Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini mkoani Mara, Mwita Waitara, ameibua hisia kali Bungeni baada ya kuhoji namna ambavyo baadhi ya wananchi wanaendelea kuteseka kwa kukosa huduma muhimu huku fedha za umma zikidaiwa kutafunwa na wachache wasiowajibika. Akichangia Bajeti ya Wizara ya Fedha leo Juni 2, 2026, Jijini Dodoma, Waitara amesema ni jambo linaloumiza kuona wananchi wakihangaika kutafuta fedha za matibabu na dawa hospitalini, wakati ripoti za ukaguzi zinaendelea kuonyesha uwepo wa matumizi mabaya ya fedha za umma katika baadhi ya taasisi za Serikali. Kwa sauti ya msisitizo, Waitara ameeleza kuwa fedha zinazotengwa na Bunge zinapaswa kuwafikia wananchi na kuleta maendeleo yaliyokusudiwa, badala ya kupotea mikononi mwa watu wachache wanaokwamisha juhudi za Serikali na matarajio ya wananchi. “Leo hii kuna mwananchi anaondoka hospitalini bila dawa kwa sababu hakuna fedha za kutosha. Wakati huo huo, ripoti za ukaguzi zinaonyesha kuna watu wamechezea fedha za umma. Hili halipaswi ku...
SERIKALI YAWEKA MIKAKATI MIPYA YA KUCHOCHEA UCHUMI, KULIPA MADENI NA KUIMARISHA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA
SERIKALI imeanika vipaumbele vinane vya kimkakati vinavyolenga kuujenga uchumi imara, kuimarisha uwajibikaji wa kifedha na kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa katika mwaka wa fedha 2026/27. Akiwasilisha Bajeti ya wizara ya Fedha Kwa mwaka wa Fedha 2026/2027 leo Jun 2,2026 Bungeni Jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb.), amesema Serikali itaendelea kusimamia kwa umakini uchumi wa Taifa kwa lengo la kufikia ukuaji wa asilimia 6.3, kudhibiti mfumuko wa bei katika kiwango cha tarakimu moja na kuhakikisha akiba ya fedha za kigeni inaendelea kuwa katika viwango vinavyokidhi mahitaji ya nchi. Katika kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, Serikali imepanga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, ugawaji wa rasilimali na usimamizi wa bajeti ili kuhakikisha fedha za wananchi zinatumika kwa tija na kuleta matokeo yanayokusudiwa. Hatua nyingine muhimu ni kuendelea kulipa kwa wakati madeni ya Serikali, ambapo zaidi ya Shilingi trilioni 15.1 zimetengwa kw...