Skip to main content

Posts

Showing posts from August 20, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MRADI WA TANGAYETU ULIVYOWANUFAISHA VIJANA KIDIJITALI

 Na MASHAKA MHANDO, Tanga  MATUMIZI ya mitandao ya kijamii jijini Tanga yamechukua sura mpya ya kiuchumi, baada ya vijana zaidi ya 150 kunufaika na mradi maalum wa ujuzi wa kidijitali uliowatoa mitaani na kuwafanya kuwa watengeneza maudhui (Content Creators) wanaojitegemea na kujingizia kipato. Mradi huo umewasaidia vijana kuachana na dhana potofu kuwa mitandao ya kijamii haina faida, na badala yake wamepewa ujuzi wa kuandaa maudhui, kupiga picha, na kuhariri kazi zenye viwango vinavyokidhi masoko ya mtandaoni. Miongoni mwa shuhuda za kusisimua za mradi huu ni ya Peter Msuya, kijana ambaye awali alikuwa fundi stadi wa kutengeneza vitanda na makochi (Sofa). Peter anasema maisha yake yamebadilika kabisa baada ya kujiunga na mafunzo hayo ya kidijitali. "Nashukuru sana mafunzo niliyopata. Leo hii ukurasa wangu unafuatiliwa na watu milioni mbili! Kama siyo mradi wa 'Tanga Yetu', saa hii ningekuwa nagombana na wateja ambao sijawatengenezea vitanda vyao kwa wakati. Sasa naweza ku...

SERIKALI YATAKIWA KUTUMIA TEKLONOJIA ZA WABUNIFU WA NDANI

 Na MASHAKA MHANDO, Tanga SERIKALI imeshauriwa kuanza kuingia mikataba ya kununua na kuwekeza kwenye teknolojia na bidhaa zinazobuniwa na vyuo vya elimu ya juu nchini, badala ya kutegemea zaidi kuagiza bidhaa hizo kutoka nje ya nchi. Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Husna Sekiboko, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua mabanda mbalimbali katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu yanayofanyika mkoani Tanga. Mhe. Sekiboko amesema hatua ya Serikali kutumia bunifu za ndani itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza utegemezi wa kiteknolojia, kujenga uwezo wa wataalamu wa ndani, kuchochea ajira kwa vijana, na kukuza mapato ya Taifa kupitia bidhaa zenye nembo ya "Made in Tanzania". Akithibitisha uwezo wa vyuo vya ndani kufanya mapinduzi, Mhe. Sekiboko alisema amevutiwa sana na kiwango cha tafiti zinazofanywa, akitolea mfano ubunifu uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Chuo h...

RC CHALAMILA AAHIDI KUWACHUKULI HATUA WANAOIHUJUMU STENDI YA MAGUGULI

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ameahidi kuwachukulia hatua za kisheria wote wanao kwamisha ajenda ya serikali juu ya matumizi ya stendi ya magufuli huku akisema kuwa Rais Samia hajatuma viongozi kuua stendi hiyo. Hayo amebainisha leo Agosti 19, 2026, Mkuu wa mkoa huyo katika ziara yake katika wilaya ya Ubungo alipofika katika stendi ya mabasi Magufuli kwa lengo la kuzungumza na wafanyabiashara na madereva katika stendi ya hiyo ambapo amesema wapo badhi ya watumishi wa umma wamekuwa sehemu ya kuhujumu mradi huwo. Chalamila amesema serikali ipo katika uchunguzi wa biashara haramu ya matumizi na usafurushaji wa madawa ya kulevya kupitia stendi ya maguguli ili kuhakikisha shughuli halamu zinakomeshwa na kuweka mifumo mizuri ya usalama katika mkoa wa Dar es salaam. Adha Mkuu wa Mkoa ameitaka LATRA kufuta vibali vya magari vyote kwa anaekaidi kutumia stendi ya magufuli ili kuweka mifumo bora ya utii wa sheria na kuongeza mnyororo wa thamani ya biashara kupitia sekta ya...

PROF. NOMBO AIPONGEZA NACTVET KWA KURATIBU MASHINDANO YA UJUZI KITAIFA 2026

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, leo Agosti 20, 2026, ametembelea na kujionea shughuli za Mashindano ya Ujuzi Kitaifa 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu. Akizungumza baada ya kutembelea eneo la mashindano hayo, Prof. Nombo amesema Serikali inaendelea kutumia mbinu mbalimbali kuwawezesha vijana kupata ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira, ikiwemo kuwapa fursa ya kujifunza katika mazingira halisi ya kazi na viwandani, badala ya kutegemea mafunzo ya darasani pekee. Amesema Mashindano ya Ujuzi Kitaifa yanafanyika kwa kuzingatia vigezo na viwango vya kimataifa, hivyo kuwapa washiriki fursa ya kuonyesha umahiri wao kwa kutumia viwango vinavyotambulika kimataifa. Prof. Nombo amesema jambo lililomfurahisha zaidi katika maandalizi ya mashindano hayo ni ushirikiano uliopo kati ya taasisi za elimu na sekta ya viwanda, ambapo sehemu...

