Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AZINDUA JENGO LA RAMANI LA JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA

 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 03 Septemba, 2026, amezindua rasmi Jengo la Ramani la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lililopo katika Mji wa Serikali, Mtumba, Jijini Dodoma. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo hilo ambalo ni sehemu ya miundombinu ya kimkakati ya Jeshi, Dkt. Nyansaho amelipongeza JWTZ kwa kukamilisha mradi huo na kupata jengo la kisasa lililowekewa vifaa na teknolojia za kisasa zitakazowezesha utoaji wa huduma kwa ufanisi na weledi zaidi. Waziri Nyansaho amesema kukamilika kwa mradi huo ni kielelezo cha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuendelea kuliwezesha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kulinda uhuru, mamlaka na usalama wa nchi.  “Kukamilika kwa mradi huu wa kimkakati ni alama ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuendelea kuliwezesha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kutimiza majukumu yake ya ulinzi na usal...
Recent posts

DKT. MWIGULU AONGOZA MKUTANO WA KAZI WA MAWAZIRI

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Septemba 03, 2026 ameongoza Mkutano wa kazi wa Mawaziri, kwenye ukumbi wa mikutano wa Hazina jijini Dodoma.

MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KIBAHA AWATAKA WAZAZI KUIMARISHA NA KUBORESHA ELIMU KWA KUSHIRIKIANA NA WALIMU

 Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dr Nicas Mawazo amewataka wazazi wa Shule zilizopo Manispaa ya Kibaha kuiga  jitihada zinazofanywa na Shule zingine katika kuimarisha na kuboresha elimu kwenye Shule zao kwa kushirikiana na walimu. Hayo ameyasema wakati wa kikao na Kamati ya Shule ya Sekondari ya Mwambisi, iliyofika katika Ofisi ya Mstahiki Meya kwa ajili ya kujadiliana na masuala mbalimbali. Akizungumza baada ya Kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yao, Mstahiki Meya Dr Nicas ameipongeza Kamati hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wanafunzi wa Shule yaSekondari Mwambisi wanaendelea kufanya vizuri kwenye mitihani yao. "Nawapongeza sana Kamati ya Shule kwa jitihada kubwa mnazofanya , Shule zingine wangekuwa wanafuata utaratibu huu ina maana tungekuwa tunafanya vizuri zaidi  na zipo baadhi ya Shule zinafanya hivyo na matokeo yao yanakuwa ni mazuri," amesema Dr Nicas. Ameongeza kuwa,, Ofisi ya Mstahiki Meya itaongezea hela ya ununuzi wa mashine ya...

KURA ZA WATANZANIA KUAMUA KAZI 294 ZILIZOFUZU SAMIA KALAMU AWARDS 2026

 Na. Mohammed Ulongo Katika kutambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari nchini, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), zimetangaza kuwa jumla ya kazi 294 zimefuzu hatua ya mwisho ya Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo za Samia Kalamu Awards 2026. Akizungumza leo Septemba 3, 2026 jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Samia Kalamu Awards 2026, Mhandisi Peter P. Mwasalyanda, amesema mkutano huo na waandishi wa habari ulikuwa na lengo la kuwaeleza wananchi namna ya kushiriki katika zoezi la kupiga kura kwa ajili ya kuwapata washindi wa tuzo hizo. Mhandisi Mwasalyanda amesema katika hatua za awali, waandaaji walipokea jumla ya kazi 3,003 zilizowasilishwa na waombaji 985 kutoka maeneo mbalimbali nchini, ambapo baada ya kupitia mchakato wa tathmini, majaji walifanikiwa kuteua kazi 294 ambazo sasa zimefika hatua ya kupigiwa kura na wananchi. Amesema zoezi l...

MWIGULU: TUWAWEZESHE WATANZANIA KUSHIKA UCHUMI WAO

 Mkuu wa Mwigulu Nchemba, Dkt. Mwigulu Nchemba, ametoa wito wa kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira, kukuza sekta binafsi, kuongeza mapato na kupunguza umaskini nchini. Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo, Alhamisi Septemba 3, 2026, wakati akifungua Kongamano la Tano la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na Uwekezaji, lililofanyika Dodoma. Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira ya kisera, kisheria na kiutendaji yatakayowawezesha Watanzania kushiriki moja kwa moja katika uchumi. “Tuwawezeshe Watanzania kushika uchumi wao. Hii ndiyo njia ya kuongeza ajira, kuongeza vyanzo vya mapato na kujenga sekta binafsi yenye nguvu,” amesema. Amesema lengo la kuwawezesha Watanzania si kuwazuia wawekezaji wa nje, bali kuongeza uwezo wa kampuni na wananchi wa ndani ili nao wanufaike na fursa zinazotokana na rasilimali na miradi mbalimbali ya maendeleo. Katika hatua nyingine...

JUWATA, UTPC KUSHIRIKIANA KUTETEA HAKI, MASLAHI YA WAANDISHI WA HABARI

 JUKWAA Huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika kulinda uhuru wa vyombo vya habari, kutetea haki na maslahi ya waandishi wa habari pamoja na kuhakikisha jamii inapata habari sahihi na kwa wakati. ‎‎Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao cha pamoja cha viongozi wa JUWATA na UTPC kilichofanyika katika ofisi za UTPC zilizopo Barabara ya Aboud Jumbe, Mtaa wa Kazembo, eneo la Uzunguni jijini Dodoma. ‎Katika kikao hicho, viongozi hao walijadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya habari, ikiwemo umuhimu wa kuwa na mshikamano miongoni mwa wadau wa habari katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini. ‎Aidha, walisisitiza umuhimu wa taasisi hizo kushirikiana katika kutetea uhuru wa vyombo vya habari, haki za waandishi wa habari na maslahi yao, huku wakitambua nafasi muhimu ya wanahabari katika kuhabarisha, kuelimisha na kuwajibika katika jam...