Na Angela Sebastian -Bukoba Jeshi la polisi mkoani Kagera linawashikilia watu watano baada ya kukutwa na mashine 12 zinazotumika kwenye boti za kuvulia samaki na pikipiki sita ambazo wanadai ni mali za wizi ambazo ziliibiwa sehemu mbalimbali mkoani humo. Kamanda wa jeshi hilo Blasius Chatanda alieleza hayo jana wakati akiongea na vyombo mbalimbali vya habari katika viwanja vya ofisi za jeshi hilo mkoa mjini Bukoba, ambapo alisema waliweza kukamata vifaa hivyo kutokana na operesheni saka waalifu iliyofanyika ndani ya ziwa victoria na maeneo yote ya mkoa huo. "Operesheni ilinza mwezi Juni mpaka Agosti 11 mwaka huu ambapo tulianzia ziwa victoria baada ya kupata taatifa ya uwepo wa wizi wa mashine zinazotumika kwa ajiliya kuvua samaki (Engene bort) kutoka kwa baadhi ya wananchi hususani wavuvi ambapo tumezikamatia mikoa ya Bariadi na Mara ambapo wamo walioiba na wanunuzi wa mali hizo za wizi"alieleza kamanda. Wakati huo huo jeshi hilo linaendelea na ufuatiliaji wa tukio la...
Marato tv - Sauti ya Jamii