Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

TANZANIA KUJIIMARISHA KUWA KITOVU CHA UTAFITI KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA

Na Mwandishi Wetu - Msumbiji SERIKALI imesema inaendelea kujipanga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utafiti katika kukabiliana na majanga katika ukanda wa Kusini mwa Afrika (SADC) na Afrika Mashariki, hatua itakayosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari na uokoaji. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi, wakati wa ziara ya kubadilishana uzoefu kati ya Tanzania na Msumbiji kuhusu hatua za mapema kabla ya majanga. Ziara hiyo ya siku tano inayofanyika jijini Maputo nchini Msumbiji kuanzia Mei 25 hadi 29, 2026, inalenga kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa, tafiti na mifumo ya utoaji wa taarifa za tahadhari mapema ili kupunguza athari za majanga. Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Yonazi alisema Tanzania imeendelea kujenga uwezo wake katika kukabiliana na majanga kupitia uwekezaji katika tafiti na matumizi ya teknolojia za kisasa ikiwemo mifumo ya kidijitali na aki...
Recent posts

MTWARA YATANUA FURSA ZA MADINI, MAPATO YA SERIKALI YAPANDA MARA NNE

📍Mtwara Mkoa wa Mtwara umeendelea kujidhihirisha kama kitovu muhimu cha uwekezaji wa madini nchini kutokana na uwepo wa rasilimali nyingi za madini ya viwandani, vito na madini mkakati, huku mapato ya Serikali kupitia sekta hiyo yakiongezeka kwa kasi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara, Winnifrida Mrema, amesema mkoa huo unafahamika zaidi kwa uwepo wa madini ya chokaa yanayotumika kuzalisha saruji katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote, jambo linalochangia kukuza uchumi wa mkoa na kuimarisha shughuli za viwanda nchini. Amesema Mkoa wa Mtwara pia una utajiri wa madini mengine ya viwandani yakiwemo chuma, shaba, kinywe, ulanga pamoja na madini ya mchanga mzito (heavy mineral sands), ambayo ni miongoni mwa madini mkakati yanayohitajika kwa kiwango kikubwa duniani katika utengenezaji wa teknolojia mbalimbali ikiwemo magari ya umeme. Aidha, amesema Bandari ya Mtwara imeendelea kuwa kiungo muhimu cha biashara na usafirishaji wa madini na bidhaa za ...

MWANAFA ASHIRIKI SWALAH YA EID JITEGEMEE, AENDA MLINGANO KUCHINJA NG'OMBE

 *EID AL-ADHA MUHEZA:* Na Mwandishi Wetu, Muheza  MBUNGE wa Muheza, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), ameshiriki Swalah ya Eid Al-Adha iliyofanyika katika uwanja wa Jitegemee wilayani hapa, na kuwataka waumini wa Kiislamu kudumisha amani. Swalah hiyo kubwa ya iliongozwa na Sheikh Khatibu, ambaye kabla ya kuanza ibada, aliwasihi Waislamu kufuata kikamilifu mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW) na kuacha kupoteza muda mwingi kwenye mambo yasiyo na msingi.  Sheikh Khatibu aliwakumbusha waumini hao umuhimu wa kufanya ibada za funga zilizowekwa kisheria katika siku kumi za mwanzo wa mwezi wa Dhul-Hijjah ili kujisogeza karibu na Mwenyezi Mungu. Akisalimia maelfu ya waumini waliofurika uwanjani hapo, Mhe. Mwinjuma aliwatakia heri ya sikukuu ya Eid na kuwasisitiza kuendelea kuwaombea viongozi wakuu wa nchi kila wanapofanya ibada zao. "Tunapoendelea kufurahia sikukuu hii ya kuchinja, nawaomba sana ndugu zangu tusiache kuwaombea viongozi wetu wa kitaifa, hususan Rais wa Jamhuri ya Muunga...

