Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mheshimiwa Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah, anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 19 Juni, 2026 kwa ziara ya kitaifa. Ziara hiyo, ambayo ni ya pili kuifanya nchini Tanzania tangu aingie madarakani, inaendelea kudhihirisha uhusiano wa kindugu na wa kihistoria kati ya Tanzania na Namibia, uliojengwa katika misingi ya harakati za ukombozi wa Afrika, mshikamano na ushirikiano wa maendeleo unaonufaisha wananchi wa pande zote mbili. Tarehe 20 Juni, 2026, Rais Nandi-Ndaitwah atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam, yatakayojikita katika masuala mbalimbali ya ushirikiano wa pande mbili pamoja na masuala ya kikanda na kimataifa katika maeneo yenye maslahi ya pamoja. Baadaye, viongozi hao wawili watazungumza na waandishi wa habari. Akiwa nchini, Rais Nandi-Ndaitwah atatembelea eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam, ambako aliwahi kuishi katika miaka ya...
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi, amewataka wafugaji nchini kuongeza mwitikio wa kuchanja mifugo dhidi ya magonjwa mbalimbali ili kuimarisha afya ya mifugo, kuongeza uzalishaji na kupunguza hatari ya maambukizi ya magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Dkt. Bitanyi ametoa wito huo leo, Juni 18, 2026, mjini Morogoro wakati wa kikao cha pamoja kati ya TVLA na timu ya Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) unaotekelezwa chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Kikao hicho kililenga kujadili maeneo ya ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo. Amesema bado kuna mwitikio mdogo wa wafugaji wadogo katika kuchanja mifugo yao licha ya uwepo wa chanjo zinazozalishwa na TVLA, huku wafugaji wakubwa wakionesha ushiriki mkubwa zaidi katika kampeni za chanjo. “Tunaona mwitikio mkubwa zaidi miongoni mwa wafugaji wakubwa, lakini kwa wafugaji wadogo bado ni mdogo. Tunao utaalamu na wataalamu. Kupitia mradi huo,...