Skip to main content

Posts

Showing posts from July 28, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Muhongo Kufanya Ziara Bukima Kuhamasisha Maendeleo

Na Shomari Binda-Musoma MBUNGE wa jimbo la Musoma vijijini Profesa Sospeter Muhongo anatarajiwa kufanya ziara kwenye Kata ya Bukima yenye lengo la kufufua ari ya kuchangia miradi ya maendeleo. Ziara hiyo itafanyika baada ya kumalizika kwa ziara na mkesha wa Mwenge wa Uhuru utakaokuwa Bukima jumatano julai 31  Taarifa iliyotolewa na ofisi ya mbunge imesema baada ya mkesha huo wa Mwenge Mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Profesa Sospeter Muhongo atafanya ziara maalum kwenye Kata ya Bukima yenye malengo ya kufufua ari ya wananchi kujitolea kuchangia miradi yao ya maendeleo. Taarifa hiyo imesema ipo miradi iliyokwama zaidi ya miaka 5 Kata ya  Bukima, ikiwemo kukosa maabara hata mmoja kwenye sekondari ya Kata huku vifaa vilivyochangwa na mbunge vikiwa stoo.  Mradi mwingine uliokwama ni wodi ya mama mtoto kwenyez ahanati ya Bukima ikiwa inajengwa kwa zaidi ya miaka mitano ambapo mbunge wa jimbo alichangia saruji ya ujenzi. Katika Kijiji cha Butata ujenzi  wa zahanati umesi...

Mhe. Mohamed Mchengerwa Azindua Bodi Mpya ya Ushauri ya Tarura

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali  za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuwasaidia na  kuwashauri watendaji wafanye kazi vizuri ili kuhakikisha anayoyaota Mhe. Rais kwa Watanzania yanatimia. Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi  wa Bodi ya Wakala huo ulofanyika  jijijni Mbeya. “Mwenyekiti wa bodi mtakuwa na kazi kubwa ya kuwashauri watendaji hawa, niwaombe mtusaidie na kutushauri kwani wananchi wanataka barabara na bajeti ya TARURA imeongezeka kutoka milioni 200 hadi kufika Tilioni  1.3”. Hata hivyo ameitaka bodi hiyo kuwa wabunifu na kujipanga ili barabara zinazosimamiwa na TARURA zikamilike pia washirikiane na wataalam kuhakikisha mchakato wa kuanzishwa kwa hati fungani unakamilika na kuzinduliwa ili kuwasaidia wakandarasi wazawa. Aidha, Waziri Mchengerwa ameipongeza TARURA kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Rais wa FEMATA John Bina Kuanza Ziara ya Kuwatembelea Wachimbaji Nchini

Rais wa shirikisho la vyama vya wachimbaji madini Tanzania FEMATA ambae pia ni mwenyekiti wa kamati tendaji  Mhe. John Wambura Bina, anataraji kuanza ziara maalum katika mikoa mbalimbali nchini, ambapo ataambatana na mwenyekiti wa TAWOMA Bi. semeni John Malale, pamoja na viongozi waandamizi wa TAWOMA kanda ya nyanda za juu kusini. Pamoja na Viongozi hao pia itaamabatana na viongoizi waandamizi wa kampuni ya bima kwa wachimbaji wa madini Tanzania (Cizass Insurance Brokers) na viongozi waandamizi wa kampuni ya vitambulisho vya Kisasa (Biometric Identification Cards) kwa wachimbaji wa madini Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa hii iliyotolewa na kurugenzi ta habari FEMATA makao makuu imesema akiwa katika awamu ya kwanza ya ziara yake Mhe. John Bina atatembelea mkoa wa Dodoma mnamo julai 30, mkoa wa Iringa Julai 31, Songwe August Mosi na Pili kisha atamalizia na Mkoa wa Mbeya. Awamu ya pili ya Ziara hiyo itahusisha mikoa ya Njombe, Ruvuma, Mtwara, Lindi na kisha Dar es salaam na Pwani. Pia...

