Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam SERIKALI imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kuhakikisha Watu Wenye Ulemavu wanapata nafasi sawa katika nyanja zote za maendeleo, ikiwa ni pamoja na kijamii, kiuchumi na kisiasa, kupitia sera, sheria na mipango jumuishi inayotekelezwa nchini. Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichowakutanisha viongozi wa vyama vya Watu Wenye Ulemavu na mashirika yasiyo ya kiserikali kujadili utekelezaji wa sera, sheria na miongozo ya ujumuishaji nchini. Amesema hatua kubwa zimeendelea kuchukuliwa katika kuhakikisha hakuna mwananchi anayeachwa nyuma, ambapo Sera ya Taifa ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2004 pamoja na Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 zimekuwa msingi muhimu wa utekelezaji wa haki na usawa kwa kundi hilo. “Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa kila sera, mpango na huduma inayotekelezwa nchini inazingatia ujumuishaji wa Watu Wenye Ulemavu tangu ha...
INADES-FORMATION TANZANIA YASHIRIKIANA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS KUANDAA MPANGO WA MAZINGIRA WILAYA YA BAHI
By Prosper Makene Katika juhudi za kuhakikisha Tanzania inafikia azma ya kuwa nchi ya kijani ifikapo mwaka 2050, Shirika la INADES-Formation Tanzania kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira limeandaa kikao kazi cha kuandaa Mpango wa Usimamizi wa Mazingira wa Wilaya ya Bahi, kwa kushirikisha wataalamu kutoka Wilaya za Chemba na Kondoa. Akifungua kikao hicho Leo katika ofisi ya Makamu wa Rais, Mtumba mjini Dodoma, Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira, Dk. Paul Deogratius, alisema ushiriki wa Wilaya za Chemba na Kondoa utasaidia kubadilishana uzoefu katika mchakato wa kuandaa mpango huo kwa Wilaya ya Bahi. Alieleza kuwa mipango ya usimamizi wa mazingira katika ngazi ya wilaya ni takwa la kisheria na ni nyenzo muhimu katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za mazingira zinazozikabili halmashauri nchini. "Kitaifa, zimetambuliwa zaidi ya changamoto 13 za mazingira, huku kila wilaya ikiwa na changamoto zake ...