Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

RAIS SAMIA NA RAIS NETUMBO WASHUHUDIA WATIAJI SAINI HATI ZA MAKUBALIANO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe.Dkt.Netumbo Nandi-Ndaitwah wakati wakishuhudia utiaji saini wa Hati nne za makubaliano ya ushirikiano katika Sekta za biashara , Maendeleo ya biashara ndogo na za kati, Ulinzi , pamoja na ushirikiano wa Miji kati ya Manispaa ya mji wa Zanzibar na Manispaa ya Swakopmund kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari, Ikulu Jijini Dar-es-salaam, tarehe 20 Juni, 2026.
Recent posts

SALVATOR:MAJI, KILIMO,BARABARA NA USAFIRI WA SGR NDIO KIPAUMBELE CHANGU MISUNGWI

 Mbunge wa Misungwi mkoani Mwanza, Silvery Salvator ameainisha vipaumbele vya maendeleo ya jimbo hilo akisisitiza umuhimu wa sekta za maji, kilimo, barabara, afya, elimu pamoja na fursa zinazotokana na Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR). Akizungumza kuhusu hali ya maendeleo ya jimbo hilo, Salvator amesema kipaumbele kikubwa kwa wananchi wa Misungwi ni upatikanaji wa maji safi na salama.  Amesema licha ya jimbo hilo kuwa na vyanzo vikubwa vya maji, bado baadhi ya maeneo yanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji. Katika sekta ya kilimo, ameeleza kuwa Misungwi ina fursa kubwa ya uzalishaji kupitia mabonde na maeneo yanayofaa kwa umwagiliaji, ambayo yanaweza kutumika kuzalisha mazao ya chakula na biashara kama mboga mboga, matunda na nafaka. Amesisitiza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya umwagiliaji utaongeza tija na kuchochea uchumi wa wananchi. Kuhusu miundombinu ya usafiri, Mbunge huyo amesema ujenzi na ukarabati wa barabara pamoja na madaraja ni muhimu katika kufungua shughuli ...

ELIMU YA ULINZI NA USALAMA BINAFSI WA MTOTO YATOLEWA KATIKA KAMBI YA WATOTO YA KANISA LA ROC DODOMA.

 Katika kuhakikisha Watoto wanakuwa na uangalizi mzuri kuanzia ngazi ya familia Kanisa la ROC Dodoma limewapatia  elimu ya ulinzi na usalama binafsi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwajengea uwezo wa kujilinda dhidi ya changamoto na vitisho mbalimbali vinavyowakabili katika jamii ya sasa. Akishiriki katika Mafunzo hayo Mkuu wa Polisi Jamii Wilaya ya Kipolisi Mtumba Mrakibu wa Polisi (ASP)Charles Mwamtobe aliwahimiza watoto kuwa waangalifu na kutambua mapema viashiria vya hatari vinavyoweza kuhatarisha usalama wao, ikiwemo ukatili, unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya teknolojia, dawa za kulevya, biashara haramu ya binadamu pamoja na ushawishi wa makundi yenye mienendo isiyofaa. Alieleza kuwa mtoto si mali ya familia pekee, bali ni tumaini la jamii na taifa la leo, hivyo anapaswa kulindwa na kupewa malezi bora yatakayomwezesha kukua katika mazingira salama, yenye maadili mema na hofu ya Mungu. “Ulinzi na usalama wa mtoto si jukumu la serikali pekee wala wazazi peke yao, b...

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE

 ðŸ“ŒAsema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima 📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko sanifu ya umeme takribani Mil 1 📌Awapongeza Wafanyakazi kwa ubunifu na jitihada za kuwahudumia wateja kwa ufanisi. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amewaondoa hofu wananchi kuhusu matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, akisema kuwa TANESCO imejipanga kujenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima. Mkurugenzi huyo amesema hayo Juni 19, 2026, alipotembelea banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, mkoani Dodoma. Amesema shirika linatambua kuwa mahitaji ya umeme yanaendelea kuongezeka kutokana na kukua kwa shughuli za kiuchumi, hivyo jitihada zinaendelea kufanyika kuhakikisha umeme unawafikia wananchi kwa ubora na uhakika kwa matumizi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi. “TANESCO inafanya kazi kubwa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Ai...

RAIS DKT. MWINYI: MFUMO WA SNR UMEFUNGUA UKURASA MPYA WA MAWASILIANO KATI YA SERIKALI NA WANANCHI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR) umechangia kupunguza urasimu, kuimarisha uwajibikaji wa watendaji wa Serikali na kujenga daraja la mawasiliano kati ya wananchi na Serikali yao.  Akizungumza katika mahojiano maalum ya kutathmini miaka mitano ya mfumo huo yaliyofanyika Ikulu, Zanzibar, amesema SNR imewawezesha wananchi kuwasilisha malalamiko na maoni yao moja kwa moja na kupatiwa ufumbuzi kwa haraka na uwazi. Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza kuwa mfumo huo unashughulikia changamoto za kijamii na kiutendaji, huku masuala ya kimahakama yakipaswa kufuata taratibu rasmi za kisheria, ikiwemo kukata rufaa pale mwananchi anapokuwa hajaridhishwa na hukumu. Katika kipindi cha miaka mitano, SNR imepokea malalamiko 22,521, ambapo 20,623, sawa na asilimia 91.6, yamepatiwa ufumbuzi. Kwa mwaka 2026, Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) imetunukiwa Tuzo ya Taasisi Bora, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Maf...

WAZIRI WA FEDHA AFUNGUA SEMINA YA TWPG KUHUSU BAJETI YENYE MLENGI WA KIJINSIA

 Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar, akiwa mgeni rasmi, amefungua Semina ya Umoja wa Wabunge Wanawake Tanzania (TWPG) kuhusu Bajeti yenye Mlengo wa Kijinsia iliyofanyika leo, tarehe 19 Juni 2026, katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma. Akizungumza katika ufunguzi wa semina hiyo, Mhe. Omar amesema bajeti yenye mlengo wa kijinsia ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha kuwa wanawake, watoto na makundi maalum wanapata fursa sawa na kunufaika kikamilifu na utekelezaji wa mipango na matumizi ya rasilimali za umma. Amesema kuwa utekelezaji wa bajeti hizo unachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza pengo la kijinsia, kupunguza umaskini na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi kwa kuzingatia usawa na ujumuishi. “Bajeti yenye mlengo wa kijinsia inatuwezesha kufanya maamuzi sahihi ya maendeleo kwa kuzingatia mahitaji halisi ya makundi mbalimbali ya kijamii, huku ikihakikisha rasilimali za umma zinatumika kwa ufanisi na kwa usawa,” amesema Mhe. Omar. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TWPG, ...