Shekh Msabaha Awataka Viongozi wa Kiislamu Kutumia Vyema Mafunzo Yaliyotolewa na Bakwata

Na Shomari Binda-Musoma SHEKH wa mkoa wa Mara Msabaha Kassim amewataka viongozi wa dini wakiwemo wa misikiti kutumia vizuri mafunzo yanayotolewa na Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) Kauli hiyo ameitoa leo julai 28/2024 alipokuwa akifunga mafunzo yaliyotolewa na Bakwata kwa viongozi hao yaliyohusu utunzaji na udhibiti wa takwimu na rasilimali Amesema elimu na mafunzo ni jambo muhimu katika kupata utambuzi na kufanya uongozi kidigitali. Msabaha amesema suala la elimu na kuongeza ujuzi limeelezwa kwenye Quran na anachofanya Mufti Shekh Abubakar Zuber ni jambo jema Shekh huyo wa mkoa wa Mara amesema mtu anapaswa kuifuata elimu lakini Mufti ameamua kuwaletea hivyo ni vyema kwenda kutumia vizuri mafunzo waliyoyapata. " Niwapongeze mlioshiriki mafunzo hayo na niwaoombe tukayafanyie kazi ili malengo yaliyokusudiwa yaweza kufanikiwa. Walimu wa madrasa tuliopata mafunzo hayo tukayatumia kupata kakwimu za wanafunzi wetu na tutumie mafunzo kubadilika na kuacha mazoea",amesema Mratibu...

Mashindano ya Klasta Compassion Cup Misimu wa 23/24 Yamalizika

Mch. Askofu Valentine Mbuki Katibu wa Wachungaji Klasta ya Misungwi amehitimisha kilele cha fainali mashindano ya Klasta Compassion CUP 23/24 ambapo  AICT Mabuki wakibuka kidedea kwa upande wa wavulana kwa ushindi wa magoli 5 - 4 dhidi ya AICT Masasi, Kwa upande wa wasichana AICT Kijima imeibuka na ushindi kwa kuichapa goli 1 sifuri timu ya KKKT Misungwi Huku kwa  mpira wa PETE AICT Mabuki wakiichabanga magoli 35 kwa 32 timu ya AICT Kijima Mashindano hayo ambayo yalishirikisha jumla ya timu 20,wavulana timu 10 na wasichana timu 10 na yamefanyika kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwili hadi kufikia tamati yake katika uwanja wa Chama cha Mapinduzi ( CCM ) Misasi.

Majaliwa Awataka Wananchi Kuzingatia Mazoezi ili Kuimarisha Afya

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Afya iendelee kuwahamasisha wananchi wabadili mitindo ya maisha ili kuepuka tabia zembe zinazochochea ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa. “Wizara ya Afya iendelee kushirikiana na wadau kuhamasisha Watanzania kubadili mwenendo wa maisha kwa kuepuka tabia zembe zinazochochea ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa. Tuendelee kuzingatia mazoezi ili kuimarisha afya zetu na kuipunguzia Serikali mzigo wa kugharamia tiba ya magonjwa yasiyoambukizwa,” amesema. Akizungumza na viongozi, wananchi na wadau mbalimbali walioshiriki mbio za NBC Dodoma Marathon za mwaka 2024 kabla ya kutoa tuzo na zawadi kwenye uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma, leo (Jumapili, Julai 28, 2024), Waziri Mkuu amesema takwimu za Wizara ya Afya zinaonesha kuwa idadi ya watu wenye magonjwa yasiyoambukiza imeongezeka. Amesema magonjwa yasiyoambukiza ambayo yanaongoza nchini ni pamoja na kisukari, moyo, figo na afya ya akili na akatumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi walioshiriki m...

Tanzania Kushirikiana na Chuo Cha Mafunzo ya Upishi Cha Hispania Kukuza Utalii wa Vyakula

Na Mwandishi Wetu- Zimbabwe Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekubaliana kushirikiana na Chuo cha Mafunzo ya Mapishi cha Basque (Basque Culinary Center) cha nchini Uhispania kilichojikita katika kutoa mafunzo, kufanya tafiti, ubunifu na kufanya uendelezaji wa utalii wa vyakula (Gastronimy Tourism) na lishe.  Lengo la kushirikiana na chuo hicho kinachoongoza duniani kwa Sayansi ya Utalii wa Vyakula, Utafiti na Ubunifu ni kukuza Utalii wa Vyakula nchini Tanzania. Hayo yamebainika leo Julai 28, 2024 katika kikao kati ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) na Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Mafunzo cha Basque, Joxe Mari Aizega wakati wa ziara ya kutembelea Kijiji cha Utamaduni cha Umuzi kilichopo jijini Victoria Falls nchini Zimbabwe iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism). Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kairuki ameomba mashirikiano na chuo hicho katika utoaji wa elimu ya mapishi, kuwajengea uwezo wapishi wa nchini...

