NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi, ameelezwa kuwa kiongozi mahiri, muadilifu na mzalendo, mwenye uwezo wa kumsaidia majukumu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, Agosti 30, 2026, ofisini kwake Dodoma, siku moja baada ya kukamilika uapisho wa kiongozi huyo, Ikulu ya Chamwino, Dodoma. Chatanda ameeleza, Ndejembi ni kiongozi wa vitendo na katika majukumu aliyoaminiwa tangu akiwa Mkuu wa wilaya ya Kongwa, Mbunge, Naibu Waziri na Waziri kamili katika wizara mbalimbali. "Kule Kongwa Dodoma akiwa Mkuu wa wilaya alifanya kazi nzuri na katika kilimo alisimamia kwa mafanikio makubwa kampeni yake aliyoiita ONJAKO yaani Ondoa Njaa Kongwa. Alihimiza wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame kama mtama, mihogo, ufuta na alizeti ili kuwaepusha wananchi na kadhia ya njaa," amesema Chatanda. Ameongeza kuwa, kampeni ya ONJAKO ilipokelewa vizuri na wakulima wa Kongwa kut...
ELIMU NA HAMASA NZURI YAWAFANYA WAZAZI NA WALEZI KATA YA MWISENGE KUHAKIKISHA WATOTO WAO WANAPATA CHANJO YA POLIO.
Na Mwandishi wetu Jovina Massano Musoma. ELIMU na hamasa nzuri kwa jamii yasababisha wazazi,watoto na walezi Kata ya Mwisenge Manispaa ya Musoma mkoani Mara kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo ya Polio awamu ya tatu. Hayo yamesemwa na wazazi na walezi Agosti 30, 2026 katika mitaa na maeneo ya Ibada mara baada ya kufikiwa na timu ya utoaji chanjo. Wamesema kuwa wahamasishaji wakiwemo wenyeviti wa mitaa na taarifa zinazotolewa katika vyombo vya habari zimewafanya wamepata hamasa na uelewa mpana wa umuhimu wa chanjo hiyo. Wakizungumza kwa Nyakati tofauti wamesema utoaji elimu mapema ni muhimu kwa kuwa inasaidia kupata taarifa na uelewa usahihi wa zoezi husika. Frank David afisa usafirishaji wa Mtakuja Kituo Cha mianzini ni miongoni mwa wazazi ambae nae mtoto wake ameweza kupata chanjo hiyo. Amesema hapo awali watu waliongea vibaya kuhusiana na chanjo ya Polio wengi walipata hofu lakini hivi sasa baada ya kupewa elimu kwa usahihi imewapa ujasiri wa kuhakikisha watoto wa...