Skip to main content

Posts

Showing posts from April 3, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mwakitinya kuzindua Aweso Vijana Cup Aprili 4

Na: Mwandishi Wetu, Pangani Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Bara, Mussa Mwakitinya, anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi wa mashindano ya mpira wa miguu wilayani Pangani yaliyopewa jina la Aweso Vijana Cup Aprili 4, 2026, katika uwanja wa mpira, Kata ya Mwera.  Mashindano hayo yamelenga kuongeza fursa ya ajira kwa vijana kupitia michezo, kuepuka magonjwa yasiyoambukiza, kujenga mahusiano na afya bora, huku Mbunge wa Jimbo la Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, akiyafadhili mashindano hayo yaliyoandaliwa na Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM wilaya ya Pangani. Pambano la uzinduzi litahusisha timu kutoka Kata za Mwera na Tungamaa. Akizungumza ofisini kwake Aprili 3, 2026, Katibu wa UVCCM wilaya ya Pangani, Nasri Mkalipa, amesema vijana wajiandae kikamilifu kushiriki mashindano hayo muhimu.  "Mbunge wetu Jumaa Aweso anawajali na kuwapenda vijana ndiyo maana amefadhili mashindano haya kwani siku hizi michezo sio burudani pekee lakini ni ajira pia, hivyo...

Upatikanaji wa Dawa Waimarika Nchini OWM-Tamisemi

OWM-TAMISEMI Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (OWM– TAMISEMI) anayeshughulikia masuala ya Afya, Mhe. Dkt. Jafari Seif, amesema kuwa hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya katika ngazi ya huduma za afya ya msingi nchini imeendelea kuimarika na kufikia kiwango cha kuridhisha ikilinganishwa na miaka iliyopita. Akizungumza Aprili 2, 2026 jijini Dar es Salaam, katika kikao kazi kilichoongozwa na Waziri wa Afya, Mhe.Mohamed Mchengerwa, pamoja na wadau wa sekta ya afya, katika ofisi za Bohari ya Dawa (MSD), Mhe. Dkt. Seif amesema kuwa tathmini ya mwaka 2026 inaonesha hali ya upatikanaji wa dawa imefikia asilimia 89 katika hospitali, asilimia 88 katika vituo vya afya, na asilimia 88 katika zahanati. Ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2024/25, vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi vilikusanya takribani Shilingi Bilioni 108, huku makusanyo hayo yakitarajiwa kuongezeka hadi kufikia Shilingi Bilioni 192 katika mwaka 2025/26.    Kwa u...

Uongozi ni Kusikiliza: Somo Kutoka Kwa Dkt. Mwigulu Nchemba

Katika siasa na utumishi wa umma, nguvu ya kiongozi mara nyingi hupimwa kwa uwezo wa kuzungumza na kuamua. Hata hivyo, kipimo cha juu zaidi ni uwezo wa kusikiliza ambacho mara nyingi hupuuzwa. Katika mazingira ya maombolezo, Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, anaonekana akitenga muda kumsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila. Hiki si kitendo cha kawaida, bali ni ishara ya uongozi uliokomaa unaotambua kuwa hekima haiko tu kwenye kutoa maagizo, bali pia kupokea mawazo ya wengine. Unyenyekevu wake kuinama, kutulia, na kuelekeza umakini kwa anayezungumza unaonyesha nidhamu ya kiakili na heshima. Hii inathibitisha kuwa kusikiliza si udhaifu, bali ni uwezo unaojenga imani, huleta uelewa sahihi, na kuimarisha mshikamano. Somo hapa ni wazi: uongozi si nani anaongea zaidi, bali nani anaelewa zaidi. Na uelewa huanza kwa kusikiliza. Kwa kifupi, Dkt. Nchemba hafundishi kwa maneno, bali kwa vitendo uongozi bora huanzia kwenye unyenyekevu wa kusikiliza wengine.

Taifa Gas Yatoa Ahadi: Bei ya Gesi Haitapanda Licha ya Soko la Dunia Kupaa

KATIKA kipindi ambacho bei ya gesi ya kupikia duniani imepanda kwa kasi ya hadi asilimia 43, kampuni ya Taifa Gas imekuja na habari njema kwa Watanzania—hakutakuwa na ongezeko la bei ya gesi ya majumbani (LPG). Hatua hii imepokelewa kama faraja kubwa kwa maelfu ya familia na wafanyabiashara wadogo wanaotegemea gesi katika shughuli zao za kila siku. Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 3, 2026, Meneja Mkuu wa Taifa Gas, Devis Deogratius, amesema kuwa soko la kimataifa limekumbwa na mabadiliko makubwa ya bei, hali iliyosababisha kuongezeka kwa gharama za ununuzi na usambazaji. Amesema licha ya changamoto hizo, kampuni imechukua uamuzi wa kipekee wa kubeba gharama hizo ili kulinda wateja wake. “Tunayo dhamira ya dhati ya kuwasaidia wateja wetu kwa kubeba athari za ongezeko la gharama ya nishati ya kupikia,” amesema Deogratius. Aidha, Amesema Usambazaji Waendelea Kuimarishwa Mbali na kudhibiti bei, Taifa Gas pia imehakikisha kuwa upatikanaji wa gesi hautatetereka. "Kupitia mtanda...