Skip to main content

Posts

Showing posts from June 30, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TNCC YAMTUNUKU TUZO WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA.

 Na Mwandishi wetu Jovina Massano Musoma. Chemba ya Taifa ya biashara (TNCC) yamtunuku tuzo maalum waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mwigulu Lameck Nchemba kwa kutambua mchango wake katika kuimarisha mazingira ya biashara, uwekezaji na kukuza ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi hapa nchini. Tuzo imetolewa katika hafla iliyowakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo, ambapo TNCC imeweza kueleza kuwa hatua hiyo inalenga kutambua watu na taasisi zilizochangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania.  Rais wa Chemba ya Taifa ya Biashara (TNCC), Bw. Vicent Minja amemwambia Waziri Mkuu kuwa tuzo hii ni ishara ya kutambua mchango wako mkubwa katika kuimarisha mazingira ya biashara nchini. " Uongozi wako umefungua milango ya ushirikiano imara kati ya serikali na sekta binafsi, jambo ambalo limeongeza imani ya wawekezaji na kuchochea ukuaji wa uchumi hapa nchini", amesema Minja Viongozi na wadau wengine pia wamewez...

WAZIRI MKUU AKAGUA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA LA HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Jumatano, Julai 1, 2026, amekagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, lililopo mjini Mugumu, mkoani Mara, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya siku tano mkoani humo. Akiwasilisha taarifa ya ujenzi huo, Msanifu Majengo wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Mara, Bw. Nicholas Jeje, alisema mradi huo unagharimu shilingi bilioni 4.5 zinazotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alisema ujenzi ulianza Aprili 10, 2025 na unatarajiwa kukamilika Aprili 9, 2028, huku utekelezaji wake ukiwa umefikia asilimia 42. Alieleza kuwa jengo hilo litakuwa na ofisi 62, zikiwemo ofisi za Mkurugenzi wa Halmashauri na Mwenyekiti wa Halmashauri, pamoja na kumbi mbili za mikutano zenye uwezo wa kuchukua watu 50 na 110 mtawalia, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma kwa wananchi. Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, alimkaribisha Waziri Mkuu mkoani humo na ku...

NAFUU YA MAFUTA YAANZA JULAI, EWURA YASHUSHA BEI ZA PETROLI, DIZELI NA MAFUTA YA TAA

 Watumiaji wa mafuta nchini wameanza mwezi Julai kwa nafuu baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kutangaza kupungua kwa bei kikomo za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kufuatia kushuka kwa bei katika soko la dunia. Akitoa taarifa kwa umma, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Gerald Maganga, amesema kuanzia Julai 1, 2026, bei za petroli zitashuka kwa Shilingi 96 kwa lita, dizeli kwa Shilingi 151 kwa lita, huku mafuta ya taa yakishuka kwa Shilingi 242 kwa lita. Amesema mabadiliko hayo yamechochewa na kuanza kutulia kwa mwenendo wa soko la mafuta duniani baada ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya Marekani na Iran kuhusu mvutano wa Mashariki ya Kati ambapo Makubaliano hayo yameruhusu meli za mafuta kuendelea kupita katika Mlango wa Bahari wa Hormuz, hatua iliyosaidia kupunguza changamoto za usafirishaji wa mafuta duniani. Aidha, kampuni za kusafisha mafuta ghafi zimeendelea kununua mafuta kutoka maeneo mengine yasiyoathiriwa na vita ili kuhakikisha upati...

KATIBU MKUU CCM AKUTANA NA BALOZI WA UMOJA WA ULAYA KUJADILI USHIRIKIANO WA MAENDELEO

 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Christine Grau, Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, katika Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, Lumumba, Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yamefanyika ikiwa ni sehemu ya ziara ya kumuaga Balozi Grau anayehitimisha kipindi chake cha uwakilishi nchini Tanzania. Viongozi hao walitathmini ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya na kujadili namna ya kuuendeleza kwa manufaa ya pande zote mbili. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu umuhimu wa kuimarisha misingi ya utawala bora, amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa kama nguzo ya maendeleo endelevu ya Taifa. Katika muktadha huo, CCM ilisisitiza dhamira yake ya kuendelea kujenga Taifa linaloongozwa kwa misingi ya haki, uwajibikaji na utulivu wa kisiasa. Pia, ilitambua changamoto zilizojitokeza nchini katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu uliopita na umuhimu wa hatua ambazo Serikali inaendelea kuzich...

WAZIRI MKUU AANZA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TANO MKOANI MARA

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Seronera, wilayani Serengeti mkoani Mara, kuanza ziara ya kikazi ya siku tano mkoani humo. Katika ziara hiyo itakayofanyika kuanzia leo, Jumatano Julai 1 hadi Julai 5, 2026, Waziri Mkuu atakagua na kuzindua miradi ya maendeleo, kuzungumza na wananchi, kusikiliza na kutatua changamoto zao katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mara.

RAIS SAMIA APOKEA GAWIO LA TRILIONI 1.3, ASISITIZA TIJA YA UWEKEZAJI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza taasisi za umma kutathminiwa kwa kuzingatia tija ya uwekezaji, ubora wa huduma, uwezo wa kujitegemea na mchango wake katika uchumi wa Taifa. Rais Dkt. Samia ameyasema hayo leo, Ikulu Dar es Salaam, wakati wa hafla ya Siku ya Gawio 2026 iliyobeba kaulimbiu isemayo, "Uwekezaji wa Umma wenye Matokeo: Nguzo ya Uchumi Shindani na Maendeleo Endelevu kuelekea Dira 2050," ambapo amepokea gawio na michango yenye thamani ya shilingi trilioni 1.327 kutoka kwa mashirika, taasisi za umma na kampuni ambazo Serikali ina hisa chache. Amesema ongezeko la gawio la mwaka huu limetokana na kuimarika kwa tija, uzalishaji na ufanisi wa taasisi za umma, huku akisisitiza kuwa mafanikio ya taasisi hayapaswi kupimwa kwa gawio pekee bali pia kwa ubora wa huduma, uwezo wa kujitegemea na mchango wake katika ukuaji wa uchumi. Rais Dkt. Samia pia ameagiza taasisi zilizoshindwa kutoa gawio, zilizotoa pungufu au zilizopung...