Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Kusaya, leo tarehe 11,septemba 2026, ameongoza hafla ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Brigedia Jenerali Evans Alfred Mtambi, kufuatia kupandishwa cheo chake cha kijeshi kutoka Kanali hadi Brigedia Jenerali. Hafla hiyo imefanyika katika viunga vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali, watumishi wa umma, viongozi wa dini pamoja na wadau wengine wa mkoa. Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Kusaya, ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara na kuwaamini viongozi wenye uwezo na uadilifu. Amesema kupandishwa cheo kwa Mkuu wa Mkoa ni ishara ya kutambua weledi, uhodari, utii na utumishi wake uliotukuka katika kulitumikia taifa. “Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara. Kupandishwa cheo kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ni heshima kubw...
Tanzania na Misri zimejadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika sekta ya ulinzi na teknolojia za anga, ikiwemo kubadilishana uzoefu, maarifa na teknolojia kwa manufaa ya pande zote. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji wa Kijeshi na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Luteni Jenerali Ashraf Salem Zaher, jijini El Alamein, Misri. Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 10, Septemba 2026, wakati Tanzania ikishiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Anga na Teknolojia za Anga za Juu ya El Alamein (ELIAS). Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamejadili fursa za kuendeleza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Misri katika maeneo ya ulinzi na teknolojia za anga, pamoja na umuhimu wa kubadilishana uzoefu, maarifa na teknolojia katika maeneo yenye maslahi ya pamoja. Ushiriki wa Tanzania katika Maonesho ya ELIAS unalenga pia kujenga na kuimarisha mahusi...