SAGINI ACHINJA NG'OMBE 400 NA KONDOO 1000 EID AL ADHA

Mbunge wa zamani wa Jimbo la Butiama Mhe. Jumanne Abdallah Sagini Kwa kushirikiana Taasisi ya ITTIFAK International kutoka nchini Uturuki amechinja Ng'ombe 400 na Kondoo 1000 na kugawanywa kwenye vitongoji 370 na taasisi zote za umma na binafsi zilizopo katika Wilaya ya Butiama ikiwemo baadhi ya misikiti Wilaya ya Musoma mkoani Mara kwa ajili ya kitoweo kwa wananchi kipindi hiki cha kusherehekea Sikukuu ya Eid Al-Adha. Zoezi hilo la Sadaka limefanyika leo Mei 27, 2026  nyumbani kwake Kijiji cha Kiabakari, Kata ya Kukirango katika Wilaya ya Butiama kama sehemu ya kuimarika kiimani na ukarimu na mshikamano na upendo. Kwa upande wake Sheikh wa Kata ya Mugango Musoma Vijijini Mwabadi Yusuph Chogero ameeleza kuwa kwa kipindi hiki Sagini amepanua wigo zaidi kwani Sadaka hiyo imewafikia hadi Misikiti Saba iliyopo Musoma Vijijini, huku Sheikh wa Kata ya Kukirango Juma Maharage amesema imekuwa ni desturi ya Sagini kuwaalika wananchi mbalimbali katika kushiriki kitoweo kwa pamoja. Baadhi ya ...

ZIARA YA MADIWANI KIBAHA YAFUNGUA FURSA MPYA ZA KUONGEZA MAPATO

MADIWANI wa Manispaa ya Kibaha wameeleza kuwa ziara yao ya mafunzo katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya na Halmashauri ya Mji Tunduma italeta manufaa makubwa katika kuongeza mapato na kuimarisha miradi ya maendeleo ya Manispaa hiyo. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Mawazo Nicas amesema madiwani pamoja na wataalamu wa halmashauri wamepata uzoefu mkubwa kuhusu usimamizi wa mapato na uendeshaji wa vitega uchumi vinavyochangia maendeleo ya wananchi. Amesema katika Jiji la Mbeya wamejifunza namna miradi ya ujenzi wa maduka, ukumbi pamoja na maeneo ya mapumziko inavyoongeza mapato ya halmashauri na kutoa huduma bora kwa wananchi na wafanyabiashara. Kwa upande wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Dkt. Nicas amesema wamevutiwa na mfumo wa parking za malori unaochangia mapato makubwa ya Halmashauri hiyo kutokana na shughuli za biashara mpakani mwa Tanzania na Zambia. “Tumepata mambo mengi ya kujifunza. Tumeona namna parking za malori zinavyoongeza mapato Tundu...

KAMPUNI YA AMBONI YABOMOA NYUMBA ZA KAYA 67, MWANAFA ALAANI

📍Wananchi waachwa wakilala nje kwenye baridi, mwekezaji adaiwa kugomea wito wa Mkuu wa Mkoa Na Mwandishi Wetu, Muheza KAMPUNI ya Amboni Plantation imewabomolea nyumba na kuwaacha wakilala nje kwenye baridi wananchi wa kaya 67, katika kitongoji cha Maisha Plus kilichopo kata ya Kigombe, wilayani Muheza mkoani Tanga. Uharibifu huo wa dharura umefanyika Ijumaa iliyopita katika Kijiji cha Mshakangoto, ambapo kampuni hiyo inayolima mkonge imetumia uamuzi wa mahakama kuondoa familia hizo, ambazo nyingi ni za vibarua na wastaafu wa shamba hilo. Mbunge wa Muheza na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), alitembelea eneo hilo Leo Mei 26 kushuhudia uharibifu huo na kulaani kitendo hicho akikitaja kuwa ni unyama uliokosa utu. Mhe. Mwinjuma alifichua kuwa, baada ya mwekezaji huyo kushinda kesi, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burihan alimwita mwekezaji ili kuweka utaratibu wa kiungwana wa kuwahamisha wananchi lakini hakupatikana kwa simu zake ...