Skip to main content

Posts

Showing posts from October 12, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Jumuiya ya Amsha yakabidhi Tuzo maalum ya Ualimu kwa hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

  Jumuiya wa wahitimu wa Shule ya Sekondari Milambo (AMSHA) imeanzisha tuzo maalum ijulikanayo kama Tuzo ya Mwalimu ili kuenzi mchango wa Mwalimu Nyerere na walimu wengine wanaofanya kazi yao kwa weledi mkubwa. Tuzo hiyo imetolewa kwa Mara ya kwanza kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius kambarage nyerere ikiwa ni kutambua mchango wake kwa Taifa pamoja Tasnia ya ualimu ikiwemo kufundisha katika shule ya Sekondari Mirambo kati ya mwaka 1946 na 1948 Akikabidhi Tuzo hiyo nyumbani kwa Mwalimu Nyerere,Mwitongo wilayani Butiama Mkoani Mara ,Mjumbe wa Bodi ya AMSHA Abdul-Razaq Badru amesema kuwa Tuzo ya Mwalimu itakuwa ikitolewa kila mwaka kwa Mwalimu aliyetoa mchango ulioleta matokeo chanya kwenye Jamii. Naye mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Derek Murusuri amesema ujio wa tuzo ya AMSHA utakuwa kichocheo kwa wahitimu wengine kuandaa tuzo kama hizo ili kuwapa motisha walimu wengine na kutambua mchango wao kwenye sekta ya elimu. Mbali na tuzo iliyokabidhiwa kwa familia ya Mwalimu Nyerere, wajumb...

Mwili wa Mej Gen Msataafu Mbuge kuzikwa Oktoba 17 Kijijini Kiabakari Wilayani Butiama

 

Veta kutoa mafunzo kwa madereva bodaboda

Ofisa habari wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi(VETA) David Edward amesema kuwa mafunzo wanayotoa kwa sasa na wanayotarajia kuyatoa katika  vyuo vingine hapa Nchini yataenda kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ajali ambazo zimekuwa zikisababishwa na madereva hao wa bodaboda.  Edward ameyasema hayo Jijini Mwanza wakati akizungumza na Jambo digital na kuongeza kuwa mafunzo hayo yatamsaidia dereva huyo kujua mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na udhibiti mwendo hali ambayo itawasaidia kuzijua sheria za usalama barabarani.   

Familia ya baba wa taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yamtaka msanii Steve Mengere kuacha kutumia ubini wa Nyerere

Na Obunde Michael  Butiama Familia ya Baba wa Taifa,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere imekemea tabia inayozidi kuota mizizi kwa baadhi wa wasanii nchini kujiita kwa ubini wa Nyerere pamoja majina ya viongozi wengine wa kitaifa na kwamba kwa kufanya hivyo hawawatendei haki wazazi wao. Akizungumza juu ya kadhia hiyo huko Mwitongo Butiama Leo oktoba 12,mtoto wa Baba wa Taifa,Madaraka Nyerere amesema wasanii kujiita majina ya viongozi pengine inaweza kuwa namna nzuri ya kuwaenzi viongozi hao, lakini kwa upande mwingine hawawatendei haki wazazi wao wanaostahili heshima hiyo kwa nafasi ya kwanza.  Madaraka alitoa mfano wa msanii maarufu wa vichekesho Steve Mengere ambaye amekuwa maarufu kwa kujiita Steve Nyerere na akasema hali hiyo imeleta sintofahamu kwa baadhi ya watu wanaoijua familia hiyo vizuri. "Hapa kuna tatizo. Sio sahihi kwa Steve kuendelea kujiita hivyo na naomba wanahabari msaidie kuliweka jambo hilo sawa kwa kuwatangaza wasanii kwa majina yao halisi," amesema Mad...

