Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

SERIKALI YAONGEZA FURSA KWA WATANZANIA KUNUFAIKA NA SEKTA YA MADINI

▪️Ni kupitia Local Content ▪️ Yatenga Huduma na Bidhaa 20 kwa ajili ya Kampuni za kitanzania pekee* ▪️ Watanzania wanufaika asilimia 86 ya manunuzi ya bidhaa na huduma migodini* ▪️ Ajira 20,421 zalizalishwa, Watanzania wachukua asilimia 94 *📍DODOMA* Serikali imeendelea kufanya maboresho katika Sheria na Kanuni za Madini kwa lengo la kuongeza ushiriki wa Watanzania katika sekta ya madini, hususan katika utoaji wa huduma, usambazaji wa bidhaa na upatikanaji wa ajira migodini. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde wakati akitoa ufafanuzi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini leo Agosti 14, 2026 Bungeni jijini Dodoma waliotaka kujua ni namna gani Serikali imejipanga kutekeleza mpango wa Uwajibikaji wa Wamiliki wa Leseni kwa Jamii na Ushirikishwaji wa Watanzania katika Uchumi wa Madini. Amesema kuwa, kupitia Tume ya Madini, Serikali imetenga bidhaa na huduma 20 zinazopaswa kusambazwa na kutolewa na Watanzania au kampuni zinazomilikiwa na Watanz...
Recent posts

RAIS SAMIA AHITIMISHA KIZIMKAZI KWA KUKARIBISHA UWEKEZAJI ZAIDI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewakaribisha wawekezaji kutumia fursa zinazoendelea kukua mkoani Kusini Unguja, kufuatia maendeleo ya miundombinu, huduma za jamii na shughuli za kiuchumi. Akihutubia katika kilele cha Tamasha la Kizimkazi, 2026 leo tarehe 14 Agosti, 2026, Rais Dkt. Samia ameeleza kuwa Wilaya ya Kusini imebadilika kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni, ikichochewa na ongezeko la uwekezaji na miradi ya maendeleo. Rais Dkt. Samia amesema fursa hizo, pamoja na uwekezaji katika miundombinu, zimeendelea kuvutia shughuli mpya za kiuchumi, akisisitiza wajibu wa viongozi kuhakikisha uwekezaji huo unaacha manufaa ya kudumu kwa wananchi. Aidha, ametoa rai kwa wawekezaji kutumia fursa mpya zitakazoambatana na ujenzi wa uwanja wa michezo Kusini Unguja, unaotarajiwa kutumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika. Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia amewataka wananchi kuendelea kulinda amani, umoja, usalama na utulivu ...

KIZIMKAZI FESTIVAL 2026: SAMIA AONGOZA SHEREHE, NCHIMBI ASHIRIKI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameshiriki Kilele cha Tamasha la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026) lililofanyika katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar. Tamasha hilo limeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

WATANZANIA WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA NA CAF KUELEKEA AFCON 2027

 DAR ES SALAAM, AGOSTI 14, 2026 Watanzania, kampuni, taasisi na watoa huduma wenye uwezo na sifa stahiki wamehimizwa kuchangamkia fursa mbalimbali za zabuni zilizotangazwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuelekea maandalizi na uendeshaji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON2027). Akitoa taarifa hiyo leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Kamati ya Ndani (LOC), Neema Msitha, amesema CAF imetangaza fursa mbalimbali za zabuni zinazohusiana na maandalizi na uendeshaji wa mashindano yake, ikiwamo AFCON 2027, ambayo Tanzania itaandaa kwa kushirikiana na Kenya na Uganda. “LOC inawahimiza Watanzania wenye uwezo, sifa na nia ya kushiriki fursa hizi kufuatilia matangazo rasmi ya zabuni hizo kupitia tovuti ya CAF ambayo ni https://www.cafonline.com/inside-caf/about-us/tenders/tenders-tab/ ili kusoma masharti ya kila zabuni na kuwasilisha maombi yao kufuatana na taratibu na muda uliowekwa na shirikisho hilo” amesisitiza Msitha. Amesema fursa hizo zinahusisha maeneo mbal...

MHE. BALOZI OMAR: AIMWAGIA SIFA TRA UKUSANYAJI WA MAPATO YA NDA

Na. Benny Mwaipaja, Kizimkazi, ZANZIBAR Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameimwagia sifa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA kwa utendaji uliotukuka uliowezesha Mamlaka hiyo kuendelea kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato kila mwezi na kueleza imani yake kwamba kwa kushirikiana na alipakodi, wataweza kuvuka lengo walilopangiwa la kukusanya zaidi ya shilingi trilioni 42 katika Mwaka wa Fedha 2026/2027. Mhe. Balozi Omar, ametoa pongezi hizo wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya TRA, Kizimkazi, Zanzibar, litakalokuwa na ghorofa moja, ambapo hadi kukamilika kwake linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.6. Sifa hizo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, zinafuatia maelezo ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA Bw. Yusuph Mwenda ambapo alisema katika mwezi Julai mwaka huu, Mamlaka yake imevuka malengo kwa kukusanya shilingi trilioni 3.2 ikilinganishwa na malengo waliyopangiwa ya kukusanya shilingi trilioni 2. Alisema kuwa mafa...

MKUU WA JESHI LA MAGEREZA AKUTANA NA BALOZI WA CHINA 'WATETA' KUHUSU USHIRIKIANO

Na INSP. Nurdini Nanyanga - DSM Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, leo Agosti 13, 2026, amefanya ziara katika Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China, jijini Dar Es Salaam na kukutana na Balozi wa nchi hiyo hapa Tanzania Mhe. Chen Mingjian. Katika ziara hiyo, CGP Katungu amesema lengo ni kuimarisha ushirikiano kati ya Jeshi la Magereza na China, hususan katika maeneo ya teknolojia na kilimo, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Jeshi la Magereza kuongeza uzalishaji na kujitosheleza kwa chakula. Amesema Jeshi la Magereza liko tayari kushirikiana na kampuni na wadau mbalimbali katika uwekezaji, kwa kuzingatia sheria, taratibu na maslahi ya pande zote. Kwa upande wake, Mhe. Chen Mingjian, amesema Tanzania na China zimekuwa na ushirikiano mzuri, huku kampuni nyingi za China zikionyesha nia ya kuwekeza nchini. Ameahidi kuyapa kipaumbele mazungumzo yao na kuendelea kubadilishana taarifa na Jeshi la Magereza ili kutafuta fursa za ushirikiano katika teknolojia na sekta ya kilimo.