Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

URUSI KUFUNGUA FURSA LUKUKI KWA TANZANIA

 Na beda msimbe,TBN, Moscow.     Urusi imesema taifa hilo litafungua fursa lukuki kwa taifa la Tanzania kwa manufaa ya pande zote mbili. Aidha taifa hilo lenye miradi 70 yenye thamani ya dola za Marekani milioni434.22 ikiwa imewezesha ajira 3018 tanzania limesema kuwa litatangaza fursa hizo katika mkutano wa uchumi wa kimataifa kesho kutwa.              Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao chake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kiongozi wa Urusi Vladimir Putin amesema Urusi imekuwa ikifuatilia kwa makini mageuzi yanayofanyika nchini tanzania na wanaona inavyokua.    Amesema amekuwa na mazungumzo yenye manufaa makubwa kwa jamii ya pande zote mbili na kuahidi kuendelea na ushirikiano na Tanzania.        Naye rais Samia amesema kuwa ziara yake katika Shirikisho la Urusi ina umuhimu mkubwa wa kihistoria kwake binafsi na kwa taifa la Tanzania kwa ujumla....
Recent posts

MAUAJI YA LAS VEGAS BAR: MSHTAKIWA WA TATU AFIKISHWA MAHAKAMANI, KESI YAPIGWA KALENDA

 *Kutoka: Dawati la Habari Polisi Mwanza* Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limemfikisha mahakamani mshtakiwa wa tatu, Benson John (19), mlinzi (Baunsa), mkazi wa Nyakabungo, Kata ya Isamilo wilayani Nyamagana na kumuunganisha katika kesi ya mauaji ya mkazi wa Mwanza, Mzafuru Faisal Yunusu. Mzafuru anadaiwa kuuawa kwa kipigo katika baa ya Las Vegas iliyopo eneo la Kona ya Bwiru, mtaa wa Nyamanoro, wilaya ya Ilemela baada ya kushindwa kulipa bili ya shilingi 8000. ​Hatua hiyo imekuja leo Juni 3, 2026, baada ya Wakili wa Serikali, Mwanahawa Changale, kuwasilisha ombi mahakamani hapo la kutaka hati mpya ya mashtaka inayomwongeza mtuhumiwa huyo ipokelewe chini ya kifungu cha 251 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023, wakati shauri hilo lilipokuja kwa ajili ya kutajwa. ​Kufuatia marekebisho hayo ya hati ya mashtaka katika shauri la jinai namba 10492 la mwaka 2026, idadi ya washtakiwa wanaokabiliwa na kesi hiyo sasa imefikia watatu, ambao ni Yohana...

RAIS SAMIA AWEKA SHADA KABURI LA ASKARI ASIYEFAHAMIKA

Na Beda Msimbe TBN, Moscow KENGELE kubwa iliyogongwa mara tisa, bendi ya jeshi ikiongoza nyimbo za maombolezo Rais Dk Samia Suluhu Hasan majira ya saa tano na dakika 23 aliweka shada la maua kwa kaburi la askari asiyefahamika, mjini hapa. Aidha Baada ya shughuli la uwekaji wa taji hilo katika eneo ambalo moto huwaka daima ikiwa ni kumbukumbu ya wapiganaji wa Urusi waliopoteza maisha katika vita kuu ya pili, gadi tatu zilipita kwa mwendo wa haraka na kutoa heshima kwa Rais Samia baada ya kupigwa kwa wimbo wa taifa la Tanzania. Hali ya  askari katika uwanja huo walioonesha nidhamu ya hali ya juu ya kusimama tisti katika maeneo yao bila kutikisika , ubadilishanaji wa gadi za ulinzi na pia mwendo wa pole ambao ulimsindikiza Rais Samia kwenda kwenye tukio la uwekeaji wa shahada. Vilikuwa vitu vinavyovutia kuangalia.Rais Samia ambaye yupo katika ziara ya kiserikali nchini hapa  baadaye alienda kukutana na mwenyeji wake Rais Vladmir Putin . Zaidi ya maofisa 300 wa Jeshi la Ulinzi la ...

WALIMU ZAIDI YA 3,000 WAONESHA UMAHIRI KATIKA MASHINDANO YA KITAIFA YA UFUNDISHAJI

 Serikali imeendelea kuimarisha juhudi za kuboresha ubora wa elimu nchini kwa kuhamasisha ubunifu na umahiri wa walimu, ambapo walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji la mwaka 2026, linalolenga kuibua mbinu bunifu za ufundishaji na kujifunzia ili kuongeza matokeo bora ya elimu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuelekea hafla ya utoaji wa tuzo kwa washindi wa mashindano hayo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Afidhi Ameir, amesema shindano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa mageuzi ya sekta ya elimu pamoja na Mpango Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa watoto wa elimu ya awali na wanafunzi wa madarasa ya chini. Amesema serikali inalichukulia shindano hilo kama jukwaa muhimu la kuwapa walimu nafasi ya kuonesha uwezo wao, kubadilishana uzoefu na kuibua mbinu mpya zinazoweza kuimarisha ufundishaji darasani. "Shindano hili linatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao, kuba...

VYUO VIKUU VYA MALAYSIA VYAANZA MAONESHO YA ELIMU DAR

 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam** Tanzania na Malaysia zimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika elimu ya juu kupitia ubia wa vyuo vikuu, tafiti za pamoja, ubadilishanaji wa wanafunzi na wahadhiri, ufadhili wa masomo pamoja na ushirikiano katika sayansi na teknolojia wakati vyuo vikuu tisa vikianza maonesho ya elimu leo katika hoteli ya Serena. Akizungumza katika kikao cha Kuimarisha Ushirikiano wa Elimu ya Juu Kati ya Tanzania na Malaysia** kilichofanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, **Prof. Daniel Mushi**, amesema ujio wa ujumbe wa elimu kutoka Malaysia ni wa wakati muafaka wakati Tanzania ikiendelea kuimarisha na kutangaza kimataifa mfumo wake wa elimu ya juu. Kikao hicho kiliandaliwa na kuratibiwa na **Education Malaysia Global Services (EMGS)**, chini ya Wizara ya Elimu ya Juu ya Malaysia, kwa kushirikiana na **Global Education Link Ltd (GEL)**. Prof. Mushi amesema ujio wa ujumbe huo umevitambulisha ...