📍Awataka viongozi wa dini kuhubiri Umoja na mshikamano *NA MWANDISHI WETU, MBEYA* MKUU wa Wilaya ya Mbeya, *Mhe. Solomon Itunda*, ametoa wito kwa viongozi wa dini na jamii kwa ujumla kuimarisha vita dhidi ya mmomonyoko wa maadili, huku akisisitiza kuwa wanawake ni nguzo muhimu katika kulea kizazi chenye nidhamu na uzalendo nchini. Mhe. Itunda ametoa kauli hiyo Jumamosi, Februari 28, 2026, alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, *Mhe. Beno Malisa*, katika ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) lililofanyika katika ukumbi wa VETA jijini Mbeya. Akihutubia washiriki wa kongamano hilo waliotoka katika mikoa zaidi ya 13 nchini, DC Itunda alisema Serikali ya Awamu ya Sita inatambua mchango wa kipekee wa wanawake katika kulinda misingi ya amani, maadili na hofu ya Mungu, mambo ambayo ni chemchemi ya ustawi wa Taifa. "Wanawake ni nguzo ya Taifa. Serikali inaendelea kuthamini ushirikiano na taasisi za kidini katika kukuza maadili na kuchochea maen...
Marato tv - Sauti ya Jamii