Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MKOA WA MARA UMEIOMBA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUANZISHA MAMLAKA ZA KUHIFADHI ZIWA VICTORIA

  Musoma. Serikali mkoani Mara imiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuanzisha Mamlaka ya Uhifadhi wa ziwa Victoria hatua ambayo itasaidia uhifadhi na uendelevu wa ziwa hilo ambalo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa mkoa na watu wake. Ombi hilo limetolewa mjii Musoma leo Jumanne Agosti 11 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Bashiru Ally ambaye yupo mkoani Mara kwa ziara ya siku nne. Kanali Mtambi amesema kutokana na shughuli za kiuchumi na kijamii zinazofanywa ndani ya ziwa hilo ipo haja ya kuwa na mamlaka maalumu itakayokuwa inasimamia ziwa hilo ili shughuli hizo ziweze kufanyika kwa ufanisi na kuleta tija zaidi bila kuathiri uhai wake. Ametolea mfano suala la ufugaji wa vizimba ambalo limepata mapokeo makubwa mkoani Mara baada ya Serikali kuanza kuwezesha wavuvi ambapo amesema vijana wengi hivi sasa wameamua kujiajiri kupitia ufugaji huo ndani ya ziwa hilo hivyo ipo haja ya kuwa na mamlaka rasmi itakayosimamia rasilimali hiyo muhimu. "Kuhus...
Recent posts

CPA WALALAZE : WALIPAKODI TUMIENI SIKU YA ALHAMISI KUWASILISHA CHANGAMOTO ZENU

 NA: MWANDISHI WETU Kodi ni chanzo muhimu cha mapato kinachoiwezesha serikali kufanikisha mipango na mikakati yake ya kimaendeleo kwa wananchi wake. Wananchi wanahitaji huduma nzuri za kijamii kama elimu, afya, maji, umeme, barabara na masoko. Aidha, wanahitaji pia kuwezeshwa kiuchumi kwa kupatiwa mikopo nafuu ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha shughuli za kibiashara na za kiujasiriamali. Ni kwamba, mambo haya mazuri na mengine mengi, hayawezi kufanikiwa endapo serikali haitakuwa na fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wao. Hapa ndipo umuhimu wa ulipaji kodi unapoonekana. Kimsingi, pamoja na umuhimu wa ulipaji kodi kwa maendeleo, walipakodi wanazo changamoto ambazo wanahitaji kuziwasilisha serikalini kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili ziweze kufanyiwa kazi. Iko hivi: Ulipaji kodi unahusisha wadau wawili yaani TRA na walipakodi. Kutokana na hili, haitawezekana ulipaji kodi ukawa na ufanisi endapo walipakodi hawatatatuliwa changamoto...

LICHA YA KUTEMBEA SAA NNE KUTAFUTA MAJI, WANAFUNZI WA KIMULI WAFANYA MAKUBWA

 Na Angela Sebastian,Kyerwa  Ushirikiano wa karibu kati ya wazazi, walezi, walimu na viongozi umeelezwa kuwa chachu ya mafanikio makubwa ya kielimu katika Shule ya Sekondari Kimuli, iliyopo Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera, baada ya shule hiyo kufanya vizuri katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2026. Shule hiyo imeibuka ya kwanza kwa shule za Serikali mkoani Kagera, ya pili kwa shule zote za mkoa huo na kushika nafasi ya 27 kitaifa, baada ya wanafunzi wote 65 waliofanya mtihani huo kupata Daraja la Kwanza. Mkuu wa Shule ya Sekondari Kimuli, Daniel Kifigo, alisema hayo wakati wa hafla ya kuwapongeza na kuwakabidhi tuzo na zawadi walimu pamoja na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa wilayani Kyerwa. Kifigo alisema mafanikio hayo yamepatikana licha ya shule hiyo kukabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo ukosefu wa maji safi na salama, hali inayowalazimu wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata maji. Alisema wanafunzi hao hutumia takribani saa n...

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA TEC

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 10 Agosti, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania kupitia Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference - TEC), Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma. Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na TEC na kujadili masuala mbalimbali ya kitaifa yanayoigusa jamii, yakiwemo ya kisiasa, imani na maendeleo, pamoja na kuimarisha amani, mshikamano na kujenga mustakabali mwema wa Taifa. Aidha, mazungumzo hayo yaligusia umuhimu wa nafasi ya madhehebu na Viongozi wa Dini katika kulea jamii yenye maadili mema, uwajibikaji na mshikamano, ikiwa ni sehemu ya mchango wao katika ustawi na maendeleo endelevu ya Taifa. Mheshimiwa Rais aliwashukuru Maaskofu hao kwa kuona umuhimu wa kukutana na kujadiliana naye masuala yenye tija kwa Taifa na kuwahakikishia dhamira yake ya kuendeleza utamaduni wa kushauriana na kushirikisha Viong...

HOSPITALI YA SINO MIKOCHENI YAUNGA MKONO DIRA YA RAIS SAMIA UTALII TIBA

  Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. WATANZANIA wameanza kunufaika na huduma za matibabu ya kibingwa zinazopatikana nchini, hali inayopunguza gharama na ulazima wa kusafiri nje ya nchi kutafuta matibabu. Mkurugenzi Mtendaji wa Universal Medical Tourism, Dk. Sharif Mollel, amesema huduma hizo zinapatikana katika Hospitali ya SINO iliyopo Mikocheni, Dar es Salaam, inayomilikiwa na wawekezaji kutoka China katika sekta ya afya. Amesema kampuni yake inashirikiana na hospitali hiyo katika kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibingwa, teknolojia za kisasa za matibabu pamoja na baadhi ya huduma zinazotokana na tiba za jadi za China, zinazojulikana kama Traditional Chinese Medicine. Dk. Mollel amesema uwepo wa huduma hizo nchini unawapa Watanzania nafasi ya kupata matibabu bila kulazimika kuingia gharama kubwa za tiketi za ndege, malazi, visa na matumizi mengine yanayotokana na safari za matibabu nje ya nchi. “Lengo letu ni kuona Watanzania wanapata huduma nyingi zaidi hapa nchini. Kama huduma...

TADB YATOA MIKOPO YA SH15 BILIONI ZANZIBAR, HEMED AWASIHI WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka wananchi hususan wakulima , wafugaji na wavuvi kuchangamkia fursa zinazotolewa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ili kukuza mitaji ya biashara zao. Ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Benki ya maendeleo ya kilimo Kanda ya Zanzibar Afisini kwake Vuga. Amesema Benki ya maendeleo ya Kilimo ina mchango mkubwa katika kuwawezesha kifedha na kuwapatia ujuzi wa kisasa wakulima, wafugaji na wavuvi ili waweze kukuza mitaji yao hivyo TADB wanapaswa kufikisha elimu kwa wananchi ili waweze kutambua fursa za kilimo na ufugaji zinazopatikana kupitia benki ya maendeleo ya Kilimo. Aidha, Mhe. Hemed amesema wananchi wengi bado hawajaziona fursa za uwekezaji wa Kilimo zinazopatikana Zanzibar hasa vijijini ambako kuna maeneo mengi ya kufanya uwekazi endelevu na stahmilivu wa Kilimo. Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka viongozi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Kanda ya zanzibar kuhakiki...