Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MWANA FA ASHUKA CCM KIRUMBA, AAHIDI KUMALIZA KERO YA TAA ZA USIKU

 Na Mashaka Mhando, MWANZA SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, imeahidi kumaliza changamoto ya ukosefu wa taa katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, ili kuwezesha uwanja huo mkongwe kutumika kwa mechi na matamasha nyakati za usiku. Ahadi hiyo nzito imetolewa leo, Agosti 8, 2026, na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma (maarufu Mwana FA), wakati alipofanya ziara maalum ya kukagua miundombinu ya uwanja huo, huku akisisitiza kushirikiana na wadau wa michezo kutatua kero hiyo. Mhe. Mwinjuma amebainisha kuwa dhamira kuu ya Serikali ni kuhakikisha miundombinu yote ya michezo nchini inaboreshwa na kufikia viwango vinavyokidhi mahitaji ya sasa. "Moja ya changamoto kubwa iliyopo hapa Kirumba ni ukosefu wa mfumo wa taa unaowezesha uwanja kutumika kwa ufanisi nyakati za usiku. Hali hii imekuwa ikipunguza fursa za kufanyika kwa baadhi ya shughuli za michezo, hususan mechi na matukio yanayohitaji matumizi ya uwanja wakati wa usiku, naahidi hili nita...
Recent posts

TREASURY REGISTRAR HOLDS TALKS WITH TDB PRESIDENT

 By the OTR Reporter Dar es Salaam. Treasury Registrar Mr Nehemiah Mchechu has held talks with Trade and Development Bank (TDB) President and Managing Director Mr Admassu Tadesse on strengthening the bank’s partnership with Tanzania, with a focus on supporting economic development and unlocking greater value from public investments. The talks, held on Friday, August 7, 2026, at the Office of the Treasury Registrar (OTR) in Dar es Salaam, brought together Mr Mchechu and Mr Tadesse alongside officials from both sides to discuss opportunities for deeper cooperation in investment financing, trade and development. The engagement is of particular significance given that the Government, through the OTR, holds an 8.3 per cent stake in TDB, making Tanzania one of the bank’s shareholders. Mr Mchechu said a stronger partnership with TDB could help expand investment, trade and access to capital for projects with the potential to generate broad economic benefits. He noted that, as a regional de...

MSAJILI WA HAZINA ATETA NA RAIS WA BENKI YA BIASHARA NA MAENDELEO

 Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam.  Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara na Maendeleo (TDB), Bw. Admassu Tadesse, kuhusu namna benki hiyo inavyoweza kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha ufanisi wa uwekezaji wa Serikali. Mazungumzo hayo yana umuhimu wa kipekee kwa Tanzania kwa kuzingatia kwamba Serikali, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, inamiliki asilimia 8.3 ya hisa katika TDB na hivyo kuwa miongoni mwa wanahisa wa benki hiyo ya maendeleo ya kikanda. Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi ya Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam yalijikita katika maeneo mbalimbali ya ushirikiano, ikiwemo namna TDB inavyoweza kuongeza mchango wake katika maendeleo ya Tanzania na kuimarisha ufanisi wa uwekezaji wa Serikali. Bw. Mchechu alisema ushirikiano kati ya Tanzania na TDB ni muhimu katika kuendeleza uwekezaji, biashara na upatikanaji wa mitaji...

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI IBADA YA MISA TAKATIFU YA JUMUIYA YA URU SEMINARI

 *ASISITIZA SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA TAASISI ZA DINI KATIKA MAENDELEO YA TAIFA HUSUSANI SEKTA YA AFYA NA ELIMU* Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango wa Taasisi za Dini ambazo kwa namna ya pekee zimekuwa zikishiriki katika kutoa mchango kwenye sekta za Afya na Elimu hapa nchini. Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki Ibada ya Misa Takatifu Maalum ya Wanajumuiya wa Uru Seminari, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kristo Mchungaji Mwema – Tabata Kimanga Jijini Dar es Salaam. Amesema kwa miaka mingi na kwa asilimia kubwa Taasisi za dini zimechangia katika utoaji wa huduma za elimu na afya, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi hizo ili kufanikiwa zaidi katika kulijenga Taifa. Makamu wa Rais amesema Malezi yanayotolewa katika Taasisi za elimu za dini ikiwemo Shule ya Uru Seminari ambayo husisitiza Sala, Kazi na Masomo yanapaswa kutiliwa mkazo katika mal...

RAIS SAMIA AKABIDHI ZAWADI MBALIMBALI WASHIRIKI WA MAONESHO YA KILIMO YA NANE NANE DODOMA

  Matukio mbalimbali katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.

RAIS SAMIA AKABIDHI ZAWADI MBALIMBALI WASHIRIKI WA MAONESHO YA KILIMO YA NANE NANE DODOMA

 Matukio mbalimbali katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.