Skip to main content

Posts

Showing posts from November 30, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mbunge Rwakatare awaasa wazazi malezi ya watoto

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Mlimba (CCM), Dk Kellen-Rose Rwakatare amewahimiza wazazi kushirikiana na walimu katika malezi ya watoto wao badala ya kuona jukumu hilo kama ni la walimu. Alitoa ushauri huo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa tamasha la kitaaluma na michezo  kwa wanafunzi wa shule ya St Mary’s Tabata . Dk Rwakatare ambaye pia ni Mkurugenzi wa shule za St Mary’s alisema kama wazazi wanatona umuhimu wa kuzingatia malezi bora kwa watoto wao, basi kwa kushirikiana na walimu watapata taifa lenye nidhamu kubwa. “Tusione kuwa tunapolipa ada tunakuwa tumemaliza, mwalimu anasehemu yake ya malezi lakini mzazi anasehemu kubwa kwasababu muda mwingi anakuwa na mtoto nyumbani,” alisema Kwenye tamasha hilo, wanafunzi walionyesha umahiri wa  vipaji mbalimbali kuanzia vipaji vya taaluma na vipaji vya michezo ya aina mbalimbali ambapo baadhi ya wanafunzi hao walimudu kuimba nyimbo mbalimbali kwa lugha ya kichina. Dk Rwakatare alisema kila mwaka wamekuwa wakiandaa matam...

Rais Samia: Polisi Waache Kumtafuta Dkt. Gwajima

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askofu Dkt. Josephat Gwajima kama walivyokuwa wametangaza awali ili aweze kuendelea shughuli zake. Amesema baada ya kutoa msamaha kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, waumini wanahitaji wamuone kiongozi wao, hivyo anatakiwa ajitokeze hadharani aendelee na kazi yake. “Mwacheni ajitokekeze tujenge umoja wa kitaifa, tushikamane kurudisha umoja wa kitaifa. Tumekutana na TEC, viongozi wa dini, wa mila na viongozi mbalimbali; twendeni sote kwenye jambo hili, tujitokeze tuhamasishe Tanzania yenye amani, huu ndio wito wa kiongozi wetu wa nchi” Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Novemba 30, 2025) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Arumeru katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Magufuli Leganga, kata ya Usa River, wilayani Arumeru mkoani Arusha. Waziri Mkuu amewataka Watanzania wakatae kushawishiwa na wanaharakati wanaochochea vurugu kwani zinarudisha nyuma ma...

Waziri Mkuu akagua uharibifu wa Mahakama ya Mwanzo maji ya chai

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Novemba 30, 2025, amekagua Mahakama ya Mwanzo iliyopo Maji ya Chai ambayo iliharibiwa na vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025, mkoani Arusha. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yupo Arusha kwa ziara ya kukagua mkoa uliojitokeza mjadala wa Oktoba 29, 2025. Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Amosi Makalla.

Waziri Mkuu akagua uharibifu Kituo cha Mafuta cha Total

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Novemba 30, 2025, amekagua Kituo cha Mafuta cha Total kilichopo Maji ya Chai ambacho kiliharibiwa kutokana na vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025, mkoani Arusha. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yupo mkoani Arusha kwa ziara ya kukagua uharibifu uliojitokeza kufuatia vurugu za Oktoba 29, 2025. Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Amosi Makalla.