Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

JKCI, GGML GLOBAL MEDICARE WAUNGANISHA NGUVU KUOKOA WATOTO 300

 Na Mwandishi Wetu, Geita GEITA Gold Mining Limited (GGML) imetenga takribani Sh bilioni 1.2 kwa kipindi cha miaka mitatu kusaidia matibabu ya watoto 300 wenye magonjwa ya moyo nchini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza upatikanaji wa huduma za kibingwa kwa watoto ambao familia zao zinaweza kushindwa kumudu gharama za matibabu. Kupitia makubaliano yaliyosainiwa leo katika ofisi za makao makuu ya Geita Gold Mining Limited (GGML) mkoani Geita, kati ya GGML na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), kampuni hiyo itatoa takribani Sh milioni 400 kila mwaka kusaidia matibabu ya watoto 100 wenye matatizo ya moyo, hivyo kufikisha jumla ya takribani watoto 300 ndani ya kipindi cha miaka mitatu. Ushirikiano huo umefikiwa kwa uratibu wa Global Medicare ya jijini Dar es Salaam, ambayo imekuwa ikiunganisha wadau na kuhamasisha upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo nchini. Makubaliano hayo yanaongeza nguvu katika juhudi za Serikali na wadau w...
Recent posts

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUPUNGUZA MUDA WA MELI ZA MAFUTA BANDARINI

 SERIKALI imeweka mkakati wa kupunguza muda ambao meli za mafuta hukaa bandarini, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika upokeaji na usambazaji wa mafuta pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji zinazoweza kuathiri bei kwa watumiaji. Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dk. James Mataragio, amesema hayo wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER), jijini Dar es Salaam. Amesema Serikali inalenga kuhakikisha meli zinazowasili nchini zinashusha mafuta kwa ufanisi na kuondoka bandarini kwa wakati, huku akisisitiza kuwa kila taasisi na mdau anayehusika katika mnyororo wa upokeaji na usambazaji wa mafuta anapaswa kutekeleza wajibu wake kwa wakati. “Ni matarajio ya Serikali kuona meli zikifika, zinashusha mafuta na kuondoka. Kila taasisi inapaswa kufahamu jukumu lake na kujipanga ipasavyo,” amesema Dk. Mataragio. Amesema baadhi ya maghala binafsi yanak...

SERIKALI YAONGEZA FURSA KWA WATANZANIA KUNUFAIKA NA SEKTA YA MADINI

▪️Ni kupitia Local Content ▪️ Yatenga Huduma na Bidhaa 20 kwa ajili ya Kampuni za kitanzania pekee* ▪️ Watanzania wanufaika asilimia 86 ya manunuzi ya bidhaa na huduma migodini* ▪️ Ajira 20,421 zalizalishwa, Watanzania wachukua asilimia 94 *📍DODOMA* Serikali imeendelea kufanya maboresho katika Sheria na Kanuni za Madini kwa lengo la kuongeza ushiriki wa Watanzania katika sekta ya madini, hususan katika utoaji wa huduma, usambazaji wa bidhaa na upatikanaji wa ajira migodini. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde wakati akitoa ufafanuzi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini leo Agosti 14, 2026 Bungeni jijini Dodoma waliotaka kujua ni namna gani Serikali imejipanga kutekeleza mpango wa Uwajibikaji wa Wamiliki wa Leseni kwa Jamii na Ushirikishwaji wa Watanzania katika Uchumi wa Madini. Amesema kuwa, kupitia Tume ya Madini, Serikali imetenga bidhaa na huduma 20 zinazopaswa kusambazwa na kutolewa na Watanzania au kampuni zinazomilikiwa na Watanz...

RAIS SAMIA AHITIMISHA KIZIMKAZI KWA KUKARIBISHA UWEKEZAJI ZAIDI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewakaribisha wawekezaji kutumia fursa zinazoendelea kukua mkoani Kusini Unguja, kufuatia maendeleo ya miundombinu, huduma za jamii na shughuli za kiuchumi. Akihutubia katika kilele cha Tamasha la Kizimkazi, 2026 leo tarehe 14 Agosti, 2026, Rais Dkt. Samia ameeleza kuwa Wilaya ya Kusini imebadilika kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni, ikichochewa na ongezeko la uwekezaji na miradi ya maendeleo. Rais Dkt. Samia amesema fursa hizo, pamoja na uwekezaji katika miundombinu, zimeendelea kuvutia shughuli mpya za kiuchumi, akisisitiza wajibu wa viongozi kuhakikisha uwekezaji huo unaacha manufaa ya kudumu kwa wananchi. Aidha, ametoa rai kwa wawekezaji kutumia fursa mpya zitakazoambatana na ujenzi wa uwanja wa michezo Kusini Unguja, unaotarajiwa kutumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika. Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia amewataka wananchi kuendelea kulinda amani, umoja, usalama na utulivu ...

KIZIMKAZI FESTIVAL 2026: SAMIA AONGOZA SHEREHE, NCHIMBI ASHIRIKI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameshiriki Kilele cha Tamasha la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026) lililofanyika katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar. Tamasha hilo limeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

WATANZANIA WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA NA CAF KUELEKEA AFCON 2027

 DAR ES SALAAM, AGOSTI 14, 2026 Watanzania, kampuni, taasisi na watoa huduma wenye uwezo na sifa stahiki wamehimizwa kuchangamkia fursa mbalimbali za zabuni zilizotangazwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuelekea maandalizi na uendeshaji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON2027). Akitoa taarifa hiyo leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Kamati ya Ndani (LOC), Neema Msitha, amesema CAF imetangaza fursa mbalimbali za zabuni zinazohusiana na maandalizi na uendeshaji wa mashindano yake, ikiwamo AFCON 2027, ambayo Tanzania itaandaa kwa kushirikiana na Kenya na Uganda. “LOC inawahimiza Watanzania wenye uwezo, sifa na nia ya kushiriki fursa hizi kufuatilia matangazo rasmi ya zabuni hizo kupitia tovuti ya CAF ambayo ni https://www.cafonline.com/inside-caf/about-us/tenders/tenders-tab/ ili kusoma masharti ya kila zabuni na kuwasilisha maombi yao kufuatana na taratibu na muda uliowekwa na shirikisho hilo” amesisitiza Msitha. Amesema fursa hizo zinahusisha maeneo mbal...