Balozi wa Amani Tanzania na Katibu wa Mahusiano wa Jumuiya ya Wachimbaji Tanzania (FEMATA), Mess Chengula, amepongeza hali ya amani na utulivu iliyoendelea kutawala jijini Mwanza, akisema ndiyo msingi wa maendeleo na ustawi wa wananchi. Akizungumza leo baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ya jiji hilo, Chengula alisema ameridhishwa kuona shughuli za kijamii na kiuchumi zikiendelea, huku baadhi ya maduka yaliyokuwa yamefungwa yakifunguliwa tena na kuanza kutoa huduma. "Ninawapongeza Watanzania kwa kuchagua amani siku hii ya leo. Furaha kubwa kwa binadamu ni kuona amani ikitawala mioyoni mwa watu," amesema. Aidha, aliiomba Serikali kuendelea kusikiliza makundi mbalimbali yenye malalamiko ili kutatua changamoto kwa njia ya mazungumzo na kuimarisha utulivu nchini. Chengula amesema amani huwezesha wananchi kujishughulisha kwa uhuru katika shughuli za uzalishaji mali, huku akisisitiza kuwa maridhiano yanayotarajiwa kufanywa kati ya Serikali, vyama vya siasa na makundi mbalimbali ...
AKIMWAKILISHA DKT.POSSI KATIKA MKUTANO WA WIPO,BALOZI TEMU ASISITIZA MAREKEBISHO YA MIFUMO YA MALI MILIKI
Na Mwandishi Wetu Geneva – Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva ametoa wito wa kuwa na mifumo ya mali miliki (Intellectual Property)inayojumuisha wote, yenye usawa na inayolenga mustakabali ili kuchochea ubunifu na maendeleo endelevu. Akizungumza katika Mkutano wa 68 wa Mabaraza ya Nchi Wanachama wa Shirika la Kimataifa la Mali Miliki WIPO, Balozi Temu aliwashukuru Mwenyekiti na Makamishna wenzake kwa uongozi wao. Pia alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa WIPO, Bw. Daren Tang, kwa kuteuliwa tena na kuipongeza Sekretarieti kwa maandalizi bora ya mkutano huo. Tanzania iliungana na tamko lililosomwa na Afrika Kusini kwa niaba ya Nchi za Afrika na Nepal kwa niaba ya Nchi Zinazoendelea. Balozi Temu, ambaye alikuwa anamwakilisha Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa na Mashirika mengine ya Kimataifa Geneva, Mhe. Dkt. Abdallah S. Possi, alisema Tanzania inatambua mali miliki kama kichocheo muhimu cha ubunifu, viwanda na maend...