Kitengo cha mahusiano Barrick kinatetea haki za binadamu

 Na Helena Magabe Watetezi tv. Meneja mahusiano wa Mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara Francis Uhadi amesema kuwa kitengo chake cha  mahusiaano kinatetea haki za Binadamu licha yakuwa lawama nyingi zimekuwa zikiwaangukia. Akizungumza na Waandishi wa habari Jana Octoba 11,2024 alisema kitengo cha mahusiano na wote walioajiliwa katika kitengo hicho ni watetezi wa haki za binadamu na kwa upande wake migodi yote aliyofanya kazi alikuwa akitetea haki za binadamu ila Kwa Mgodi wa north mara wamekuwa wakitupiwa lawama ambazo hawastahili. Alisema asilimia 51 ya ajira katika Mgodi huo ni Wananchi kutoka Mara na wanatokea Nyamongo na Tarime ikiwa ni pamoja na kuajiri walinzi shirikishi 560 kutoka maeneo ya jirani na mgodi hivyo wanazingatia ajira kwa Wazawa. Meneja Mkuu wa Mgodi huo Aporinaly Lyambiko alisema kwa Sasa kuna ongezeko la ajira kwa Watanzania Kwa asilimia 31 tofauti na mwaka 2022 kulikuwa na asilimia 20 pekee. Alisema asilimia asilimia 98 ya Waajiliwa katika Mgodi huo ni...

Zaidi ya Vijana 500 wanufaika na elimu ya mazingira na mabadiliko ya tabia nchi

Na Mwandishi wetu  Mwanza Akitoa elimu ya mazingira na mabadiliko ya tabia nchi bi Ester Kusekwa amewataka vijana ambao ni wanufaika wa elimu hiyo kuwa mabarozi wazuri kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa maana uchafuzi wa mazingira unaathari kubwa ndani ya jamii ikiwemo miripuko ya magonjwa ambayo yanaweza yakasababisha vifo na kupoteza nguvu kazi ya Taifa. Ester Kusekwa ambae ni mratibu miradi kutoka shirika lisilo la serikali la Mwanza Youth And Children amesema ili dunia iendelee kuwa salama ni lazima kila mwananchi ndani ya jamii ahakikishe anatunza mazingira vizuri kwa kufanya usafi katika eneo lake analoishi na kupanda miti ya kutosha. Miongoni mwa maada zilizo tolewa kwa vijana katika kongamano hilo ni fursa za kiuchimi kwa vijana pamoja na uzalendo Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge ndugu Godfrey Mzava amewata viongozi wilayani Magu kuongeza idadi ya makongamo walau yafike manne ili vijana wapate elimu kwa kina  

Waziri Mavunde amesema Maonesho ya Madini Geita kuboreshwa kufikia hadhi ya Kimataifa

 -Rais Samia Suluhu Hassan kufunga maonesho -Idadi ya washiriki wa nje ya nchi waongezeka -RC Shigela aeleza mpango wa kujenga majengo ya kudumu na kuboresha miundombinu 📍Bombabili EPZ, Geita Waziri wa Madini *Mh. Anthony Mavunde* amepongeza maonesho ya 7 ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita kwa kuendelea kukua na kuongeza idadi kubwa zaidi ya washiriki wa ndani na nje ya nchi na hivyo kufikisha idadi ya zaidi ya washiriki 800 kwa mwaka huu 2024 na hivyo kuutaka mkoa wa Geita kuimarisha miundombinu ya eneo la Maonesho ili kuyafanya ya Kimataifa. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Geita,wakati akikagua maonesho na kutoa hati za pongezi,ushiriki na ushindi kwa waoneshaji wa bidhaa na huduma. “Ni dhamira ya Serikali kuona maonesho haya yanakuwa na kufikia hadhi ya kimataifa,hivyo Wizara ya Madini na Mkoa wa Geita tutashikiriana kwa ukaribu ili azma na ndoto hii kutimia. Maonesho ya mwaka huu yamevutia udhamini mkubwa na ushiriki wa wadau wengi sana wa nje na ndani ya nchi,na hii ni da...