MBUNGE wa Jimbo la Butiama, Mhe. Dkt. Charles Mahera, ameiiomba Serikali kuharakisha uwekaji wa taa za barabarani katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo yanayopitiwa na barabara ya Mkutano,Natta kupitia Nyamwisuwa. Akizungumza bungeni jijini Dodoma Mei 26, 2026 wakati akiuliza swali la nyongeza, Dkt. Mahera amesema barabara hiyo ilianza kujengwa muda mrefu huku kipande cha Mkutano hadi Nyamwisuwa kikikamilika tangu mwaka 2007, lakini wananchi bado hawajanufaika na huduma ya taa za barabarani. “Barabara hii inapitia maeneo mengi sana ya Jimbo la Butiama lakini maeneo hayo hayana taa kuanzia Nyambange, Nyakanga, Butuguri, Mbusegwe, Kiguri, Kiarano hadi Bisale. Wananchi wa Butiama wanasubiri taa hizi kwa muda mrefu tangu mwaka 2023,” amesema Dkt. Mahera. Dkt. Mahera ameiomba Serikali kuhakikisha wananchi wa Butiama wanapatiwa huduma hiyo muhimu ili kuongeza usalama pamoja na kuchochea shughuli za kijamii na kiuchumi katika maeneo hayo. Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhan...
Mbunge wa Jimbo la Serengeti, Mary Daniel Surati, ameendelea kuweka historia ya maendeleo katika jimbo hilo baada ya kutoa na kugawa shilingi milioni 88 kwa ajili ya miradi ya huduma za kijamii. Mary alitoa fedha hizo kupitia Mfuko wake wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo, katika hafla maalum iliyofanyika Mei 20, 2026 wilayani Serengeti na kuhudhuriwa na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, viongozi wa serikali na wananchi. Mbunge huyo alisisitiza dhamira yake ya kuhakikisha wananchi wa Serengeti wanapata huduma bora za afya, elimu na maendeleo ya kijamii kwa ujumla. Katika mgao huo wa fedha, kiasi cha shilingi milioni 25 kimetengwa kwa ajili ya kugharimia ukamilishaji wa Zahanati ya Kisaka, mradi unaotarajiwa kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa wakazi wa eneo hilo na kupunguza adha ya wananchi kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu. Mbunge Mary akikabidhi hundi ya mfano ya milioni 25/- Mbali na fedha hizo, Mbunge Mary pia alikabidhi madawati kadhaa yenye thamani ya shilingi...