Skip to main content

Posts

Showing posts from March 25, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Mstaafu Kikwete Awasilisha Ujumbe Maalum Kutoka Kwa Rais Samia Kwa Rais wa Algeria, Tebboune

Algiers, Machi 26, 2025 – Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, amewasilisha Ujumbe Maalum kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa Mhe. Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria. Katika mazungumzo yao, viongozi hao wawili walijadili kwa kina kuhusu uhusiano wa muda mrefu na wa kindugu kati ya Tanzania na Algeria, wakisisitiza mshikamano na ushirikiano imara ulioanzia enzi za harakati za ukombozi wa Afrika, na waasisi wa mataifa hayo mawili. Pia walijadili njia za kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano katika sekta kama biashara, uwekezaji, elimu, afya na ulinzi. Mhe. Kikwete aliwasilisha dhamira ya Mhe. Rais Samia ya kuimarisha ushirikiano kati ya mataifa haya mawili, akibainisha maono ya pamoja ya ukuaji wa uchumi na utulivu wa kikanda. Kwa upande wake, Rais Tebboune alieleza kuwa anathamini sana urafiki wa Tanzania na akaeleza utayari wa Algeria wa kuendeleza ushirikiano ka...

Waziri Mkuu Aagiza Kituo cha Afya Mama Ngoma Kupandishwa Hadhi

- Asema muwekezaji amefanya kazi kubwa lazima Serikali imuunge mkono. - Awagiza watendaji wa Halmashauri kusimamia ukamilishaji wa miradi. WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa, amemuagiza Waziri wa Afya, Jenista Mhagama na watendaji wa Wizara hiyo kukutana na kufanya mapitio ya vigezo ili kukipandisha hadhi kituo cha Afya cha Mama Ngoma kilichopo kata ya Kwakoa Wilaya ya Mwanga Mkoani kilimanjaro kuwa hospitali. Amesema mwekezaji huyo amefanya uwekezaji mkubwa wa zaidi ya Shilingi Bilioni tano kwa kujenga majengo yenye hadhi na kuweka vifaa vya kisasa hivyo ni lazima Serikali imuunge mkono kwa kukipandisha kituo hicho. "Maliza hatua iliyobaki ipewe hadhi ya hospitali kama kuna eneo mnadhani linatakiwa kufanyiwa marekebisho mshirikiane nae, kazi anayofanya huyu ni kubwa ya kuiunga mkono Serikali ya kuwahudumia Watanzania tunamuachaje?". Alihoji Ametoa maelekezo hayo (jana Jumanne Machi 25, 2023) alipokuwa akizungumza na wananchi baada ya kuzindua Kituo Cha Afya cha Mama Ngoma kilichop...

Mbunge Muhongo Achangia Mifuko 250 ya Saruji Kwenye Harambee Sekondari ya Nyabakangara

  Na Shomari Binda-Musoma  MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo amechangia mifuko 250 ya saruji kwenye ujenzi wa shule ya sekondari Nyabakangara. Harambee hiyo iliyofanyika machi 25,2025 kwenye Kitongoji cha  cha Kamatondo Kata ya Nyambono ilihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wakiwemo wa CCM,wazawa wa Kata hiyo na wadau wa maendeleo wakiwemo wa elimu. Akizungumza kwenye harambee hiyo mbunge Muhongo amesema elimu bado ni kipaumbele ndani ya jimbo na ndiyo inayopelekea jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule. Amesema ili kumsaidia mwananchi wa Musoma Vijijini ni pamoja na kumpa elimu mtoto wake kwa manufaa ya baadae. Mbunge Muhongo amesema kila mmoja anakaribishwa kwenye jimbo la Musoma vijijini kuchangia maendeleo ya elimu ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa. "Ndugu zangu kipaumbele chetu namba moja bado ni elimu na ndio maana tunafanya jitihada mbalimbali zikiwa ni pamoja na kuendesha harambee za ujenzi wa shule na kuandaa mi...

Waziri Wa Mambo ya Nje wa Drc Awasili Nchini

Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mhe. Félix Antoine Tshisekedi ambaye pia ni  Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Mhe. Mhe. Therese Kayikwamba Wagner amewasili nchini. Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam Mhe. Wagner amelakiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Londo. Akiwa nchini Mhe. Wagner anatarajia kuwasilisha ujumbe maalum wa Mheshimiwa Rais Tshisekedi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rc Mtambi Afikisha Salamu za Pole za Rais Dkt.Samia Kwa Waathirika wa Janga la Mvua Musoma

Na Shomari Binda-Musoma  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa wananchi wa manispaa ya Musoma waliothiriwa makazi yao kutokana na mvua kali iliyoambatana na upepo iliyonyesha usiku wa kuamkia jana machi 24,2025. Salamu hizo za pole zimewasilishwa leo machi 25,2025 na mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi alipowatembelea waathirika hao. Akizungumza kwenye maeneo walikoifadhiwa wananchi hao amesema ametumwa na Rais kufikisha salamu hizo wakati serikali ikiendelea kufanya tathimini kutokana na athari iliyotokea. Amesema kaya 319 zinadaiwa kuathirika kutokana na taarifa ya awali na msaada wa kibinadamu umeshawafikia walengwa kwenye makambi waliyopo. Kanali Mtambi amesema katika kipindi hiki upendo zaidi unahitajika kwa wahanga wakati jitihada nyingine zikiendelea. " Mheshimiwa Rais amenituma niwafikishie salamu za pole katika kipindi hiki kigumu mlichonacho kutokana na athari ya mvua. " Nitumie fursa hii pia kuwaomba kuzidis...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Awafunda Kisawa Sawa Mawakili wa Serikali

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari amewakumbusha Mawakili wa Serikali kufanya kazi kwa haraka, kwa wakati  na kwa kuzingatia ubora. Johari ameyasema hayo tarehe 25 Machi, 2025 wakati akizungumza na Mawakili wa Serikali kwenye Mafunzo maalumu kwa  Mawakili hao yanayofanyika Jijini Arusha. Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewataka Mawakili wa Serikali kufanya kazi kwa haraka na kwa wakati ili waweze kuiishi kauli mbiu ya weledi na ubora pamoja na kutoa huduma bora kwa wananchi.  “ili tuifikie kauli mbiu yetu ya weledi na ubora ni lazima tuwe na tabia ya kufanya kazi kwa haraka na kwa wakati.” Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.  Aidha ameeleza kuwa mafunzo hayo kwa mawakili wa Serikali yatasaidia kuongeza umahiri kwa  Mawakili wa Serikali na kuwawezesha kutoa huduma bora za kisheria zitakazochangia katika kuletea maendeleo kwa Taifa. “Ili kuweza kutoa huduma bora za kisheria, kitu cha kwanza kwa Mwanasheria ni kuhakikisha kila jambo analifanya kwa wakat...