Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

NAIBU MTENDAJI SUMA JKT ATEMBELEA BANDA LA MALIASILI NANE NANE

📌Aipongeza Wizara kwa kushirikisha wadau wa mazao ya misitu na nyuki 📌Asema kazi ya uhifadhi inafanyika kwa weledi mkubwa *Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma*  NAIBU Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi leo Agosti 03, 2026 ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kujionea wadau mbalimbali wanaoshirikiana na wizara kwenye uzalishaji wa bidhaa za misitu na asali na kuipongeza wizara kwa kushirikiana na wadau hao. Brigedia Jenerali Shija amesema wadau hao wamekuwa wakifanya kazi nzuri katika kuhakikisha mazao hayo ya bidhaa za nyuki ikiwemo asali, miche ya miti na mazao ya misitu yanakuwa na soko ndani na nje ya nchi. Brigedia Jenerali Shija alipata wasaa wa kutembelea wanyamapori hai waliopo kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kama njia mojawapo ya kuutangaza utalii wa ndani.
Recent posts

BALOZI DKT. NCHIMBI: USHIRIKA WENYE UADILIFU NI MSINGI WA UCHUMI IMARA

 MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika nchini ili kuhakikisha vinaendeshwa kwa uwazi, uwajibikaji na uadilifu, akisisitiza kuwa ushirika wenye misingi hiyo ndiyo nguzo muhimu ya kukuza uchumi jumuishi na kuvutia uwekezaji. Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo leo katika Siku Maalum ya Ushirika, iliyofanyika ndani ya Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane 2026 kwenye Viwanja vya John Malecela, Nzuguni mkoani Dodoma, ambapo pia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha sekta ya ushirika ili iwe kichocheo cha maendeleo ya kilimo na uchumi wa Taifa. Amesema Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) linapaswa kuendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyama vya ushirika ili kudhibiti ubadhirifu wa rasilimali, kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na kuongeza uwazi katika uendeshaji wa vyama hivyo. "Ushirika wenye uadilifu unajenga iman...

BALOZI DKT. NCHIMBI APONGEZA MCHANGO WA TADB KUIMARISHA KILIMO NA VIWANDA VYA MAFUTA

 MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) katika Maonesho ya 33 ya Nanenane na kujionea mchango wa benki hiyo katika kuimarisha uzalishaji wa kilimo, kuongeza thamani ya mazao na kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo nchini. Akiwa ameambatana na Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, Makamu wa Rais alipokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Mipango, Ushauri na Mahusiano ya Taasisi wa TADB, Mkani Waziri, ambaye alisema benki hiyo imeendelea kutoa mikopo na huduma mbalimbali za kifedha zinazowawezesha wakulima, wafugaji, wavuvi na wawekezaji kuongeza uzalishaji, tija na usalama wa chakula nchini. Katika ziara hiyo, Mkurugenzi wa Kiwanda cha Mafuta ya Kula cha Trolle Meesle, Daniel Amulike, ameeleza namna ufadhili wa TADB ulivyowezesha kampuni yake kujenga kiwanda cha kisasa na kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula kwa kiwango kikubwa. "Baada ya kufadhiliwa na TADB, tumetoka kuzalisha tani 30 kwa mwezi hadi kufikia tani 624 za ...

TUMEANZA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA 2050 TUKIWA NA MISINGI MIZURI YA KIUCHUMI - RAIS SAMIA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania imeanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ikiwa na misingi mizuri ya kiuchumi, hali inayoweka mazingira bora ya kufikia malengo ya maendeleo yaliyowekwa kwa kipindi cha miaka 25 ijayo. Rais Samia ameyasema hayo leo Jumatatu Agosti 03, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa nyenzo za utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na kushiriki katika mkutano wa mazungumzo maalum na sekta binafsi kuhusu utekelezaji wa dira hiyo. Amesema uchumi wa Tanzania umeendelea kuwa himilivu, mfumuko wa bei umedhibitiwa, uwekezaji umeongezeka na nchi imeendelea kujenga nafasi yake kama lango muhimu la biashara kwa nchi za Afrika Mashariki, Ukanda wa Maziwa Makuu na Kusini mwa Afrika. “Ni muhimu kutambua tumeanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 tukiwa na msingi mzuri wa kiuchumi. Uchumi wetu umeendelea kuwa himilivu, mfumko wa bei unadhibitiwa, uwekezaji umeongezek...

MBUNGE BULAYA AZINDUA 'OPERATION GAWA PHOTOCOPY' KUIMARISHA ELIMU BUNDA MJINI

 Na,George Marato-Bunda MBUNGE wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Bulaya, amezindua rasmi programu maalumu ya "Operation Gawa Photocopy Bunda Mjini", inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi kupitia upatikanaji wa nakala za masomo, mitihani na nyenzo nyingine muhimu za elimu. Uzinduzi wa programu hiyo ni sehemu ya juhudi za Mbunge huyo kuendelea kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Sekta ya Elimu pamoja na kuwekeza katika sekta ya elimu kwa kuondoa baadhi ya changamoto zinazowakabili wanafunzi na walimu, hususan upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia vinavyohitajika katika mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Bulaya amesema elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya jamii na taifa, hivyo kuna umuhimu wa kuhakikisha kila mwanafunzi anapata fursa sawa ya kujifunza bila kukwamishwa na ukosefu wa nyenzo muhimu. Amesema programu ya "Operation Gawa Photocopy Bunda Mjini" itasaidia kupunguza gharama ambazo w...

MATUNDA YA ZIARA YA RAIS SAMIA URUSI YAANZA KUONEKANA

   ….Kampuni ya Betaren yaanza kuingiza mbegu bora aina ya Bombadier, Daha, Bazik na Krechet Na Mwandishi Wetu Ziara ya kikazi ya siku tatu aliyofanya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi Juni 3 mwaka huu imeanza kulipa baada ya kampuni za kutoka nchini humo ikiwemo Betaren kuja kuwekeza kwenye mbegu za kisasa za mazao. Kampuni ya Sky Business and Investment Company Ltd imeingia ubia na kampuni hiyo yenye asili ya Urusi ya Betaren kwaajili ya kusambaza mbegu bora za kisasa, mbolea na viuatilifu kwa wakulima Tanzania. Aina ya mbegu ambazo kampuni hiyo imeanza kuingiza nchini ni pamoja na mbegu aina ya Bombadier, Daha, Bazik na Krechet ambazo ziko kwenye hatua za mwisho kupata kusajili. Akizungumza mara baada ya kutembelea banda la kampuni hiyo kwenye maonesho ya nane nane mkoani Dodoma, Mbunge wa Kisarawe, Seleman Jafo alisema ujio wa kampuni hiyo kuwekeza nchini ni matokeo ya diplomasia ya uchumi ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyetembelea Urusi hivi karibuni. Alisema wawekezaj...