Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RAIS SAMIA AZINDUA MELI NNE, AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SGR, TABORA-KIGOMA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua meli nne mpya za mizigo katika Ziwa Tanganyika na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Tabora hadi Kigoma, yenye urefu wa kilomita 506. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua meli hizo leo Jul 20,2026 Mkoani kigoma ambapo amesema kuwa Serikali inaendelea kujenga mfumo jumuishi wa uchukuzi nchini unaounganisha reli, bandari, barabara na viwanja vya ndege ili kupunguza gharama za usafirishaji, kuongeza ushindani wa biashara na kufungua masoko mapya. "Kigoma haitakuwa tena mwisho wa reli. Itakuwa mwanzo wa kufunguka kwa fursa za biashara na uwekezaji," amesema Rais Dkt. Samia. Ameongeza kuwa, reli ya Tabora-Kigoma, itakapokamilika, itaunganisha mkoa huo na Bandari ya Dar es Salaam pamoja na mtandao wa bandari za kisasa katika Ziwa Tanganyika, hivyo kurahisisha usafirishaji wa mizigo ndani na nje ya nchi. Rais Dkt. Samia amesema uwekezaji unaoendelea kufany...
Recent posts

WAZIRI KOMBO AKUTANA NA KATIBU MKUU WA OACPS, WAKAZIA MAGEUZI NA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amekutana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS), Mhe. Moussa Saleh Batraki, katika mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na OACPS pamoja na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya mageuzi ndani ya Jumuiya. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 20 Julai 2026, Waziri Kombo amesisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuunga mkono mageuzi yanayolenga kuifanya OACPS kuwa taasisi yenye ufanisi, uwajibikaji na uwezo mkubwa wa kuhudumia nchi wanachama.  Aidha, Waziri Kombo ameeleza umuhimu wa OACPS kuwa daraja na kiungo muhimu cha kuimarisha ushirikiano kati ya nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki, pamoja na kuwa na usimamizi bora wa rasilimali na utekelezaji wenye matokeo wa programu za Jumuiya ili kuongeza imani ya nchi wanachama na washirika wa maendeleo. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa OACPS, Mhe.Batraki...

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MZEE JOSEPH BUTIKU

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema maendeleo ya kweli ya Taifa yanategemea kujenga wananchi wenye maadili, uzalendo, uwajibikaji na mshikamano, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha utawala wa sheria na taasisi za umma. "Hakuna maendeleo ya kudumu bila kujenga watu wenye maadili, uzalendo na uwajibikaji. Kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kuwekeza katika kujenga tabia ya wananchi pamoja na kuimarisha taasisi zetu," amesema. Waziri Mkuu amesema hayo leo (Jumatatu, Julai 20, 2026) alipokutana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo, Mzee Butiku alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi wake na juhudi anazoendelea kuzifanya katika kuiongoza nchi. Pia, alimpongeza Waziri Mkuu kwa mchango wake katika kumsaidia Mheshimiwa Rais kusimamia Serikali na kuhakikisha utekelezaji wa majukum...

MHE. MWINJUMA AFUNGA MASHINDANO YA 'CRDB NANAUKA CUP 2026'

 MTWARA Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amehitimisha rasmi mashindano ya soka ya 'CRDB Nanauka Cup 2026' yaliyokuwa sehemu ya tamasha kubwa la Mtwara Festival, huku Naliendele FC ikiibuka kidedea na kutwaa ubingwa.  Katika fainali hiyo ya kusisimua iliyopigwa Julai 18 2026 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara, Naliendele FC iliibuka na ushindi wa mikwaju ya penati dhidi ya Vigaeni FC baada kutoshana nguvu kwa sare ya 1-1 na kufanikiwa kukabidhiwa kombe, medali, na kitita cha shilingi milioni tatu. Vigaeni FC iliyoshika nafasi ya pili iliondoka na medali pamoja na shilingi milioni mbili, huku mshindi wa tatu akijinyakulia shilingi milioni moja.  Mashindano haya yameandaliwa na kuratibiwa na Mbunge wa Mtwara Mjini ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Maendeleo ya Vijana, Mhe. Dkt. Joel Arthur Nanauka. Akizungumza kwenye hafla hiyo, Naibu Waziri Mwinjuma amewapongeza waandaaji kwa kufikia asilimia 100 ya malengo yao, h...

WAZIRI MKUU MWIGULU NA UWT WASHIRIKIANA KUCHANGISHA FEDHA ZA MATIBABU BMH

 NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, ameshiriki hafla iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwezesha Mfuko wa Gharama za Matibabu kwa Wagonjwa wa Figo na Upandikizaji Uloto katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH). Hafla hiyo imefanyika Julai 16, 2026, katika Ukumbi wa Mabele Mabeyo Jijini Dodoma, ambapo Dk. Mwigulu amesema, jambo hilo ni jema kwani linawezesha kuokoa maisha ya wagonjwa wengi hasa wasio na uwezo wa kugharamia matibabu hayo. "Tunachokifanya leo ni kurejesha matumaini kwa wagonjwa na familia zao. Kila anayeguswa na jambo hili aendelee kushiriki ili wananchi wengi zaidi wanufaike na huduma hizi muhimu," amesema Dk. Mwigulu. Aidha, amesema serikali inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuwekeza fedha nyingi ili kuboresha sekta ya afya kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora. Naye, Wazi wa Afya, Mohamed Mchengerwa amesema, dhamira ya serikali ni kuhakikisha Tanzania inakuw...

SPIKA ZUNGU AILEZA DUNIA HATUA ZINAZOCHUKULIWA KUCHOCHEA MATUMIZI YA MAGARI YA UMEME NA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

 New York, Marekani Spika wa Bunge Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb) amesema Bunge la Tanzania limechukua hatua madhubuti za kuhimiza matumizi ya magari ya umeme pamoja na gesi. Amesema hatua hizo zimelenga kuimarisha utekelezaji wa mipango ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs). Mheshimiwa Spika ameyasema hayo leo Julai 14, 2026 wakati akiwasilisha taarifa ya Bunge la Tanzania kuhusu matumizi ya Nishati Safi kwenye  Jukwaa la Kibunge katika Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (HLPF) 2026. Mkutano huo umefanyika  katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN), jijini New York, nchini Marekani. Amesema Bunge la Tanzania limepitisha marekebisho ya sera na sheria za kodi yaliyopunguza ushuru wa magari ya umeme kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 na kwamba misamaha mbalimbali ya ushuru na kodi kwa baadhi ya magari yanayotumia umeme na gesi imetolewa ili kuongeza matumizi ya usafiri r...