Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

TANZANIA'S SENIOR FEMALE MILITARY DIPLOMAT LEAVES LEGACY IN ZAMBIA

 By Prosper Makene, LUSAKA, Zambia Tanzania's senior female military diplomat, Colonel Bula Bulali, has concluded her four-year tour of duty in Zambia, leaving behind a legacy of strengthened defence ties and groundbreaking cooperation between the two historic allies. Col. Bulali, who has served as Tanzania's Defence Advisor accredited to the Republic of Zambia since 2022, officially bade farewell to Zambia's Ministry of Defence and its Services on Tuesday, 17th September 2026. According to a Press Statement issued by the Ministry of Defence, her tenure was marked by tangible achievements in defence diplomacy, military training, and joint cooperation. Reflecting on her service, Col. Bulali said Zambia and Tanzania had scored significant success in enhancing people-to-people ties and military collaboration. She singled out the signing of a landmark Memorandum of Understanding (MoU) between the Zambia National Service (ZNS) and Tanzania's Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) earl...
Recent posts

KIKWETE AELEZA ALIVYOPAMBANA NA SARATANI YA TEZI DUME

 Na Mwandishi Wetu RAIS mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amewataka wanaume kujenga utamaduni wa kupima tezi dume mara kwa mara ili waweze kutibiwa mapema wanapogundulika kuwa na dalili za saratani. Alitoa wito huo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya mwezi wa uelewa wa saratani ya tezi dume yaliyofanyika katika hospitali ya Kairuki Mikocheni. Rais Kikwete alitembelea mtambo wa kuondoa uvimbe bila upasuaji hospitalini hapo wa High Intensity Focused Ultrasound HIFU ambao unaondoa vimbe mbalimbali mwilini bila upasuaji kwa kutumia mwangwi wa sauti (Ultrasound). Alisema yeye binafsi ni mwathiriwa wa ugonjwa huo kwani baada ya kugundulika mapema mwaka 2014 alichukua hatua ya kwenda kupima vipimo vingine nchini Marekani na ilipothibitika kuwa na ugonjwa huo alikubali kufanyiwa upasuaji na mpaka sasa ni mzima wa afya. Aliwataka wanaume wasiogope kwenda kupima saratani ya tezi dume kwani teknolojia kwa sasa imekwenda mbali zaidi na ugonjwa unaweza ...

MOTSEPE: AFCON 2027 HAIONDOKI TANZANIA, KENYA NA UGANDA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe, amesisitiza kuwa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 itaendelea kufanyika Tanzania, Kenya na Uganda, akikanusha taarifa na madai yanayodai kuwa mashindano hayo yanaweza kuhamishiwa katika nchi nyingine. Dkt. Motsepe ameyasema hayo leo, Septemba 17, 2026, mara baada ya kuwasili Tanzania kwa ajili ya kukagua maendeleo ya maandalizi ya mashindano hayo, ambayo Tanzania, Kenya na Uganda zimepewa dhamana ya kuwa wenyeji. Amesema amekuwa akisikia taarifa mbalimbali zinazodai kuwa CAF inaweza kuanza kufikiria mpango mbadala wa kuhamishia AFCON 2027 katika nchi nyingine, akisisitiza kuwa hilo halitatokea. “Baadhi ya watu, kutokana na yale ambayo tayari yameripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari barani Afrika na sehemu nyingine duniani, wanasema Rais wa CAF anapaswa kuanza kufikiria mpango B na mpango C na kuiondoa AFCON Tanzania, Kenya na Uganda, hilo halitatokea,” amesema Motsepe. Aidha, Rais huyo wa CAF ...