Wanawake Kata ya Kitaji Watakiwa Kujitokeza Kushiriki Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Na Shomari Binda-Musoma WANAWAKE wa Kata ya Kitaji manispaa ya Musoma wametakiwa kujitokeza Kushiriki Katika Uchaguzi wa serikali za Mitaa pamoja na kushikamana na kupendana Ili kuwa na umoja. Kauli hiyo imetolewa leo julai 28  na diwani wa viti maalum Asha Muhamed kwenye sherehe ya kumaliza mwaka ya kikundi cha wanawake wa ( UWT ) mtaa wa Kitaji D. Amesema wanawake wanayo nafasi ya kuongoza na uchaguzi unaokuja wa serikali za mitaa wajitokeze kuomba nafasi. Licha ya kuomba nafasi ya uongozi wanawake hao wametakiwa kushiriki kwenye uboreshaji wa daftari la wapiga kura na makazi. Akizungumzia kikundi hicho cha Kitaji Women Group Asha amewasihi kuwa na siri ya kikundi wanapokuwa wanajadili mambo yao. Amesema mafanikio ya kikundi ni kuwa wamoja na kushirikiana wakiongozwa na kuwa na usiri ndani ya kikundi ili kuweza kufikia malengo makubwa zaidi. " Niwapongeze wanawake wa Kitaji mtaa D kwa mafanikio ya kikundi chenu na mafanikio mliyoyapata kwa kipindi cha mwaka mmoja. " Licha y...

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna Afanya Ziara Kanda ya Magharibi

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna, akiambatana na viongozi wengine wa Benki, amefanya ziara ya kikazi katika Kanda ya Magharibi ya Tanzania, ikijumuisha mikoa ya Kigoma, Katavi, Tabora, Simiyu, Shinyanga, na Mwanza. Katika ziara hiyo ya wiki moja, Bi. Ruth Zaipuna amekutana na wafanyakazi wa Benki ya NMB, wateja, na wadau mbalimbali, akilenga kuimarisha uhusiano na kutoa mwongozo kuhusu utekelezaji wa mikakati ya Benki katika maeneo hayo. Pamoja na mambo mengine, Bi. Ruth Zaipuna amefanya vikao na viongozi wa baadhi ya mikoa hiyo yenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha na kuchangia katika ukuaji wa kiuchumi. Aidha, ziara hiyo pia ilitoa fursa ya kusikiliza maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau na kudhihirisha dhamira yetu ya kuendelea kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya Watanzania katika ngazi zote. Ziara hii ni muendelezo wa juhudi zetu katika kuhakikisha huduma bora za kifedha zinawafikia Watanzania katika kila kona ya nchi. #NMBKaribuYako

Dkt.Emmanuel Nchimbi Azuru Kaburi la Hayati Benjamin Mkapa Lupaso

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi ametembelea kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya 3, hayati Benjamin William Mkapa katika Kijiji cha Lupaso mkoani Mtwara, leo Julai 28, 2024, kuhani familia na kuzungumza na wananchi wa Lupaso. Balozi Nchimbi amesema “naomba nikiri kuwa mimi ni mwanafunzi wa hayati na nimekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Taifa (UVCCM), katika kipindi chake. Ndiye alinilipia ada ya kusoma chuo kikuu na alikuwa mfuatiliaji sana na alitulea vizuri.  Amesema sio sisi tu, bali Watanzania wote aliwalea pia. Alikuwa mzalendo kwa nchi, alifanya mabadiliko makubwa kwa nchi yake na kwa Chama chake, lakini yote CCM chini ya Dkt Samia tutaendelea kuyaenzi yale yote aliyoyoacha hayati Benjamin Mkapa. Pamoja hayo nimeambiwa kero za hapa na tumezichukua. CCM inatoa shilingi milioni 10 kuanza kukarabati shule ya hapa Lupaso.” Katika ziara hii Dk Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amosi Makalla, Katibu wa NEC-Or...