Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WAZIRI MKUU AWASISITIZA WATANZANIA KUWAHUDUMIA WENYE MAHITAJI

 _Asema mambo ya kutegemea wahisani yamepitwa na wakati_   WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania kushirikiana na Serikali katika kutunza na kuhudumia vituo vya watoto wenye mahitaji maalumu na wasiojiweza badala ya kutegemea wahisani kutoka nje kwani mambo hayo yamepitwa na wakati. Ametoa kauli hiyo leo Jumapili, Juni 21, 2026 katika harambee ya uchangiaji wa jengo la kitega uchumi cha kanisa la Anglika jijini Dodoma. “Mambo ya misaada yamepitwa na wakati na hata katika bajeti Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kusisitiza kuwa na bajeti ya nchi ambayo inategemea rasilimali za ndani ya nchi”.  Pia, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa rai halmashauri zote nchini ziandae orodha ya vituo vya kulelea watoto wenye mahitaji maalumu na wasiojiweza na kuona namna ya kuvisaidia ambapo amesisitiza si vema kuwaandikia watu hao barua za kwenda kuomba misaada pindi wanapofika kwenye ofisi za umma. Waziri Mkuu amesema awali katika maeneo mbalimbali nchini ili...
Recent posts

UKAGUZI WA LESENI ZA MADINI WAIMARISHA UZINGATIAJI WA SHERIA NCHINI

 📍DODOMA Tume ya Madini imeendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa leseni za madini nchini kwa lengo la kufuatilia maendeleo ya leseni hizo na kuhakikisha shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini zinafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa. Akizungumza katika Banda la Tume ya Madini kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma, Mtakwimu kutoka Kurugenzi ya Leseni ya Tume ya Madini, Azihar Kashakara, amesema ukaguzi huo ni muhimu katika kuhakikisha wamiliki wa leseni wanatimiza masharti na wajibu unaotokana na leseni walizopewa. Amesema kuwa, pamoja na kufuatilia maendeleo ya leseni, Kurugenzi ya Leseni ina jukumu la kutoa na kusimamia leseni za madini, kutafsiri na kusambaza takwimu za leseni, pamoja na kuwezesha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali yatokanayo na umiliki wa leseni hizo. Kashakara ameeleza kuwa utoaji wa leseni za madini unazingatia masharti na vigezo vilivyowekwa kisheria, hi...

PANGANI YAPATA 'CLEAN SHEET' MIRADI YA MWENGE 2026

 NA: MWANDISHI WETU, PANGANI Kiongozi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, Wazo Mwang'onda, ameridhishwa na ubora wa miradi ya maendeleo pamoja na thamani ya fedha (value for money) zilizotumika kutekeleza miradi hiyo katika halmashauri ya wilaya ya Pangani mkoani Tanga. Kiongozi huyo ameyasema hayo Juni 20, 2026, ambapo amesisitiza kuwa miradi yote iliyotekelezwa katika halmashauri hiyo ina ubora, jambo linalothibitisha umakini wa viongozi katika kusimamia miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa wananchi na kuchochea maendeleo nchini. "Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, umeridhishwa na miradi ya maendeleo iliyotekelezwa Pangani. Hongereni sana viongozi kwa usimamizi mzuri," amesema Mwang'onda. Katika hatua nyingine, Mbunge wa Jimbo la Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema, viongozi ndani ya halmashauri ya Pangani wako makini linapokuja suala lenye maslahi kwa wananchi. "Tunampongeza Rais wetu, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi za miradi ya maendeleo,...

PROF. SHEMDOE AWAASA VIJANA KUWA WAADILIFU, WAZALENDO WANAPOTUMIKIA UMMA NA TAIFA

 Na OWM - TAMISEMI, Morogoro Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa vijana wa vyuo vikuu kuwa waadilifu na wazalendo pindi watakapoajiriwa Serikalini kuwatumikia wananchi au kupata fursa za uongozi wa kulitumikia taifa. Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa vijana hao Juni 20, 2026, wakati akifungua Kongamano la Vijana (Youth Uongozi Forum) kwa niaba ya Mhe. Prof. Palamagamba John Aaidan Kabudi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) ambalo linalofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro, lililoandaliwa na taasisi ya Tanzania Leadership Foundation (TLF). “Vijana wangu, watoto wangu, wadogo zangu mjitahidi sana kuwa waadilifu na wazalendo kwani mkishindwa kuwa waadilifu na wazalendo hamtaweza kudumu katika nafasi mtakazoaminiwa kuzitumikia,” amesisitiza Prof. Shemdoe. Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka vijana hao kuwa wanyenyekevu watakapopa...

WAZIRI MKUU AKICHAPA KAZI NDANI YA TRENI

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akiwa katika majukumu yake ya kazi ndani ya Treni ya kisasa (SGR) akitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma leo Juni 20, 2026.

RAIS SAMIA NA RAIS NETUMBO WASHUHUDIA WATIAJI SAINI HATI ZA MAKUBALIANO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe.Dkt.Netumbo Nandi-Ndaitwah wakati wakishuhudia utiaji saini wa Hati nne za makubaliano ya ushirikiano katika Sekta za biashara , Maendeleo ya biashara ndogo na za kati, Ulinzi , pamoja na ushirikiano wa Miji kati ya Manispaa ya mji wa Zanzibar na Manispaa ya Swakopmund kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari, Ikulu Jijini Dar-es-salaam, tarehe 20 Juni, 2026.