SHULE ya Sekondari Mwembeni mkoani Mara imepata msukumo mpya wa kuinua kiwango cha taaluma baada ya Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Agnes Marwa, kukabidhi projector ya kufundishia pamoja na taulo za kike kwa wanafunzi wa shule hiyo, huku akiwataka wanafunzi kujituma katika masomo na kuwa walinzi wa amani ya Taifa. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi Projector ya kufundishia pamoja na Taulo za Kike katika shule ya sekondari Mwembeni, Mhe. Agnes Marwa Mbunge viti Maalumu Mkoa wa Mara, amesema ndoto yake ni kuona Shule ya Sekondari Mwembeni ikitajwa miongoni mwa shule zinazofanya vizuri kitaifa, akisisitiza kuwa mafanikio hayo yatapatikana kupitia nidhamu, juhudi na kujituma kwa wanafunzi. "Natamani sana kuisikia Mwembeni iking'ara kitaifa. Ninyi ndiyo mtakaolibeba na kulipandisha jina la shule yenu. Kumbukeni kuwa elimu mnayoipata ni uwekezaji wa maisha yenu wenyewe, hivyo jitumeni kwa bidii ili kutimiza ndoto zenu," amesema Mhe. Agnes. Mhe. Agnes amesema msaad...
📍_Dar es Salaam_ Mjiolojia kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Njombe, Abbas Mruma, amesema Tanzania inaendelea kujijengea nafasi muhimu duniani kutokana na kuwa na hifadhi kubwa ya madini muhimu ya kimkakati, yakiwemo graphite, lithium na rare earth elements, ambayo ni nguzo muhimu katika maendeleo ya teknolojia za kisasa na nishati safi. Mruma ameyasema hayo wakati akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Richard Stanslaus Muyungi, alipotembelea banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba). Amesema mahitaji ya madini ya lithium yanaendelea kuongezeka kwa kasi duniani kutokana na matumizi yake katika utengenezaji wa betri za magari ya umeme, simu za mkononi, kompyuta mpakato (laptops) na vifaa vingine vya kisasa vya kielektroniki. Amefafanua kuwa nchini Tanzania, madini ya lithium yanapatikana zaidi katika maeneo ya Dodoma na Ikungi, mkoani Singida. Akizungumzia madini ...