*_Kiwengwa FC yaibuka bingwa wa michuano hiyo._* Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa ameshuhudia mchezo wa fainali ya kombe la jimbo maarufu Jimbo cup kati ya Stand fc na Kiwengwa FC uliofanyika katika uwanja wa mpira wa miguu wa Majaliwa, Ruangwa Mkoani Lindi. Katika mchezo huo uliopigwa Novemba 25, 2024, timu ya kiwengwa Fc iliibuka bingwa baada ya kuwatandika Stand Fc kwa mikwaju ya Penati 4-1. Akizungumza baada ya mchezo huo Mheshimiwa Majaliwa amesema michezo hiyo inatumika kuboresha maendeleo ya mpira wa miguu katika wilaya hiyo. “Nitazungumza na chama cha makocha Taifa ili watupatie wakufunzi ambao watakuja kuwapa mafunzo makocha wa wilaya ya Ruangwa ya namna bora ya kusimamia timu zetu” Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amesema kwa kuwa Wilaya ya Ruangwa imeamua kujidhatiti kwenye mpira wa miguu ni muhimu kuwa na waamuzi wenye uwezo mkubwa wa kusimamia michezo “Chama cha Mpira cha Wilaya orodhesheni marefa waliopo katika wilaya hii, nitaomba uongozi wa marefa tup...
Marato tv - Sauti ya Jamii