WATANZANIA 669 waliopo Afrika Kusini wanatarajiwa kurejea nchini kwa hiari yao kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha kurejea nyumbani na kuungana na familia zao. Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, James Bwana, ameyasema hayo leo kuwa utekelezaji wa mpango huo utaanza na kundi la kwanza la Watanzania 241 kutoka Durban, Jimbo la KwaZulu-Natal, watakaorejea nchini Agosti 26, 2026 kwa ndege ya Air Tanzania. Kwa mujibu wa Balozi Bwana, Watanzania hao watafanyiwa uhakiki Agosti 25 na 26 kwa kushirikisha Ubalozi wa Tanzania na mamlaka za Afrika Kusini, kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini. Amesema mpango huo umeanza baada ya Watanzania hao kuomba kwa hiari yao msaada wa Serikali ili waweze kurejea Tanzania, baada ya kuishi Afrika Kusini kwa muda mrefu. “Mheshimiwa Rais amewakaribisha tena nyumbani na amenielekeza kama Balozi wake hapa Afrika Kusini kuhakikisha Watanzania walio tayari kurejea...
▪︎ Ataka kazi ifanyike usiku na mchana inapowezekana ▪︎ Asisitiza mashindano hayo ni fursa kubwa ya kiuchumi kwa Tanzania WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kuongezwa kasi ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ili vikamilike kwa wakati na kukidhi viwango vinavyotakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Amesema kazi hiyo inapaswa kufanyika kwa kasi, ikiwemo kuongeza muda wa kufanya kazi pale inapobidi, ili viwanja vikamilike kwa wakati na Tanzania iwe tayari kabla ya ukaguzi wa maandalizi unaotarajiwa kufanywa na CAF. Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo (Ijumaa, Agosti 21, 2026) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vya Farasi na Leaders Club jijini Dar es Salaam, ambavyo ni miongoni mwa viwanja vitakavyotumika katika maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027 yatakayofanyika kwa ushirikiano wa Tanzania, Kenya na Uganda. Amesema Tanzania haipaswi kusubiri hadi dakika za mwisho...