Wahitimu wa vyuo vya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania wanatarajiwa kuwa na ujuzi unaoendana zaidi na mahitaji ya soko la ajira, kufuatia hatua inayochukuliwa kupitia Mradi wa ESPJII wa kuandaa viwango vya Kazi. Mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia unalenga kukuza viwango vya ujuzi nchini kwa kuimarisha mifumo ya mafunzo, kuwajengea uwezo walimu pamoja na kuboresha matumizi ya teknolojia katika sekta ya TVET. Akizungumza kuhusu mchakato huo leo Agosti 27,2026 Mratibu wa Mradi huo Bw. Aggrey Mleli amesema maandalizi ya miongozo ya Viwango vya kazi ni hatua muhimu katika kuhakikisha mafunzo yanayotolewa katika taasisi za TVET yanaendana na mahitaji halisi ya ulimwengu wa kazi. Mleli amesema kikao cha wadau kilichofanyika ni sehemu ya hatua ya pili ya kupitia na kukusanya maoni kutoka kwa wadau kabla ya miongozo hiyo kupelekwa katika ngazi za juu kwa ajili ya kuidhinishwa na kuanza kutumika katika maandalizi ya kuandaa vi...
Na S'SGT. Ponsiano Lindi - DSM Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amempongeza Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, kwakazi kubwa anayoifanya katika kuleta mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza, akieleza kuwa ni miongoni mwa viongozi wachache waliofanikiwa kuleta mabadiliko ndani ya muda mfupi. Mhe. Mpogolo, ametoa pongezi hizo, Agosti 27, 2026, wakati akishiriki zoezi la upandaji miti katika eneo la Kambi ya Magereza Mvuti, Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam. "Natoa pongezi za dhati kabisa kwa Jeshi la Magereza kwa kubuni na kuanzisha Kampeni ya “Magereza Nuru ya Mabadiliko”, kwa kushirikiana na TBC, ni kampeni muhimu katika kuufahamisha umma kuhusu kazi kubwa inayofanywa na Jeshi la Magereza katika kuwabadilisha wafungwa na kuwaandaa kurejea katika jamii wakiwa raia wema na wenye tija" amesema Mhe. Mpogolo Aidha, Mhe. Mpogolo, amesema Jeshi la Magereza lina uwezo wa kubadilisha maisha ya wafungwa kupitia programu mbalimbali za urekebishaj...