa miundombinu, makazi na shughuli za kiuchumi.  Amesema mpango huo umeandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikisha Wizara, Idara na Taasisi za Serikali, Mikoa na Halmashauri, mashirika ya kitaifa na kimataifa, ...

JWTZ LATAJA MCHANGO WA MIAKA 62, LAVUTIA USHIRIKIANO WA MAJESHI YA EAC KATIKA KUWA HUDUMIA WANANCHI

 Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeadhimisha miaka 62 tangu kuanzishwa kwake Septemba 1, 1964, huku maadhimisho hayo yakifanyika sambamba na kufungwa kwa Wiki ya Sita ya Ushirikiano wa Kijeshi na Kiraia ya Majeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Viwanja vya Gofu vya Lugalo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Jacob John Mkunda, amesema historia ya JWTZ imejengwa kupitia utekelezaji wa majukumu ya kulinda taifa pamoja na kushiriki katika shughuli zinazogusa maisha ya wananchi. Jenerali Mkunda amesema JWTZ limeendelea kuimarisha uwezo wa askari wake ili kukabiliana na majukumu mbalimbali ya kitaifa, huku misingi ya uzalendo, weledi na uwajibikaji ikiendelea kuwa sehemu ya utendaji wa jeshi hilo. Kwa mujibu wa Jenerali Mkunda, maadhimisho hayo yamekuja wakati ambapo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinaendelea kutafuta njia za kuongeza ushirikiano wa majeshi yao, si katika masuala ya kijeshi...

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA MRADI WA VIJANA WA VIZIMBA VYA SAMAKI HALMASHAURI YA BUKOBA

 Na Angela Sebastian, Bukoba MWENGE wa Uhuru mwaka 2026 umekagua na kupongeza mradi wa vijana 47 wanaojishughulisha na ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba, unaotekelezwa na vikundi saba katika Kata ya Kemondo, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera.  Mradi huo upo chini ya programu ya Jenga Kesho Iliyobora (BBT-Uvuvi), inayolenga kuwawezesha vijana na wanawake kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi kupitia sekta za kilimo, mifugo na uvuvi. Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026, Wazo Mwang’onda, alimpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuwawezesha vijana kupitia miradi ya kiuchumi, huku akiipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba kwa usimamizi mzuri wa mradi huo.  Alisema Serikali imeendelea kuhakikisha vikundi vinavyonufaika vinapatiwa nyenzo za kazi, mafunzo kwa vitendo, mikopo yenye masharti nafuu pamoja na pembejeo zinazohitajika katika shughuli za uvuvi na ufugaji wa samaki. “Tumeukagua mradi huu na kuona kuwa ni mzuri,...

BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI*

 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei za bidhaa za mafuta kwa mwezi Septemba 2026. Bei ya petroli imeshuka kwa Shilingi 102 kwa lita, huku bei ya dizeli ikishuka kwa Shilingi 101 kwa lita. Bei hizo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 2 Septemba 2026, saa 6:01 usiku. EWURA inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia, ambapo mabadiliko ya bei yanaendelea kuathiriwa pamoja na mambo mengine na hali ya kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati. Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015, bei za mafuta zinaendelea kupangwa kwa kuzingatia mfumo wa soko. Wafanyabiashara wote wa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zisizozidi bei elekezi, na wananchi wanashauriwa kutoa taarifa EWURA kwa kituo chochote cha mafuta kitakachouza zaidi ya bei elekezi.

WAZIRI WA ULINZI NA JKT AKUTANA NA VIJANA WALIOSHIRIKI UJENZI WA IKULU YA CHAMWINO

 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb),Tarehe 01 Septemba 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) walioshiriki katika ujenzi wa mradi wa kihistoria wa Ikulu ya Chamwino, jijini Dodoma. Mazungumzo hayo yalilenga kuwasikiliza vijana hao, kuwapongeza na kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa katika kutekeleza ujenzi wa Ikulu ya Chamwino, ambayo ni moja ya alama muhimu za Taifa na Ofisi ya Juu katika mfumo wa Utawala na Uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akizungumza na vijana hao, Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt. Rhimo Nyansaho, amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatambua na kuthamini mchango, uzalendo na kujituma kwa vijana hao katika utekelezaji wa mradi huo wa kihistoria. Dkt. Nyansaho amesema Serikali inatambua uvumilivu, nidhamu na kujitolea kwa vijana hao, ambao walishir...