Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

Miaka 25 ya St Anne Marie Academy ilivyoleta Tabasamu Kwa Watanzania

Recent posts

Vyuo Bora vya Malaysia Kuonesha Fursa za Masomo Serena Hotel, Dar es salaam

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Tanzania inatarajiwa kupokea ujumbe mkubwa wa viongozi wa elimu ya juu kutoka Malaysia, wakiwemo viongozi kutoka Wizara ya Elimu ya Malaysia, Education Malaysia Global Services (EMGS), pamoja na wawakilishi wa vyuo vikuu tisa vitakavyoshiriki Maonesho ya Elimu ya Malaysia yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 1 hadi 3, 2026 katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam. Ujumbe huo wa watu 19 kutoka Malaysia unatarajiwa kuwasili nchini tarehe  ikiwa ni maandalizi ya kushiriki maonesho hayo pamoja na kufanya vikao vya kimkakati na wadau mbalimbali wa elimu nchini, ikiwemo Wizara ya Elimu, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), vyuo vikuu vya Tanzania, shule, wazazi, walezi na wanafunzi. Maonesho hayo, yanayoratibiwa kwa ushirikiano wa Global Education Link (GEL) na wadau wa elimu kutoka Malaysia, yanalenga kufungua fursa za udahili, ufadhili wa masomo, ushirikiano wa kitaaluma, pamoja na kuimarisha mahusiano ya elimu ya juu kati ya Tanzania na Malaysia. Akizungu...

Doyo amtaka msajili wa vyama kuvifuta vyama korofi

  Na Mwandishi Wetu, Tanga CHAMA cha National League for Democracy (NLD), kimeitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kutosita kuvifuta au kuvifungia vyama vyote vya siasa vinavyokiuka sheria na kuhatarisha amani ya nchi, kikitaka wanasiasa wanaoshindwa kufuata sheria wajitoe na kuwa wanaharakati. Wito huo umetolewa Leo mei 25 jijini Tanga na Katibu Mkuu wa NLD, Doyo Hassan Doyo, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya kisiasa nchini, kufuatia hatua ya CHADEMA kuitisha maandamano ya nchi nzima kushinikiza kuachiwa kwa Mwenyekiti wao, Tundu Lissu. Doyo alisema Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2019, na kuwataka Watanzania kuacha tabia ya kulalamika na kuishutumu mamlaka hiyo kuwa inaegemea upande mmoja pale inapochukua hatua za kisheria. "Msajili haipendelei chama chochote, kila chama kinaonywa na kuadhibiwa kadiri kinavyofanya makosa. Baada ya CHADEMA kutoa kauli zinazoashiria uvunjifu wa am...

Masoko Rasmi, Bei Elekezi Yapunguza Utoroshaji wa Madini Ruvuma

📍Ruvuma Uanzishwaji wa masoko rasmi ya madini pamoja na matumizi ya mfumo wa bei elekezi mkoani Ruvuma, umetajwa kupunguza kwa kiasi kikubwa vitendo vya utoroshaji wa madini huku ukiongeza mapato ya Serikali na kuwanufaisha wachimbaji wadogo. Mkoa wa Ruvuma kwa sasa una masoko rasmi ya madini mawili likiwemo Soko la Dhahabu na Vito la Songea Mjini pamoja na Soko la Dhahabu na Vito Tunduru, lililozinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan Septemba 26, 2024. Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi, amesema mafanikio hayo yametokana na maboresho yaliyofanywa na Serikali katika usimamizi wa biashara ya madini kupitia masoko rasmi yenye uwazi na ushindani wa kibiashara. Amesema kabla ya kuanzishwa kwa masoko hayo, baadhi ya wachimbaji walikosa maeneo rasmi ya kuuza madini yao hali iliyochochea biashara holela na utoroshaji wa madini, jambo lililoikosesha Serikali mapato na kuwafanya wachimbaji wadogo kuuza madini yao kwa ...

