Skip to main content

Posts

Showing posts from March 17, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mbunge Shangazi amshukuru Rais mradi wa Maji Mlalo

  Na Mashaka Mhando, Lushoto  ZAIDI ya wakazi 2,000 wa vijiji vya Mkundi-Mtae na Mkundi-Mbaru vilivyopo kata ya Mnazi tarafa ya Mtae, Jimbo la Mlalo wilayani Lushoto, watanufaika na mradi mkubwa wa Maji unaoendelea kutekelezwa na serikali. Mradi huo wenye thamani ya sh. 787,204,963 unatekelezwa katika vijiji hivyo ambavyo vipo katika uwanda wa tambarare wilayani hapa na kwa muda mrefu vilikuwa vikikabiliwa na tatizo ya shida ya maji. Akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo tarehe 17/3 , Mbunge wa Mlalo, Rashid Shangazi alimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha ambazo zitasaidia upatikanaji wa maji katika eneo hilo. Alisema mradi huo utakamilika mwaka huu, wananchi watapata maji safi na salama baada ya kipindi kirefu kutumia maji ya visima. "Ndugu wananchi mradi huu utakamilika mwaka huu, tumpongeze sana Rais wetu kwa kutuletea fedha za mradi huu, hongera sana Mama Samia Mlalo huna deni," alisema Shangazi ambaye ni Katibu wa wabunge wa CCM bungeni. Shangazi alis...

Madini ya Bati fursa zipo nyingi njooni – Mkopi

  · *Hutumika kwenye mifumo ya kielektroniki ya simu, ndege, vyuma vya reli* · *Yaleta ukombozi  kwa wananchi Kyerwa* *KAGERA* MADINI ya Bati (Tin) yameendelea kuwa  na mchango kwenye  maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini mkoani Kagera huku watanzania wakitakiwa kuchangamkia fursa za uchimbaji wa madini hayo. Akizungumza katika mahojiano maalum,  Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Kagera, Nobert Mkopi amesema, mkoani Kagera kuna fursa nyingi zikiwemo  za huduma za maabara kuweza kufanyia uchunguzi wa madini yanayopatikana, makampuni ya ulinzi kwenye migodi na wafanyabiashara wakubwa wa Madini, makampuni ya uuzaji mitambo pamoja na fursa za  leseni za uchimbaji mdogo na mkubwa. “Watu waje wawekeze kwenye uchimbaji wa madini ya Bati, maeneo bado yapo mengi katika maeneo ya Nyaruzumbura , Katera , Murongo n.k wilayani Kyerwa, uchimbaji unaoendelea ni mdogo wa maduara, wachimbaji wakubwa kutoka ndani na nje tunawakaribisha,”amesema Mkopi na kuongeza, “Sok...

Ccm yaahidi Kuendelea Kumuenzi Dk.Magufuli,Kuchangia Milioni 50 Kukamilisha Ujenzi Wa Kanisa Chato

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara John Mongella ameshiriki Ibada ya Shukrani ya kumbukizi ya miaka minne ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Magufuli, aliyefariki dunia Machi 17 mwaka  2021. Akiwasilisha salamu za CCM kwa niaba ya Katibu Mkuu,  Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo Machi 17,2025 Mongella amesema kuwa Chama kitaendelea kumuenzi Hayati Dkt. Magufuli kwa kazi kubwa aliyoifanya katika ujenzi wa Taifa na ustawi wa Chama. Wakati huo huo katika harambee ya kumalizia ujenzi wa Kanisa la Katoliki Chato, Geita, Mongella ametangaza kuwa CCM itachangia Shilingi milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo, ambalo ni miongoni mwa miradi iliyoasisiwa na Hayati Magufuli.

Waziri Lukuvi Amwakilisha Rais Samia Kwenye Ibada ya Kumuombea Hayati Magufuli Chato

Leo Machi 17, 2025 ni kumbukizi ya miaka 4 toka kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya 5 Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Wilayani Chato mkoani Geita kumefanyika misa takatifu ya kumuombea ambapo familia ya Hayati Magufuli ikiongozwa na mjane wake Mama Janeth Magufuli na viongozi mbalimbali wa kitaifa, mkoa na Chama wameshiriki.  Misa hiyo ya ibada ya kumuombea Hayati Magufuli imefanyika katika Jimbo Katoliki la Lulenge Ngara Parokia ya Mt. Yohana Maria Muzeyi Mlimani huku Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye ibada hiyo.  Viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwemo Naibu Katibu Mkuu CCM Taifa Ndugu John Mongela, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Innocent Bashungwa, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigela, Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Rehema Sombi na wengine wa Chama na Serikali wamehudhuria misa hiyo.

Kampeni ya Ujenzi wa Maabara za Masomo ya Sayansi na Uanzishwaji wa "High Schools" yaendelea Musoma Vijijini

  Na Shomari Binda-Musoma  KAMPENI kabambe ya ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi na uanzishwaji wa shule za "High Schools" imepamba moto katika jimbo la Musoma vijijini. Lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha kila shule ya sekondari inakuwa na maabara tatu za masomo ya sayansi ambayo ni Fizikia, Kemia na Bailojia Akizungumza leo machi 17 2025 na GMTV mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Profesa Sospeter Muhongo  amesema jimbo linao mradi kabambe wa ujenzi wa maabara hizo tatu kwa kila sekondari ya Kata. Amesema wanavijiji na viongozi wao wanashirikiana na Halmashauri ya (Musoma DC) na serikali kuu kuchangia ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi kwenye sekondari hizo za Kata. Mbungo Muhongo amesema mradi huo ni kuboresha ufundishaji, ujifunzaji, uelewa na ufaulu wa masomo ya sayansi kwa wanafunzi wa jimboni humo Amesema uanzishwaji wa "High Schools" za masomo ya sayansi ni muhimu kwani kwa sasa  "High School"ipo  moja tu nayo ni ya masomo ya "arts...

Mbeya imebeba Historia Muhimu ya Ukombozi Afrika - Wasira

Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,  Stephen Wasira amewaeleza vijana mkoani Mbeya kuwa mkoa huo una historia kubwa katika ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika, hivyo ni jukumu lao kuilinda. Wasira amesema hayo leo machi 17 mwaka 2025 alipokuwa akipokewa rasmi mkoani humo katika Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya. "Nataka niwaambie hapa mkoani Mbeya, Chama chetu ni Chama cha historia, sisi ni muungano wa vyama vilivyoikomboa Tanzania na Afrika kwa ujumla, sisi sio chama cha kawaida. "Vijana ambao hawaelewi ni kwamba sisi ndio tuliosaidia kuikomboa Afrika. Hapa Mbeya ndipo alipopitia Nelson Mandela, hapa Mbeya ndipo alipopitia Sam Nujoma, na wote walipopita hapa kulikuwa na mzee wetu mwanzilishi wa Chama cha TANU alikuwa anaitwa Mwakangale na yeye ndiye aliewasindikiza kutoka hapa mmoja baada ya mwengine kwenda Dar es Salaam kwa Mwalimu Julius Nyerere..." amesema. Amesema viongozi hao waliokuwa katika harakati za ukombozi wa nchi zao hatimaye walifanikiwa kuwaondoa wakoloni ...

Rais Samia Azindua Sera ya Taifa ya ardhi

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofautitofauti aliposhiriki hafla ya Uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 toleo la Mwaka 2023 ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention center Dodoma leo Machi 17,2025.