Arusha Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Victor Seff ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji Tanzania kwa Awamu ya Pili (TACTIC) jijini Arusha kutabadilisha muonekano na mandhari ya jiji hilo kuendana na hadhi yake ya mkoa wa kitalii, kuongeza fursa za ajira, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha hali ya biashara na hivyo pia kuchangia maendeleo ya kijamii. Mhandisi Seff amebainisha hayo hivi karibuni jijini Arusha wakati wa utiaji saini wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo utakaohusisha ujenzi wa kituo kikuu cha Mabasi Bondeni city, Ujenzi soko kuu la Kilombero, Ujenzi soko la Morombo pamoja na uboreshaji wa bustani ya mapumziko ya Themi Living Garden, miradi itakayotekelezwa na mkandaradi M/s Mohammed Builders Limited kwa gharama ya 30,625,112,436.85 bila ya VAT. Kulingana na Mhandisi Seff kukamilika kwa Kituo kikuu cha Mabasi Jiji la Arusha kutawezesha uwepo wa vibanda vya wafanyabiashara 900 kutoka 250 v...
Marato tv - Sauti ya Jamii