Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe.Dkt.Netumbo Nandi-Ndaitwah wakati wakishuhudia utiaji saini wa Hati nne za makubaliano ya ushirikiano katika Sekta za biashara , Maendeleo ya biashara ndogo na za kati, Ulinzi , pamoja na ushirikiano wa Miji kati ya Manispaa ya mji wa Zanzibar na Manispaa ya Swakopmund kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari, Ikulu Jijini Dar-es-salaam, tarehe 20 Juni, 2026.
Mbunge wa Misungwi mkoani Mwanza, Silvery Salvator ameainisha vipaumbele vya maendeleo ya jimbo hilo akisisitiza umuhimu wa sekta za maji, kilimo, barabara, afya, elimu pamoja na fursa zinazotokana na Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR). Akizungumza kuhusu hali ya maendeleo ya jimbo hilo, Salvator amesema kipaumbele kikubwa kwa wananchi wa Misungwi ni upatikanaji wa maji safi na salama. Amesema licha ya jimbo hilo kuwa na vyanzo vikubwa vya maji, bado baadhi ya maeneo yanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji. Katika sekta ya kilimo, ameeleza kuwa Misungwi ina fursa kubwa ya uzalishaji kupitia mabonde na maeneo yanayofaa kwa umwagiliaji, ambayo yanaweza kutumika kuzalisha mazao ya chakula na biashara kama mboga mboga, matunda na nafaka. Amesisitiza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya umwagiliaji utaongeza tija na kuchochea uchumi wa wananchi. Kuhusu miundombinu ya usafiri, Mbunge huyo amesema ujenzi na ukarabati wa barabara pamoja na madaraja ni muhimu katika kufungua shughuli ...