Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

KATIBU TAWALA MKOA WA MARA AONGOZA HAFLA YA KUMPONGEZA MKUU WA MKOA BRIGEDIA JENERALI EVANS MTAMBI.

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Kusaya, leo tarehe 11,septemba 2026, ameongoza hafla ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Brigedia Jenerali Evans Alfred Mtambi, kufuatia kupandishwa cheo chake cha kijeshi kutoka Kanali hadi Brigedia Jenerali. Hafla hiyo imefanyika katika viunga vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali, watumishi wa umma, viongozi wa dini pamoja na wadau wengine wa mkoa. Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Kusaya, ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara na kuwaamini viongozi wenye uwezo na uadilifu. Amesema kupandishwa cheo kwa Mkuu wa Mkoa ni ishara ya kutambua weledi, uhodari, utii na utumishi wake uliotukuka katika kulitumikia taifa. “Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara. Kupandishwa cheo kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ni heshima kubw...
Recent posts

TANZANIA, MISRI ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KATIKA ULINZI NA TEKNOLOJIA ZA ANGA

 Tanzania na Misri zimejadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika sekta ya ulinzi na teknolojia za anga, ikiwemo kubadilishana uzoefu, maarifa na teknolojia kwa manufaa ya pande zote. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji wa Kijeshi na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Luteni Jenerali Ashraf Salem Zaher, jijini El Alamein, Misri. Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 10, Septemba 2026, wakati Tanzania ikishiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Anga na Teknolojia za Anga za Juu ya El Alamein (ELIAS). Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamejadili fursa za kuendeleza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Misri katika maeneo ya ulinzi na teknolojia za anga, pamoja na umuhimu wa kubadilishana uzoefu, maarifa na teknolojia katika maeneo yenye maslahi ya pamoja. Ushiriki wa Tanzania katika Maonesho ya ELIAS unalenga pia kujenga na kuimarisha mahusi...

WAZIRI WA ULINZI NA JKT ZIARANI MISRI, AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA ULINZI NA AMIRI JESHI MKUU WA MISRI

 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 10 Septemba 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji wa Kijeshi na Amiri  Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mheshimiwa Luteni Jenerali Ashraf Salem Zaher, jijini El Alamein, Misri. Mazungumzo hayo ya viongozi hao waandamizi yalilenga kujadili na kuimarisha maeneo mbalimbali ya ushirikiano baina ya Wizara za Ulinzi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, ambazo ni nchi rafiki zenye uhusiano wa muda mrefu na wa kihistoria. Aidha, viongozi hao walijadili masuala mbalimbali ya kiulinzi na usalama, pamoja na utekelezaji wa mambo yaliyojadiliwa wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mheshimiwa Abdel Fattah el-Sisi, nchini Tanzania mnamo  Julai 18, 2026, ambapo alifanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mazungumzo hayo yalisisitiza umuhi...

WAITARA:JKT NI MUHIMU KUWAANDA VIJANA KUKABILIANA NA MAISHA

  Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini na mzazi wa mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mwita Waitara, amelipongeza Jeshi hilo kwa kuendelea kuwajenga vijana katika misingi ya uzalendo, nidhamu, uwajibikaji na kujitegemea, akisema mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa katika kuwaandaa vijana kukabiliana na changamoto za maisha. Waitara ameyasema hayo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, Operesheni Linda Amani na vijana waliojitolea, iliyofanyika katika Kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mlandizi, mkoani Pwani, ambapo amesema vijana wanaomaliza mafunzo hayo wanapaswa kutumia ipasavyo maarifa na stadi walizopata ili kujiajiri, kushiriki katika shughuli za maendeleo na kuwa raia wema wenye mchango kwa Taifa. Aidha, Waitara amehimiza matumizi sahihi ya teknolojia ya Akili Bandia (AI) katika kuwaandaa vijana kwa mazingira ya sasa, akisema teknolojia hiyo inaweza kutumika kuwaongezea maarifa na stadi mbalimbali zitakazowasaidia kukabiliana na mahit...

OFISI ZINAZOTEMBEA ZA TRA ZINAVYORAHISISHA HUDUMA KWA WANANCHI

 NA: DK. REUBENI LUMBAGALA Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatekeleza kwa vitendo mkakati wake wa kuwahudumia wananchi kwa kuhakikisha wanawapatia huduma bora na kwa urahisi kule walipo. Katika kutekeleza hilo, Februari 25, 2026, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Omar, akishirikiana na Kamishna Mkuu wa TRA, CPA Yusuph Mwenda, walizindua ofisi zinazotembea (mobile offices) Jijini Dar es Salaam ambazo ni magari yenye maofisa wa TRA na vifaa vya kazi, tayari kwa kuwahudumia wananchi. Kupitia ofisi hizo zinazotembea, maofisa hao wamekuwa wakiwafikia wateja na wananchi kwa kuwapa elimu na ushauri wa masuala ya kodi. Pia kufanya usajili na kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). Huduma nyingine ni kupata leseni za udereva, kutoa makadirio na namba za malipo ya kodi. Pia, wananchi wanapata elimu na ufafanuzi kuhusiana na mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi yaliyofanyika katika mwaka wa fedha 2026/2027. Kimsingi, ofisi hizo zimekuwa na manufaa kwani zinawafikia wananchi kule wal...

AWESO CUP 2026: JUKWA LA KUKUZA VIPAJI NA UWEKEZAJI PANGANI

 NA: DK. REUBENI LUMBAGALA  Michezo ni sekta muhimu inayotoa ajira kwa vijana wengi duniani. Kutokana na hilo, mipango madhubuti huwekwa ili kuhakikisha vijana wanapata ajira kupitia michezo na kuchangia maendeleo ya nchi. Tanzania si kisiwa. Kwa namna michezo ilivyobadili hali za maisha za watu wengi, hatuna budi kuipa msukuma sekta hiyo muhimu ili vijana wengi waweze kupata kipato. Mbunge wa Jimbo la Pangani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ameipa kipaumbele sekta ya michezo Jimboni kwake. Aidha, amedhamiria kutumia michezo kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji na biashara zinazopatikana wilayani Pangani ili wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wazitumie katika kukuza maendeleo. Kwa miaka mingi, Aweso amekuwa mfadhili wa mashindano mbalimbali ya michezo ili kuibua na kuendeleza vipaji vya vijana. Mei 16, 2026, Aweso alikuwa Mgeni Rasmi wa fainali ya mashindano ya Aweso Vijana Cup, yaliyoratibiwa na Jumuiya ya Vijana ya Chama Cha Ma...