Na Mwanamkuu Mwandoro,Lushoto. Jeshi la polisi mkoani Tanga limemtia mbaroni mtuhumiwa wizi wa mtoto mchanga katika hospitali ya wilaya ya Lushoto aliyefahamika Kwa jina la Habiba Fundi. Akizungumza na waandshi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Almachius Mchunguzi amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Juni 21,2026,saa Moja usiku katika kitongoji Cha Gerekaya,Kijiji Cha kwemashai wilayani Lushoto akiwa na mtoto huyo. Mchunguzi amesema Juni 19,majira ya saa Moja jioni mama mzazi wa mtoto huyo Mwanaidi Nyaki ,mkazi wa Kijiji Cha Kwemakame aliripoti kupotelewa na mtoto wake wa siku Moja. Kamanda mchunguzi amesema uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa mwanamke huyo ambaye hakufahamika Kwa wakati huo alijenga ukaribu na mama mzazi pamoja na ndugu walikuwa wakimuhudumia hospitalini,na baada ya kujenga urafiki na kuaminiwa alitumia fursa hiyo kumchukuwa mtoto huyo mchanga na kumuweka kwenye beseni lenye nguo na kutoweka nae. Aidha kamanda huyo pia aliongeza kuwa aliidanganya f...
Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa watakiwa kuharakisha utatuzi wa migogoro na kusimamia matumizi bora ya leseni za madini_ 📍MOROGORO Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, amewataka watendaji wa Tume ya Madini nchini kuendelea kuimarisha usimamizi wa Sekta ya Madini kupitia usimamizi madhubuti wa leseni za madini, utatuzi wa migogoro kwenye uchimbaji wa madini pamoja na kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za mnyororo wa thamani wa madini ili sekta hiyo iendelee kutoa mchango mkubwa katika Pato la Taifa. Akizungumza katika kikao cha Menejimenti ya Tume ya Madini kilichofanyika mkoani Morogoro, Mhandisi Samamba amesisitiza umuhimu wa Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kuhakikisha leseni zinazotolewa kwa wachimbaji zinaendelezwa kwa mujibu wa masharti ya leseni hizo, akibainisha kuwa Serikali haitasita kufuta leseni zisizoendelezwa na kuzipatia kwa wawekezaji au waombaji wenye uwezo na dhamira ya kuziendeleza. Aidha, amewataka Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kushugh...