Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

IPU LEADERSHIP MEETS SPEAKER ZUNGU IN NEW YORK, RECEIVES ASSURANCE OF TANZANIA’S READINESS TO HOST 153RD ASSEMBLY IN ARUSHA

By Prosper Makene New York, USA– The Speaker of the Parliament of the United Republic of Tanzania, Hon. Musa Azzan Zungu, MP, has assured the Inter-Parliamentary Union (IPU) that Tanzania is fully ready to host the 153rd IPU Assembly scheduled for October 2025 in Arusha. Hon. Zungu made the assurance during a meeting with the IPU President, Hon. Dr. Tulia Ackson, MP, and the IPU Secretary General, Ambassador Anda Filip in New York, USA.  The meeting focused on reviewing the status of preparations, logistical arrangements, and overall readiness ahead of the global parliamentary gathering. The Speaker expressed satisfaction with the work of the National Organizing Committee that has been coordinating the event. All logistical, protocol and security arrangements are progressing according to plan, and that Tanzania is committed to delivering a world-class Assembly that reflects Tanzanian hospitality and efficiency. Hon. Zungu emphasized that hosting the Assembly is a matter of national...
Recent posts

KIFUNGO KILICHOBADILI MAISHA: MWENDWA AMSHUKURU HAKIMU ALIYEMHUKUMU

 LAMU, Kenya:  Baada ya kutumikia kifungo cha miaka minne gerezani, mwanamume aitwaye Mwendwa Kilatya alirejea kumtafuta Hakimu Mkazi Eugene Pascal Nabwana, aliyekuwa amemhukumu katika Mahakama ya Mpeketoni, Kaunti ya Lamu, ili kumshukuru na kumuomba msaada wa kuendelea na masomo ya chuo kikuu. Kilatya alihukumiwa kifungo cha miaka minne jela kwa kosa la wizi wa mifugo. Kabla ya hukumu hiyo, alikuwa ameacha shule akiwa Kidato cha Tatu, licha ya kuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri darasani. Akiwa gerezani, aliamua kurejea masomoni na kufaulu kwa matokeo mazuri, jambo lililompa matumaini ya kuendelea na elimu ya juu baada ya kumaliza kifungo chake. Baada ya kuachiwa huru, Kilatya alisafiri hadi Mahakama ya Wamunyu, Kaunti ya Machakos, ambako Hakimu Nabwana alikuwa amehamishiwa, ili kumshukuru kwa uamuzi wake ambao anasema ulimsaidia kubadili maisha yake na kumwelekeza katika njia sahihi. Akiguswa na simulizi na juhudi za Kilatya, Hakimu Nabwana aliahidi kuwashirikisha ...

SAKATA LA MAGENDO HOROHORO: WAZIRI WA FEDHA AAGIZA DORIA KALI, AONYA HATARI KWA USALAMA WA TAIFA

Na MASHAKA MHANDO, Horohoro  SERIKALI imeagiza kuimarishwa mara moja kwa doria na msako mkali dhidi ya biashara haramu ya magendo katika mpaka wa Horohoro, uliopo Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, ikiwa ni hatua madhubuti ya kudhibiti uvujaji wa mapato na kulinda usalama wa Taifa. Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, alipofanya ziara ya kimkakati katika Kituo cha Forodha cha Horohoro kujionea shughuli za ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa biashara ya kimataifa kati ya Tanzania na Kenya. Balozi Omar aliweka wazi kuwa udhibiti wa magendo sio tu suala la kuongeza mapato ya Serikali, bali ni msingi mkuu wa kulinda usalama wa nchi na kuhakikisha Taifa linakuwa na takwimu sahihi za kiuchumi. Jukumu Sio Kukusanya Mapato Tu Waziri huyo aliwapongeza maofisa wa forodha kwa kazi wanayofanya, lakini aliwataka kuongeza umakini maradufu kudhibiti bidhaa zilizopigwa marufuku kuingia nchini na zile zinazokwepa kufuata masharti ya kisheria. "Tusipotekeleza jukumu...

SERIKALI YAAHIDI KUTOA SH. MIL 750 KUMALIZA KITUO CHA AFYA

 NA MASHAKA MHANDO, Tanga SERIKALI imetoa ahadi ya kutoa Shilingi milioni 750 ili kukamilisha ujenzi wa majengo yaliyosalia katika Kituo kipya cha Afya cha Maweni, jijini Tanga, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha huduma za afya  kwa wananchi. Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar  wakati wa ziara yake ya kikazi jijini Tanga ambapo alikagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kituo cha afya Maweni sambamba na mradi wa mabweni katika shule ya sekondari Usagara na kuridhishwa na hatua iliyofikiwa. Balozi Omar alibainisha kuwa kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026, Serikali imejitahidi kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika Mkoa wa Tanga kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo. "Kwa mwaka huu wa fedha uliopita, Mkoa wa Tanga ulipangiwa kutumia Shilingi bilioni 528.1, na Serikali imewasilisha kiasi cha bilioni 487.5. Hii ni zaidi ya asilimia 92 ya fedha zote za maendeleo zilizopangwa," alisisitiza Balozi Omar. Katika hali ya kuonyesha kuridhishwa na usim...

CHATANDA: MAMA TIBAIJUKA, TUJENGE MSINGI WA UTII WA SHERIA NA SI MASHINIKIZO YA KUFUTA KESI KWA JINA LA MARIDHIANO

 NA: MWANDISHI WETU Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, amemshauri aliyewahi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka, kuwa balozi wa kuhimiza viongozi na wananchi kutii sheria za nchi ili kuepuka kuingia katika mikono ya vyombo vya sheria. Chatanda ameyasema hayo Julai 14, 2026, kufuatia ujumbe alioandika Prof. Tibaijuka katika Mtandao X, kuhusiana na kesi inayomkabili Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu. Katika ujumbe wake, Prof. Tibaijuka amesema "Dkt. Samia Suluhu, Mhe. Rais naendelea kushauri kwa dhati Tundu Lissu aachiwe huru kwani kesi haikamiliki, hekima na busara iliyotufanya kuitangaza sera ya 4Rs ulipoingia madarakani ikuongoze tena katika jambo hili". "Simulizi hizi za kutisha za vyombo vya habari vya kimataifa zinainua hisia kali hasa kwa vijana, hata wazee tumekumbushwa kadhia ya operation Sogeza na iliyounda Vijiji vya Ujamaa 1974-1976, taarifa hizi z...

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA MIFUMO YA UKUSANYAJI WA MAPATO KUPITIA USIMAMIZI MAKINI WA FORODHA

 Na Mwanamkuu Mwandoro,Mkinga. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) amesema Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato kupitia usimamizi makini wa forodha ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, kukuza biashara halali na kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Mhe. Waziri amesema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kituo cha Forodha cha Horohoro kilichopo Wilaya ya Mkinga, mkoani Tanga, ambapo alipata fursa ya kutathmini utendaji wa kituo hicho na kujionea mafanikio yaliyopatikana katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Alisema mafanikio yaliyofikiwa na Kituo cha Forodha cha Horohoro yanaonesha kuwa juhudi za Serikali za kuimarisha usimamizi wa forodha zinaendelea kuzaa matunda, huku mapato yanayokusanywa yakitoa mchango mkubwa katika kugharamia miradi ya maendeleo na kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi. "Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato k...