Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

TUNAAMUA MAMBO YETU KWA MASLAHI YA NCHI-WASIRA

 Aelezea ziara ya Rais Samia nchini Urusi Na MWANDISHI WETU SAME - Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema ziara ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi inathibitisha dhamira ya Tanzania kutofungamana na upande wowote. Akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wilayani Same mkoani Kilimanjaro Juni 9, 2026 wakati wa kuhitimisha ziara ya kukagua uhai wa Chama na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, Wasira alisema waasisi wa Taifa wakiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere waliitaka Tanzania kukaa katikati pale pande mbili zinapogombana. “Tulitaka tuwe huru na uhuru uwe wa kudumu. Kazi yetu ni kudumisha uhuru na kudumisha uhuru ni kutupa haki ya kuamua mambo tunayoona yanatufaa sisi, sio kutegemea wengine wakuambie mfanye nini,” alisema. Akizungumzia maswali kuhusu ziara ya Rais Samia Urusi, Wasira alidai: “Na juzi Rais wetu ameenda Urusi wengine wanauliza ameenda kufanya nini. Mbona alivyoenda China hamkuuliza, mbona alipoenda Marekani hamkuuliza. Akienda Urusi...
Recent posts

TANZANIA NA SINGAPORE ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

 Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, wamekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji ili kuongeza manufaa kwa wananchi wa mataifa hayo mawili kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. Kupitia makubaliano hayo, yalitofanyika mapema hii leo June 9, Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais samia ameeleza kuwa licha ya ukuaji wa biashara kati ya Tanzania na Singapore, kiwango cha sasa cha dola milioni 299 za Marekani bado hakijafikia matarajio ya pande zote. Kwa sasa Singapore imewekeza katika miradi 36 nchini Tanzania, huku makubaliano yaliyofikiwa yakilenga kuongeza uwekezaji, biashara na fursa mpya za ushirikiano katika sekta mbalimbali za uchumi. Tanzania pia imeiomba Singapore kufungua ubalozi wake nchini ili kuimarisha zaidi mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi, pamoja na kuanzisha mfumo wa mashauriano ya mara kwa mara kwa ajili ya kuratibu maeneo ya ushirikiano. Katika sekta ya kilimo, nchi hizo zimeonyesha nia ya k...

RC MARA AWAPOKEA MAOFISA WA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA, AWAHAKIKISHIA HALI YA USALAMA NI SHWARI

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi, leo Juni 09, 2026 amekutana na kuzungumza na ujumbe wa maofisa kutoka Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Jeshi la Wananchi wa Tanzania walioko mkoani humo kwa kazi ya ukaguzi wa utayari wa ulinzi wa mipaka. Ujumbe huo uliongozwa na Mkurugenzi wa Operesheni Jeshini, Kanali Victor Magare pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano Jeshini, Kanali Herry Juma Masokola, ambao wamefika mkoani Mara kufanya tathmini ya hali ya kiusalama na kuangalia namna vikosi vilivyo tayari kulinda mipaka ya nchi. Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mhe. Mtambi aliwakaribisha wageni hao na kuwahakikishia kuwa Mkoa wa Mara uko salama, huku wananchi wakiendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii bila hofu. Ameongeza kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa, hususan katika maeneo ya mipakani. Ujumbe huo wa MMUT unaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Mara kwa le...

WANANCHI WATAKIWA KUTHAMINI FEDHA ZA SERIKALI.

  Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga  WANANCHI mkoani tanga wametakiwa kuthamini fedha zinazowekezwa na serikali katika ujenzi wa miundombinu hasa barabara. Wito huo umetolewa na meneja wa TARURA mkoa wa Tanga George Tarimo alipokuwa akitoa taarifa ya miradi ya barabara inayotarajiwa kuzinduliwa na mwenge wa uhuru na mingine kuwekewa jiwe la msingi. "Gharama zinatotumika ni kubwa sana sasa ni vema wananchi Kila mmoja akawa milinzi wa mwingine,kutotupa taka katika mitaro ambayo husababisha mitaro hiyo kuziba na kuharibika Kwa Barbara kitu ambacho ni hasara Kwa serikali",alisema Tarimo.  Aidha Tarimo alisema kuna miradi nane ambayo itapitiwa na mwenge wa uhuru mwaka huu ambayo ipo katika wilaya ya Kilindi,Pangani Handeni ,Korogwe, Lushoto,Bumbuli Muheza na Tanga jiji. Pamoja na hayo pia mradi wa Kilindi Dc ni Daraja ambalo lipo kwenye (hatua ya Box), na barabara ya mapanga Mlingotini ambayo gharama yake ni milioni 22.5 ambayo inajengwa na mkandasi Negron Buiders Company limited ...

BUTIAMA KUNUFAIKA NA MPANGO WA UJENZI WA SOKO LA KIABAKARI

 Serikali imeeleza mpango wake wa kuendelea kuisaidia Halmashauri ya Wilaya ya Butiama katika jitihada za kuboresha miundombinu ya biashara, hususan ujenzi wa soko katika eneo la Kiabakari, linalokua kwa kasi kiuchumi. Akijibu swali la Mbunge wa Butiama, Mheshimiwa Charles Mahera leo Jun 9,2026 Bungeni Jijini Dodoma,Naibu Waziri wa TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange amesema kuwa Butiama ni miongoni mwa halmashauri zenye mapato ya ndani ya chini, hivyo Serikali inaendelea na mkakati wa kuziwezesha halmashauri hizo kuongeza vyanzo vya mapato. Dkt. Dugange amebainisha kuwa eneo la Kiabakari tayari limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko, ambalo litakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi, hususan wanawake wanaojishughulisha na biashara katika eneo hilo, pamoja na kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri. Aidha, Serikali imeitaka Halmashauri ya Butiama kuanza kutenga fedha ndani ya bajeti yake kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa soko hilo, huku ikiahidi kuendelea kusaidia mradi huo kadri ya upatika...

SERIKALI YAAGIZA TATHMINI YA HARAKA IFANYIKE KORONGO LA STAREHE TARIME MJINI

Serikali imeahidi kuchukua hatua za kudumu kukabiliana na tatizo la mmomonyoko wa ardhi na mafuriko yanayosababishwa na Korongo la Starehe katika Jimbo la Tarime Mjini, mkoani Mara. Kauli hiyo imetolewa leo Juni 10, 2026, Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Festo Dugange, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Esther Matiko, kuhusu hatua za Serikali kudhibiti korongo hilo ambalo limeendelea kuhatarisha maisha, mali na makazi ya wananchi. Dkt. Dugange amesema Serikali imeweka kipaumbele katika kuondoa maeneo hatarishi na kuboresha miundombinu ya kudhibiti mafuriko na mmomonyoko wa ardhi katika maeneo mbalimbali nchini. "Tutafanya tathmini ya kina kubaini sababu zinazofanya korongo hili kuendelea kuharibika licha ya jitihada zilizowahi kufanyika, na tutachukua hatua za kitaalamu kuhakikisha suluhisho la kudumu linapatikana," amesema. Aidha, ameelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Mara pamoja na Meneja wa TARURA Tarime Mjini ...