Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WAITARA: WALA FEDHA ZA UMMA WACHUKULIWE HATUA NA IKIBIDI WANYONGWE

 Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini mkoani Mara, Mwita Waitara, ameibua hisia kali Bungeni baada ya kuhoji namna ambavyo baadhi ya wananchi wanaendelea kuteseka kwa kukosa huduma muhimu huku fedha za umma zikidaiwa kutafunwa na wachache wasiowajibika. Akichangia Bajeti ya Wizara ya Fedha leo Juni 2, 2026, Jijini Dodoma, Waitara amesema ni jambo linaloumiza kuona wananchi wakihangaika kutafuta fedha za matibabu na dawa hospitalini, wakati ripoti za ukaguzi zinaendelea kuonyesha uwepo wa matumizi mabaya ya fedha za umma katika baadhi ya taasisi za Serikali. Kwa sauti ya msisitizo, Waitara ameeleza kuwa fedha zinazotengwa na Bunge zinapaswa kuwafikia wananchi na kuleta maendeleo yaliyokusudiwa, badala ya kupotea mikononi mwa watu wachache wanaokwamisha juhudi za Serikali na matarajio ya wananchi. “Leo hii kuna mwananchi anaondoka hospitalini bila dawa kwa sababu hakuna fedha za kutosha. Wakati huo huo, ripoti za ukaguzi zinaonyesha kuna watu wamechezea fedha za umma. Hili halipaswi ku...
Recent posts

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI MIPYA YA KUCHOCHEA UCHUMI, KULIPA MADENI NA KUIMARISHA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA

SERIKALI imeanika vipaumbele vinane vya kimkakati vinavyolenga kuujenga uchumi imara, kuimarisha uwajibikaji wa kifedha na kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa katika mwaka wa fedha 2026/27. Akiwasilisha Bajeti ya wizara ya Fedha Kwa mwaka wa Fedha 2026/2027 leo Jun 2,2026 Bungeni Jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb.), amesema Serikali itaendelea kusimamia kwa umakini uchumi wa Taifa kwa lengo la kufikia ukuaji wa asilimia 6.3, kudhibiti mfumuko wa bei katika kiwango cha tarakimu moja na kuhakikisha akiba ya fedha za kigeni inaendelea kuwa katika viwango vinavyokidhi mahitaji ya nchi. Katika kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, Serikali imepanga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, ugawaji wa rasilimali na usimamizi wa bajeti ili kuhakikisha fedha za wananchi zinatumika kwa tija na kuleta matokeo yanayokusudiwa. Hatua nyingine muhimu ni kuendelea kulipa kwa wakati madeni ya Serikali, ambapo zaidi ya Shilingi trilioni 15.1 zimetengwa kw...

MAPATO YA MICHEZO YA KUBAHATISHA YAFIKIA SH. BILIONI 18.76, BAHATI NASIBU YA TAIFA YAZALISHA AJIRA 484

 Serikali imeendelea kuimarisha usimamizi wa sekta ya michezo ya kubahatisha nchini, hatua iliyowezesha ukusanyaji wa Shilingi bilioni 18.76 hadi Aprili 2026 pamoja na kudhibiti kwa ufanisi shughuli haramu zinazohusiana na sekta hiyo. Akiwasilisha Bungeni jijini Dodoma mapitio ya utekelezaji wa mpango na bajeti ya mwaka 2025/26 pamoja na makadirio ya mwaka 2026/27, Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar, amesema Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania imefanikiwa kutoa leseni 7,747, kufanya kaguzi tisa za kiudhibiti na kutekeleza operesheni tatu maalumu za kukabiliana na michezo haramu ya kubahatisha. Waziri Omar amesema mafanikio hayo yanaenda sambamba na juhudi za kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kupitia kampeni za “Elimika na GBT”, “Mkeka Unachana” na “Wakati Wao Bado”, ambazo zimeendelea kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha, amesema Bahati Nasibu ya Taifa iliyoanzishwa Aprili 2025 imeendelea kuwa chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuch...

SERIKALI KUIMARISHA MIFUMO YA USIMAMIZI WA MAAF

 Na mwandishi wetu, Morogoro SERIKALI imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inayotolewa inawafikia walengwa kwa wakati, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vya kimataifa. Hayo yameelezwa leo tarehe 02 Juni, 2026 na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Kanali Selestine Masalamado, wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura, mkoani Morogoro. Amesema utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wa dharura ni nguzo muhimu zinazowezesha kuokoa maisha ya wananchi walioathiriwa na maafa, kupunguza mateso ya waathirika na kuharakisha urejeshaji wa hali za kawaida katika maeneo yaliyoathirika. “Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakiki...

SERIKALI KUIMARISHA MIFUMO YA USIMAMIZI WA MAAFA

 Na mwandishi wetu, Morogoro SERIKALI imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inayotolewa inawafikia walengwa kwa wakati, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vya kimataifa. Hayo yameelezwa leo tarehe 02 Juni, 2026 na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Kanali Selestine Masalamado, wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura, mkoani Morogoro. Amesema utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wa dharura ni nguzo muhimu zinazowezesha kuokoa maisha ya wananchi walioathiriwa na maafa, kupunguza mateso ya waathirika na kuharakisha urejeshaji wa hali za kawaida katika maeneo yaliyoathirika. “Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakiki...

WASTAAFU WAVUNA MATUNDA YA MAGEUZI: PENSHENI YA CHINI YAPAA HADI SH. 250,000

 Hatua za Serikali za kuendelea kuboresha maisha ya wastaafu nchini zimezaa matunda baada ya kima cha chini cha pensheni kuongezwa kutoka Shilingi 100,125.87 hadi Shilingi 250,000 kwa mwezi, ongezeko kubwa linalolenga kuongeza ustawi na kuimarisha maisha ya wanufaika wa pensheni wanaolipwa na Hazina. Akiwasilisha Bungeni Jijini Dodoma leo Juni 2, 2026, mapitio ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya mwaka 2025/26 pamoja na mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka 2026/27, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb.), amessema Serikali imeendelea kutekeleza kwa vitendo dhamira yake ya kuhakikisha wastaafu wanapata haki na stahiki zao kwa wakati. Amesema hadi Aprili 2026, Serikali imelipa mafao ya wastaafu yenye thamani ya Shilingi bilioni 577.41, hatua inayodhihirisha uwajibikaji na utayari wa Serikali wa kuheshimu mchango wa watumishi waliolitumikia Taifa kwa miaka mingi. Kwa upande wa hifadhi ya jamii, Serikali pia ililipa michango ya kisheria yenye thama...