Skip to main content

Posts

Showing posts from September 6, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mkuu wa Mkoa Songwe Awataka Wananchi,Kamati ua Ulinzi na Usalama Kuwa Macho na Miradi ya Umwagiliaji *

NA MWANDISHI WETU MKUU wa Mkoa wa Songwe Jabir Makame, amewataka wananchi wa mkoa huo na kamati ya Ulinzi na Usalama kuwa macho na kutocheka na yeyote anayehujumu  miradi ya Umwagiliaji. Amesema fedha zinazowekezwa na Serikali katika miradi hiyo ni nyingi na Imelenga kupunguza umaskini kwa wakulima hivyo anayehujumu miradi ya Umwagiliaji anapaswa kuchukuliwa hatua kwa kuwa analihujumu Taifa  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Jabir amesema hayo wakati wa hafla ya kumkabidhi mkandarasi eneo la ujenzi wa mradi wa skimu ya Umwagiliaji Naming’ongo uliopo kata ya Chitete mkoani humo. Amesema mradi huwo wa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 24 utatekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ambapo ndani ya mradi huo kutakuwa na ujenzi wa barabara za ndani, ajira zaidi ya 2000 huku wakulima zaidi ya 6000 wakiwa wanufaika wa eneo hilo. “Wananachi na kamati ya ulinzi na usalama tuchukue hatua kwa watu wanaoharibu miundombinu ya Umwagiliaji, kamati yetu ichukue hatua ili kukomesha tabia hizo, shughu...

Tcra Yasitisha Leseni ya Jamii Forum

 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesitisha Leseni ya Maudhui Mtandaoni ya JamiiForums kwa muda wa siku 90 na kuzuia upatikanaji wa jukwaa hilo, kwa maelezo ya kukiuka Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kuhusu maudhui mtandaoni TCRA imesema uamuzi huu umetokana na JamiiForums kuchapisha taarifa ya Mwanasiasa Humphrey Polepole kuhusu Rostam kumiliki mgodi wa makaa ya mawe kwa asilimia 70 na taarifa za uhusiano kati ya Rais wa Tanzania na "Mfanyabiashara" Wicknell Chivayo bila kuzingatia mizania. Kwa mujibu wa TCRA, JamiiForums ilishindwa kutafuta maoni ya Mamlaka husika/Msemaji wa Rais/Serikali, kuthibitisha uhalisia wa picha (za Rais na Chivayo) zilizotumika, na hivyo kuuaminisha Umma taarifa za upande mmoja. Aidha, TCRA imeeleza kuwa jukwaa la JamiiForums halikudhibiti maudhui yenye lugha ya matusi, kashfa na kejeli dhidi ya Rais wa Tanzania, na kuendelea kuhifadhi maudhui hayo ambayo bado yanapatikana kwa umma. TCRA imeongeza kuwa maudhui hayo yanakinzan...

Balozi Dkt Nchimbi Awasili Jimbo la Biharamulo Magharibi Kuomba Kura

 Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwasili katika uwanja wa mpira CCM Majengo,katika jimbo la Biharamulo Magharibi mkoa wa Kagera,ambapo baadae atawatubia Wananchi waliofika kumsikiliza leo Jumamosi Septemba 6,2025 akitokea mkoa wa Geita. Dkt Nchimbi anaendelea na mikutano yake ya kampeni nchi nzima, kusaka kura za ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Balozi Dkt.Nchimbi Awaomba Kura Wananchi wa Bwanga

 Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwasalimia na kuwahutubia Wananchi wa kata ya Bwanga,wilayani Geita leo Jumamosi Septemba 6,2025 akielekea mkoa wa Kagera. Dkt Nchimbi anaendelea na mikutano yake ya kampeni nchi nzima, kusaka kura za ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Nchimbi Ndani ya Katoro,Geita Hapatoshi

Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi  akiwahutubia Wananchi wa kata ya Katoro , leo Jumamosi Septemba 6,2025 Wilaya ya Geita, Mkoani Geita . Dkt Nchimbi anaendelea na mikutano yake ya kampeni mkoani Geita leo, kusaka kura za ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),akitokea mkoani Shinyanga. Maara baada ya kuwahutubia Wananchi wa jimbo la Katoro, Dkt Nchimbi  aliwanadi wagombea Ubunge,akiwemo Mgombea Ubunge wa Jimbo la Katoro,Mhandisi Kija Limbu Ntemi pamoja na Madiwani.