Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA AFUA ZA UKIMWI NCHINI

 Na. MWANDISHI WETU, MWANZA Serikali imedhamiria kuendelea kuimarisha afua za masuala ya UKIMWI nchini kwa kuboresha mazingira ya utekelezaji wa shughuli hizo, huku ikihimiza ushirikiano na wadau mbalimbali katika kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, alipotembelea na kujionea utekelezaji wa shughuli zinazotekelezwa na vikundi vya watu wanaoishi na Maambukuzi ya Virusi vya UKIMWI katika Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza. Akiwa katika ziara hiyo, Dkt. Yonazi amesema Serikali imeendelea kuboresha mazingira na kutenga bajeti inayosaidia kuratibu na kutekeleza afua za masuala ya UKIMWI nchini, huku ikishirikiana na wadau mbalimbali. “Ushirikiano ni muhimu sana kwani, tunaamini unauwezo wa kutuvusha katika mapambano dhidi ya VVU, ambapo tumeendelea kuunganisha nguvu pamoja katika mapambano hayo,” alisema Dkt. Yonazi. Aliongeza kuwa Ofisi ya Waziri...
Recent posts

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA AFUA ZA UKIMWI NCHINI

 Na. MWANDISHI WETU, MWANZA Serikali imedhamiria kuendelea kuimarisha afua za masuala ya UKIMWI nchini kwa kuboresha mazingira ya utekelezaji wa shughuli hizo, huku ikihimiza ushirikiano na wadau mbalimbali katika kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, alipotembelea na kujionea utekelezaji wa shughuli zinazotekelezwa na vikundi vya watu wanaoishi na Maambukuzi ya Virusi vya UKIMWI katika Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza. Akiwa katika ziara hiyo, Dkt. Yonazi amesema Serikali imeendelea kuboresha mazingira na kutenga bajeti inayosaidia kuratibu na kutekeleza afua za masuala ya UKIMWI nchini, huku ikishirikiana na wadau mbalimbali. “Ushirikiano ni muhimu sana kwani, tunaamini unauwezo wa kutuvusha katika mapambano dhidi ya VVU, ambapo tumeendelea kuunganisha nguvu pamoja katika mapambano hayo,” alisema Dkt. Yonazi. Aliongeza kuwa Ofisi ya Waziri...

MKUU WA MKOA DAR ES SALAAM ASILIKILIZA KILIO CHA WANANCHI WA TWANGOMA

Wananchi wa kata ya Twangoma jijini Dar es Salaam wameiomba Serikali kuwajengea daraja la kudumu eneo la Goloka B kwa Kibajaji, kwani lililopo sio salama na linahatarisha usalama wa watu hususani kipindi cha mvua. Hayo amebainisha baada ya kukagua daraja hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambapo ameagiza TARURA kufanya ukaguzi na kutoa tathimini kwenye eneo la daraja hilo ambapo Tathimini hiyo itabaini kama panafaa kujengwa daraja jipya au ipendekezwe eneo jingine litakalokuwa linaungana na barabara ili daraja hilo liweze kujengwa kwa haraka. Chalamila amesema ujenzi wa daraja la kudumu ni muhimu ili kuondoa hofu na usumbufu unaowapata wananchi kila msimu wa mvua. Amesisitiza kuwa Serikali haiwezi kuruhusu miundombinu inayoweka maisha ya wananchi hatarini iendelee kutumika bila kuboreshwa. Chalamila ametoa maagizo hayo leo Agosti 17, 2026 katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya Masaki iliyopo Toangoma pamoja na ya Ndunguru iliyopo Kibondemaji Wilaya ya Temeke...

WANANCHI WA MKOA WA TANGA WAMEOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA MAONESHO YA ELIMU NA UBUNIFU

Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewataka wananchi kujitokeza Kwa wingi kesho Agast 18 katika uzinduzi wamaonesho ya wiki ya kitaifa ya elimu ,ujuzi na ufubunifu yanafanyika katika viwanja vya usagara jijini Tanga ambapo mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri wa elimu,sayansi na teknolojia Mh. Adolf Mkenda. Aidha Balozi Batilda amesema lengo kuu la maonesho hayo ni kuonyesha mchango wa elimu ujuzi,sayansi, teknolojia na ubunifu katika kufikia malengo mielekoleo/dira ya elimu 2050. Akizungumza huhusu maandalizi ya maonesho hayo Balozi Batilda amesema mkoa umejipanga vizuri na wapo tayari kumpokea pro. Adolf Mkenda sambamba na washiriki wengine huku ulinzi na usalama ukiimarishwa zaidi. Katika maonesho hayo pia washiriki zaidi ya 300 wanatarajia kushiriki wakiwemo wawakilishi kutoka vyuo vikuu,vyuo vya mafunzo na ufundi stadi,taasisi za utafiti na maendeleo pamoja na taasisi zinazohusiana na sayansi na teknolojia. Mkoa wa Tanga umepokea kisai Cha ...

WANANCHI WA MKOA WA TANGA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA

  Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Wananchi mkoani Tanga wametakiwa kuchangamkia fursa zilipo mkoani humu huku wawekezaji wa ndani na nje ya nchi nao wakikaribishwa kuwekeza katika sekta ya madini. Wito huo umetolewa na kaimu afisa madini mkoa wa Tanga Mhandisi Laurent Bujashi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufutia fursa zilizo ongezeka katika mkoa kutokana na upanizi wa bandari uliofanywa na serikali. Mhandisi Bujashi amesema mpaka sasa fursa zilizopo ni kama biashara,utalii,uvuvi,kilimo,huduma, uchukuzi na mawasiliano,viwanda,nishati,ujenzi,fedha,pamoja na madini ambapo katika madini unaweza kujikita kwenye utafiti,uchimbaji,uchongaji,ama uuzaji wa madini. Aidha Bujashi ameongeza kuwa hadi sasa mkoani Tanga hakuna wachongaji wa madini badala yake hutegemea Vito vilivyo chongwa kutoka mkoani Arusha au Dar es salaam wakati madini mengi hupatikana Tanga. Bujashi alimalizia kwa kusema kuwa Kila penye mafanikio hapakosi changamoto na mpaka sasa changamoto kubwa katika sek...

RAIS DKT. MWINYI AHIMIZA KUIMARISHWA KWA DIPLOMASIA YA UCHUMI NA MALAYSIA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amemtaka Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Meja Jenerali Mbaraka Naziad Mkeremy, kutumia nafasi yake kuimarisha diplomasia ya uchumi, hususan katika kuvutia uwekezaji, kukuza biashara na kuongeza watalii kutoka Malaysia wanaotembelea Zanzibar. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 17 Agosti 2026, alipokutana na Balozi Mkeremy, aliyefika Ikulu Zanzibar kuaga na kupokea maelekezo kabla ya kuelekea katika kituo chake kipya cha kazi nchini Malaysia. Amesisitiza umuhimu wa kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar katika utalii, hoteli na makaazi, uvuvi, mafuta na gesi pamoja na maeneo mengine ya Uchumi wa Buluu. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amemtaka Balozi Mkeremy kuimarisha ushirikiano wa Zanzibar na Malaysia katika elimu, ikiwemo kuongeza fursa za ufadhili wa masomo na ushirikiano baina ya vyuo vikuu. Naye Balozi Mkeremy amesema amepokea maelekezo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi katika utekelezaj...