Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WANANCHI WAMKATAA DIWANI MBELE YA VIONGOZI WA CCM KATA YA ZUZU DODOMA

 Wananchi wa Kata ya Zuzu, Jijini Dodoma, wameibuka na malalamiko makali yenye hisia nzito na machungu makubwa, wakimlenga Diwani wa kata hiyo kwa kumtuhumu kuhusika katika kufungwa kwa eneo la uchimbaji wa kokoto na mchanga ambalo lilikuwa mkombozi wao wa maisha kwa zaidi ya wananchi 300. Kwa sauti zilizotawaliwa na huzuni, hasira na wakati mwingine machozi yakibubujika, wananchi hao wamesimulia jinsi maisha yao yalivyoporomoka ghafla kufuatia kufungwa kwa eneo hilo, wakisema walikuwa wakitegemea uchimbaji huo kama chanzo kikuu cha kipato cha kila siku. Wamesema kupitia shughuli hizo walikuwa wakigharamia mahitaji ya familia, ada za shule za watoto na matumizi ya msingi ya nyumbani, lakini sasa wamebaki wakikabiliwa na hali ngumu ya maisha isiyo na uhakika wala matumaini. Kwa hisia kali na maumivu ya wazi, wananchi hao wamedai kuwa uamuzi wa kufungwa kwa eneo hilo ulifanyika bila kushirikishwa wala kufanyika mkutano wa pamoja wa wananchi, jambo ambalo wamesema limeongeza hasira, m...
Recent posts

RAIS DKT. MWINYI AWASILI JIJINI MOMBASA, KENYA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Moi, jijini Mombasa, Kenya, leo tarehe 17 Juni 2026, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Rais Dkt. Mwinyi ameambatana na ujumbe wake, wakiwemo Mhe. Mama Mariam Mwinyi na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe. Rais Dkt. Mwinyi amepokelewa uwanjani hapo na Waziri wa Michezo, Uchumi Ubunifu na Vijana wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Salim Mvurya Mgala, Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Mhe. Masoud Ali Mohamed, pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dkt. Bernard Yohana Kibesse. Katika ziara hiyo, Rais Dkt. Mwinyi atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa 11 wa Masuala ya Bahari (11th Our Ocean Conference).

WADAU WA MADINI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA SHERIA KUONGEZA MANUFAA KWA TAIFA

 📍DODOMA Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi. Mwanasheria wa Tume ya Madini, Janeth Kanyasu, amesema hayo kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma, ambapo Tume inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali kuhusu masuala ya Sekta ya Madini. Amesema elimu hiyo inahusu Sheria ya Madini Sura ya 123 na kanuni zake, ikijumuisha utoaji wa leseni mbalimbali, biashara ya madini, uwekezaji, shughuli za uchimbaji na usimamizi wa mazingira ili kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika kwa tija na kwa kuzingatia matakwa ya sheria. “Kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ni msingi wa kuhakikisha Sekta ya Madini inaendeshwa kwa uwazi, uadilifu na kuendelea kutoa manufaa kwa taifa na wananchi,” amesema Kanyasu. Amesema pia wananchi wanaelimishwa kuhus...

WAHANDISI TANROADS, TARURA WATAKIWA KUTUMIA MIFUMO MIPYA KULINDA BARABARA

 📍Ampongeza Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha barabara nchini Na Mwandishi Wetu, Mbeya  SERIKALI imewagiza mameneja na wahandisi wa TANROADS na TARURA nchini kutumia mifumo mipya ya kielektroniki kulinda hifadhi za barabara na kutekeleza miradi kwa viwango. Agizo hilo limetolewa Jijini Mbeya Leo Juni 17 2026  na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Beno Malisa, kufungua mafunzo ya viongozi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA). Mafunzo hayo ya siku nne yaliyoanza Jumatatu, Juni 15, 2026, yamewakutanisha Mameneja, Wahasibu, na Wahandisi kutoka mikoa ya kimkakati ya kiuchumi ikiwemo Mbeya, Songwe, Rukwa, Ruvuma, Mtwara, na Lindi. Teknolojia na Udhibiti wa Miundombinu Mhe. Itunda amebainisha kuwa lengo kuu la semina hiyo ni kuwajengea uwezo viongozi hao katika kusimamia miradi ya miundombinu kwa ufanisi, hasa kupitia matumizi ya mfumo mpya wa kielektroniki unaod...

ZUNGU AWATAKA WABUNGE WANAWAKE KUONGOZA MAPINDUZI YA NISHATI SAFI

   Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, ameuagiza Umoja wa Wabunge Wanawake Tanzania (TWG) kutumia ushawishi wao katika jamii kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za wananchi, kuhifadhi mazingira na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya taifa ya nishati safi. Akifungua mafunzo ya wabunge hao yaliyoandaliwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) leo Jun 16,2026 jijini Dodoma, Spika Zungu amesema bado kuna dhana potofu zinazowazuia wananchi wengi kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi, hivyo akawataka wabunge kuwa mabalozi wa mabadiliko hayo katika maeneo yao. Amesema baadhi ya wananchi wanaamini kimakosa kuwa nishati safi ni ghali, ngumu kutumia na huathiri ladha ya chakula, jambo ambalo si la kweli.  Sambamba na hayo amewataka wabunge hao kwenda kwa wananchi na kutoa elimu sahihi ili kuondoa mitazamo hiyo na kusaidia kufikia lengo la Serikali la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya ku...

JESHI LA MAGEREZA LASHIRIKI MAADHIMISHO YA KITAIFA YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026

 Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma. Jeshi la Magereza kwa mara nyingine tena linashiriki kikamilifu kwenye Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026 Maadhimisho ambayo ni moja ya Maazimio ya Umoja wa Afrika (AU).  Hivyo, Jeshi la Magereza linawakaribisha wananchi wote wa Tanzania kutembelea Banda la Magereza katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma kuanzia Leo Juni 16 hadi 23, 2026. Maonesho hayo yatawakutanisha Wananchi, Taasisi za Umma na Wadau mbalimbali kwa lengo la kuelezea Dhima, Dira, Mafanikio, Changamoto zilizopo katika suala zima la urekebishaji Wafungwa, kutoa  huduma na taarifa mbalimbali muhimu kuhusu shughuli zinazotolewa na Serikali kwa Wananchi  kupitia Jeshi la Magereza na kuueleza Umma juu ya Mageuzi ya kisayansi yanayofanywa sasa na Jeshi katika uendeshaji na urekebishaji Wafungwa. Pamoja na kutoa huduma hizo, Jeshi la Magereza kupitia Maadhim...