Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasalimu Wananchi wa Mbuyuni, Wilayani Moshi waliokusanyika kumlaki akiwa katika ziara binafsi mkoani Kilimanjaro leo tarehe 01 Septemba 2026. Akiwasalimu wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Amesema kwa imani ya maombi ataweza kumsaidia kwa hekima na utii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Makamu wa Rais amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi. Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema: “Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,” kauli ambayo aliitoa pia mkoani Dodoma, kwa wananchi wa Chamwino, mara baada ya kuapishwa. Awali, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo alipokelewa na v...
Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde, amekutana na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mheshimiwa Marianne Young, jijini Dodoma, ambapo wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya madini na kuongeza fursa za uwekezaji kati ya Tanzania na Uingereza. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamejadili kwa kina maeneo ya uwekezaji katika sekta ya madini, uongezaji wa thamani ya madini nchini, pamoja na namna ya kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuwa chachu ya ukuaji wa uchumi jumuishi na wenye manufaa kwa wananchi. Mkutano huo pia umeangazia umuhimu wa kuendeleza mazingira yatakayowezesha ushirikiano na uwekezaji wenye tija katika sekta ya madini, huku Tanzania ikiendelea kutumia rasilimali zake za madini kama fursa ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi. Tanzania na Uingereza zimeeleza dhamira ya kuendelea kushirikiana katika maeneo yenye manufaa kwa pande zote mbili, kwa lengo la kuimarisha mahusiano ya nchi hizo na kukuza ustawi na maendeleo ya wananchi wa ma...