MWANA DIPLOMASIA MWANAMKE WA JESHI LA TANZANIA AHITIMISHA UTUMISHI WA MIAKA MINNE ZAMBIA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

 Na Prosper Makene Mshauri wa Ulinzi wa Tanzania aliyeko nchini Zambia, Kanali Bula Bulali, amehitimisha utumishi wake wa miaka minne uliogusa mafanikio makubwa ya kidiplomasia ya kijeshi. Taarifa rasmi ya Wizara ya Ulinzi ya Zambia iliyotolewa Jumanne Septemba 17, 2026 na Afisa Uhusiano Mkuu Bw. Paul Shalala, imesema Kanali Bulali ameaga rasmi Wizara hiyo na Majesi yake baada ya kuitumikia nafasi hiyo tangu 2022. Katika kipindi cha miaka minne, Kanali Bulali amewezesha kuimarika kwa ushirikiano wa mafunzo ya pamoja, kubadilishana uzoefu wa kijeshi na kuimarisha urafiki kati ya wananchi wa mataifa hayo mawili. Mafanikio makubwa aliyoyaacha ni kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano kati ya Jeshi la Kujenga Taifa la Zambia (ZNS) na Jeshi la Kujenga Taifa la Tanzania (JKT), inayolenga uwekezaji katika biashara na kilimo. Katibu Mkuu Kaimu wa Wizara ya Ulinzi Bi. Millicent Mwenda amesema Kanali Bulali atakuwa anakumbukwa kama mjenzi wa madaraja ya urafiki. Uteuzi wa Mshauri mpya wa Ulinzi w...

MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YAHAMASISHWA KUELIMISHA JAMII DHIDI YA ELI NINO.

 Na Jovina Massano Musoma. Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Musoma mkoani Mara yahamasisha mashirika yasiyo ya kiserikali ( NGO) kuelimisha jamii dhidi ya tahadhali ya mvua za el nino kama ilivyotolewa na Mamlaka ya hali ya hewa hapa nchini. Hayo yamesemwa wakati wa kongamano la Mwaka la mashirika yasiyo ya kiserikali lililohisisha mashirika zaidi ya 50 yaliyopo katika Manispaa hiyo. Kongamano hilo lenye lengo la kujenga fikra mpya katika upatikanaji wa rasilimali fedha kupitia vyanzo vya ndani limeweza kufanya majadiliano mbalimbali yanayohusu jamii ikiwemo uwasilishaji wa taarifa kwa NGO za mwaka 2025/2026. Aidha mashirika yametakiwa kushirikiana na kuhakikisha yanaboresha taarifa zao kupitia mfumo uliopo kuwezesha taarifa kupatikana kwa urahisi ikiwemo uwasilishaji. Akitoa hamasa hiyo Loserian Mollel Saning'o afisa mradi kutoka shirika la Victory Hope Foundation Tanzania (VIHOFOTA) kwa niaba ya Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa hiyo amesema mashirika yashiriki kikamil...

OKTOBA 2026, MACHO YOTE ARUSHA: TANZANIA KUITANGAZA DIRA YA 2050 MBELE YA DUNIA

 Na Mwandishi Wetu  Tanzania inajiandaa kuitangaza Dira yake ya Taifa ya 2050 mbele ya jukwaa kubwa zaidi la wabunge duniani. Tukio hilo la kihistoria litafanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 5 hadi 9 Oktoba 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) ambapo Mkutano wa 153 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) utafanyika.  Huu ndio mkutano mkubwa zaidi kuwahi kuandaliwa Afrika Mashariki na utawaleta pamoja Maspika na Wabunge kutoka nchi zaidi ya 170 na wajumbe zaidi ya 2,000 wakiwemo watumishi wa mabunge, waangalizi na vyombo vya habari. Kwa muda mrefu Tanzania imekuwa ikienda nje kutafuta mikutano ya kuelezea mipango yake ya maendeleo. Safari hii historia inabadilika, dunia yenyewe ndiyo inakuja Tanzania kusikiliza. Na ujumbe mkuu ambao Tanzania itaupeleka mbele ya mabunge hayo 170 ni Dira ya 2050. Dira ambayo inaeleza wazi kuwa ifikapo mwaka 2050 Tanzania inataka kuwa nchi yenye ustawi, iliyo ya viwanda, yenye demokrasia imara, na inayoheshimika kimataifa...