Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

SERIKALI YATANGAZA MIRADI YA LIGANGA NA MCHUCHUMA KUANZA RASMI MWAKA HUU WA FEDHA

Recent posts

Serikali Yatangaza Miradi ya Liganga na Mchuchuma Kuanza Rasmi Mwaka Huu wa Fedha

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali imekamilisha majadiliano ya utekelezaji wa Mradi Unganishi wa Chuma cha Liganga na Makaa ya Mawe ya Mchuchuma kupitia mwekezaji mpya wa Kampuni ya Shudao Investment Group Company Limited (SDIG) kwa kushirikiana na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC). Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Amesema kupitia majadiliano hayo, pande zote zimefikia makubaliano muhimu kuhusu mgawanyo wa hisa, muundo wa uwekezaji, usimamizi wa mradi, kiwango cha mtaji pamoja na uongezaji thamani wa madini ya chuma, vanadium na titanium hapa nchini. Aidha, rasimu za mikataba ya ubia (JVAs) na wanahisa (SHAs) tayari zimekamilika huku hatua za mwisho za idhini zikiendelea katika mamlaka husika. Serikali inatarajia mikataba hiyo kusainiwa katika nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha 2026/2027 kabla ya kuanza rasmi kwa ujenzi wa mradi utakaotekelezwa...

Kapinga: Tunaleta Intelijensia ya Masoko

  WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema Serikali imepanga kuanzisha Kitengo cha Intelijensia ya Masoko na Viwanda kwa lengo la kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la kimataifa. Akizungumza leo Mei 22, 2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Waziri Kapinga amesema hatua hiyo inalenga kusaidia upatikanaji wa taarifa sahihi za masoko, teknolojia na fursa za biashara duniani. “Katika mazingira ya sasa ya ushindani wa biashara na viwanda duniani, taarifa sahihi za masoko na teknolojia ni msingi muhimu wa maendeleo ya sekta ya viwanda na biashara,” amesema Kapinga. Amesema Serikali imebaini changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa taarifa za masoko ya kimataifa, mahitaji ya bidhaa katika misimu tofauti, viwango vya ubora pamoja na vikwazo vya kibiashara. “Kumekuwapo changamoto ya kutokujua bidhaa zinazohitajika katika misimu mbalimbali, viwango vya ubora na vikwazo vya kibiasha...

Kapinga:Tumekamata Vifaa vya Kuzalisha Pombe Haramu

  Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, akiwasilisha Bungeni jijini Dodoma Mei 22, 2026, amesema Serikali imeendelea kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia nchini kupitia Mamlaka ya Ushindani (FCC) pamoja na taasisi nyingine husika. Amesema hadi Aprili 2026, FCC ilitekeleza operesheni maalum katika maeneo mbalimbali, hususan mkoa wa Dar es Salaam, ambapo jumla ya chupa 4,251 za vinywaji bandia zilikamatwa, pamoja na chupa tupu 286 na katoni tupu 250. Katika operesheni hiyo, pia vifaa vya uzalishaji na ufungashaji wa bidhaa hizo vilikamatwa, vikiwemo mashine za kuchapisha maelezo ya bidhaa, kipima kilevi, mashine za kufunga vifuniko, mizani, ethanoli pamoja na vifaa vya kuchanganyia na kuchujia pombe. Aidha, FCC imebaini uwepo wa bidhaa nyingine bandia za vipuri na vilainishi, ambazo pia zilikamatwa, huku wahusika wakichukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria. Waziri Kapinga amesema Serikali imeweka mkakati madhubuti unaolenga kuimarisha uchunguzi wa kiintelijensi...

