NAIROBI, Kenya. Mustakabali wa kisiasa wa Naibu Rais wa zamani wa Kenya,Rigathi Gachagua umeendelea kugubikwa na sintofahamu huku macho ya Wakenya yakielekezwa mahakamani kusubiri hukumu muhimu inayotarajiwa kutolewa Jumatatu kuhusu uhalali wa mchakato uliomwondoa madarakani. Uamuzi huo unatarajiwa kuwa wa kihistoria kwa kiongozi huyo ambaye kwa miaka ya hivi karibuni amekuwa mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi mkubwa nchini Kenya, hasa katika eneo la Mlima Kenya ambalo lina uzito mkubwa wa kisiasa. Gachagua aliingia madarakani mwaka 2022 akiwa Naibu Rais chini ya utawala wa Rais . Hata hivyo, baada ya kipindi cha mvutano wa kisiasa ndani ya serikali, alikumbwa na mchakato wa impeachment uliopitishwa na Bunge la Taifa mwezi Oktoba 2024 na baadaye kuridhiwa na Seneti, hatua iliyomwondoa rasmi katika nafasi hiyo. Tangu kuondolewa madarakani, Gachagua ameendelea kuwa sauti muhimu katika siasa za Kenya, akifanya mikutano ya kisiasa na kukosoa baadhi ya sera za serikali huku akijijenga ...
Marato tv - Sauti ya Jamii