MSALALA, SHINYANGA Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kuhakikisha inatekeleza kwa wakati mapendekezo yote yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), akisisitiza kuwa hatua hiyo itaimarisha uwajibikaji, uwazi na matumizi sahihi ya rasilimali za umma. Mhe. Mhita ametoa maelekezo hayo leo, Julai 8, 2026, wakati akifungua Baraza Maalumu la kujadili na kupitia hoja za ukaguzi wa CAG kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30, 2026, lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Amesema utekelezaji wa hoja za CAG si suala la hiari, bali ni wajibu wa kila taasisi ya umma kuhakikisha dosari zilizobainishwa zinarekebishwa kwa wakati ili kuongeza ufanisi wa usimamizi wa fedha za Serikali na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi. "Hoja za CAG zinapaswa kutazamwa kama fursa ya kuboresha utendaji wetu. Hakikisheni kila hoja inafanyiwa kazi kwa wakati na kufungwa kwa mujibu wa taratibu," amesis...
Balozi wa Amani Tanzania na Katibu wa Mahusiano wa Jumuiya ya Wachimbaji Tanzania (FEMATA), Mess Chengula, amepongeza hali ya amani na utulivu iliyoendelea kutawala jijini Mwanza, akisema ndiyo msingi wa maendeleo na ustawi wa wananchi. Akizungumza leo baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ya jiji hilo, Chengula alisema ameridhishwa kuona shughuli za kijamii na kiuchumi zikiendelea, huku baadhi ya maduka yaliyokuwa yamefungwa yakifunguliwa tena na kuanza kutoa huduma. "Ninawapongeza Watanzania kwa kuchagua amani siku hii ya leo. Furaha kubwa kwa binadamu ni kuona amani ikitawala mioyoni mwa watu," amesema. Aidha, aliiomba Serikali kuendelea kusikiliza makundi mbalimbali yenye malalamiko ili kutatua changamoto kwa njia ya mazungumzo na kuimarisha utulivu nchini. Chengula amesema amani huwezesha wananchi kujishughulisha kwa uhuru katika shughuli za uzalishaji mali, huku akisisitiza kuwa maridhiano yanayotarajiwa kufanywa kati ya Serikali, vyama vya siasa na makundi mbalimbali ...