Wananchi wa Kata ya Zuzu, Jijini Dodoma, wameibuka na malalamiko makali yenye hisia nzito na machungu makubwa, wakimlenga Diwani wa kata hiyo kwa kumtuhumu kuhusika katika kufungwa kwa eneo la uchimbaji wa kokoto na mchanga ambalo lilikuwa mkombozi wao wa maisha kwa zaidi ya wananchi 300. Kwa sauti zilizotawaliwa na huzuni, hasira na wakati mwingine machozi yakibubujika, wananchi hao wamesimulia jinsi maisha yao yalivyoporomoka ghafla kufuatia kufungwa kwa eneo hilo, wakisema walikuwa wakitegemea uchimbaji huo kama chanzo kikuu cha kipato cha kila siku. Wamesema kupitia shughuli hizo walikuwa wakigharamia mahitaji ya familia, ada za shule za watoto na matumizi ya msingi ya nyumbani, lakini sasa wamebaki wakikabiliwa na hali ngumu ya maisha isiyo na uhakika wala matumaini. Kwa hisia kali na maumivu ya wazi, wananchi hao wamedai kuwa uamuzi wa kufungwa kwa eneo hilo ulifanyika bila kushirikishwa wala kufanyika mkutano wa pamoja wa wananchi, jambo ambalo wamesema limeongeza hasira, m...
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Moi, jijini Mombasa, Kenya, leo tarehe 17 Juni 2026, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Rais Dkt. Mwinyi ameambatana na ujumbe wake, wakiwemo Mhe. Mama Mariam Mwinyi na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe. Rais Dkt. Mwinyi amepokelewa uwanjani hapo na Waziri wa Michezo, Uchumi Ubunifu na Vijana wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Salim Mvurya Mgala, Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Mhe. Masoud Ali Mohamed, pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dkt. Bernard Yohana Kibesse. Katika ziara hiyo, Rais Dkt. Mwinyi atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa 11 wa Masuala ya Bahari (11th Our Ocean Conference).