Na Na Angela Sebastian ;Kagera Wananchi wa Kijiji cha Kaitambunzi, Kata ya Isingiro wilayani Kyerwa, wameiomba Serikali kuchunguza utaratibu unaotumiwa na baadhi ya maafisa wa Uhamiaji wakati wa operesheni za usiku za kusaka wahamiaji haramu, wakidai zimekuwa zikisababisha hofu hata kwa raia wasiokuwa na makosa. Kero hiyo iliwasilishwa katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, Khalid Nsekela, ambapo wananchi walisema wanaunga mkono juhudi za Serikali za kudhibiti uhamiaji haramu, lakini wakasisitiza operesheni zifanyike kwa kuzingatia sheria, taratibu na haki za wananchi. Alistidia Mbatina ni mkazi wa kijiji hicho amesema kuwa licha ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kudhibiti uhamiaji haramu, wanahitaji operesheni hizo kufanyika kwa kuzingatia sheria, taratibu na haki za wananchi ili kuepusha taharuki na hofu isiyo ya lazima ambayo inawakabili kwa sasa. "Operesheni zinazofanyika nyakati za usiku wa manane zimekuwa zikitutia hofu,wanakuja watu wanakamat...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Abdel Fattah El-Sisi, wamefungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kimkakati kwa kusaini makubaliano yatakayoongeza kasi ya maendeleo katika sekta za biashara na uwekezaji, kilimo, uchukuzi, afya, elimu na nishati. Makubaliano ambayo yanatarajiwa kuimarisha uchumi wa mataifa yote mawili na kufungua fursa mpya za maendeleo kwa wananchi. Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya mazungumzo rasmi na mgeni wake aliyekuwa katika ziara ya kikazi ya siku moja nchini, Rais Samia amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Misri tayari umezaa matokeo makubwa, ikiwemo kuwapatia huduma za upasuaji wa kwa wagonjwa wa moyo wa kitanzania wapatao 420 pamoja na utekelezaji wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) wenye thamani ya takribani shilingi trilioni 7.4. Rais Samia pia amesema viongozi hao wamekubaliana kuendeleza maboresho ya Bandari ya Bagamoyo kwa kuiunganisha na mtandao w...