▪️Waziri Mavunde akutana na Mwekezaji wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma ▪️Ni kiwanda cha Oriental Casting and Forging Ltd cha China ▪️Kiwanda kikubwa kujengwa Buzwagi Kahama ▪️Tanzania yajipanga kuwa kitovu cha uzalishaji wa bidhaa za migodini Afrika 📍 Dar es salaam Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini. Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini. Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini il...
📍Itafanya tathimini ya uchaguzi uliopita na Hali ya kisiasa nchini Na MASHAKA MHANDO,DAR ES SALAAM CHAMA cha National League for Democracy (NLD), kimetangaza kuitisha kikao kizito cha kimaamuzi cha Kamati Kuu ya chama hicho kwa muda wa siku mbili mkoani Dar es Salaam, kikiwa na lengo la kujadili mustakabali wa chama na kufanya tathmini ya kina ya kisiasa baada ya kumalizika kwa michakato ya uchaguzi. Kikao hicho muhimu kinatarajiwa kufanyika kesho Jumatano, Julai Mosi, na keshokutwa Alhamisi, Julai 2, 2026, katika Ukumbi wa Popex uliopo Buguruni Sheli, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. Akizungumza kupitia taarifa rasmi kwa umma iliyotolewa leo Jumanne, Juni 30, 2026, Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano ya Umma wa NLD, Bw. Pogora Ibrahim Pogora, alibainisha kuwa kikao hicho kimebeba ajenda kuu nne mahususi zinazolenga kukivusha chama hicho kuelekea hatua mpya ya ushindani wa kisiasa. "Chama cha National League for Democracy (NLD) kinapenda kuwajulisha wanachama, wadau na u...