Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

CHATANDA: NDEJEMBI ANA UWEZO MKUBWA WA KUMSAIDIA MAJUKUMU RAIS WETU

NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi, ameelezwa kuwa kiongozi mahiri, muadilifu na mzalendo, mwenye uwezo wa kumsaidia majukumu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, Agosti 30, 2026, ofisini kwake Dodoma, siku moja baada ya kukamilika uapisho wa kiongozi huyo, Ikulu ya Chamwino, Dodoma. Chatanda ameeleza, Ndejembi ni kiongozi wa vitendo na katika majukumu aliyoaminiwa tangu akiwa Mkuu wa wilaya ya Kongwa, Mbunge, Naibu Waziri na Waziri kamili katika wizara mbalimbali. "Kule Kongwa Dodoma akiwa Mkuu wa wilaya alifanya kazi nzuri na katika kilimo alisimamia kwa mafanikio makubwa kampeni yake aliyoiita ONJAKO yaani Ondoa Njaa Kongwa. Alihimiza wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame kama mtama, mihogo, ufuta na alizeti ili kuwaepusha wananchi na kadhia ya njaa," amesema Chatanda. Ameongeza kuwa, kampeni ya ONJAKO ilipokelewa vizuri na wakulima wa Kongwa kut...
Recent posts

ELIMU NA HAMASA NZURI YAWAFANYA WAZAZI NA WALEZI KATA YA MWISENGE KUHAKIKISHA WATOTO WAO WANAPATA CHANJO YA POLIO.

Na Mwandishi wetu Jovina Massano Musoma. ELIMU na hamasa nzuri kwa jamii yasababisha wazazi,watoto na walezi  Kata ya Mwisenge Manispaa ya Musoma mkoani Mara kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo ya Polio awamu ya tatu. Hayo yamesemwa na wazazi na walezi Agosti 30, 2026 katika mitaa na maeneo ya Ibada mara baada ya kufikiwa na timu ya utoaji chanjo. Wamesema kuwa wahamasishaji wakiwemo wenyeviti wa mitaa na taarifa zinazotolewa katika vyombo vya habari zimewafanya wamepata hamasa na uelewa mpana wa umuhimu wa chanjo hiyo. Wakizungumza kwa  Nyakati tofauti wamesema utoaji elimu mapema ni muhimu kwa kuwa inasaidia kupata taarifa na uelewa usahihi wa zoezi husika. Frank David afisa usafirishaji wa Mtakuja Kituo Cha mianzini ni miongoni mwa wazazi ambae nae mtoto wake ameweza kupata chanjo hiyo. Amesema hapo awali watu waliongea vibaya kuhusiana na chanjo ya Polio wengi walipata hofu lakini hivi sasa baada ya kupewa elimu kwa usahihi  imewapa ujasiri wa kuhakikisha watoto wa...

DKT. MWIGULU AWASILI KATAVI KUSHIRIKI JUBILEI YA MIAKA 25 YA JIMBO KATOLIKI LA MPANDA

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Agosti 30, 2026, amewasili Mpanda mkoani Katavi kuwa Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 25 ya Jimbo Katoliki la Mpanda. Maadhimisho hayo yanafanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari St. Mary, Mpanda, mkoani Katavi.

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MISA YA IBADA TAKATIFU KANISA KATOLIKI DODOMA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, pamoja na familia yake wameungana na waumini mbalimbali katika kushiriki Ibada ya Misa Takatifu ya Jumapili, katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Paulo wa Msalaba Jimbo Kuu Katoliki Dodoma. Tarehe 30 Agosti 2026.

SILLO:MICHEZO,BURUDANI NI NGUZO YA AFYA YA AKILI NA UFANISI KAZINI

 NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Daniel Sillo, amesema michezo na burudani ni nguzo muhimu katika kupunguza msongo wa mawazo, kuimarisha utimamu wa akili na kuongeza ufanisi katika kazi. Mhe. Sillo ameyasema hayo jana Agosti 29, 2026, wakati wa tamasha la NMB Bunge Bonanza lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlini jijini Dodoma, likiwakutanisha zaidi ya washiriki 1,000 kutoka Bungeni, Wizara 14 na Taasisi 10, wakiwemo wadau na wadhamini wa tamasha hilo. Bonanza hilo lililobeba kaulimbiu “Pamoja AFCON 2027: Tanzania Tupo Tayari”, limeelezwa kuwa si tu fursa ya kufanya mazoezi na kujenga afya, bali pia ni jukwaa la kuimarisha mshikamano, kufahamiana na kujenga umoja miongoni mwa watumishi na viongozi kutoka taasisi mbalimbali. “Michezo ni fursa ya kipekee inayotuwezesha kufahamiana, kujenga mshikamano na kuimarisha umoja wetu. Bunge lipo tayari kushirikiana na Serikali kuhakikisha michuano ya AFCON 2027 inafanyika kwa ubora wa hali...

MKUU WA MKOA WA KAGERA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MWENGE WA UHURU KUIBUA FURSA ZA KIUCHUMI

 NA Angela Sebastian; MULEBA Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahya Ramadhani Kido, ameeleza kuwa Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026 utakuwa chachu ya kuimarisha maendeleo, amani na mshikamano mkoani humo, huku akiwataka wananchi kuutumia mwenge huo kuibua fursa za kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa jana wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika Kijiji cha Nyakabango, Wilaya ya Muleba, ambapo Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Mohamed Gombati, alikabidhi mwenge huo kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Steven Ndanki. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Michael Mwang’onda, alizitaka taasisi za manunuzi na Halmashauri zote nane za Kagera kutenga asilimia 30 ya bajeti ya manunuzi kwa ajili ya vikundi vilivyosajiliwa vya vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu. Alisema hatua hiyo itasaidia makundi hayo kupata fursa za kiuchumi, mikopo na mitaji ya kuanzisha miradi itakayoongeza kipato na kupunguza umaskini. A...