WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania waendelee kuhimizana kuhusu ulinzi wa Taifa na kamwe wasipuuze viashiria vya uvunjifu wa amani. "Tuendelee kuhimizana kuhusu suala la ulinzi wa Taifa letu. Ulinzi wa Taifa letu ni wa kila Mtanzania na amani yetu ni ya kila Mtanzania." "Sasa hivi hatupaswi kupuuzia viashiria vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Hatutakiwi kuvipuuza kwa sababu vimetuachia doa," amesema. Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 28, 2026) katika ibada maalumu ya kilele cha harambee iliyofanyika kwenye usharika wa Amani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kati, mjini Singida. Harambee hiyo ambayo ni ya nne kufanyika, ililenga kukusanya sh. bilioni 1.4 kwa ajili ya kuboresha vituo vya huduma za afya, kuimarisha vituo vya huduma za elimu, utumishi na uinjilisti vya Dayosisi hiyo ambavyo vinapaswa kukamilika ifikapo Desemba, mwaka huu. Jumla ya sh. bilioni 1.331 zilikusanywa zikiwa ni fedha taslimu na ...
Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Leo wamefanikiwa kupanda miti isiopungua 1000 katika shule ya sekondari Ummy Mwalimu iliyopo katika kata ya maweni wilayani na hii ikiwa ni muendelezo wa shughuli za kijamii wanazoshiki katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake. Wakiwa katika zoezi hilo mgeni rasmi Naibu kamishna shughuli za ufundi - Kodi za ndani Ted Frank silkiluwasha amesema TRA pamoja na shughuli ilizonazo lakini pia imekuwa mstari wa mbele katika kushiriki mambo ya kijamii na hii na inadhihisha ushirikiano mzuri uliopo baina ya Mamlaka ya mapato Tanzania na jamii. Aidha Silkiluwasha pia amesisitiza utunzaji wa miti hiyo kwani Kwa kuilinda itasaidia kuilinda ozone laya,leya inayozuia mionzi ya jua kufika katika uso wa dunia ambayo ni hatari sana Kwa afya ya wanadamu na viumbe vingine vilivyopo. Sambamba na hilo amemtaka Meneja wa TRA mkoa wa Tanga kuendelea kutoa elimu ya Kodi kwani elimu hiyo inapaswa kuwa endelevu na ili kuboresha ha...