Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

APANDISHWA KIZIMBANI AKIDAIWA KUMUUA MAMA YAKE MZAZI

 Na: Dawati la Habari Polisi Geita Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita limemfikisha mahakamani Lufuta Magoma (40) Mganga wa Kienyeji na mkazi wa kijiji cha Rutunguru akituhumiwa kwa mauaji ya Dotto Magoma Nyara (70) ambaye ni mama yake mzazi. Mshtakiwa huyo amepandishwa kizimbani leo Ijumaa Julai 10, 2026, katika Mahakama ya Wilaya ya Chato na kusomewa shtaka la Mauaji. ​Akisoma shauri hilo la jinai namba 15471 la mwaka 2026 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Chato, Mhe. Erick Kagimbo, Wakili wa Serikali Mashaka Said, aliieleza mahakama kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 04.06.2026 katika Kijiji cha Rutunguru, wilaya ya Geita. ​Mshtakiwa akiwa katika eneo la Rutunguru anadaiwa kumshambulia na kumuua Mama yake mzazi kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023. ​Hata hivyo, mshtakiwa huyo hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kusikiliza mashauri y...
Recent posts

SMAUJATA KUFANYA ZIARA YA KUPINGA UKATILI MKOANI MARA

 Leo Julai 10,2029, Viongozi pamoja na watendaji wa Taasisi isiyo ya kiserikali SMAUJATA ( Shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii Tanzania) Wamefika katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Mtambi kwaajili yakumsalimia pamoja na kumueleza kuhusu ziara yao mkoa wa Mara yenye lengo kutoa elimu ya kupinga ukatili kwa watoto, wanawake na wababa mkoani hapo yenye kauli mbiu isemayo " Kataa ukatili, wewe ni shujaa", wakiwa wameambatana na wawakilishi vya mikoa mingine iliyopo kanda ya Ziwa.

SOYA ONE, ELIAKIMU MASWI WAPONGEZWA KWA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS SAMIA KUBORESHA ELIMU TARIME

 Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele, ameipongeza Kampuni ya Soya One Limited pamoja na Eliakim Maswi kwa kujitolea kutoa vifaa vya TEHAMA kwa shule za sekondari wilayani humo, akisema mchango huo ni kielelezo cha uzalendo na unaunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha sekta ya elimu nchini. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo, Meja Gowele amesema Serikali ya Wilaya inaamini maendeleo ya elimu hayawezi kuachwa mikononi mwa Serikali pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo wawekezaji, wafanyabiashara, viongozi wa kisiasa na wananchi. Amesema kila mwenye uwezo anapaswa kuchangia maendeleo ya elimu kwa kiwango anachoweza, akisisitiza kuwa hakuna mchango mdogo unapolenga kuboresha maisha ya watoto na mustakabali wa Taifa. "Sio lazima uwe na uwezo mkubwa ndiyo uchangie elimu. Hata mchango mdogo unaweza kuleta mabadiliko makubwa. Tunawapongeza Soya One Limited na Eliakim Maswi kwa moyo wao wa kujitolea. Huu ni mfano mzuri u...

BMH YAREJESHA TABASAMU KWA WATOTO WA BURUNDI BAADA YA UPASUAJI WA MOY

 Watoto watatu kati ya sita kutoka nchini Burundi wenye matatizo ya matundu ya moyo wamefanyiwa upasuaji wa kuziba matundu hayo kwa mafanikio katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), hatua inayodhihirisha uwezo wa Tanzania katika huduma za kibingwa na kuimarisha ushirikiano wa afya katika ukanda wa Afrika Mashariki. Huduma hiyo imetolewa kupitia ushirikiano kati ya Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na wataalamu wa afya kutoka Burundi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukuza tiba utalii na kubadilishana utaalamu wa kitabibu. Akizungumza na waandishi wa habari Julai 9, 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa BMH, Prof. Abel Makubi, alisema watoto wote waliopatiwa matibabu wanaendelea vizuri na wameonyesha maendeleo ya kuridhisha baada ya kufanyiwa upasuaji huo. “Mafanikio haya yanaonyesha uwezo wa taasisi zetu za afya kushirikiana kutoa huduma za kibingwa zinazokidhi viwango vya kimataifa. Ushirikiano huu pia umefungua fursa ya kubadilishana ...

MRADI WA MINARA 758 WAIPA TANZANIA TUZO YA KIMATAIFA YA WSIS 2026

 Tanzania imepata heshima ya kutunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya WSIS Prizes 2026 kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano ulioongeza upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya vijijini na ambayo hayakuwa na huduma ya mawasiliano nchini. Tuzo hiyo imepokelewa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki(Mb.) katika hafla iliyofanyika Geneva, Uswisi, ikiwa ni utambuzi wa mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha miundombinu ya mawasiliano. Mradi huo ulizinduliwa rasmi na Mhe. Rais tarehe 10 Aprili, 2026. Mbali na kutwaa tuzo hiyo, Tanzania ilipata uteuzi katika vipengele saba (7) vya Tuzo za WSIS 2026 na kufanikiwa kuibuka na tuzo mbili kwa ujumla, huku pia ikitunukiwa vyeti vya kutambua miradi iliyofanya vizuri.

CHATANDA: MARIDHIANO CCM NA ACT-WAZALENDO YAMEZINGATIA MASLAHI YA ZANZIBAR

 NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Maridhiano baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Alliance For Change and Transparency (ACT-Wazalendo) kuelekea uundwaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) Zanzibar, umepongezwa kwani umezingatia maslahi ya nchi ambayo ni muhimu kuliko maslahi binafsi ya wanasiasa. Hayo yameelezwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM na Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, Julai 9, 2026, Jijini Dodoma. Akitoa maoni yake baada ya kumalizika hafla hiyo ya Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa baina ya vyama hivyo, Chatanda amesema, Wazanzibar wameshasahau siasa za chuki, kipaumbele chao sasa ni umoja, mshikamano na maendeleo. "Wazanzibar ni watu rahimu sana, wao wanataka amani, mshikamano na maendeleo na kitendo cha vyama hivi viwili kufikia muafaka, ni ishara ya ukomavu wa kisiasa na kuzingatia maslahi ya nchi," amesema Chatanda. Aidha, amesema maridhiano hayo yana maana kubwa katika kuhakikisha SUK inaundwa kwa ukamilifu wake kwani SUK ...