Skip to main content

Posts

Showing posts from September 7, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MFANYAKAZI WA PREMER CASINO MWANZA AILILIA SERIKALI

  MFANYAKAZI WA PREMER CASKNO MWANZA AILILIA SERIKALI. Na Mwandishi Wetu, Mwanza MFANYAKAZI wa Premer Casino ya Mwanza katika Idara ya Ulinzi Bw Nassor Butondo amelalamikia kitendo cha kushambuliwa na wachina Agosti ak 30, mwaka huu, majira ya usiku wakati anatekeleza majukumu yake ya ulinzi, Jambo Digital imeelezwa. Aidha Butondo ameulalamikia uongozi wa Casino hiyo iliyoko katika Jengo la Rock City Mall Wilayani Ilemela kwa kushindwa kumhudumia kimatibabu mlinzi wao huku wakitumia fedha nyingi kuwatibisha wachina walioanzisha fujo ndani ya Casino. "Mwajili wangu anawathamini zaidi wachina kuliko mimi, ndio maana pengine ni kwasababu ndio wateja wa kamali, hivyo matusi yao ya nguoni inabidi wafanyakazi wayavumilie tu, wakati mwingine huwadhalilisha wafanyakazi wa kike kwa kuwaingizia vidole sehemu ambazo sio rasmi, Serikali itusaidie" alifafanua Butondo. Imedaiwa kuwa siku hiyo kulitokea kutoelewana kati ya mchina na mzungu baada ya mchina (jina tunalo) kuliwa kwenye ...

Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Msalato Dodoma Wafikia Asilimia 72

Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato uliopo jijini Dodoma umefikia hatua ya asilimia 72 katika ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege, wakati jengo la abiria likiwa limekamilika kwa asilimia 39.

SERIKALI KUJENGA SKIMU YA UMWAGILIAJI WILAYANI IRAMBA

  Tume ya Taifa ya Umwagiliaji(NIRC) imewaelekeza wataalam wake kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kupata mahali pa kujenga skimu ya Umwagiliaji katika bonde la Ulemo-Nzinziligi-Mbelekese lililopo wilayani Iramba Mkoani Singida. Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Raymond Mndolwa ametoa maelekezo hayo wilayani Iramba wakati akimuonesha Waziri wa Fedha Dokta.Mwigulu Nchemba ramani ya Jiografia ya Bonde hilo. Kwa mujibu wa Mndolwa,Baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu,Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji katika bonde hilo utakaohusisha Bwawa,uchimbaji wa visima pamoja na Miundombinu ya umwagiliaji. Bonde la Ulemo-Nzinziligi-Mbelekese lina ukubwa wa hekta 43,000 ambapo Ujenzi wa skimu ya Umwagiliaji unatarajia kunufaisha wakulima katika kata sita za Ulemo,Ndago,Mbelekese,Mukulu, Kaselya pamoja na Kiengege.

DKT.BITEKO ASHIRIKI DUA YA MZEE MAJID NSEKELA

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameiasa jamii kuwa na utaratibu wa kuwatunza na kuwajali wazazi wao na kuendelea kuwaombea ambao hawapo hai. “ Tuendelee kuwakumbuka na kuwaombea ndugu na wazazi waliotangulia mbele za haki ni jambo zuri na wajibu wetu tuliobaki, Sheikh wetu katika mawaidha yake ameliongelea kwa uzuri sana. Tulitilie maanani na sote tuendelelee kufanya hivi, na kama huwa hatuwafanyii hivi ndugu zetu, hatuna budi tuanze kwa moyo wote.” Amesema Dkt. Biteko. Dkt. Biteko ameyasema hayo leo Septenba 7, 2024 akiwa Nyakatuntu, Kyerwa mkoani Kagera wakati aliposhiriki katika dua ya kuwaombea baba mzazi na ndugu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Bw. Abdulmajid Mussa Nsekela Ameongeza “Ndugu zangu tusisahau mapito yetu. Katika mapito huwa kuna watu. Katika watu hawa, kuna wazazi wetu. Kama wazazi wako wapo hai, mmoja au wote au wale waliokulea, jua nawe una wajibu wa kuwalea na kuwatunza, siyo kifedha tu bali pia kwa mahusiano mema hasa ya ki...

