Na MASHAKA MHANDO, Tanga Serikali imetoa maagizo kwa wizara na taasisi za utafiti nchini kuhakikisha zinakamilisha taratibu zote za kimataifa za kupata ithibati, ili dawa zinazotokana na mimea zikishapita maabara na kuzalishwa viwandani ziache kuitwa 'dawa za asili' na badala yake zitambulike kama dawa za kisasa kutoka Tanzania. Maagizo hayo yametolewa leo Augosti 24 na Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, jana wakati akifunga kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi, na Ubunifu yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga kuanzia Agosti 18 hadi 24, mwaka huu. Akifafanua kuhusu dhana hiyo, Dkt. Mwigulu alitolea mfano dawa ya kutibu tezi dume iliyotengenezwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), akieleza kuwa kuendelea kuziita 'dawa za asili' kunawafanya baadhi ya watu kuwa na ukakasi na mashaka nazo, licha ya kuwa zimepitia michakato yote ya kimaabara kama dawa nyingine za kigeni. "Tuendelee kufanya ...
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Kanali Evans Alfred Mtambi, leo tarehe 24 Agosti 2026, amezindua na kuongoza hafla ya ugawaji wa pampu 113 za umwagiliaji kwa wakulima wadogo wa Mkoa wa Mara, iliyofanyika katika viunga vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara. Hafla hiyo imeandaliwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuimarisha kilimo cha umwagiliaji na kuongeza uzalishaji wa mazao. Akizungumza katika hafla hiyo, Mheshimiwa Kanali Mtambi amewahimiza wananchi wa Mkoa wa Mara, hususan wakulima, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na Serikali kwa kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kuinua uchumi wa wananchi. Aidha, amemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara kupitia uwekezaji katika sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo kilimo, afya, elimu, miundombinu na hu...