Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RC MHITA AITAKA MSALALA KUFUNGA HOJA ZA CAG KWA WAKATI

MSALALA, SHINYANGA  Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kuhakikisha inatekeleza kwa wakati mapendekezo yote yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), akisisitiza kuwa hatua hiyo itaimarisha uwajibikaji, uwazi na matumizi sahihi ya rasilimali za umma. Mhe. Mhita ametoa maelekezo hayo leo, Julai 8, 2026, wakati akifungua Baraza Maalumu la kujadili na kupitia hoja za ukaguzi wa CAG kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30, 2026, lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Amesema utekelezaji wa hoja za CAG si suala la hiari, bali ni wajibu wa kila taasisi ya umma kuhakikisha dosari zilizobainishwa zinarekebishwa kwa wakati ili kuongeza ufanisi wa usimamizi wa fedha za Serikali na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi. "Hoja za CAG zinapaswa kutazamwa kama fursa ya kuboresha utendaji wetu. Hakikisheni kila hoja inafanyiwa kazi kwa wakati na kufungwa kwa mujibu wa taratibu," amesis...
Recent posts

BALOZI WA AMANI ASIFIA UTULIVU ULIOJITOKEZA MWANZA

 Balozi wa Amani Tanzania na Katibu wa Mahusiano wa Jumuiya ya Wachimbaji Tanzania (FEMATA), Mess Chengula, amepongeza hali ya amani na utulivu iliyoendelea kutawala jijini Mwanza, akisema ndiyo msingi wa maendeleo na ustawi wa wananchi. Akizungumza leo baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ya jiji hilo, Chengula alisema ameridhishwa kuona shughuli za kijamii na kiuchumi zikiendelea, huku baadhi ya maduka yaliyokuwa yamefungwa yakifunguliwa tena na kuanza kutoa huduma. "Ninawapongeza Watanzania kwa kuchagua amani siku hii ya leo. Furaha kubwa kwa binadamu ni kuona amani ikitawala mioyoni mwa watu," amesema. Aidha, aliiomba Serikali kuendelea kusikiliza makundi mbalimbali yenye malalamiko ili kutatua changamoto kwa njia ya mazungumzo na kuimarisha utulivu nchini. Chengula amesema amani huwezesha wananchi kujishughulisha kwa uhuru katika shughuli za uzalishaji mali, huku akisisitiza kuwa maridhiano yanayotarajiwa kufanywa kati ya Serikali, vyama vya siasa na makundi mbalimbali ...

AKIMWAKILISHA DKT.POSSI KATIKA MKUTANO WA WIPO,BALOZI TEMU ASISITIZA MAREKEBISHO YA MIFUMO YA MALI MILIKI

Na Mwandishi Wetu Geneva – Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva ametoa wito wa kuwa na mifumo ya mali miliki (Intellectual Property)inayojumuisha wote, yenye usawa na inayolenga mustakabali ili kuchochea ubunifu na maendeleo endelevu. Akizungumza katika Mkutano wa 68 wa Mabaraza ya Nchi Wanachama wa Shirika la Kimataifa la Mali Miliki WIPO, Balozi Temu aliwashukuru Mwenyekiti na Makamishna wenzake kwa uongozi wao. Pia alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa WIPO, Bw. Daren Tang, kwa kuteuliwa tena na kuipongeza Sekretarieti kwa maandalizi bora ya mkutano huo. Tanzania iliungana na tamko lililosomwa na Afrika Kusini kwa niaba ya Nchi za Afrika na Nepal kwa niaba ya Nchi Zinazoendelea. Balozi Temu, ambaye alikuwa anamwakilisha Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa na Mashirika mengine ya Kimataifa Geneva, Mhe. Dkt. Abdallah S. Possi, alisema Tanzania inatambua mali miliki kama kichocheo muhimu cha ubunifu, viwanda na maend...

REPRESENTING DR.POSSI, AMBASSADOR TEMU CHAMPIONS INTELLECTUAL PROPERTY SYSTEMS REFORM

  By Prosper Makene  Geneva- Deputy Permanent Representative of the United Republic of Tanzania to the United Nations in Geneva has called for inclusive, balanced, and future-oriented intellectual property systems to drive innovation and sustainable development. Addressing the 68th Series of Meetings of the Assemblies of Member States of WIPO, Ambassador Temu thanked the Chairperson and Vice-Chairs for their leadership. She also congratulated WIPO Director General Mr. Daren Tang on his re-appointment and commended the Secretariat for excellent preparations. Tanzania aligned itself with statements delivered by South Africa on behalf of the African Group and Nepal on behalf of the Least Developed Countries. Ambassador Temu, who represented the Permanent Representative of Tanzania to the United Nations and other international organizations in Geneva, H.E. Dr. Abdallah S. Possi, said Tanzania recognizes intellectual property as a strategic driver of innovation, creativity, industr...

DKT. KIRUSWA: MAGEUZI SEKTA YA MADINI YAIFANYA TANZANIA KUWA KITOVU CHA UWEKEZAJI AFRIKA*

🔶_Tume ya Madini yaeleza usimamizi wa leseni za madini na Local Content unavyowanufaisha Watanzania_ 🔶_Fursa za uwekezaji zatangazwa kuanzia utafiti, uchimbaji hadi uongezaji thamani wa madini_ 📍Dar es Salaam Serikali imesema mageuzi yanayoendelea kutekelezwa katika sekta ya madini chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yameifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye mazingira bora ya uwekezaji barani Afrika, huku ikiwakaribisha wawekezaji kuwekeza katika utafiti, uchimbaji, uchenjuaji, uchakataji na uongezaji thamani wa madini. Kauli hiyo imetolewa leo, Julai 8, 2026, na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, wakati akifungua Kongamano la Madini lililofanyika katika Ukumbi wa Dome, ndani ya Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu Sabasaba. Dkt. Kiruswa amesema maboresho ya sera, sheria na mifumo ya usimamizi wa sekta ya madini yameongeza uwazi, uwajibikaji na ushiriki wa sekta binafsi, hatua zilizochochea ongezeko la uwekezaji...

BARABARA YA MZUNGUKO DODOMA MWAROBAINI MSONGAMANO WA MAGARI

▪️ Madereva Waeleza Inavyorahisisha Safari ▪️Wafanyabiashara Washerehekea *Na Adelina Johnbosco – MAELEZO* Barabara za Mzunguko Jijini Dodoma imechangia kwa kiasi kikubwa kuondoa msongamano wa magari katikati ya jiji, hususan magari makubwa ya mizigo ya ndani na yanayokwenda nchi za nje. Mradi huu wa barabara ya njia nne kwa kiwango cha lami una urefu wa jumla ya kilometa 112.3 huku sehemu ya kwanza (lot 1) yenye kilometa 52.3 ikiwa imekamilika kwa asilimia 93.3. Barabara hii imeunganisha barabara kuu za mikoa minne, bandari kavu Ihumwa - Morogoro, Veyula - Arusha, Nala - Singida na Matumbulu – Iringa ambako sehemu ya pili ya ujenzi (lot 2) inaanzia. Shughuli za usafiri na usafirishaji tayari zimeanza katika barabra hiyo, watumiaji wanashuhudia urahisi wa safari kutokana na kutokuwepo foleni.  “Imeturahisishia sana, inafanya safari iwe fupi kutokana na ukweli kwamba njia hii haina foleni hata kidogo kama kule mjini kati, mwanzoni kutoka Ihumwa hadi Nala ilikuwa tunatumia takribani ...