Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa (JKT)Dkt Rhimo Nyansaho ametoa Vizimba vitano vya ufugaji wa Samaki kwa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Mara ili kusaidia jumuiya kujiimarisha kiuchumi. Vizimba hivyo vitano ambavyo vitatumika kufugia samaki katika ziwa Victoria vina thamani ya shilingi Milioni 125. Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo ya uongozi ya UWT mkoa wa Mara mjini Musoma June 18 mwaka huu 2026 dkt Nyansaho amesema lazima jumuiya hiyo muhimu ya chama cha Mapinduzi iweze kuimarika kiuchumi. Waziri Nyansaho amesema kutokana na ukubwa wa Jumuiya hiyo inahitaji kuwa na mapato yake ili waweze kujitegemea katika uendeshaji wa shughuli zake na kujitegemea hasa nyakati za chaguzi. Amesema Jumuiya hiyo ni miongoni mwa Jumuia kubwa na muhimu ndani ya CCM hivyo wataendelea kutafuta fursa mbalimbali za kiuchumi ili kukuza uchumi wa Jumuia, familia na Taifa kwa ujumla. Sambamba na hilo Waziri huyo pia ameiahidi Jumuia hiyo kuwa ...
Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga Vijana wametakiwa kuchangamkia fursa ilikuweza kutimizandoto zao na kukuza vipaji kwani bila kufanya hivyo watabaki kuona maisha magumu Kila siku. Hayo yamesemwa na mkurungenzi mtendaji wa kituo cha kulea na kukuza vipaji kwa upande wa soka Mohamed Mgandi kilichopo wilayani Korogwe Cha KOROGWE YOUTH SOCCER CENTER ambacho mpaka sasa kina mwaka mmoja. Mgandi amesema lengo la kituo hicho ni kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vilivyopo kwani mpira sasa ni biashara na ili iweze kuuzika ni lazma ipikwe vizuri kuanzia hatua za awali. "Vipaji ni vingi sana ,Kwa kuliona hilo tukaona tuanzishe kituo ambacho kitazalisha wanasoka Bora na wenye ujuzi wa kutosha kwani sisis tuna pokea watoto kuanzia umri wa miaka sita mpaka kumi na sita (6-16),hapa utaona mtoto huyo lazima awe Bora kwani tunaanza kumpika angali bado mchanga kabisa", alisema Mgandi. Aidha kituo hicho pia kimekuwa kikishirikiana na vituo vingine katika kuendeleza vipjia ikiwemo Azam na mpaka s...