NA MASHAKA MHANDO, Tanga TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga, imefichua kukwama kwa miaka miwili kwa mradi wa madarasa na vyoo katika Shule ya Sekondari Chongoleani Jijini Tanga. Mradi huo wa thamani ya Sh. 93,816,506, ulishindwa kuanza utekelezaji tangu fedha zilipotolewa Machi 4, 2024 kutokana na kasoro kubwa za kiutawala na mfumo wa manunuzi wa halmashauri ya Jiji la Tanga. Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhani Ndwata, aliwaambia waandishi wa Habari ofisini kwake Leo Juni 8 2026 wakati wa kutoa taarifa ya utendaji wa robo ya kwanza ya mwaka (Januari–Machi, 2026), ambapo alisema uingiliaji kati wa taasisi hiyo umeokoa hasara ya jumla ya Sh. 116,216,506 katika sekta ya elimu. Uchunguzi wa TAKUKURU ulibaini kuwa, makadirio ya bei ya vifaa vya ujenzi wa madarasa hayo mawili yalikuwa chini ya bei halisi ya soko, hali iliyosababisha mfumo wa manunuzi wa kielektroniki wa Serikali (*NeST*) kukataa zabuni zote na kukwamisha maendeleo ya wanafunzi ...
Marato tv - Sauti ya Jamii