NA: DK. REUBENI LUMBAGALA Chama cha siasa kinapaswa kuwa na mikakati madhubuti ya kuwafikia wananchi wake, kuzungumza masuala mbalimbali ya maendeleo, kujadili changamoto zao na namna bora ya kuzitatua. Katika ulimwenguni huu wa maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia, suala la matumizi ya vifaa vya kisasa vya mawasiliano hayana budi kutumika. Katika shughuli za Chama na mikutano ya hadhara, matumizi ya mziki hayaepukiki katika kuhakikisha hadhira yote inasikia kinachozongumzwa katika meza kuu au jukwaani. Hivyo basi, katika kuhakikisha shughuli na mikutano ya hadhara inawafikia wananchi wengi zaidi, Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Tanga, kimenunua mziki mkubwa na wa kisasa kufanikisha azma hiyo. Mziki huo wenye vyombo vya kisasa, gari la matangazo na jenereta kubwa, vimenunuliwa na Mwenyekiti wa CCM mkoani humo na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu (MCC), Rajab Abdallah, maarufu 'Ustadhi Rajab.' Vyombo hivyo vya kisasa vinatarajiwa kutumika katika shughuli na mikut...
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, imewaonya wananchi dhidi ya taarifa za uongo zinazotengenezwa kwa muonekano wa taarifa rasmi na kusambazwa mitandaoni, huku zikidaiwa kutolewa na Ikulu au kuhusishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika taarifa yake kwa umma, Kurugenzi hiyo imesema imebaini kuwepo kwa taarifa hizo ambazo zinatumia jina, nembo na utambulisho unaoweza kuwafanya wananchi kuamini kuwa zimetolewa rasmi na Ikulu. Kurugenzi imeeleza kuwa taarifa zote rasmi zinazohusu shughuli za Mheshimiwa Rais hutolewa kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, na wananchi wanapaswa kuzihakiki kupitia vyanzo rasmi kabla ya kuzipokea au kuzisambaza. Vyanzo rasmi vilivyotajwa ni pamoja na ukurasa wa Instagram wa Ikulu Tanzania (@ikulu_mawasiliano), Facebook wa Ikulu Tanzania (@ikulu.mawasiliano) pamoja na tovuti rasmi ya Ikulu. Aidha, Kurugenzi imewakumbusha wananchi kuwa utengenezaji na usambazaji wa taarifa za uongo kwa kutumia jina, nembo...