Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WASIRA:UJAMAA BADO NI MSINGI WA MAENDELEO NCHI

*Elimu bila malipo, Bima ya Afya kwa Wote ni ushindi* MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, Stephen Wasira, amesema ujamaa bado ni msingi mkuu unaoendesha sera na mipango ya maendeleo nchini. Akizungumza na wanachama wa CCM mjini Moshi, leo Juni 6 2026, Wasira alisema alikana madai kuwa mfumo huo umepitwa na wakati. "Wale wanaojidanganya hawaujui. Misingi inayoendesha nchi sasa ni ileile ya ujamaa. Tuanzie na elimu bila malipo, tuendelee na jitihada za kuanzisha Bima ya Afya kwa wote. Haya yote ni mafanikio ya ujamaa," alisema. Wasira alitoa mfano wa Mkoa wa Kilimanjaro, akibainisha kuwa kama sio ujamaa, ardhi na mashamba ya kahawa yangekuwa yamenunuliwa na watu binafsi na wananchi wasingeweza kumiliki. "Kama hapa Kilimanjaro tungekosa ujamaa, kahawa yote ingenunuliwa. Ni uongo kusema ingekuwa bado mikononi mwa wananchi," alieleza. Pia, alizungumzia umuhimu wa uwekezaji wa sekta binafsi, akisema ni jambo la kawaida na la lazima kwa ukuaji wa uchumi wa ...
Recent posts

DKT. MWIGULU AAGIZA UCHUNGUZI WA MAPATO YA MAEGESHO IFUNDA

  WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amemwagiza Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa kufanya uchunguzi wa kina kuhusu ukusanyaji wa mapato ya maegesho katika eneo la Ifunda wilayani Iringa na kuwasilisha taarifa kamili kuhusu namna mapato hayo yalivyokuwa yakikusanywa kabla na baada ya mabadiliko ya mfumo wa ukusanyaji pamoja na matumizi yake. Ametoa agizo hilo leo Jumamosi, Juni 6, 2026 wakati akizungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Jimbo la Kalenga katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ifunda wilayani Iringa mkoani Iringa. Agizo hilo lilitolewa baada ya Waziri Mkuu kuwataka viongozi wa TANROADS, Halmashauri na TAKUKURU kutoa maelezo kuhusu mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya maegesho katika eneo hilo na mabadiliko yaliyofanyika katika usimamizi wake. “Nataka ripoti yote ya zoezi la ukusanyaji jinsi ambavyo limefanyika, kabla na sasa. Nataka tujue fedha hizi zimeenda wapi na wahusika walikuwa nani,” alisema Dkt. Mwigulu. Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kupitia mifumo...

TANZANIA YA KIJANI: MAAMUZI YA LEO, URITHI WA KESHO

 Na Gideon Gregory - Dodoma  Katika kipindi ambacho dunia inaendelea kukabiliwa na ongezeko la joto, uchafuzi wa mazingira mjadala kuhusu mazingira haupo tena kwenye uhifadhi pekee bali umehamia kwenye namna ambavyo mataifa yanajenga maendeleo yanayodumu.  Takwimu za Umoja wa Mataifa za miaka ya hivi karibuni zinaonyesha kuwa shinikizo la mazingira linaongezeka kila mwaka na kufanya hatua za sasa kuwa msingi wa maisha ya vizazi vijavyo. Ni katika muktadha huo ambapo maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu kwa Tanzania yamekuja na ujumbe wa “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania” kauli inayobeba zaidi ya kampeni ya kupanda miti ili kurejesha uoto wa asili. Akizungumza kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyila Jijini Dodoma Mei 5,2026 Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi anabainisha kuwa mazingira yanamchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa taifa na ustawi wa wananchi.  "Pale ambapo mazingira yametunzwa vyema basi uchumi na ustawi wa maisha ya wa...

