Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MWENGE WA UHURU KIZINDUA MIRADI 73 TANGA

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mwenge wa Uhuru unatarajia kuwasili mkoani Tanga June 17 mwaka huu katika kijiji cha Mtoro Kata ya Tunguri wilaya ya Kilindi ukitokea mkoani Morogoro. Ukiwa mkoani hapa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri 11 kwa umbali wa kilometa 1340 ukikagua, kuzindua, kufungua na kuweka mawe ya misingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 27  Akizungumza na waandishi wa habari ofisini  kwake mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Burian amesema baada ya kukamilisha mbio zake mkoani hapa Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa mkoani mkoani Kilimanjaro June 28 mwaka huu. "Mwenge huu wa Uhuru utaweka mawe ya misingi jumla ya miradi 34, utafungua na kuzindua jumla ya miradi 26, utatembelea na kukagua jumla ya miradi 11 ya shughuli za vijana na miradi miwili ya maendeleo ya sekta ya maji, miradi hii yote ina jumla ya thamani ya shilingi bilioni 27, milioni 764, laki 390 na 480.01" Amesema Batilda. "Ujumbe wa mwenge kwa mwaka huu wa ...
Recent posts

WABUNGE WATAKIWA KUPANUA WIGO WA HIFADHI YA JAMII

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, amewataka Waheshimiwa Wabunge kutumia majukwaa yao kuhamasisha wananchi, hususani waliojiajiri, kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ili waweze kunufaika na huduma na mafao mbalimbali yanayotolewa na mifuko hiyo. Amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza wigo wa hifadhi ya jamii kwa makundi ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakishiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa, lakini bado hayajafikiwa ipasavyo na huduma za hifadhi ya jamii. Bw. Mshomba ameeleza kuwa kuongezeka kwa wanachama katika mifuko ya hifadhi ya jamii kutasaidia juhudi za Serikali za kupunguza umaskini wa kipato, kuongeza tija katika uzalishaji mali, kukuza uchumi wa nchi na kuimarisha ustawi wa wananchi. Kauli hiyo ameitoa leo Juni 15, 2026, katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, wakati wa mafunzo maalumu kwa Waheshimiwa Wabunge yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana...

KAZALA:AMEISHAURI SERIKALI KUIMARISHA KILIMO, VIWANDA NA UWEZESHAJI WA VIJANA

 Mbunge wa Kasulu Vijijini, Mhe. Edibilly Kazala, ametoa msisitizo kwa Serikali kuongeza kasi ya uwekezaji katika sekta za uzalishaji hususan kilimo na viwanda, akieleza kuwa ndiyo nguzo kuu za kupunguza umaskini na kuimarisha uchumi wa Taifa. Akichangia Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027 leo Juni 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma, Mhe. Kazala alianza kwa kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake imara unaoendelea kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi. Pia amewapongeza Mawaziri pamoja na wataalam wa Wizara ya Fedha kwa kuendelea kuboresha mifumo ya kiuchumi na kuyafanyia kazi maoni ya Wabunge, akisema kuwa hatua hizo zimeleta mabadiliko chanya katika baadhi ya sekta muhimu. Aidha, Mbunge huyo ameeleza kufurahishwa na juhudi za Serikali katika kulinda viwanda vya ndani, hususan sekta ya nguo (textile industry), akisisitiza kuwa sera hizo zimeanza kuleta matokeo chanya katika kuongeza thamani ya mazao ya ndani. Hata hivyo, ameishauri Seri...

PAC:TRA IMARISHENI UKUSANYAJI WA KODI

 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Devotha Minja, imekutana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kujadili taarifa ya ukaguzi wa hesabu kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2025, iliyokaguliwa na Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Katika kikao hicho, PAC imeitaka TRA kurekebisha mapungufu yote yaliyoainishwa na CAG, hususan katika maeneo ya ukusanyaji wa kodi na usimamizi wa mapato ya Serikali. Aidha, Kamati hiyo imeielekeza TRA kuimarisha mifumo ya usimamizi wa kodi nchini kwa kuongeza ufanisi wa ukaguzi, uhakiki wa mapato na kuboresha mifumo ya ufuatiliaji wa makusanyo ili kuongeza uwazi na uwajibikaji. Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, amesema taasisi hiyo imepokea maelekezo yote ya Kamati na itayafanyia kazi ndani ya muda uliopangwa ili kuboresha utendaji na kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato. Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TRA, Uledi Mussa, amesema majadiliano hayo yamekuwa furs...

KILIMANJARO INTERNATIONAL LEATHER INDUSTRIES CHATAJWA KUWA KIWANDA BORA CHA UZALISHAJI BIDHAA ZA NGOZI TANZANIA

   Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSSSF), Bw. Fortunatus Makore Magambo, amewataka Waheshimiwa Wabunge kuwa mabalozi wa bidhaa za ngozi zinazozalishwa nchini kwa kuzitumia na kuzitangaza, hatua itakayosaidia kukuza viwanda vya ndani, kuongeza ajira na kuimarisha uchumi wa taifa. Akizungumza katika Ukumbi wa Msekwa leo Jun 15,2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya shughuli na mafanikio ya Kiwanda cha Ngozi cha Kilimanjaro (Kilimanjaro International Leather Industries Company Limited - KLICL), Bw. Magambo amesema Tanzania ina uwezo mkubwa wa kuzalisha bidhaa bora za ngozi zinazoweza kushindana katika soko la kikanda na kimataifa kutokana na upatikanaji wa malighafi za kutosha na uwekezaji uliofanywa katika sekta hiyo. Amesema KLICL, imeendelea kuwa miongoni mwa viwanda vikubwa vya uchakataji wa ngozi nchini kwa kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwemo viatu, mikanda, mabegi na bidhaa nyingine zinazokidhi viwango vya ubora vya kimataifa. “Tunawaomba ...

MAGAMBO AWAOMBA WABUNGE KUWA MABALOZI WA BIDHAA ZA NGOZI KIWANDA CHA KILIMANJARO

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSSSF), Bw. Fortunatus Makore Magambo, amewataka Waheshimiwa Wabunge kuwa mabalozi wa bidhaa za ngozi zinazozalishwa nchini kwa kuzitumia na kuzitangaza, hatua itakayosaidia kukuza viwanda vya ndani, kuongeza ajira na kuimarisha uchumi wa taifa. Akizungumza katika Ukumbi wa Msekwa leo Jun 15,2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya shughuli na mafanikio ya Kiwanda cha Ngozi cha Kilimanjaro (Kilimanjaro International Leather Industries Company Limited - KLICL), Bw. Magambo amesema Tanzania ina uwezo mkubwa wa kuzalisha bidhaa bora za ngozi zinazoweza kushindana katika soko la kikanda na kimataifa kutokana na upatikanaji wa malighafi za kutosha na uwekezaji uliofanywa katika sekta hiyo. Amesema KLICL, imeendelea kuwa miongoni mwa viwanda vikubwa vya uchakataji wa ngozi nchini kwa kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwemo viatu, mikanda, mabegi na bidhaa nyingine zinazokidhi viwango vya ubora vya kimataifa. “Tunawaomba Waheshi...