Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

KONGOLE CCM TANGA KWA UNUNUZI WA 'MZIKI MNENE' WA SHUGHULI ZA CHAMA

 NA: DK. REUBENI LUMBAGALA  Chama cha siasa kinapaswa kuwa na mikakati madhubuti ya kuwafikia wananchi wake, kuzungumza masuala mbalimbali ya maendeleo, kujadili changamoto zao na namna bora ya kuzitatua. Katika ulimwenguni huu wa maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia, suala la matumizi ya vifaa vya kisasa vya mawasiliano hayana budi kutumika. Katika shughuli za Chama na mikutano ya hadhara, matumizi ya mziki hayaepukiki katika kuhakikisha hadhira yote inasikia kinachozongumzwa katika meza kuu au jukwaani. Hivyo basi, katika kuhakikisha shughuli na mikutano ya hadhara inawafikia wananchi wengi zaidi, Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Tanga, kimenunua mziki mkubwa na wa kisasa kufanikisha azma hiyo. Mziki huo wenye vyombo vya kisasa, gari la matangazo na jenereta kubwa, vimenunuliwa na Mwenyekiti wa CCM mkoani humo na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu (MCC), Rajab Abdallah, maarufu 'Ustadhi Rajab.' Vyombo hivyo vya kisasa vinatarajiwa kutumika katika shughuli na mikut...
Recent posts

IKULU YATOA ONYO KALI....

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, imewaonya wananchi dhidi ya taarifa za uongo zinazotengenezwa kwa muonekano wa taarifa rasmi na kusambazwa mitandaoni, huku zikidaiwa kutolewa na Ikulu au kuhusishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika taarifa yake kwa umma, Kurugenzi hiyo imesema imebaini kuwepo kwa taarifa hizo ambazo zinatumia jina, nembo na utambulisho unaoweza kuwafanya wananchi kuamini kuwa zimetolewa rasmi na Ikulu. Kurugenzi imeeleza kuwa taarifa zote rasmi zinazohusu shughuli za Mheshimiwa Rais hutolewa kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, na wananchi wanapaswa kuzihakiki kupitia vyanzo rasmi kabla ya kuzipokea au kuzisambaza. Vyanzo rasmi vilivyotajwa ni pamoja na ukurasa wa Instagram wa Ikulu Tanzania (@ikulu_mawasiliano), Facebook wa Ikulu Tanzania (@ikulu.mawasiliano) pamoja na tovuti rasmi ya Ikulu. Aidha, Kurugenzi imewakumbusha wananchi kuwa utengenezaji na usambazaji wa taarifa za uongo kwa kutumia jina, nembo...

FEMATA YAFIKA KIZIMKAZI KUMPA POLE RAIS SAMIA

 Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA), John Wambura Bina , leo Septemba 8, 2026, amefika Kizimkazi, Zanzibar, nyumbani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan , kwenda kumpa pole kufuatia kifo cha mama mzazi wa Rais, Mzee Hafidh Ameir . Mzee Hafidh Ameir alifariki dunia jana, Septemba 7, 2026, na kuzikwa leo katika eneo la Kizimkazi, Zanzibar. Katika ziara hiyo, Rais wa FEMATA ameambatana na Makamu wa Rais wa FEMATA, Victor Michael Tesha , Mwenyekiti wa Wachimbaji wa Mkoa wa Geita, Charles Titus Kabuo , pamoja na Mama Sara Masasi , mmoja wa wamiliki wa kiwanda cha kusafisha dhahabu nchini. Viongozi hao wametoa salamu za pole kwa Rais Samia, familia na ndugu wa marehemu, huku wakimuomba Mwenyezi Mungu awape nguvu, faraja na uvumilivu katika kipindi hiki cha majonzi. Rais wa FEMATA amesema wamefika Kizimkazi kwa ajili ya kuonesha upendo, mshikamano na umoja wenye utu kwa Rais Samia na familia yake katika kipi...

TBN SEEKS STRATEGIC PARTNERSHIP WITH PSSSF TO EXPAND SOCIAL SECURITY EDUCATION

 DAR ES SALAAM The Tanzania Bloggers Network (TBN) has expressed its readiness to collaborate with the Public Service Social Security Fund (PSSSF) to expand public education on social security, pension schemes and investments undertaken by the Fund. Speaking during a meeting between TBN leaders and a PSSSF delegation at the network’s headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam, TBN Chairman Beda Msimbe said the organisation has more than 200 members across Tanzania and in the Diaspora, with the capacity to reach a broad audience through various digital platforms. Msimbe said TBN was prepared to use the expertise, experience and extensive reach of its members’ platforms to provide accurate information about the operations, services, investments and schemes managed by PSSSF. He, however, emphasised the importance of providing TBN members with comprehensive training on the Fund’s operations and services so that they could educate the public accurately and effectively. He said the partn...

TCU YAFUNGUA AWAMU YA PILI YA UDAHILI WA VYUO

Na Mwandishi Wetu - Dodoma Wanafunzi waliokosa nafasi katika awamu ya kwanza ya udahili wa Shahada ya Kwanza sasa wamepata fursa nyingine baada ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kufungua Awamu ya Pili ya Udahili kwa mwaka wa masomo 2026/2027. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Septemba 8,2026 na Katibu Mtendaji wa TCU Prof. Charles Kihampa amesema awamu hiyo itafunguliwa hadi Septemba 21, 2026, huku waombaji ambao hawakuweza kukamilisha maombi au hawakupata nafasi katika awamu ya kwanza wakitakiwa kutumia fursa hiyo kuomba katika vyuo wanavyopenda. "Taarifa hiyo inakuja wakati ambapo idadi kubwa ya vijana imeonyesha uhitaji wa kuendelea na elimu ya juu nchini, katika awamu ya kwanza, jumla ya waombaji 149,645 waliomba kujiunga na vyuo 93 vinavyodahili wanafunzi katika Shahada ya Kwanza",amesema. Amesema idadi ya programu za masomo zilizowasilishwa pia imeongezeka kutoka 894 mwaka 2025/2026 hadi 1,019 mwaka huu ikiwa ni sawa na ongezeko la programu 125. "Wanafunzi z...

PSSSF NA MTANDAO WA WANABLOGU TANZANIA (TBN) WAJENGA USHIRIKIANO MKAKATI WA KUONGEZA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII

 Dar es Salaam Katika kile kinachoelezwa kuwa ni hatua madhubuti ya kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika makao makuu ya muda ya Tanzania Bloggers Network (TBN) yaliyoipo Dar es salaam, Kijitonyama na kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wakuu wa mtandao huo. Mazungumzo hayo yaliyolenga kujenga ushirikiano wa manufaa ya pande zote mbili  yamejikita katika kuimarisha uhusiano wa kisekta kwenye masuala ya habari, uelimishaji wa umma, na usambazaji wa maarifa sahihi kuhusu mifumo ya pensheni na uwekezaji nchini. Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alieleza utayari wa mtandao huo kusimama kidete kama chombo cha kutoa elimu na kusambaza maarifa sahihi kwa umma na katika nyanja za kidijitali (space). Hata hivyo, alisisitiza kuwa ili kufikia malengo hayo kwa ufanisi zaidi, ni muhimu wanachama wa TBN wenyewe wakapatiwa kwanza mafun...