Mbunge wa Jimbo la Ilala na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, amemtaka mkandarasi anayejenga Shule ya Sekondari ya Mfano ya CRDB iliyopo Kata ya Upanga Mashariki jijini Dar es Salaam kuongeza kasi ya ujenzi ili mradi huo ukamilike kwa wakati na kuanza kutumika Januari 2027. Mhe. Zungu ametoa maelekezo hayo Juni 7, 2026 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo akiwa ameambatana na TullyEsther Mwambapa. Akizungumza katika ukaguzi huo, Mhe. Zungu ameipongeza CRDB Bank chini ya uongozi wa Abdulmajid Nsekela kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha sekta ya elimu nchini. Amesema mradi huo wenye thamani ya takribani shilingi bilioni tano ni uwekezaji muhimu utakaosaidia kuongeza upatikanaji wa elimu bora kwa wanafunzi wa Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi. Kabla ya ukaguzi huo, Mhe. Zungu alishiriki mkutano wa kikanuni wa maendeleo wa wananchi wa Kata ya Upanga...
*Asisitiza Tsh Trilioni 1.2 zimewekezwa Kilimanjaro, sasa ni zamu ya mfumo wa Usambazaji.* MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Baraa, Stephen Wasira, ameiagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Same (SAUWASA) kuhakikisha inatatua kwa haraka changamoto ya upatikanaji maji inayowakabili wananchi wa mji wa Same. Wasira alitoa agizo hilo leo Juni 8, 2026 alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM wa Shina Namba 9, Tawi la Same, Kata ya Same, wilayani Same mkoani Kilimanjaro. Akijibu malalamiko ya wananchi kuhusu ukosefu wa maji, alisema haikubaliki kwa wakazi wa Same kuendelea kukosa huduma hiyo muhimu wakati maji yanapatikana kwa wingi kupitia miradi iliyotekelezwa na serikali. “Ninaiagiza SAUWASA kuhakikisha wananchi wa Same wanapata maji. Haiwezekani watu wa Same waendelee kuyasikia au kuyaona maji bila kuyapata kwa matumizi yao ya kila siku, mfumo wa usambazaji uharakishwe ili wananchi wanufaike na huduma hiyo muhimu,” alisema Wasira. Alibainisha kuwa, serika...