Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MICHEZO NI DARASA LA USHIRIKIANO KATI YA POLISI NA JAMII – RC MTANDA

 Na Dawati la Habari Polisi;Mwanza  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura, kwa hatua ya kuirejesha timu ya Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027. Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Agosti 9, 2026, wakati akifungua rasmi Mashindano ya Polisi Jamii Cup Kanda Namba 7 yanayofanyika katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. Amesema kurejea kwa Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ni hatua muhimu inayopaswa kuungwa mkono, huku akisisitiza umuhimu wa michezo katika kuimarisha mahusiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi. “Nitumie nafasi hii kumpongeza IGP Camillus Wambura kwa hatua ya kuirejesha timu ya Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ya NBC. Hii ni hatua nzuri na muhimu kwa Jeshi la Polisi na tunapaswa kuiunga mkono timu yetu ili iweze kufanya vizuri,” alisema Mtanda. Mkuu huyo wa Mkoa amesema michezo ni kiungo muhimu katika kujenga uaminifu, umoja na mshikamano kati ya Jeshi la Polisi na jamii, ak...
Recent posts

KUTOKA WIZARANI HADI JUKWAANI: MWANA FA AAMSHA DUDE MWANZA, EAST COAST TEAM YAUNGANA TENA

 Na Mashaka Mhando, MWANZA NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (maarufu kama Mwana FA au 'Falsafa'), ameacha historia mpya jijini Mwanza baada ya kufanya maajabu jukwaani akiungana na kundi lake la zamani la East Coast Team. Tukio hilo la kukata na shoka limejiri usiku wa Agosti 8, 2026, katika ukumbi wa Climax uliopo Rock City Mall, wakati wa Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 30 ya muziki wa Bongo Fleva, ambapo Mhe. Mwinjuma alihudhuria kama Mgeni Rasmi. Badala ya kuishia kutoa hotuba za kiserikali pekee, Mhe. Mwinjuma aliwapa mashabiki suprise ya kufa mtu alipopanda jukwaani na kuimba sambamba na wakali wenzake wa East Coast Team waliotikisa anga la muziki miaka ya nyuma, akiwemo Crazy GK, AY, na Snare. Muunganiko huo wa East Coast Team jukwaani uliamsha shangwe za mashabiki na kukumbusha enzi za dhahabu za muziki huo, huku Mwana FA akidhihirisha kuwa makali yake ya kuchana mistari bado yako palepale licha ya kubeba majukumu mazito ya ki...

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

 ▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini  ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde aelekeza uchunguzi kuwabaini na kukamata wahusika zaidi ▪️Mgeni mmoja kutoka nje ya nchi ahusishwa na utoroshaji ▪️Madini,fedha na vitendea kazi vyashilikiwa na serikali Ikiwa ni sehemu ya usimamizi thabiti wa sekta na kuhakikisha Serikali inapata mapato yake ipasavyo kupitia mfumo rasmi wa masoko ya madini nchini, soko bubu la madini lagunduliwa jijini Dar es Salaam. Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb) ameyasema hayo  leo tarehe 09 Agosti, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam na kubainisha kuwa zaidi ya watuhumiwa 14 wamekamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya utoroshaji wa madini na watafikishwa kwenye vyombo vya sheria hivi karibuni. "Hawa wenzetu pamoja na Serikali kuwezesha masoko na vituo vya ununuzi vilivyosambaa Nchi nzima, wao wameona waje kupanga nyumba na kuigeuza soko la madini ambapo ni kinyum...

MWANA FA ASHUKA CCM KIRUMBA, AAHIDI KUMALIZA KERO YA TAA ZA USIKU

 Na Mashaka Mhando, MWANZA SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, imeahidi kumaliza changamoto ya ukosefu wa taa katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, ili kuwezesha uwanja huo mkongwe kutumika kwa mechi na matamasha nyakati za usiku. Ahadi hiyo nzito imetolewa leo, Agosti 8, 2026, na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma (maarufu Mwana FA), wakati alipofanya ziara maalum ya kukagua miundombinu ya uwanja huo, huku akisisitiza kushirikiana na wadau wa michezo kutatua kero hiyo. Mhe. Mwinjuma amebainisha kuwa dhamira kuu ya Serikali ni kuhakikisha miundombinu yote ya michezo nchini inaboreshwa na kufikia viwango vinavyokidhi mahitaji ya sasa. "Moja ya changamoto kubwa iliyopo hapa Kirumba ni ukosefu wa mfumo wa taa unaowezesha uwanja kutumika kwa ufanisi nyakati za usiku. Hali hii imekuwa ikipunguza fursa za kufanyika kwa baadhi ya shughuli za michezo, hususan mechi na matukio yanayohitaji matumizi ya uwanja wakati wa usiku, naahidi hili nita...

TREASURY REGISTRAR HOLDS TALKS WITH TDB PRESIDENT

 By the OTR Reporter Dar es Salaam. Treasury Registrar Mr Nehemiah Mchechu has held talks with Trade and Development Bank (TDB) President and Managing Director Mr Admassu Tadesse on strengthening the bank’s partnership with Tanzania, with a focus on supporting economic development and unlocking greater value from public investments. The talks, held on Friday, August 7, 2026, at the Office of the Treasury Registrar (OTR) in Dar es Salaam, brought together Mr Mchechu and Mr Tadesse alongside officials from both sides to discuss opportunities for deeper cooperation in investment financing, trade and development. The engagement is of particular significance given that the Government, through the OTR, holds an 8.3 per cent stake in TDB, making Tanzania one of the bank’s shareholders. Mr Mchechu said a stronger partnership with TDB could help expand investment, trade and access to capital for projects with the potential to generate broad economic benefits. He noted that, as a regional de...

MSAJILI WA HAZINA ATETA NA RAIS WA BENKI YA BIASHARA NA MAENDELEO

 Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam.  Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara na Maendeleo (TDB), Bw. Admassu Tadesse, kuhusu namna benki hiyo inavyoweza kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha ufanisi wa uwekezaji wa Serikali. Mazungumzo hayo yana umuhimu wa kipekee kwa Tanzania kwa kuzingatia kwamba Serikali, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, inamiliki asilimia 8.3 ya hisa katika TDB na hivyo kuwa miongoni mwa wanahisa wa benki hiyo ya maendeleo ya kikanda. Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi ya Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam yalijikita katika maeneo mbalimbali ya ushirikiano, ikiwemo namna TDB inavyoweza kuongeza mchango wake katika maendeleo ya Tanzania na kuimarisha ufanisi wa uwekezaji wa Serikali. Bw. Mchechu alisema ushirikiano kati ya Tanzania na TDB ni muhimu katika kuendeleza uwekezaji, biashara na upatikanaji wa mitaji...