Skip to main content

Posts

Showing posts from September 16, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

DKT. MWIGULU: NDANI YA WIKI MOJA TUTACHUKUA HATUA KUSHUSHA BEI YA SARUJI

 WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema ndani ya wiki moja, Serikali itachukua hatua ya kuhakikisha bei ya saruji inakuwa himilivu kwa wananchi, baada ya kubaini malalamiko ya kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Simiyu. Ametoa kauli hiyo jana (Jumanne, Septemba 15, 2026) wakati akizungumza na wananchi wa Bariadi Mjini, mkoani Simiyu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya CCM Saba Saba. “Serikali tumeliona hilo. Serikali sikivu tumesikia hilo. Nimewatuma wataalamu ndani ya wiki moja wawe wameshapata ufumbuzi. Tutatoa tamko la njia ya kushusha bei ya saruji ili kila Mtanzania aweze kumudu. Katika baadhi ya maeneo bei ya saruji imefikia zaidi ya sh. 26,000 na katika baadhi ya mikoa ya mipakani imefikia sh. 32,000,” amesema na kusisitiza kuwa Serikali inataka wananchi waweze kumudu gharama za ujenzi wa nyumba na miradi mingine ya maendeleo. Kuhusu zao la pamba, Waziri Mkuu amesema ameielekeza Wizara ya Kilimo ikutane na wadau wa pam...

THBUB KUJA NA MWONGOZO WA KUTATHMINI MISINGI YA UTAWALA BORA NCHINI

   Na. Zawadi Msalla Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), ipo mbioni kuzindua mwongozo wa tathmini ya misingi ya utawala nchini.  Mwongozo huo umelenga kuangalia hali ya uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora na kuweka mfumo unaoweza kutumika kupima namna taasisi za umma, binafsi na mifumo ya utawala inavyotekeleza misingi ya utawala bora.  Mwongozo huo pia imelenga kuwa nyenzo muhimu katika kubaini mafanikio yaliyofikiwa, changamoto zilizopo na maeneo yanayohitaji maboresho katika nyanja ya utawala bora. Akizungumza katika kikao kazi cha kupitia rasimu hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa Jijini Dodoma leo, Kaimu Katibu Mtendaji wa THBUB, Bi. Suzan Ndeona amesema kazi ya uandaaji wa nyaraka hiyo muhimu kwa nchi, ilianza rasmi mwaka 2023 kwa kuangalia vigezo mbalimbali na uhitaji wa nchi wa kuwepo mwongozo na nyenzo itakayotumika katika kufanya tathmini ya Utawala Bora nchini.  Bi. Suzan amesema mwongozo huo umeweka vigezo vyote muhimu...

WIZARA YA MADINI YAJA NA SHERIA KUSIMAMIA TAALUMA YA WAJIOLOJIA

 *Sheria kuanzisha Bodi ya Wajiolojia kusimamia na kuratibu taaluma nchini* *Serikali kutenga asilimia 10 ya mapato ya madini kwa utafiti wa jiosayansi* *Taarifa sahihi za jiolojia kuimarisha uwekezaji na kuwalinda wadau wa madini* Wizara ya Madini imewasilisha pendekezo la kuanzishwa kwa Sheria ya Usimamizi wa Wajiolojia nchini katika Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri, hatua inayolenga kuweka mfumo madhubuti wa kusimamia taaluma hiyo na kuhakikisha taarifa za jiosayansi zinazotolewa nchini zinakuwa sahihi na zenye kuaminika. Hayo yamebainishwa leo, Septemba 16, 2026, jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya ya Wajiolojia Tanzania (TGS). Dkt. Kiruswa amesema endapo Sheria hiyo itapitishwa, itaanzishwa Bodi ya Wajiolojia itakayokuwa na jukumu la kusimamia, kuratibu na kuimarisha taaluma hiyo, ikiwemo kuweka viwango vya kitaaluma na kuhakikisha wataalamu wanaohusika na shughuli za jiosayansi wanatambulika na kuwaj...