USHIRIKISHWAJI WA TAWA MAONESHO YA UWINDAJI WA KITALII ABU DHABI KUZAA MATUNDA

Maonesho ya Kimataifa ya Uwindaji wa Kitalii yanayojulikana kwa Jina la "Abu Dhabi International Hunting and Equestrian Exhibition - ADIHEX 2024" yamezaa matunda kufuatia idadi kubwa ya wawekezaji waliohudhuria katika maonesho hayo yaliyoanza tarehe 31 Agosti hadi 08 Septemba, 2024 kuonesha nia ya kuwekeza nchini. Miongoni mwa mafanikio ya maonesho hayo ni mazungumzo mahsusi yaliyofanywa baina ya Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA Mabula Misungwi Nyanda na wawekezaji walioonesha nia ya kuwekeza kwenye biashara ya uwindaji wa kitalii, ujenzi wa hoteli za kulala watalii ndani ya Hifadhi na uwekezaji mahiri (Special Wildlife Investment Concession Areas - SWICA) mazungumzo yaliyoongozwa na Kaimu Balozi wa Tanzania katika nchi za umoja wa falme za kiarabu Bw. Hangi L. Mgaka Bw. Hangi Mgaka ameipongeza TAWA kwa ushiriki wake kwenye maonesho hayo ambayo kwasasa ni mara ya tatu tangu Taasisi hiyo ianze kushiriki mwaka 2022, maonesho yanayotaj...

Rais Dkt Mwinyi: Tanzania na Msumbiji Zitaendelea Kudumisha Undugu Wake

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Tanzania ilitoa mchango mkubwa katika harakati za kupatikana kwa Uhuru wa Msumbiji, ikizingatiwa kwamba Chama cha Frelimo kilianzishwa Dar es Salaam mnamo mwaka 1962 chini ya uongozi wa Hayati Eduardo Chivambo Mondlane. Aidha, Tanzania ilitoa mchango mkubwa kwa kuwafundisha wapiganaji wa chama hicho sambamba na kutoa askari wake kusaidia mapambano dhidi ya Wareno. Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo katika Sherehe za Miaka 50 ya Siku ya Ushindi zilizofanyika katika kiwanja cha Matola, Msumbiji. Vile vile, Rais Dk. Mwinyi amesema siku ya maadhimisho hayo yana umuhimu mkubwa kwetu sote kwa kutambua mchango wa Tanzania katika kusaidia kupata uhuru pamoja na kuwa sehemu ya historia hiyo. Dk. Mwinyi ameeleza kuwa Tanzania na Msumbiji zitaendelea kuimarisha uhusiano wake kwa sababu nchi hizo mbili zinashirikiana katika nyanja nyingi zikiwemo za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kitamaduni, na udugu ul...

MIUNDOMBINU YA TAASISI YA TAALUMA YA WANYAMAPORI PASIANSI KUIMARISHWA

Serikali inakusudia kuboresha miundombinu ya Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi iliyoko wilayani Ilemela Mkoani Mwanza ili kuboresha mazingira ya kujifunza na kufundishia Naibu waziri wa Maliasili na Utalii DUSTAN KITANDULA amesema kuwa katika mwaka huu wa fedha,Serikali imetenga shilingi millioni Mia tano kwa ajili ya kuanza maboresho hayo ikiwemo kuanza ujenzi wa miundombinu mipya ya utoaji wa elimu.  KITANDULA amebainisha hayo wakati wa Mahafali ya 59 ya Taasisi hiyo baada ya kuelezwa kuhusu changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba pamoja na uchakavu wa baadhi ya miundombinu ikiwemo Mabweni,Madarasa na nyumba za watumishi.  Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi pia inakabiliwa na uhaba wa vifaa vya kisasa vya mafunzo ikiwemo GPS, Darubini,Radio calls na Silaha pamoja na uhaba wa magari ya kisasa Kwa ajili ya Mafunzo yakiwemo ya Waongoza Watalii. Mkuu wa Taasisi hiyo Jeremiah Msigwa amesema kuwa changamoto hizo zinachangia katika kupunguza ufanisi wa utoaji wa elimu ...

Matumizi ya Teknolojia Mbadala Yatapunguza Gharama za Ujenzi- Mhandisi Mativila

Matumizi ya Teknolojia mbadala na malighafi zinazopatikana maeneo ya kazi kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja imeweza kupunguza gharama zaidi ya asilimia 70. Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila alipotembelea banda la TARURA kwenye Maadhimisho ya 21 ya Siku ya Wahandisi katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.  "Ujenzi wa madaraja na barabara kwa kutumia teknolojia ya mawe unapunguza gharama kwa asilimia 70 ukilinganisha na zege lakini pia tuna teknolojia ya kutumia kemikali kuboresha udongo unaopatikana maeneo ya kazi ili kupata ufanisi wa gharama za ujenzi", amesema. Ameongeza kwamba TARURA imeweza kuondoa vikwazo sehemu zisizopitika kwa kujenga madaraja ya gharama nafuu kwa kutumia teknolojia mbadala hasa maeneo ya vijijini na kuwezesha wananchi kuzifikia huduma za kijamii na kiuchumi kwa urahisi zaidi. "Kwa bajeti ya shilingi bil. 1 unayoweza kujenga daraja 1 unajenga ma...