Kazala: Sekta ya Nguo Imeporomoka,Viwanda vya Ndani Vilindwe

MBUNGE wa Jimbo la Kasulu Vijijini Edibilly Kazala amesema Tanzania inapaswa kuchukua hatua za haraka kuvilinda viwanda vya ndani na kukuza uwekezaji wenye tija, akionya kuwa sekta ya viwanda vya nguo nchini inaendelea kudorora kwa kasi. Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma jana Mei 22, 2026, Kazala amesema pamoja na ongezeko la wawekezaji wa kigeni nchini, bado kuna baadhi ya uwekezaji mdogo usio na manufaa makubwa kwa Taifa huku ukichukua nafasi ambazo Watanzania wana uwezo wa kuzifanya wenyewe. “Lazima kama Taifa tuangalie namna ya kudhibiti baadhi ya uwekezaji usio na tija kubwa kwa wananchi wetu,” amesema. Kazala amesema takwimu za ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kuwa mwaka 2002 Tanzania ilikuwa na zaidi ya viwanda 50 vya nguo, lakini sasa vimebaki takribani vitatu pekee vinavyoendelea kufanya kazi, hali inayodhihirisha kuporomoka kwa sekta hiyo muhimu. Amesema kushuka kwa sekta ya textile kumeathiri pia ajira, ambapo mwaka 2015 sek...

Tanzania na Marekani Zaendeleza Ushirikiano wa Kimkakati Katika Sekta Muhimu

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Ellen Maduhu, amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Andrew Lentz, kuhusu kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Marekani. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walijadili namna ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, huduma za kibalozi, biashara na uwekezaji, usalama, nishati pamoja na utekelezaji wa mipango ya kimkakati ya maendeleo. Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Dkt. Elsie S. Kanza, ambaye alishiriki katika majadiliano yaliyolenga kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili. Aidha, pande zote mbili zilisisitiza dhamira yao ya kuendelea kushirikiana na kufanya mazungumzo yenye tija kwa manufaa ya mataifa hayo mawili.

Waziri Mkuu Avitaka Vyombo Vya Ulinzi na Usalama Kuwa Macho Dhidi ya Wavunja Amani

_▪️Aonya dhidi ya vitendo vya uchochezi, kujiteka na propaganda zinazolenga kuwagombanisha Watanzania_ _▪️Asema Serikali imejikita kusikiliza wananchi na kutatua kero zao badala ya mijadala ya uchaguzi_ _▪️Awataka wananchi kuendelea kulinda mshikamano na utulivu wa Taifa_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuendelea kuwa macho dhidi ya vitendo vinavyolenga kuvuruga amani ya nchi huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kusimamia usalama wa wananchi na mali zao. “Kuweni macho na njama za aina hii, shughulikeni na waovu wa aina hii. Mliweza lile la Kibiti, mliweza lile la Amboni na mambo mengine mengi mmeweza. Kuweni macho kuhakikisha michezo ya aina hiyo haifanikiwi huku mkihakikisha usalama wa raia wetu na mali zao unaendelea kulindwa,” amesema Dkt. Mwigulu. Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumamosi, Mei 23, 2026 alipozungumza na wananchi wa Manispaa ya Iringa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Kichangani mkoani Iringa. Amesema ...

Tutazifanya Mbio za Siku ya Afrika kuwa za Kimataifa - Makonda

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali inafikiria kuzifanya Mbio za Siku ya Afrika kuwa za kimataifa ili kufanikisha lengo la kuleta maendeleo ya pamoja kwa bara la Afrika.  Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mbio hizo jijini Dar es Salaam Mei 23, 2026, Mhe. Makonda alisema mbio hizo zimeendelea kuwa alama ya umoja, mshikamano na maendeleo ya Waafrika. Alisema Serikali inalenga kukuza mbio za Siku ya Afrika ili ziwe jukwaa la kimataifa litakalokutanisha Waafrika kutoka mataifa mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano na diplomasia kupitia michezo. Akizungumzia mshikamano na uwajibikaji wa Waafrika, Waziri Makonda alisema hakuna Mtu atakayekuja kutupa hela ili kuijenga au kuilinda Tanzania na Afrika isipokuwa Waafrika wenyewe na kusisitiza kuwa ni wajibu wa Watanzania na Waafrika kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha wanailinda na kuiendeleza Afrika kwa kutumia nguvu, umoja na rasilimali walizonazo.  “Sisi ni Waafrika, tunapas...