Skip to main content

Posts

Showing posts from August 23, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

JESHI LA POLISI LAANIKA WATEKAJI...

KISHINDO CHA MJUMBE WA KAMATI KUU CHANG'OA 24 RUANGWA

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa ameshuhudia wanachama 24 wa vyama vya CUF na ACT-Wazalendo wakirejea CCM ndani ya siku mbili. Mheshimiwa Majaliwa alishuhudia wanachama hao wakikabidhi kadi zao kwa Katibu wa CCM wa Wilaya ya Ruangwa, Bw. Abbas Mkwenda (Agosti 23 na 24, 2024) wakati akizungumza na wakazi wa vijiji vya Mtondo (Kata ya Nambilanje) na Namikulo (Kata ya Chunyu), wilayani Ruangwa, Lindi ambako alifanya ziara ya jimboni kwake. Katika kijiji cha Mtondo, wanachama tisa wa CUF walirejesha kadi zao wakiongozwa na Mzee Bakari Abdallah Nanyambo ambaye alikuwa Mwenyekiti wa CUF Kata ya Nambilanje. Wengine ni Abdallah Ally Manjawila, Bakari Ally Nyanga, Bakari Abdallah Nampota, Mwanahawa Abdallah Komaje, Zaituni Omary Mitachi, Mwanahawa Rashid Chomwingo, Somoe Omary Mkupete na Amina Musa Pachela. Katika kijiji cha Namikulo, wanachama watano wa ACT-Wazalendo walikabidhi kadi zao wakiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT Kata ya C...

KISHINDO CHA JWTZ MBELE YA RAIS SAMIA

Amri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Dr Samia Suluhu Hassan,amesema anaridhishwa na utendaji wa jeshi la ulinzi wa wananchi (JWTZ) na kusema Serikali itatumia kila uwezo wake katika kuimarisha jeshi hilo. Rais Samia ametoa kauli hiyo katika viwanja vya mazoezi ya kijeshi Msata mkoani Pwani,wakati akizungumza na maafisa na wapiganaji wa jeshi hilo wakati wa kufunga zoezi la Medani la miaka 60 ya JWTZ.   Huku akionesha furaha yake baada ya kujionea zoezi hilo la utayari ambalo limefanywa na askari wa JWTZ katika viwanja hivyo vya mapambano,Rais Samia amesema jeshi hilo limeonesha kuwa na uwezo mkubwa hata kuwa mwalimu kwa wengine. Amesema Serikali itaunga mkono juhudi hizo kubwa za ulinzi wa mipaka yete zinazofanywa na JWTZ kwa kuendelea kuliwezesha kwa kukarabati miundo mbinu na kununua zana za kisasa zinazoenda na wakati ili kurahisha utendaji wa kazi. Rais Samia amesema hivi sasa mipaka ya nchi yetu ipo salama na kwamba wakati huu...