Skip to main content

Posts

Showing posts from September 14, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Watanzania waaswa kuthamini uwekezaji unaofanywa na Serikali katika miradi ya maendeleo

Wananchi wamehimizwa kuachana na imani potofu kuwa Miradi ya maendeleo ikiwemo ya ujenzi wa skimu za umwagiliaji inayotekelezwa na Serikali kwenye maeneo yao ni matambiko.  Waziri wa kilimo Hussein Bashe amesema kuwa imani hizo zikiwemo za kutaka miradi hiyo isitishwe haikubaliki na kuwataka watanzania   kuthamini uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali katika miradi ya maendeleo ikiwemo miradi ya skimu za umwagiliaji  Bashe ameyaeleza hayo katika mwendelezo wa ziara yake ya kikazi  Mkoani Tabora ambapo ametembelea eneo la mradi  wa Umwagiliaji wa Mwasimbo Igunga, Mwampuli, Mwanzugi na Makomero.  Waziri Bashe, ameeleza kushangazwa na hatua ya baadhi ya wananchi wa halmashauri yaNzega vijijini kupinga utekelezaji wa miradi ya skimu za umwagiliaji unaohusisha ujenzi wa miundombinu ya bwawa la Nsembo, ujenzi wa barabara, madaraja madogo na mitaro ya kupitisha maji pembezoni mwa barabara.  Wananchi  wa eneo hilo wanapinga miradi hiyo kwa imani potofu ...

Waziri Mavunde awataka Watanzania kuchangamkia Manunuzi ya Trillioni 3.2 Migodini

  Waziri wa Madini  Anthony Mavunde amewataka watanzania wanaoshiriki kwenye mnyororo wa thamani wa sekta ya madini kuchangamkia fursa  iliyopo ya manunuzi ya bidhaa na utoaji huduma migodini ambayo kwa mwaka wa fedha 2023/24 Jumla ya kiasi cha Tsh Trilioni 3.1 zimetumika katika eneo la manunuzi ya bidhaa na huduma. Waziri Mavunde ameyasema hayo jana Jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa Chama cha Watoa Huduma na Wasambazaji wa bidhaa Migodini (TAMISA) “Uwekezaji nchini Tanzania kwenye sekta ya madini unakua siku hadi siku na hii inatokana na mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyowekwa na serikali chini ya uongozi wa Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.  Chama hiki kitasaidia kuwa na sauti ya pamoja katika kuwajengea uwezo watanzania na kuwaimarisha ili kuwa shindani katika utoaji wa huduma na usambazaji wa bidhaa migodini. Natamani sana kuziona hizi Trilioni 3.1 zinabaki mikononi mwa watanzania ili kuchochea uchumi wa nchi yetu kwa kuanzisha viwanda vya ku...

Marathon ni Mpango Mkakati wa Kujenga Afya za Watanzania -Majaliwa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema marathon zinazofanyika kila kona nchini ni mpango mkakati wa kuwafanya Watanzania wawe na afya njema na wakae pamoja ili kubadilishana mawazo. “Ni mkakati wa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahamasisha wananchi wetu kufanya mazoezi ili kupunguza magonjwa yasiyoambukiza kama vile kisukari na presha,” amesema. Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Septemba 14, 2024) wakati akizungumza na viongozi na wadau mbalimbali walioshiriki Ruangwa Marathon 2024 (Msimu wa Pili) katika viwanja vya Madini, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi. “Mbio hizi za Ruangwa ni zaidi ya mbio kwa sababu malengo yake makubwa ni kuhamasisha wana-Ruangwa tuwe na umoja; tuimarishe ujenzi wa afya zetu, tupate fursa ya kufahamiana na kuimarisha urafiki,” amesema. Waziri Mkuu Majaliwa ambaye pia ni mbunge wa Ruangwa, amewataka Wana-Ruangwa wajitokeze kusimamia miradi ya maendeleo iliyomo kwenye wilaya hiyo na kupitia mkusanyiko mkubwa kama huo watengeneze mijadala ya kiuchumi katika ngazi na ...

Wafanyabiashara Ruvuma Wamshukuru Rais Dkt Samia Kwa Fursa ya Tamasha la Utamaduni

Na Elizabeth Cornely KUFUATIA Tamasha la Utamaduni la Taifa kupelekwa mkoani Ruvuma, baadhi ya wakazi mkoani humo wamefurahia na kuelezea namna ambavyo wamejipanga kunufaika nalo kupitia fursa mbalimbali zitakazopatina katika kipindi chote ambacho litafanyika mkoani kwao. Pia wamemshukuru Rais Samia kwa kuanzisha utaratibu huo wa kuwa na tamasha la utamaduni kwa kuwa pamoja na kuwakumbusha kuenzi tamaduni zao lakini wanalitumia kujinufaisha kiuchumi. Tito Mbilinyi, mkazi wa Songea mkoani Ruvuma, anasema kwamba matamanio yao kwa miaka mingi ilikuwa kuona tamaduni zao zinaendelezwa, hivyo wanampongeza Rais Samia kwa kuliona hilo na kuruhusu kufanyika. “Mimi namshukuru sana Rais Samia kwa kutuletea tamasha hili, tulilisubiri sana, kwa hiyo tunashukuru sana.  Sisi kama wafanyabiashara tunasema hivi, karibu mgeni, mwenyeji apone, kwa sababu hata mwenye nyumba ya kulala wageni, mama lishe, anayejishughulisha na usafirishaji,wote tutanufaika kwa sababu ugeni utakaokuja ni mkubwa sana,”ame...

Majenerali na Maafisa wa JWTZ Wavishwa Nishani Mbalimbali

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda kwa niaba ya Mhe Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan amewavisha nishani mbalimbali Majenerali, Maafisa na Askari wa JWTZ mjini Morogoro tarehe 14 Septemba 2024. Nishani hizo ni Nishani ya Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, Nishani ya Miaka 60 ya Muungano pamoja na Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ.