Mwenyekiti wa Taasisi ya Mkono wa huruma Tanzania (MWAHUTA), Araphaty Japhary Mayala amesema taasisi hiyo imefanikiwa kuchinja takribani ng’ombe 700 mwaka huu kwa ajili ya kugawa nyama kwa makundi mbalimbali yenye uhitaji, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza huduma za kijamii na kusaidia wananchi wasiojiweza. Matendo hayo ya huruma ni kutokana na mafundisho ya dini ya kiislamu kama anavyosema Mwenyezi Mungu katika QUR'AN tukufu inapofika sikukuu ya Eid ul-Adha ni vema kuchinja Mnyama ili Kutoa sadaka Kwa jamii inayokuzunguk Akizungumza jijini Dodoma, wakati akitekeleza ibada ya kuchinja Mayala amessema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mkubwa kutoka kwa wadau, viongozi wa serikali, viongozi wa mitaa na wananchi walioshiriki kufanikisha zoezi hilo muhimu. Mayala pia Ametoa shukrani za dhati kwa viongozi wote waliowaunga mkono, hususan Mkuu wa Wilaya ambaye alisema amekuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano ikiwemo kuhakikisha upatikanaji wa ulinzi na huduma za madaktari kwa ajili ya...
WANAFUNZI 246,197 WALIOPANGIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO WANAPASWA KURIPOTI SHULENI JULAI 04, 2026 - PROF. SHEMDOE
Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 246,197 wakiwemo wasichana 114,102 na wavulana 132,095 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2026 wanatakiwa kuripoti shuleni kuanzia Julai 04, 2026 hadi Julai 31, 2026 kwakuwa muhula wa kwanza wa masomo utaanza Julai 06, 2026. Prof. Shemdoe amesema hayo leo Juni 01, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo ya Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Magogoni Jijini Dar es Salaam, wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi kwa mwaka 2026. “Wanafunzi 172,114 sawa na asilimia 69.9 wakiwemo wasichana 85,987 na wavulana 86,127 wenye sifa wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule za sekondari za Serikali 856 zikiwemo shule za bweni 825, kutwa 25 na kutwa na bweni sita (06),” amefafanua Prof. Shemdoe. Aidha, Prof. S...