Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

WAZIRI NYANSAHO ATANGAZA FURSA KWA UWT MARA

 Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa (JKT)Dkt Rhimo Nyansaho ametoa Vizimba vitano  vya ufugaji wa Samaki kwa Umoja wa  Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Mara ili kusaidia jumuiya kujiimarisha kiuchumi.  Vizimba hivyo vitano ambavyo vitatumika kufugia samaki katika ziwa Victoria vina thamani ya shilingi Milioni 125. Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo ya uongozi ya UWT mkoa wa Mara mjini Musoma June 18 mwaka huu 2026 dkt  Nyansaho amesema lazima jumuiya hiyo muhimu ya chama cha Mapinduzi iweze kuimarika kiuchumi.  Waziri Nyansaho amesema kutokana na ukubwa wa Jumuiya hiyo inahitaji kuwa na mapato yake ili waweze kujitegemea katika uendeshaji wa shughuli zake na kujitegemea hasa nyakati za chaguzi.  Amesema Jumuiya hiyo ni miongoni mwa Jumuia kubwa na muhimu ndani ya CCM hivyo wataendelea kutafuta fursa mbalimbali za kiuchumi ili kukuza uchumi wa Jumuia, familia na Taifa kwa ujumla. Sambamba na hilo Waziri huyo pia ameiahidi Jumuia hiyo kuwa ...
Recent posts

KUIBUA,KUKUZA NA KUENDELEZA VIPAJI NI JUKUMU LETU"MGANDI

Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga  Vijana wametakiwa kuchangamkia fursa ilikuweza kutimizandoto zao na kukuza vipaji kwani bila kufanya hivyo watabaki kuona maisha magumu Kila siku. Hayo yamesemwa na mkurungenzi mtendaji wa kituo cha kulea na kukuza vipaji kwa upande wa soka Mohamed Mgandi kilichopo wilayani Korogwe Cha KOROGWE YOUTH SOCCER CENTER ambacho mpaka sasa kina mwaka mmoja. Mgandi amesema lengo la kituo hicho ni kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vilivyopo kwani mpira sasa ni biashara na ili iweze kuuzika ni lazma ipikwe vizuri kuanzia hatua za awali. "Vipaji ni vingi sana ,Kwa kuliona hilo tukaona tuanzishe kituo ambacho kitazalisha wanasoka Bora na wenye ujuzi wa kutosha kwani sisis tuna pokea watoto kuanzia umri wa miaka sita mpaka kumi na sita (6-16),hapa utaona mtoto huyo lazima awe Bora kwani tunaanza kumpika angali bado mchanga kabisa", alisema Mgandi. Aidha kituo hicho pia kimekuwa kikishirikiana na vituo vingine katika kuendeleza vipjia  ikiwemo Azam na mpaka s...

MWANAFA AFUNGA UMITASHUMTA, AELEZA MKAKATI WA SERIKALI

📍 Bilioni 15 kukamilisha ujenzi akademia ya michezo Malya NA Mashaka Mhando, Iringa SERIKALI imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 15 katika mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Akademia ya Taifa ya Michezo iliyopo Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya. Hatua hiyo ya kiserikali inalenga kuweka mfumo thabiti na wa kudumu wa kuibua, kulelea, na kukuza vipaji vinavyopatikana kupitia mashindano ya shule za msingi na sekondari (UMITASHUMTA na UMISSETA). Hayo yamebainishwa jana, Juni 17, 2026, na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), wakati akifunga rasmi mashindano ya UMITASHUMTA yaliyokuwa yakifanyika mkoani Iringa. Mhe. Mwinjuma alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza kwa nguvu kubwa katika sekta ya michezo na sanaa, ikitambua mchango wake katika kuzalisha ajira, kujenga afya, na kuongeza ushindani wa Taifa kimataifa. Malya Academy na Matunda ya Serengeti Boys Akifafanua...

MASOKO YA MADINI YAIMARISHA UWAZI, KUDHIBITI UTOROSHAJI

 📍Dodoma Tume ya Madini imesema kuanzishwa kwa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini nchini kumeongeza uwazi katika biashara ya madini na kusaidia kudhibiti utoroshaji wa rasilimali hiyo, hatua iliyochangia kuongezeka kwa mapato ya Serikali. Akizungumza leo katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, Afisa wa Tume ya Madini kutoka Kurugenzi ya Ukaguzi na Biashara ya Madini, Ibrahim Akyoo, amesema mfumo huo umewezesha wachimbaji na wafanyabiashara kuuza madini kupitia njia rasmi na hivyo kuimarisha usimamizi wa sekta hiyo. Amesema kwa sasa nchini kuna masoko ya madini 44 na vituo vya ununuzi wa madini 120 vinavyorahisisha biashara ya madini na kuhakikisha Serikali inapata mapato stahiki yatokanayo na rasilimali hizo. Akyoo amesema miongoni mwa majukumu ya Kurugenzi ya Ukaguzi na Biashara ya Madini ni kusimamia biashara ya madini nchini, kuhakikisha ushiriki wa Watanzania katika sekta hiyo unaongezeka, kudhibiti ut...

DKT. RHIMO NYANSAHO AKIWASILI MUSOMA KUFUNGA KONGAMANO LA UWT MKOA WA MARA

 MATUKIO KATIKA PICHA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MH DKT RHIMO NYANSAHO AKIWASILI MJINI MUSOMA KWA AJILI YA KUFUNGA KONGAMANO LA UMOJA WANAWAKE TANZANIA UWT MKOA WA MARA