Na Shomari Binda-Musoma MBUNGE wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo na Meya wa manispaa ya Musoma Patrick Gumbo wameahidi kuzitafutia ufumbuzi kero mbalimbali za wananchi. Viongozi hao wameyasema hayo wakati wakijibu kero mbalimbali za wananchi walizozitoa leo agosti 14 kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Makoko ambapo wamesema kero za wananchi zinapaswa kutatuliwa na viongozi. Katika mkutano huo, wananchi wametoa kero mbalimbali ikiwemo migogoro ya viwanja na mikopo ya asilimia 10 itolewayo na halmashauri ya manispaa. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Amina Said, amesema kero yake ni kiwanja chake kuingiliwa na kukosa njia ya kupitia Akijibu kero hiyo pamoja nyingine Meya wa manispaa ya Musoma Patrick Gumbo amesema hakuna kero ambayo haita shughulikiwa kwa kuwa ndio kazi ya viongozi. Gumbo ambaye pia ni diwani wa Kata ya Makoko amesema kero nyingi zimetatuliwa na miradi mingi ya maendeleo imepelekwa kwenye Kata ya Makoko. Mbunge wa jimbo la Musoma mjin...
Marato tv - Sauti ya Jamii