Skip to main content

Posts

Showing posts from June 30, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TANZANIA YAVUTIA UWEKEZAJI WA UJENZI WA VIWANDA VYA KUZALISHA BIDHAA ZA MIGODINI

     ▪️Waziri Mavunde akutana na Mwekezaji wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma ▪️Ni kiwanda cha Oriental Casting and Forging Ltd cha China ▪️Kiwanda kikubwa kujengwa Buzwagi Kahama ▪️Tanzania yajipanga kuwa kitovu cha uzalishaji wa bidhaa za migodini Afrika 📍 Dar es salaam Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini. Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini. Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini il...

CHAMA CHA NLD CHAITISHA KIKAO KIZITO CHA KAMATI KUU DAR KESHO

 📍Itafanya tathimini ya uchaguzi uliopita na Hali ya kisiasa nchini  Na MASHAKA MHANDO,DAR ES SALAAM CHAMA cha National League for Democracy (NLD), kimetangaza kuitisha kikao kizito cha kimaamuzi cha Kamati Kuu ya chama hicho kwa muda wa siku mbili mkoani Dar es Salaam, kikiwa na lengo la kujadili mustakabali wa chama na kufanya tathmini ya kina ya kisiasa baada ya kumalizika kwa michakato ya uchaguzi. Kikao hicho muhimu kinatarajiwa kufanyika kesho Jumatano, Julai Mosi, na keshokutwa Alhamisi, Julai 2, 2026, katika Ukumbi wa Popex uliopo Buguruni Sheli, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. Akizungumza kupitia taarifa rasmi kwa umma iliyotolewa leo Jumanne, Juni 30, 2026, Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano ya Umma wa NLD, Bw. Pogora Ibrahim Pogora, alibainisha kuwa kikao hicho kimebeba ajenda kuu nne mahususi zinazolenga kukivusha chama hicho kuelekea hatua mpya ya ushindani wa kisiasa. "Chama cha National League for Democracy (NLD) kinapenda kuwajulisha wanachama, wadau na u...

RAIS DKT. MWINYI AISHUKURU INDIA KWA KUIMARISHA USHIRIKIANO, APOKEA MWALIKO RASMI WA KUTEMBELEA INDIA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru Serikali ya India kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano wake na Zanzibar katika sekta mbalimbali za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 30 Juni 2026, alipokutana na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey, pamoja na ujumbe wake, waliofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo. Katika mazungumzo hayo, Rais Dkt. Mwinyi amepongeza uwekezaji unaofanywa na wawekezaji na taasisi binafsi za India nchini na kueleza utayari wa Zanzibar kuimarisha ushirikiano na India katika elimu ya ufundi na mafunzo ya amali. Aidha, amesifu mchango wa Taasisi ya Teknolojia ya India Madras, IIT Madras Zanzibar, katika utoaji wa elimu na mafunzo ya kitaalamu, pamoja na kuleta mageuzi katika sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. IIT Madras Zanzibar ni kampasi ya kwanza ya kimataifa ya taasisi hiyo nje ya India. Kwa upande wake, Balozi Bishwadip Dey amemkabidhi ...

AGNESS MARWA AWATAKA KINA MAMA KUWALINDA VIJANA DHIDI YA VURUGU

 Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara, Mhe. Agness Marwa, amewatembelea wajasiriamali wa Soko la Free Park, Manispaa ya Musoma, na kujionea shughuli zao za kila siku. Mbali na kuungana nao katika shughuli za biashara ya dagaa, Mhe. Marwa amewataka kina mama kuendelea kuzungumza na watoto wao kuhusu umuhimu wa kudumisha amani na kuepuka kujihusisha na vitendo vinavyoweza kuvunja utulivu wa nchi, ikiwemo kuitikia wito wa maandamano au vurugu. Aidha, amewahimiza wajasiriamali hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kujiongezea kipato na kuchangia maendeleo ya familia na taifa. Kwa upande wao, wajasiriamali wa soko hilo wamesema wamefarijika na ziara ya Mbunge huyo, wakieleza kuwa amekuwa karibu nao mara kwa mara na anaelewa changamoto zao. Pia wamemtakia mafanikio katika majukumu yake ya uongozi.

TANZANIA YAVUTIA UWEKEZAJI WA UJENZI WA VIWANDA VYA KUZALISHA BIDHAA ZA MIGODINI*

  ▪️Waziri Mavunde akutana na Mwekezaji wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma ▪️Ni kiwanda cha Oriental Casting and Forging Ltd cha China ▪️Kiwanda kikubwa kujengwa Buzwagi Kahama ▪️Tanzania yajipanga kuwa kitovu cha uzalishaji wa bidhaa za migodini Afrika 📍 Dar es salaam Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini. Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini. Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini ili Tanzania ku...

RAIS DKT. MWINYI AIHIMIZA PBZ KUWEKEZA ZAIDI KATIKA TEKNOLOJIA NA AKILI MNEMBA (AI)

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameihimiza Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) kuendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa, usalama wa mifumo ya kifedha, ubunifu wa bidhaa na huduma, pamoja na matumizi ya Akili Mnemba (AI), ili kuongeza ufanisi na ushindani katika utoaji wa huduma. Akizungumza leo, tarehe 30 Juni 2026, katika Maadhimisho ya Miaka 60 ya PBZ yaliyofanyika Hoteli ya Golden Tulip Zanzibar Airport, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza benki hiyo kwa mafanikio katika huduma za kidijitali na kuitaka iongeze juhudi ili iwe miongoni mwa benki bora nchini. Aidha, ameihimiza PBZ kuimarisha mtaji wake, kuendelea kubuni bidhaa na huduma za kifedha, kuwawezesha vijana na wanawake kiuchumi, kuwekeza katika rasilimali watu, kuimarisha utawala bora na usimamizi wa vihatarishi, pamoja na kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Rais Dkt. Mwinyi amesema gawio la shilingi bilioni 15.3 lililotolewa na PBZ...

WAZIRI NDEJEMBI AMKOROMEA MKANDARASI KITUO CHA KUZALISHA UMEME HALE

 Na MASHAKA MHANDO, Korogwe SERIKALI imempa mwezi mmoja hadi Julai 31 mwaka huu mkandarasi anayekarabati Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe mkoani Tanga, kukamilisha mradi huo wa Shilingi Bilioni 64 (Dola Milioni 24.81) ambao kwa sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji nyanjani. Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, wakati akikagua maendeleo ya kituo hicho jana, Juni 29, 2026, ambapo alisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba hata kwa siku moja ili wananchi wapate nishati ya uhakika. "Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika, sambamba na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi," alisema Waziri Ndejembi. Akifafanua umuhimu wa mradi huo, Waziri Ndejembi alibainisha kuwa kukamilika kwa ukarabati wa kituo hicho kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa nishati hiyo kwa uhakika...