Algiers, Machi 26, 2025 – Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, amewasilisha Ujumbe Maalum kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa Mhe. Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria. Katika mazungumzo yao, viongozi hao wawili walijadili kwa kina kuhusu uhusiano wa muda mrefu na wa kindugu kati ya Tanzania na Algeria, wakisisitiza mshikamano na ushirikiano imara ulioanzia enzi za harakati za ukombozi wa Afrika, na waasisi wa mataifa hayo mawili. Pia walijadili njia za kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano katika sekta kama biashara, uwekezaji, elimu, afya na ulinzi. Mhe. Kikwete aliwasilisha dhamira ya Mhe. Rais Samia ya kuimarisha ushirikiano kati ya mataifa haya mawili, akibainisha maono ya pamoja ya ukuaji wa uchumi na utulivu wa kikanda. Kwa upande wake, Rais Tebboune alieleza kuwa anathamini sana urafiki wa Tanzania na akaeleza utayari wa Algeria wa kuendeleza ushirikiano ka...
Marato tv - Sauti ya Jamii