Skip to main content

Posts

Showing posts from June 7, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

JUMATATU JUNI 8,2026 KUAMUA HATMA YA RIGATHI GACHAGUA KISIASA

NAIROBI, Kenya.  Mustakabali wa kisiasa wa Naibu Rais wa zamani wa Kenya,Rigathi Gachagua umeendelea kugubikwa na sintofahamu huku macho ya Wakenya yakielekezwa mahakamani kusubiri hukumu muhimu inayotarajiwa kutolewa Jumatatu kuhusu uhalali wa mchakato uliomwondoa madarakani. Uamuzi huo unatarajiwa kuwa wa kihistoria kwa kiongozi huyo ambaye kwa miaka ya hivi karibuni amekuwa mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi mkubwa nchini Kenya, hasa katika eneo la Mlima Kenya ambalo lina uzito mkubwa wa kisiasa. Gachagua aliingia madarakani mwaka 2022 akiwa Naibu Rais chini ya utawala wa Rais . Hata hivyo, baada ya kipindi cha mvutano wa kisiasa ndani ya serikali, alikumbwa na mchakato wa impeachment uliopitishwa na Bunge la Taifa mwezi Oktoba 2024 na baadaye kuridhiwa na Seneti, hatua iliyomwondoa rasmi katika nafasi hiyo. Tangu kuondolewa madarakani, Gachagua ameendelea kuwa sauti muhimu katika siasa za Kenya, akifanya mikutano ya kisiasa na kukosoa baadhi ya sera za serikali huku akijijenga ...

WANANCHI WAELIMISHWE KUANDIKISHANA MIKATABA YA ARDHI - DKT. MWIGULU

*Asema uaminifu unazidi kupungua WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka viongozi nchini wawaelimishe wananchi umuhimu wa kuandikishana mikataba wanapopeana ardhi badala ya kuendelea kufanya hivyo kwa kuaminiana. "Viongozi mliopo hapa waambieni wananchi hivi sasa masuala ya ardhi wasifanye kwa kuaminiana, wawe wanaandikishana kwa mikataba na tena katika ofisi za kijiji ili watambulike," amesema.  Ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 7, 2026) wakati akizungumza na viongozi wa kada mbalimbali wa mkoa wa Iringa katika kikao cha majumuisho ya ziara zake kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, mjini Iringa.  "Ninawasihi wananchi tusiogope kurasmisha mambo yetu kwa sababu uaminifu unaenda unapungua. Tunaporasmisha, tunaepusha migogoro siku za usoni," amesisitiza.  Waziri Mkuu ametoa rai hiyo kutokana na wingi wa kero zinazojitokeza kwenye mikutano aliyoishaifanya na hasa kwenye sekta ya ardhi.  Amewataka viongozi wanapotaka kufanya uendele...

DKT. MWIGULU AMALIZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI IRINGA, ASISITIZA HAKI NA UWAJIBIKAJI

 WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amehitimisha ziara yake ya kikazi mkoani Iringa kwa kuwataka viongozi na watumishi wa umma kuendelea kusimamia haki, uwajibikaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi pamoja na kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yote yaliyotolewa katika kutatua kero za wananchi. Ametoa maelekezo hayo leo Jumapili (Juni 7, 2026) wakati akifunga ziara yake ya kikazi mkoani Iringa kwa kufanya kikao cha majumuisho na viongozi pamoja na watumishi wa umma kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Dkt. Mwigulu amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika sekta mbalimbali za maendeleo hivyo ni wajibu wa viongozi na watumishi kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na haki zao zinalindwa. Amesema ameridhishwa na namna Mkoa wa Iringa ulivyoshughulikia changamoto mbalimbali za wananchi na kuwataka viongozi kuendelea kuwa mbele ya matukio kwa kusikiliza na kutatua kero kabla hazijafikia ...

ZIARA YA RAIS SAMIA URUSI YAFUNGUA FURSA MPYA ZA USHIRIKIANO KATIKA MAENEO TISA YA KIMKAKATI - PROF. MKUMBO

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, amesema ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, nchini Urusi imefanikiwa kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo kati ya Tanzania na Urusi katika maeneo tisa ya kimkakati yanayotarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi wa pande zote. Akizungumza na waandishi wa habari Juni 7, 2026 jijini Dar es Salaam, Prof. Mkumbo alieleza kuwa Tanzania na Urusi zimeendelea kudumisha uhusiano wa kirafiki wa muda mrefu, huku ziara ya Rais Samia ikifungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika sekta mbalimbali muhimu. Profesa Kitila alitaja maeneo ya ushirikiano kuwa ni pamoja na kilimo, elimu na mafunzo, nishati, madini, viwanda, usafiri, utalii, uchumi wa kidijitali, biashara na uwekezaji na kuongeza kuwa hatua za utekelezaji wa ushirikiano huo zimeanza kuzaa matunda, ambapo makubaliano kadhaa yalifikiwa kati ya taasisi za Tanzania na Urusi kwa lengo la kuimarisha mah...

UWEKEZAJI WA URUSI WAFUNGUA FURSA MPYA ZA UKUAJI WA UCHUMI TANZANIA- BALOZI ULANGA

 Serikali ya Tanzania imeendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi kwa mafanikio makubwa baada ya kuvutia wawekezaji kutoka Urusi katika sekta mbalimbali za kimkakati, hatua inayotarajiwa kuongeza ukuaji wa uchumi, ajira na maendeleo ya viwanda nchini. Mafanikio hayo yamepatikana kufuatia ziara ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi iliyofanyika kuanzia Juni 3 hadi 6, 2026. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari uliolenga kueleza mafanikio ya ziara hiyo, Mkurugenzi wa Biashara ya Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi John Ulanga, amesema Tanzania imepokea mwitikio mkubwa kutoka kwa wawekezaji wa Urusi walioonesha nia ya kuwekeza katika sekta mbalimbali muhimu za maendeleo ya taifa. Balozi Ulanga amesema wawekezaji hao wamevutiwa na fursa zilizopo nchini katika sekta za madini ya kimkakati, nishati, afya na dawa, kilimo pamoja na teknolojia ya kidijitali. Ameeleza kuwa maeneo ha...

MBUNGE MWAKIOJA AINGILIA TATIZO LA VIJANA KUKOSA NIDA

 Na Mwandishi Wetu, Mkinga MBUNGE wa Jimbo la Mkinga, mkoani Tanga, Twaha Mwakioja ameingilia kati tatizo la vijana wengi wanaoishi maeneo ya mpakani wilayani humo kukabiliwa na changamoto ya kukosa mikopo kutokana na kucheleweshewa namba za NIDA. Hali hiyo ilibainishwa na Mjumbe wa Bodaboda, Ali Selemani Rasi, wakati wa kikao maalum kati ya Mbunge wa Jimbo la Mkinga, Mhe. Twaha Mwakioja, na waendesha pikipiki wa kijiwe cha Duga Maforoni kilichofanyika leo Juni 7, 2026. Rasi alisema vijana wa Duga Maforoni wanakosa fursa za kupata mikopo inayotolewa na Serikali ya asilimia 10 kutoka kwenye mapato ya ndani ya halmashauri kwa kuwa hawana vitambulisho hivyo vya taifa. "Mheshimiwa Mbunge, sisi vijana tunaoishi mipakani tuna tatizo kubwa la kukosa namba za NIDA ambazo zinatufanya tushindwe kupata mikopo ya vijana," alisema Rasi na kumuomba Mbunge awasaidie ili waweze kupata mikopo hiyo kama wenzao wengine nchini. Akijibu malalamiko hayo, Mbunge Mwakioja alitoa agizo la kimkakati a...