Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

ESPJ II: VIWANGO VIPYA VYA KAZI KUJA KUZIBA PENGO LA UJUZI KWA WAHITIMU WA TVET

Wahitimu wa vyuo vya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania wanatarajiwa kuwa na ujuzi unaoendana zaidi na mahitaji ya soko la ajira, kufuatia hatua inayochukuliwa kupitia Mradi wa ESPJII wa kuandaa viwango vya Kazi. Mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia unalenga kukuza viwango vya ujuzi nchini kwa kuimarisha mifumo ya mafunzo, kuwajengea uwezo walimu pamoja na kuboresha matumizi ya teknolojia katika sekta ya TVET. Akizungumza kuhusu mchakato huo leo Agosti 27,2026 Mratibu wa Mradi huo Bw. Aggrey Mleli amesema maandalizi ya miongozo ya Viwango vya kazi ni hatua muhimu katika kuhakikisha mafunzo yanayotolewa katika taasisi za TVET yanaendana na mahitaji halisi ya ulimwengu wa kazi. Mleli amesema kikao cha wadau kilichofanyika ni sehemu ya hatua ya pili ya kupitia na kukusanya maoni kutoka kwa wadau kabla ya miongozo hiyo kupelekwa katika ngazi za juu kwa ajili ya kuidhinishwa na kuanza kutumika katika maandalizi ya kuandaa vi...
Recent posts

MKUU WA WILAYA YA ILALA ALIPONGEZA JESHI LA MAGEREZA KWA MABADILIKO CHANYA

 Na S'SGT. Ponsiano Lindi - DSM Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amempongeza Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, kwakazi kubwa anayoifanya katika kuleta mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza, akieleza kuwa ni miongoni mwa viongozi wachache waliofanikiwa kuleta mabadiliko ndani ya muda mfupi. Mhe. Mpogolo, ametoa pongezi hizo, Agosti 27, 2026, wakati akishiriki zoezi la upandaji miti katika eneo la Kambi ya Magereza Mvuti, Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam. "Natoa pongezi za dhati kabisa kwa Jeshi la Magereza kwa kubuni na kuanzisha Kampeni ya “Magereza Nuru ya Mabadiliko”, kwa kushirikiana na TBC, ni kampeni muhimu katika kuufahamisha umma kuhusu kazi kubwa inayofanywa na Jeshi la Magereza katika kuwabadilisha wafungwa na kuwaandaa kurejea katika jamii wakiwa raia wema na wenye tija" amesema Mhe. Mpogolo Aidha, Mhe. Mpogolo, amesema Jeshi la Magereza lina uwezo wa kubadilisha maisha ya wafungwa kupitia programu mbalimbali za urekebishaj...

WAZIRI KIKWETE: SOMALIA IMEKUJA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA MATUMIZI YA MIFUMO YA KIDIJITARI KATIKA UTUMISHI WA UMMA NCHINI TANZANIA

Na Lusungu Helela, Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini. Mhe. Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi Jama Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu. Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi. “Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokif...

FDH YAIPONGEZA TACAIDS KWA KUJUMUISHA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

Shirika la Foundation for Disabilities Hope (FDH) limeipongeza Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) kwa juhudi zake za kuhakikisha watu wenye ulemavu wanajumuishwa kikamilifu katika programu na mikakati ya mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) nchini. Mkurugenzi Mtendaji wa FDH, Maiko Salali, amesema ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika mapambano dhidi ya UKIMWI ni muhimu kwa kuwa kundi hilo ni sehemu ya jamii na linahitaji kupata elimu, taarifa na huduma za afya zinazozingatia mahitaji yao. Amesema TACAIDS imekuwa ikishirikisha watu wenye ulemavu katika programu mbalimbali za kuongeza uelewa kuhusu VVU na UKIMWI, hatua ambayo imewawezesha kushiriki kikamilifu katika juhudi za kitaifa za kudhibiti maambukizi. “Tunapongeza sana TACAIDS kwa namna ambavyo imekuwa ikiwajumuisha watu wenye ulemavu katika mapambano dhidi ya UKIMWI. Tume imekuwa ikiweka mikakati ya kuhakikisha hakuna Mtanzania anayeachwa nyuma,” amesema Salali. Salali amesema pamoja na juhudi hiz...

RAIS SAMIA ATEUA NA KUHAMISHA WAKUU WA MIKOA, MAKATIBU TAWALA

  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa katika mikoa mbalimbali nchini. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, mabadiliko hayo yanahusisha uteuzi wa Wakuu wapya wa Mikoa minne, uhamisho wa Wakuu wa Mikoa sita pamoja na mabadiliko katika nafasi za Makatibu Tawala wa Mikoa. Wakuu wapya wa Mikoa Katika uteuzi huo, CP. Salum Rashid Hamduni, aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Alexander Pastory Mnyeti ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, huku Stanslaus Haroon Nyongo akiteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Aidha, Jumanne Abdallah Sagini ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya. Wakuu wa Mikoa waliohamishwa Kwa upande wa uhamisho, Martine Reuben Shigela amehamishwa kutoka Mkoa wa Geita na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara. Said Mohamed Mtanda amehamishwa kutoka Mwanza kwenda Simiyu, akichuku...

TUME YA UMWAGILIAJI NA TUME YA TAIFA YA MIPANGO ZAUNGANISHA NGUVU KUIMARISHA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

📍Dodoma, Tanzania Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imekutana na Tume ya Taifa ya Mipango,Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji; kwa lengo la kujadili namna bora ya kuoanisha mipango, miradi na utekelezaji wa shughuli zake ili kuongeza tija katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Akizungumza katika kikao hicho, Naibu Katibu Mtendaji wa Menejimenti ya Utendaji na Tathmini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango, Bw. Sosthenes Kewe, amesema ni umuhimu kwa miradi ya Umwagiliaji kuwa na matokeo yanayoonekana kwa jamii pamoja na kuzingatia vipaumbele vya taifa.  Ameeleza kuwa ni muhimu taasisi zote kuhakikisha miradi yao inaendana na mipango ya maendeleo ya muda mfupi na muda mrefu, huku ikionesha uwajibikaji na kuinua uchumi wa wananchi  “Tunapaswa kuzingatia miradi yenye matokeo zaidi kwa jamii, inayotanguliza vipaumbele vya taifa na kuonesha matokeo halisi yanayoboresha maisha ya Watanzania,” amesisitiza. Amesema, sekta ya Umwagiliaji ...