Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg, Urusi BODI ya Utalii Tanzania (TTB) inajipanga kumega keki ya utalii inayotengenezwa na Urusi kwa lengo la kulipatia taifa zaidi ya dola za Marekani 500 kwa mwaka. Zaidi ya wananchi milioni 13.4 wa Urusi hutalii sehemu mbalimbali duniani na kutokana na kuwa watumiaji wazuri wa vipato vyao, Tanzania ikipata angalau asilimia 1 ya watu hao ambacho ni sawa na watu 134,000 ambao wataingiza dola milioni 500. Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la Petersburg (SPIEF’26) linaloendelea mjini hapa. Mafuru alisema katika mikakati hiyo wanataka katika miaka 10 ijayo kufikisha watalii mara mbili ya hao na hivyo kuliingizia pato taifa la dola za Marekani bilioni moja. Akiwa katika banda la Tanzania katika jukwaa hilo alisema anafurahi kwa Rais Samia kuendelea kuelekeza maono kwa vitendo katika kusaka wawekezaji. Pia kufungua fursa za Watanzania kwa ziara zinazojumuisha watendaji wakuu wa maen...
Na Beda Msimbe, TBN, St Petersburg Rais Samia Suluhu Hassan leo anahitimisha ziara yake nchini Urusi kwa kushiriki katika kongamano la kibiashara kati ya Tanzania na Urusi sanjari na Jukwaa la Kimataifa la Biashara la St Petersburg. Katika jukwaa hilo Rais Samia anatarajiwa kuinadi Tanzania katika sekta za uwekezaji na biashara. Ziara ya Rais Samia imekuwa na mafanikio makubwa hasa hakikisho la ushiriano wa karibu na Urusi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ya uendelezaji wa rasilimaliwatu na ukuzaji wa teknolojia. Ziara hiyo katika taifa lenye nguvu kubwa kiteknolojia, uchakataji na uzalishaji kwenye kilimo au viwandani imekuja wakati Tanzania inajiandaa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kulifanya taifa kuwa na pato la dola trilioni moja kwa mwaka. Kwa sasa serikali ime...