Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

ILANI ZA RAILA ODINGA KUANZA KUFUNDISHWA CHUONI

BAADHI ya manifesto ambazo aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Amolo Odinga alitumia katika kampeni zake za urais zitakuwa sehemu ya masomo katika Chuo cha Uongozi na Utawala cha Raila Amolo Odinga kinachoanzishwa chini ya Chuo cha Serikali Kenya (KSG). Chuo hicho, kilichozinduliwa Jumanne na Rais William Ruto wakati wa maadhimisho ya miaka 100 ya KSG, kinalenga kuhifadhi na kufundisha falsafa za Raila kuhusu utawala bora, demokrasia, huduma kwa umma na maendeleo ya bara Afrika. Mkurugenzi Mkuu wa KSG, Profesa Nura Mohamed, alisema kundi la kwanza la wanafunzi linatarajiwa kuanza masomo mwezi Septemba. Alisema mtaala wa chuo hicho utajengwa juu ya nguzo tano kuu zilizotawala maisha ya kisiasa ya Raila; umoja wa Afrika, uongozi ushirikishi, utawala bora, elimu na ubunifu, pamoja na amani na haki.  “Alipokuwa akiwania urais alikuwa na manifesto mbalimbali, na baadhi yake zitajumuishwa katika masomo ya chuo hiki ili maono yake yaweze kutekelezwa,” alisema. Profesa Mohamed alisema walipol...
Recent posts

ROYAL POLYCLINIC YAREJESHA MATUMAINI MARA, NHIF KUANZA KUTUMIKA HIVI KARIBUNI

 WANANCHI wa Mkoa wa Mara wanatarajia kupata ahueni ya huduma za afya baada ya Hospitali ya Royal Polyclinic kutangaza kuwa ipo katika hatua za mwisho za kuanza kutoa huduma kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), hatua inayotarajiwa kupunguza usumbufu wa kusafiri nje ya mkoa kutafuta matibabu ya kibingwa. Akizungumza katika Hospital ya Royal Polyclinic Musoma, Mkurugenzi wa Royal Polyclinic, Stella Eyembe, amesema hospitali hiyo imekamilisha taratibu muhimu za kuingia mkataba na NHIF na muda si mrefu wanachama wa mfuko huo wataanza kupata huduma zote za matibabu katika hospitali hiyo. "Kwa muda mrefu wananchi wengi wa Mkoa wa Mara walitamani huduma za NHIF zipatikane Royal Polyclinic. Sasa tupo katika hatua za mwisho za kukamilisha mkataba, na hivi karibuni wanachama wa NHIF wataanza kuhudumiwa hapa kwa urahisi na kwa viwango vya juu," amesema. Ameongeza kuwa mbali na NHIF, hospitali hiyo tayari inapokea wagonjwa kupitia bima nyingine mbalimbali huku ikiendelea kupanu...

MAGAMBO AGHARAMIA UJENZI WA MADARASA MATANO SHULE YA MSINGI RING'WAN

 KATIKA kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha sekta ya elimu nchini, mdau wa maendeleo wa Kata ya Nyamatare, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Bw. Fortinatus Magambo, amewekeza zaidi ya shilingi milioni 125 kugharamia ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa katika Shule ya Msingi Ring'wani. Bw. Magambo, ambaye ni mzaliwa wa Kata ya Nyamatare na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), amechukua hatua hiyo baada ya kushuhudia hali duni ya miundombinu ya shule hiyo, ambapo wanafunzi walikuwa wakisomea katika madarasa chakavu yasiyokidhi mazingira bora ya kujifunzia. Akiamini kuwa elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya jamii, aliamua kutumia sehemu ya fedha zake binafsi pamoja na kuhamasisha marafiki zake kuchangia mradi huo, ili kuhakikisha watoto wa Ring'wani wanapata mazingira salama, bora na yanayowapa fursa ya kujifunza kwa ufanisi. Ujenzi wa madarasa hayo unatarajiwa kuondoa changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa, kupunguza msongaman...