CHATANDA: USHIRIKIANO TANZANIA NA DRC KONGO UTATIRIRISHA FURSA LUKUKI ZA UCHUMI

 NA: MWANDISHI WETU Ushirikiano baina ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), umeelezwa kuwa na manufaa mengi yenye mchango wa kukuza maendeleo baina ya nchi hizo mbili.  Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu (MCC), Mary Chatanda, Agosti 18, 2026. Chatanda amesema, ziara ya siku mbili ya Rais Felix Tshisekedi wa DRC Kongo nchini Tanzania ni kielelezo cha uhusiano mzuri ambao hauishii kuwa urafiki wa kawaida bali nyenzo ya kushirikiana katika kukuza uchumi na maendeleo. "Rais Dk. Samia na mwenzake Tshisekedi wamekubaliana kushirikiana katika kuboresha sekta za uchukuzi, madini, nishati, uwekezaji, biashara, barabara, bandari, usafiri wa majini, jambo linaloongeza kasi ya ukuaji uchumi," amesema. Aidha, Chatanda amehimiza uzingatiaji wa maslahi ya wananchi katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wa nchi zote. "Wananchi wetu wanapas...

BUNIFU ZA KISHINDO TANGA: MUHAS YAGUNDUA DAWA YA TEZI DUME, CHUO CHA NELSON MANDELA CHAGEUZA KOROSHO KUWA KEMIKALI YA NGOZI

 Na MASHAKA MHANDO, Tanga Vyuo Vikuu nchini vimekuja na majibu ya vitendo dhidi ya changamoto za kiafya na kiuchumi zinazoikabili jamii, baada ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kugundua dawa ya kinga na tiba ya ugonjwa wa tezi dume, huku Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) ikibuni kemikali ya kusindika ngozi inayotokana na maganda ya korosho. Bunifu hizi za kihistoria zimebainishwa jijini Tanga wakati wa Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea jijini humo kwenye viwanja vya shule ya sekondari ya Usagara. Akielezea ugunduzi huo wa kimatibabu, Daktari kutoka MUHAS, Dkt. Benson Peter, amesema chuo hicho kimefanya tafiti za kina tangu mwaka 2006 na kugundua mmea wenye kemikali zinazoweza kutibu tezi dume, mgonjwa akapona kabisa. Matokeo ya utafiti huo yamezaa dawa iliyopewa jina la Brucan, ambayo tayari imetengenezwa katika mfumo wa vidonge na kuanza kutumika kwa wagonjwa na hata wasiokuwa wagonjwa kwa a...

PROF. KABUDI AWATAKA WANANCHI KUZINGATIA TAHADHARI ZA MAAFA

 Na, Mwandishi wetu – Dar es Salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu–Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Prof. Palamagamba Kabudi, amewataka wananchi kuzingatia tahadhari na maelekezo yanayotolewa na wataalamu na mamlaka husika ili kupunguza madhara yanayotokana na majanga na maafa. Prof. Kabudi ametoa wito huo tarehe 19 Agosti, 2026 wakati akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Watoa Huduma za Misaada ya Kibinadamu Duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. “Ushiriki wa wananchi ni muhimu katika kuimarisha ustahimilivu wa jamii dhidi ya majanga, huku akiwataka kuendelea kufuata taarifa na maelekezo rasmi kutoka kwa wataalamu na mamlaka zinazohusika na masuala ya maafa.” Katika hatua nyingine, alisema Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari za mapema na kujenga ustahimilivu wa jamii ili kuongeza uwezo wa wananchi kukabiliana na majanga na kupunguza madhara yanayotokana na matukio hayo. Alisema uwezo wa nchi katika kukabiliana na majanga kwa ufanisi unategemea ...

WASIRA ATAKA WANA CCM WAKUTANE, WASIINGIE MKENGE KWA MANENO YA MITANDAONI.

 _Na Mwandishi Wetu - Singida_ Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Stephen Wasira, amewataka wanachama wa CCM kukutana mara kwa mara katika vikao rasmi vya chama ili kujadili masuala muhimu na kuepuka kupotoswa na taarifa zisizo na ukweli zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii. Akizungumza leo tarehe 19 Agosti, 2026 Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wakati wa kuanza ziara rasmi ya kikazi ya kukagua uhai wa chama, Wasira amesema vikao hivyo vinawapa wanachama fursa ya kupata taarifa sahihi na kuambizana ukweli. "Wanachama wetu nchi nzima, kwa mujibu wa Katiba mna vikao vya wanachama. Mkutane muambizane. Siku hizi kwenye mitandao kuna uongo mwingi sana. Usipoangalia unaweza hata wewe kushirikishwa kusema uongo," amesema. Amesisitiza kuwa ni muhimu wanachama kukutana na kujadili madai yanayosambaa, kisha kumtafuta mtu mwenye ujuzi awasaidie kuyafafanua. "Kwa hiyo ni vizuri kukutana mkasema hili jambo limesemwa sana, maana yake ni nini? Mkamwita mtu a...