Kuelekea fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, washiriki wa fani ya upishi katika Mashindano ya Kitaifa ya Ujuzi WorldSkills Tanzania 2026 wametakiwa kujiandaa kuwa mabalozi wa utalii na ukarimu wa Tanzania kupitia umahiri wao wa kupika. Wito huo umetolewa leo Agosti 22,2026 na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Bi. Bernadetta Ndunguru, alipotembelea mashindano yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga. Ndunguru amesema washiriki hao tayari wameonesha kiwango cha juu cha taaluma na wanapaswa kujiona kama wapishi wakubwa watakaokuwa sehemu ya kuipokea Afrika wakati Tanzania itakapokuwa mwenyeji wa AFCON 2027. Kwa mujibu wa Ndunguru, ubora wa huduma za chakula na ukarimu vinatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya taswira ya Tanzania mbele ya maelfu ya wageni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika. "Niwahimize vijana muendelee kuboresha ujuzi wenu na kutumia fursa ya WorldSkil...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kila kitu katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) kimekamilika na kinafanya kazi, akieleza kuwa kukamilika kwa mradi huo ni fahari kubwa kwa Taifa na uthibitisho kwamba ndoto ya kuwa na mradi mkubwa wa kuzalisha umeme imetimia. Rais Samia amesema hayo leo Agosti 22, 2026, wakati wa hafla ya uzinduzi wa JNHPP iliyofanyika Rufiji mkoani Pwani, ambapo amezindua Kituo cha Kuzalisha Umeme, kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme, pamoja na kukagua tuta kuu na kituo cha kupokea na kusafirisha umeme kwenda kwenye Gridi ya Taifa. Amesema Desemba 22, 2022 alifika katika eneo hilo kushuhudia kufungwa kwa njia ya kugeuza maji ya Mto Rufiji na kuanzishwa rasmi kwa ujazaji wa maji katika bwawa, wakati huo ujenzi wa mradi huo ukitarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka mitatu. Kwa mujibu wa Rais Samia, kwa neema ya Mungu, bwawa hilo lilijaa ndani ya mwaka mmoja na nusu na kuanza majaribio ya uzalishaji ...