Skip to main content

Posts

Showing posts from July 17, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MRADI WA SHILINGI MILIONI 69.9 WABORESHA MAISHA YA WAZEE KAMBI YA SAMARIA HOMBOLO

 MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amewataka wakazi wa Kambi ya Samaria iliyopo Hombolo kulinda na kutunza miundombinu ya huduma za kijamii iliyojengwa kupitia mradi wenye thamani ya shilingi milioni 69.9, ili iweze kudumu na kuendelea kuwanufaisha kwa miaka mingi ijayo. Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi miradi ya maji, umeme na majiko banifu iliyotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhe. Senyamule alisema jukumu la kutunza miundombinu hiyo sasa liko mikononi mwa wanufaika. "Miradi hii imewekwa na inahitaji kutunzwa. Tumeshawekewa umeme, kazi ya kutunza balbu ni yetu, si ya REA tena. Tumewekewa maji karibu na makazi yetu, kazi ya kutunza koki ni yetu, si ya STAMICO tena. Ilindeni na kuitunza miundombinu yote mlioletewa kwa sababu thamani yetu ni kuitunza," alisema. Aidha, aliwahimiza wakazi wa kambi hiyo kutumia huduma hizo kujiongezea kipato kupitia shughuli za uzalishaji, hususan ki...

RAIS DKT. MWINYI ATEMBELEA VITUO VYA UTAFITI NA UBUNIFU IIT MADRAS-INDIA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea idara, vituo vya utafiti na maabara mbalimbali za Taasisi ya Teknolojia ya IIT Madras, jijini Chennai, nchini India leo tarehe 17 Julai, 2026. Ziara hiyo imetoa fursa ya kujionea maendeleo yaliyofikiwa na Taasisi hiyo katika teknolojia, tiba, ubunifu na utafiti, pamoja na kubadilishana uzoefu kuhusu namna elimu, maarifa na teknolojia vinavyoweza kutumika kutatua changamoto za kiafya na kijamii. Miongoni mwa maeneo aliyotembelea ni Kituo cha Sayansi ya Urithi, Kituo cha Taaluma na Tiba Asili za India, vituo vya utafiti wa sayansi na teknolojia za tiba, pamoja na Kituo cha Utafiti wa Kina wa Ubongo kwa kutumia Mbinu za Kisasa na Jumuishi za Anatomia ya Mfumo wa Neva. Aidha, ametembelea Maabara ya Anatomia na kujionea matumizi ya teknolojia za kisasa katika ufundishaji, uchunguzi na tafiti za afya. Ziara hiyo inatarajiwa kufungua fursa zaidi za kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali ya ...

MWENYEKITI WA ACT WAZALENDO AMTEMBELEA SHEIKH RASHID HOSPITALINI

  MWENYEKITI wa Taifa wa ACT Wazalendo, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, Leo Ijumaa ya Tarehe 17 Julai 2026, akiambatana na mke wake Mama Zainab Kombo Shaib, amefika na kumjulia hali Sheikh Rashid Hamad Othman (kaka yake), anayepatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, Jijini Dar es Salaam. Mheshimiwa Othman yupo Jijini Dar es Salaam kwa ziara Maalum ya Kikazi na kijamii.

WAZIRI MKUU AKAGUA MAANDALIZI YA SIKU YA MASHUJAA

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Julai 17, 2026 amekagua na kupokea taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika Julai 25, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa, Mtumba, jijini Dodoma. Katika ukaguzi huo, Waziri Mkuu ameridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuwataka wote wanaohusika kuendelea kukamilisha maandalizi yaliyobaki kwa wakati ili maadhimisho hayo yafanyike kwa utaratibu na hadhi inayostahili. Maadhimisho hayo yataongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu.

VIJANA 10,000 MAFUNDI WA JIMBO LA MTUMBA WENYE UJUZI KUPATIWA VYETI VYA UFUNDI NA KUTAMBULIWA NA VETA

  ▪️Ni vijana wenye ujuzi lakini hawajapitia mfumo rasmi wa mafunzo ▪️Mbunge Mavunde aahidi kuwafikia Vijana 10,000 wenye ujuzi wa Jimbo la Mtumba ▪️Ni kupitia ya Programu ya Mama Samia ya Utambuzi wa Ujuzi chini ya VETA ▪️Mkurugenzi Mkuu VETA awataka vijana kujiunga pamoja na kuchangamkia fursa Dodoma Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mh. Anthony Mavunde amesema kupitia Programu ya Mama Samia ya Kutambua Ujuzi wa Mafundi chini ya VETA anategemea kutambuliwa kwa zaidi ya Vijana 10,000 wenye ujuzi lakini ambao hawajapitia mfumo rasmi wa mafunzo ifikapo mwaka 2030. Mh. Mavunde ameyasema hayo jana tahere 16 Julai 2026 Jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vyeti vya Ufundi kwa vijana 100 wenye ujuzi waliotambuliwa kupitia Chuo cha VETA. “Tunaishukuru Serikali kupitia programu hii ya Mama Samia ya kutambua ujuzi wa vijana kupitia VETA. Vijana hawa wengi walikuwa na ujuzi lakini hawakupata nafasi ya kupata mafunzo rasmi ya ufundi kupitia vyuo vya Ufundi. Kutambuliwa kwa ujuzi wao bila ...