Wizara ya Katiba na Sheria, imeanza kutoa Huduma za Msaada wa Kisheria kwa wananchi wa Mkoa wa Njombe, 18 Septemba, 2026 kwa Lengo la kuhakikisha wananchi wote wanapata haki kwa wakati na Usawa. Akizungumza katika viwanja vya stendi ya zamani mjini Njombe, Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria ambaye pia ni mratibu wa zoezi la utoaji wa huduma za kisheria Geofrey Mwachai alisema kuwa huduma hizi zinatolewa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria Awamu ya Pili lengo kuu ikiwa ni kuwafikia wananchi wote na kuhakikisha wanapata haki zao. ‘’Wananchi wengi hawafahamu wapi wanaweza kupata haki zao ama namna gani wanaweza kuzitunza, ila kupitia Kampeni hii ya Msaada wa Kisheria awamu ya pili tutatoa elimu ya kisheria katika maeneo mbalimbali ikiwemo elimu ya haki, wajibu na uraia, ndoa, mirathi, ukatili wa kijinsia na matunzo ya Watoto ili kuwawezesha wananchi kutambua haki zao na pia kufahamu nini wafanye pale wanapodhulumiwa haki hizo”alisema Wak...
Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza matokeo ya Mitihani ya Kati Awamu ya Pili ya Taaluma ya Mnyororo wa Ugavi, ambapo watahiniwa 275 kati ya 528 waliofanya mitihani hiyo wamefaulu, sawa na asilimia 52.1. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Sept 18,2026 Jijini Dodoma wakati wa kutangaza matokeo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya wataalamu WA ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi, amesema jumla ya watahiniwa 567 walidahiliwa kufanya mitihani hiyo iliyofanyika kuanzia Agosti 30 hadi Septemba 4, 2026. "Kati yao, watahiniwa 528 walifanya mitihani, huku 39 wakishindwa kufanya kwa sababu mbalimbali". Amesema Mbanyi amesema watahiniwa 232, sawa na asilimia 43.9, wamepata nafasi ya kurudia baadhi ya masomo (referral), huku 21, sawa na asilimia 4.1, wakifeli na hivyo kulazimika kuanza upya masomo yao katika ngazi husika. "Tunawapongeza watahiniwa waliofaulu katika ngazi mbalimbali, wakiwemo waliokidhi sifa za kutunukiwa vyeti vya Professional Diploma,...