Skip to main content

Posts

Showing posts from October 20, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TRA Yawashauri Wananchi Umuhimu wa Kudai Risiti Wanaponunua Bidhaa

 Na Angela Sebastian-Bukoba MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA ) imewashauri wananchi kutambua umuhimu wa faida za kudai na kutoa risiti pindi wanaponunua na kuuza bidhaa kwani hiyo inasaidia na kuwalinda pale ikatokea changamoto hususani wizi,pia  inaongeza ulipaji kodi kwa ufanisi. Hayo yameelezwa na Afisa uhusiano mkuu kutoka TRA makao makuu Hudson Kamoga wakati akiongea na waandishi wa habari wa  mkoa wa Kagera katika mafunzo ya siku moja yaliyotolewa na mamlaka hiyo, kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutoa elimu juu ya kazi zinazofanywa na TRA hususani wajibu wa ulipaji kodi kwa ihari. "Wanaponunua na kudai risiti wanatimiza wajibu wako kisheria,ni uzalendo kwa nchi yao pia ni ulinzi wa bidhaa waliyoinunua mfano amenua simu bila risiti ikatokea kuna mtu mwingine aliibwa simu kama ya kwako huwezi kujitetea kwamba hiyo ni mali yako kwasababu, huna uthibitisho ambao ni risiti inayoonyesha uhalali wa umiliki wa mali hiyo"anasema Kamoga Amesema waandishi wa habari wanao wajib...

Gachagua atoka hospitalini na kushusha tuhuma nzito kwa Rais Ruto

  Rigathi Gachagua: 'Mheshimiwa Rais, Usiniue, usiue watoto wangu' Aliyekuwa Naibu Rais wa Kenya amedai kuwa, " Ruto hakuwa na nia ya kufanya kazi nami", alitaka tu kunitumia kupata watu kushinda uchaguzi", ameambia wanahabari.  amezungumza hayo akiwa anatoka katika Hospitali ya Karen alipokuwa anatibiwa. Rigathi Gachagua ameendelea kudai kuwa kuna baadhi ya watu ambao wamejaribu kumuua kwa kumuwekea sumu kwenye chakula mara mbili. "Kwa mara ya kwanza, niseme ilikuwa mnamo Agosti 30, huko Kisumu, walinzi wa siri waliingia chumbani kwangu Kisumu na kuingia kwa nguvu na mmoja wao akajaribu kunitilia sumu kwenye chakula changu, lakini tuligundua na tukaweza kuepuka mpango huo." Gachagua amesema. "Nilitakiwa kuuawa kwa kuwekewa sumu, na mnamo Septemba huko Nyeri, timu nyingine ilikuja na kujaribu kunitilia sumu kwenye chakula ambacho kilichokusudiwa kuwa changu na Baraza la Wazee wa Kikuyu." Rigathi Gachagua ameendelea kumshutumu Rais William Ruto...

Tawfiq Turky aangazia fursa za Utalii Comoro

Mwenyekiti wa Makampuni ya Vigor ya Zanzibar ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mpendae,Tawfiq Salim Turky amekutana na Waziri wa Utalii na Mazingira wa Comoro Abubakar ben Mahamoud na  kumueleza azma yake ya kuongeza uwekezaji katika sekta ya hoteli nchini humo. Mheshimiwa Turky ambaye tayari amewekeza Comoro katika sekta za Nishati na mifumo ya Fedha na awali alikuwa mwendeshaji wa hoteli kubwa zaidi nchini hapa yuko nchini Comoro kwa ziara ya kibiashara ambapo ameeleza azma yake ya kuongeza wigo wa uwekezaji wa makampuni yake ili wawe na hoteli kadhaa za hadhi ya juu nchini hapa.Mazungumzo yake na Waziri wa Utalii yalihudhuriwa pia na Balozi wa Tanzania nchini Comoro,Saidi Yakubu na Shaaban Battash,Mjumbe wa Baraza la Ulamaa,Zanzibar. Kwa upande wake,Mheshimiwa Waziri Mahamoud alimhakikishia Mheshimiwa Turky kuwa Comoro kwa sasa ina uhitaji mkubwa wa wawekezaji katika sekta hiyo na amefika wakati muafaka ambapo nchi hiyo inajiandaa kuwa mwenyeji wa mashindano ya michezo ya Baharin...

Madiwani wa vyama vya upinzani wajiunga na ccm mbele ya waziri mkuu

*Yumo pia Katibu Kata wa CUF MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa mwishoni mwa wikii hii, ameshuhudia madiwani wawili na Katibu Kata kutoka vyama vya CUF na ACT-Wazalendo wakirejea Chama cha Mapinduzi.  Akiwa kwenye kijiji cha Milola katika siku ya kwanza ya ziara yake, Mheshimiwa Majaliwa alishuhudia madiwani wa Kata za Milola na Rutamba wakitambulishwa na Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mama Salma Kikwete katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye senta ya Milola, Kata ya Milola, Manispaa ya Lindi. Viongozi waliorejea CCM ni Diwani wa Milola, Bw. Hussein Kimbyoko kutoka Chama cha Wananchi (CUF) na Diwani wa Rutambi, Bw. Athumani Mmaije kutoka Chama cha ACT – Wazalendo.  Akiwa katika siku ya pili ya ziara yake jimboni Ruangwa, Mheshimiwa Majaliwa alishuhudia wanachama wengine wawili wakikabidhi kadi zao kwa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Ruangwa, Mzee Ibrahim Issa Ndoro katika mkutano uliofanyika kwenye viwanja vya Wandorwa, wi...

Rais Mwinyi anzisheni kozi zitakazochangia maendeleo ya nchi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, amezishauri taasisi za elimu ya juu zilizo nchini kuanzisha kozi muhimu zenye uhitaji na uhaba wa wataalamu, ambazo zitachangia maendeleo ya nchi. Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa hatua hiyo itasaidia sekta ya afya kuwa na wataalamu wa kutosha katika kada mbalimbali, watakaotoa huduma kwa kuzingatia utaalamu na weledi, hivyo kuimarisha sekta ya afya. Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo kwenye mahafali ya 12 ya Zanzibar School of Health leo, tarehe 19 Oktoba 2024, katika viwanja vya Mao Tse Tung, Mkoa wa Mjini Magharibi.  Rais Dk. Mwinyi ametoa wito kwa wahitimu wa kada tofauti wazingatie nidhamu na maadili ya kazi katika utoaji wa huduma wanapoingia kwenye majukumu yao, na kuwa msaada muhimu kwa jamii. Aidha, amewasisitiza vijana kusoma kozi zenye umuhimu na uhitaji, hususan zinazoanzishwa na Zanzibar School of Health, huku akiipongeza juhudi zinazochukuliwa na chuo hicho kuanzisha kozi mpya. Halikadhalika ...