WAZEE WA MILA WA KOO 12 TARIME WATOA WITO WA KULINDA AMANI, WAMUOMBA RAIS SAMIA KUMTOA TUNDU LISSU

 Wazee wa Mila wa Koo 12 za Wakuria, Wilaya ya Tarime mkoani Mara, wametoa wito kwa vijana nchini kutokubali kutumiwa katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani ya Taifa, huku wakimuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuendelea na ajenda ya maridhiano kwa kuzingatia ombi la kumwachia huru Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Tundu Lissu. Akizungumza katika kikao Cha wazee wa Mila wa Koo 12 za wakuria, Mzee Morisi Mung'oso, mzee wa Koo ya Butimbaru, amesema kikao chao kilijadili masuala matatu muhimu ambapo walimpongeza Rais Samia na Serikali yake kwa hatua walizochukua katika kudumisha amani na utulivu nchini baada ya matukio ya vurugu yaliyoshuhudiwa mwaka 2025. Mzee Mung'oso Amesema wazee hao wanaamini amani ndiyo msingi wa maendeleo na kwamba Serikali imeonyesha uthabiti katika kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao unalindwa. Pili, amesema wamekemea kauli za viongozi wanaodaiwa kutumia lugha ya matusi na uchochezi dhidi ya viongozi ...

ELIMU YA UMEME NA NISHATI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANANCHI WA ARUMERU MASHARIKI

📌*Umeme sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji* 📌*Nishati safi ya Kupikia kwa kila mwananchi* 📍*Arusha* Wananchi wa Wilaya ya Arumeru Mashariki mkoani Arusha wameendelea kupata elimu kuhusu huduma za umeme na matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia ziara ya uhamasishaji iliyofanywa na maafisa wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Elimu hiyo ilitolewa leo wakati maafisa wa REA walipotembelea baadhi ya vijiji na vitongoji vinavyotekelezwa miradi mbalimbali ya nishati, ikiwemo miradi ya usambazaji wa umeme katika vitongoji pamoja na uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kama vile gesi na majiko banifu. Katika ziara hiyo, wananchi walipatiwa elimu kuhusu taratibu za kufanya maombi ya kuunganishiwa umeme, gharama za uunganishaji wa huduma hiyo pamoja na tahadhari ya kujiepusha na matapeli maarufu kama vishoka, ambao huwalaghai wananchi kwa kuwatoza fedha kinyume na utaratibu rasmi. Aidha, wananchi walihimizwa kujiunga na huduma ya umeme wakati mkandarasi bado yupo katika eneo l...

JOHARI:MAWAKILI WA SERIKALI WAWE NGUZO YA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050

 Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari, amewataka Mawakili wa Serikali nchini kuwa mstari wa mbele katika kuimarisha utawala wa sheria, kuendana na kasi ya maendeleo ya teknolojia na kutoa ushauri wa kisheria wenye tija ili kuiwezesha Tanzania kutimiza malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Johari alitoa kauli hiyo Julai 15, 2026, alipofungua rasmi msimu wa tatu wa Mafunzo ya Bespoke kwa Mawakili wa Serikali yanayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), yatakayodumu hadi Julai 17, 2026. Amesema mafanikio ya Dira ya Taifa 2050 hayatapatikana kwa uwekezaji pekee, bali yanahitaji mifumo imara ya sheria, sera zenye mwelekeo sahihi, taasisi zenye uwezo na wataalamu wa sheria watakaoisimamia Serikali kwa weledi na uadilifu. "Nitumie fursa hii kuwakumbusha washiriki wote kuwa, tunapoendelea kufikia malengo ya Dira ya Taifa 2050 ni muhimu kufahamu kuwa Taifa linahitaji zaidi ya utaalamu wetu wa sheria," amesema Johari. Ameeleza kuwa Mawakili wa...