Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, TIC, Dkt. Binilith Mahenge ametoa wito kwa Wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania, kutokana na amani na utulivu pamoja na uwepo ya maeneo ya kutosha kwa ajili ya uwekezaji. Pia Dkt. Mahenge amewakaribisha Wawekezaji wote kuja kuwekeza nchini kutokana na uwepo wa fursa mbalimbali kwenye uwekezaji. Amesema hayo akiwa kama Mgeni rasmi kwenye Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na India (Haryana India), kwenye Maonesho ya 48 ya Biashara ya Sabasaba, Vile vile, Dkt. Mahenge amesema kuwa nchi za Tanzania na India zimedumisha mwelekeo wa masoko kwenye masuala ya biashara na uwekezaji katika sekta mbalimbali, zikiwemo sekta muhimu za Afya na Elimu.
Marato tv - Sauti ya Jamii