Kapinga:Tumezidisha Mapambano Dhidi ya Lumbesa Kumlinda Mkulima

  WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali itaendelea kuimarisha udhibiti wa changamoto ya “Lumbesa” ili kulinda wakulima, wafanyabiashara na walaji nchini. Akizungumza leo Mei 22, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Waziri Kapinga amesema Wakala wa Vipimo (WMA) una jukumu la kuhakikisha matumizi sahihi ya vipimo katika biashara kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo Sura ya 340. “Wizara kupitia WMA inaendelea kusimamia matumizi sahihi ya vipimo ili kulinda wakulima, wauzaji, wanunuzi na wasafirishaji wa mazao,” amesema Waziri Kapinga. Ameeleza kuwa sheria hiyo inazuia mazao yaliyofungashwa kwa idadi au uzito kuzidi kilo 100, huku ikiruhusu kiwango cha ziada kisichozidi asilimia 5 (tolerance limit), pamoja na kuwajibisha wafanyabiashara kutumia mizani iliyohakikiwa angalau mara moja kwa mwaka. “Sheria inaelekeza wazi kuwa vipimo lazima vizingatie viwango vilivyowekwa ili kuhakikisha ...

Wizara ya Viwanda na Biashara Yalenga Kuimarisha Uzalishaji na Ubunifu Kwa Vijana

  WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma leo Mei 22, 2026, amesema mpango na bajeti ya wizara umeandaliwa kwa kuzingatia miongozo ya kitaifa ikiwemo Dira ya Maendeleo 2050.  Amedema pia imezingatia Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa (2026/2027–2030/2031), Ilani ya CCM ya mwaka 2025, sera na sheria mbalimbali, pamoja na maoni ya kamati za Bunge na maagizo ya viongozi wakuu wa serikali. Aidha, Amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, wizara itatekeleza vipaumbele vyake ambavyo ni kuendeleza miradi ya kielelezo na kimkakati ya viwanda, kuimarisha uzalishaji viwandani kupitia ujenzi wa kongani za viwanda (Industrial Clusters) na maeneo maalum ya viwanda (Industrial Estates) kwa viwanda vidogo na vya kati, pamoja na kuchochea maendeleo ya viwanda na biashara kupitia ubunifu, teknolojia za kisasa na mafunzo ya ujuzi. Amevitaja vipaumbele vingine ni kuimarisha upatika...

Mradi wa Kokoto Wafungua Fursa Mpya za Uchumi Njombe

📍Njombe Mradi mkubwa wa uzalishaji wa kokoto uliopo mtaa wa Kambarage kata ya Njombe Mjini, unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa kokoto na kuchochea shughuli za kiuchumi na kuongeza mapato ya Serikali katika Mkoa wa Njombe. Mradi huo unaomilikiwa na mchimbaji mdogo wa madini ya ujenzi, Isaya Boniface, umefungwa mtambo mkubwa wa kusaga kokoto wenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 1,000 kwa siku kwa kushirikiana na kampuni ya India ya Shree Sonal Earth Ltd iliyotoa usaidizi wa kitaalam katika utekelezaji wake. Akizungumza kuhusu mradi huo, Boniface amesema uwekezaji huo utamaliza changamoto ya upatikanaji wa kokoto ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikisafirishwa kutoka mikoa ya Iringa, Dodoma na Pwani, hususan Lugoba, kwa matumizi ya miradi mbalimbali ya ujenzi mkoani Njombe. Amesema mradi huo utasaidia kupunguza gharama za ujenzi, kuongeza ajira kwa wananchi, kukuza mzunguko wa fedha pamoja na kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayohitaji kokoto kwa kiwango kikubwa. Kwa upand...

SUA Yafikisha Miradi 130 ya Utafiti inayotekelezwa Nchini

Na Farida Mangube Morogoro  Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeanza utekelezaji wa miradi mipya 12 ya utafiti yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 3.4 kwa lengo la kukuza maarifa na kutatua changamoto katika sekta za kilimo, mifugo, mazingira na maendeleo ya jamii kwa ujumla.  Hayo yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Profesa Raphael Chibunda, wakati wa mahafali ya 47 ya chuo hicho ambapo jumla ya wahitimu 877 walitunukiwa shahada mbalimbali na Mkuu wa Chuo, Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba. Profesa Chibunda amesema kuanza kwa miradi hiyo kumefanya chuo hicho kufikisha jumla ya miradi ya utafiti 130 inayoendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini. “Chuo kinaendelea kuhimiza matumizi ya matokeo ya tafiti zetu katika kuchangia sera na mipango ya taifa. Katika kipindi hiki cha taarifa, chuo kimeanza utekelezaji wa miradi mipya yenye thamani ya shilingi bilioni 3.4,” alisema Profesa Chibunda. Kwa upande wake, Mwenyekiti ...

