Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Profesa Palamagamba Kabudi, amesema Serikali imeendelea kupata mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya kupitia operesheni maalumu za ufuatiliaji na udhibiti nchini. Akiwasilisha taarifa kuhusu hali ya dawa za kulevya kwa waandishi wa habari leoei 29,2026 jijini Dodoma, Profesa Kabudi amesema mwaka 2025 jumla ya tani 26.36 za mirungi zilikamatwa, ikiwa ni ongezeko la asilimia 42.88 ikilinganishwa na mwaka 2024. Amesema ongezeko hilo linaonyesha kuimarika kwa ufanisi wa operesheni za ufuatiliaji na udhibiti, hususan katika maeneo ya mipaka na njia zinazotumika kusafirisha dawa hizo nchini. Kwa upande wa dawa za kulevya za viwandani, Profesa Kabudi amesema Serikali ilikamata kilogramu 907.18 za methamphetamine, kilogramu 672.23 za heroin, kilogramu 4.89 za cocaine, pamoja na gramu 178 za MDMA na gramu 7.82 za MDA. Aidha, amebainisha kuwa kwa mara ya kwanza mwaka 2025, Serikali ...
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Profesa Palamagamba Kabudi, amesema Serikali imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kuhakikisha waathirika wanapata huduma za tiba na marekebisho ya tabia. Profesa Kabudi ameyasema hayo leo Mei 29,2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2025. Amesema katika mwaka huo, jumla ya watu 85,425 wenye uraibu wa dawa za kulevya walipatiwa huduma za tiba kupitia vitengo vya afya ya akili vilivyopo katika hospitali za rufaa za mikoa na kanda, kliniki za MAT pamoja na nyumba za upataji nafuu nchini. Ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuhakikisha waathirika wanapata huduma stahiki zinazowasaidia kurejea katika maisha ya kawaida na kuwa sehemu ya kuchangia maendeleo ya taifa. Aidha, Profesa Kabudi amesema Serikali pia imeendelea kuimarisha elimu kwa umma kuhusu madhara ya dawa...