Na Dawati la Habari Polisi;Mwanza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura, kwa hatua ya kuirejesha timu ya Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027. Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Agosti 9, 2026, wakati akifungua rasmi Mashindano ya Polisi Jamii Cup Kanda Namba 7 yanayofanyika katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. Amesema kurejea kwa Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ni hatua muhimu inayopaswa kuungwa mkono, huku akisisitiza umuhimu wa michezo katika kuimarisha mahusiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi. “Nitumie nafasi hii kumpongeza IGP Camillus Wambura kwa hatua ya kuirejesha timu ya Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ya NBC. Hii ni hatua nzuri na muhimu kwa Jeshi la Polisi na tunapaswa kuiunga mkono timu yetu ili iweze kufanya vizuri,” alisema Mtanda. Mkuu huyo wa Mkoa amesema michezo ni kiungo muhimu katika kujenga uaminifu, umoja na mshikamano kati ya Jeshi la Polisi na jamii, ak...
Na Mashaka Mhando, MWANZA NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (maarufu kama Mwana FA au 'Falsafa'), ameacha historia mpya jijini Mwanza baada ya kufanya maajabu jukwaani akiungana na kundi lake la zamani la East Coast Team. Tukio hilo la kukata na shoka limejiri usiku wa Agosti 8, 2026, katika ukumbi wa Climax uliopo Rock City Mall, wakati wa Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 30 ya muziki wa Bongo Fleva, ambapo Mhe. Mwinjuma alihudhuria kama Mgeni Rasmi. Badala ya kuishia kutoa hotuba za kiserikali pekee, Mhe. Mwinjuma aliwapa mashabiki suprise ya kufa mtu alipopanda jukwaani na kuimba sambamba na wakali wenzake wa East Coast Team waliotikisa anga la muziki miaka ya nyuma, akiwemo Crazy GK, AY, na Snare. Muunganiko huo wa East Coast Team jukwaani uliamsha shangwe za mashabiki na kukumbusha enzi za dhahabu za muziki huo, huku Mwana FA akidhihirisha kuwa makali yake ya kuchana mistari bado yako palepale licha ya kubeba majukumu mazito ya ki...