MAVUNDE: USHIRIKIANO NA URUSI UTAONGEZA UTAFITI WA MADINI TANZANIA

  WAZIRI  wa Madini Nchini Tanzania Anthon Mavunde Leo June 5,2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Serikali ya Urusi kwenye sekta ya madini ukiongozwa na Naibu Waziri wa Maliasili(Madini) na Mazingira wa Shirikisho la Urusi, *Mh. Tetenkin Dmitry Dmitrievich*. “Pamoja na kuendelea kukua kwa kasi kwa sekta yetu ya madini, Nchi yetu imefanikiwa kufanya utafiti wa kina kwa asilimia 16 pekee. Hivyo, iwapo tutaongeza eneo kubwa litakalokuwa limefanyiwa utafiti, kutatanua wigo wa taarifa zaidi za mashapo ya madini na kuvutia zaidi wawekezaji, Eneo hili la utafiti tunaona ni fursa kubwa ya kuanza nayo katika kuimarisha mashirikiano yetu na Serikali ya Urusi kutokana na hatua kubwa mliyopiga hususan katika utafiti wa kijiolojia na teknolojia ya kisasa kupitia maabara zenye vifaa bora”  Tumezungumza juu uwepo wa Hati ya Makubaliano(MoU) baina ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) na Chuo Kikuu cha Urusi ambayo bado haijakamilika na kumwomba kuiwekea nguvu i...

DKT. MWIGULU NCHEMBA ATATUA MGOGORO WA ARDHI ULIDUMU MIAKA 41 NYOLOLO MUFINDI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ametatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka 41 kati ya Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana  Mtume Nyololo wilayani Mufindi Mkoa wa Iringa na Familia ya   Yosefa Mgavilenzi ambaye ni msimamizi wa mirathi ya marehemu Michael Bakari Seveyage. Akihutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Igowole Mufindi Kusini, Waziri Mkuu alipokea malalamiko ya familia ya  Yosefa Mgavilenzi kuwa eneo lake lenye ukubwa wa ekari 107 limechukuliwa na Kanisa hilo bila fidia na aliomba Waziri Mkuu amsidie ili alipwe. Mapema wiki hii Waziri Mkuu alituma timu ya wataalamu kutoka ofisi yake ambao walikwenda katika kata ya Nyololo na kufanya vikao vya maridhiano na viongozi wa Kanisa Katoliki, familia ya Yosefa, Wazee, viongozi wa Kata ya Nyololo na  kijiji  cha Nyololo Shuleni walioko madarakani na wastaafu pamoja na wananchi.  Baada ya majadiliano yaliyochukuwa siku tatu pande mbili husika zilikubaliana kumaliza mgogoro kwa njia y...

MAKUSANYO MADINI YAVUKA LENGO, YAKUSANYA TRILIONI 1.27

✅️ *Sawa na Asilimia 105.8, Zikiwa Zimebaki siku 26 Kufunga Mwaka wa Fedha 2025/26* ✅️ *Watumishi Watakiwa Kuongeza Weledi Kufikia Sh Trilioni 1.4 Mwaka 2026/27* ✅️ *Watumishi  Watakiwa kuhudumia wananchi bila ubaguzi* *Na Mwandishi Wetu, Dodoma* WIZARA ya Madini imevuka lengo la ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 baada ya kukusanya Sh trilioni 1.27 hadi Juni 5, 2026, dhidi ya lengo la Sh trilioni 1.2, huku ikitarajia kufikia Sh trilioni 1.3 ifikapo  Juni 30, 2026. Kutokana na mafanikio hayo, watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake wametakiwa kuondokana na uzembe, kuongeza bidii na kufanya kazi kwa weledi ili kufikia lengo jipya la ukusanyaji wa Sh trilioni 1.4 lililowekwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Akizungumza katika kikao cha watumishi wote wa Wizara ya Madini na taasisi zake ambazo ni GST, TEITI, Tume ya Madini, STAMICO na TGC, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, amesema mafanikio yaliyopatikana yanapaswa kuwa chachu ya kuon...