Nyansaho, Balozi wa Uingereza Wajadili Kuimarisha Ushirikiano wa Ulinzi

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Rhimo Nyansaho leo tarehe 20 Mei 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa United Kingdom nchini Tanzania, Marianne Young katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Kikombo jijini Dodoma. Katika mazungumzo hayo, pande hizo mbili zilijadili namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Uingereza katika sekta ya ulinzi na usalama, ikiwemo mafunzo, mapambano dhidi ya ugaidi pamoja na usalama wa majini. Balozi Marianne Young alisema Tanzania ni mshirika muhimu wa Uingereza kutokana na historia na uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya mataifa hayo mawili, huku akieleza utayari wa serikali ya Uingereza kuendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali zikiwemo uchumi, utamaduni na maendeleo ya kijamii. Aidha, Balozi huyo aliipongeza Wizara ya Ulinzi na JKT pamoja na serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan kwa kuzindua M...

Sheria ya Elimu ni Nyenzo Muhimu ya Utekelezaji wa Mageuzi ya Elimu-Prof.Mkenda

Mageuzi ya elimu nchini yanahitaji mfumo imara wa kisheria utakaowezesha utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014, Toleo la 2023 na mitaala iliyoboreshwa. Hayo yameelezwa Mei 21, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda katika Kikao cha kujadili taarifa ya awali ya mapitio ya Sheria ya Elimu Sura 353 ambapo amesema maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu mageuzi ya elimu yameweka msingi wa maboresho ya sera, mitaala na sheria. Amebainisha kuwa tayari timu ya wataalamu imekamilisha kazi ya awali ya mapitio, na sasa Wizara inaendelea kukusanya maoni kutoka kwa wadau ili kukamilisha mchakato huo na kuwezesha kuwasilisha mapendekezo katika ngazi mbalimbali ngazi za maamuzi.  Aidha, amesema Serikali inatambua mchango mkubwa wa wadau wote wa elimu ikiwemo hivyo amesisitiza umuhimu wa ushirikishwaji mpana katika kutoa maoni kwa ajili ya mapitio ya Sheria. "Mhe. Rais alielekeza mageuzi yote yanayofanyika katika sekta ya elimu yashi...

Reo Ferdinand Akoshwa na Uwanja mpya wa AFCON 2027 Arusha

Nyota wa zamani wa mpira wa miguu wa timu ya Taifa ya Uingereza na Klabu ya Manchester United amesema, Uwanja wa  Arusha ambao utatumika katika Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027)  umejengwa kwa kiwango bora kilichozingatia viwango vya kisasa duniani. Amesema hayo Mei 21, 2026 wakati alipotembelea uwanja huo,ikiwa ni muendelezo  ziara yake hapa nchini, hususani  jijini Arusha ambapo aliongozana na mwenyeji wake, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe Paul Makonda. "Nimecheza kwenye viwanja vingi duniani lakini kiwanja hiki ni kizuri na chenye viwango, niwapongeze wajenzi, wakandarasi na watalaam wote wanaofanya kazi hii nzuri" alisema Rio. Ameweka bayana furaha yake na kufurahisha na namna alivyopokelewa na kukaribishwa na Watanzania akiahidi kurudi tena. Rio amesifu namna alivyokaribishwa na watanzania akisema  haijawahi kutokea kokote alikotembelea duniani. Ameisitiza kuwa amekaribishwa kwa tabasamu na upendo mkubwa, ch...

Serikali yaahidi kuboresha maslahi ya watumishi wa umma

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuboresha maslahi na mazingira ya kazi kwa watumishi wa umma nchini ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi. Waziri Kikwete amesema hayo leo Mei 21, 2026 wakati akishiriki ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 13 wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) uliofanyika Ngurdoto, Arusha. Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emanuel Nchimbi, na umehusisha zaidi ya wajumbe 5,050 kutoka Serikali Kuu, halmashauri na taasisi mbalimbali za Tanzania Bara na Zanzibar. Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Waziri Kikwete  ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha ustawi wa watumishi wa umma, ikiwemo kupandisha madaraja, kubadili miundo na vyeo pamoja na kulipa madeni ya mishahara. Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza maboresho hayo kila panapopatikana...