Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuthamini na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi katika sekta ya elimu kutokana na mchango wake mkubwa kwenye kuongeza ubora wa elimu na kuandaa rasilimali watu yenye maarifa, ujuzi na maadili yanayohitajika katika maendeleo ya Taifa. Dkt. Mwigulu amesema hayo alipokuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 11 ya wahitimu wa Kidato cha Nne (Year 11–IGCSE) wa mwaka wa masomo 2025/2026 ya Shule ya Kimataifa ya Feza yaliyofanyika Salasala, Dar es Salaam, leo Ijumaa, Juni 12, 2026. "Nimekuja leo kwa kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambua ubia huu muhimu ambao shule yenu imekuwa ikifanya katika sekta ya elimu. Hatuwezi kuyataja mafanikio katika sekta ya elimu bila kutaja mchango wa shule za sekta binafsi, na kwa umuhususi shule za Feza," amesema Dkt. Mwigulu. Amesema Taasisi ya Feza ni miongoni mwa taasisi zilizochangia kwa kiasi kikubwa mageuz...
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 12 Juni, 2026 ameshiriki uzinduzi wa majaribio ya kutua na kuruka kwa ndege katika Uwanja wa Ndege Musoma na kumuomba Waziri wa Uchukuzi Mhe. Profesa Makame Mbarawa kuanza utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya uchukuzi ya Mkoa wa Mara. Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtambi ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa reli kwa kiwango cha SGR kutoka Tanga hadi Musoma, mradi wa ukarabati na upanuzi wa Bandari ya Musoma na Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Serengeti. “Kasi hii ya ukamilishaji wa Uwanja wa Ndege Musoma ninaomba ije pia katika miradi hii ya kimkakati ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla” amesema Mhe. Mtambi. Mhe. Mtambi amesema miradi hiyo muhimu katika kukuza uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara na mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa ujumla kwani itafungua fursa nyingi za kiuchumi nchini Tanzania na nchi jirani zinazopakana na Tanza...