Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imewataka wananchi nchini kuhakikisha wanamiliki ardhi zao kisheria, ikieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kupunguza migogoro ya ardhi na kuongeza fursa za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Leonard Akwilapo amesema umiliki rasmi wa ardhi unasaidia kulinda haki za wananchi, kuongeza thamani ya maeneo yao pamoja na kuweka mazingira salama ya uwekezaji na uzalishaji. Akizungumza leo Mei 28,2026 bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Dkt. Akwilapo amesema serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kurasimisha umiliki wa ardhi ili wananchi wengi zaidi waweze kupata hati na nyaraka halali za maeneo yao. Amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026 wizara ilijiwekea lengo la kuandaa na kusajili hatimiliki 500,000, kutoa hati za hakimiliki ya kimila 520,000, hati za sehemu ya jengo 1,000 pamoja na vyeti vya ardhi ya vijiji 100 na kushughulik...
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Leonard Akwilapo amesema serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Kudhibiti Migogoro ya Ardhi nchini, hatua inayolenga kumaliza changamoto ya migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikiathiri wananchi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania. Akizungumza leo Mei 28 bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha bajeti ya wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Dkt. Leonard Akwilapo amesema mkakati huo umeandaliwa kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu na kuhakikisha matumizi ya ardhi yanafanyika kwa utulivu, haki na maendeleo endelevu. Amesema hatua hiyo inatekelezwa kufuatia maelekezo ya Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba aliyeitaka Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuandaa mpango maalumu wa kushughulikia chanzo cha migogoro hiyo nchini. Kwa mujibu wa Dkt. Akwilapo, mkakati huo umehusisha makundi yote muhimu yanayotumia ardhi ikiwemo wakulima, wafugaji, wawek...