Na,Saleh Lujuo-Dodoma KATIBU wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenan Kihongosi, amemshukia Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Bara), John Heche, akimtaka kuacha kutoa kauli za uchumi zisizo na takwimu. Akizungumza na waandishi wa habari leo April 7,2026 jijini Dodoma, Kihongosi amesema kuwa mjadala wa uchumi, hususani suala la mafuta, hauhitaji siasa za majukwaani bali unahitaji uhalisia unaoongozwa na Takwimu na uelewa wa kina. Kwa msisitizo, Kihongosi Amesema kuwa kauli zisizo na uthibitisho zinaweza kupotosha umma na kuongeza hofu kwa wananchi, hasa katika kipindi ambacho gharama za maisha na bei ya mafuta vinajadiliwa kwa uzito mkubwa nchini. “Uchumi haujadiliwi kwa hisia au siasa nyepesi. Ni eneo linalohitaji takwimu, uchambuzi na uelewa wa kina kabla ya kuzungumza,” amesisitiza. Kadhalika, Ameongeza kuwa ni vyema kwa viongozi kutumia muda kujifunza na kufahamu hali halisi ya mambo kabla ya kujitokeza hadharani kutoa matamko yanayoweza kupotosh...