NA MASHAKA MHANDO WIZARA ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kupitia Taasisi ya Hakimiliki nchini (COSOTA), inatarajia kuweka historia mpya kwa kugawa zaidi ya shilingi bilioni moja kama mirabaha kwa wasanii wa kampuni mbalimbali nchini ifikapo Januari 23, 2026. Hatua hiyo inakuja baada ya imani ya kimkakati kati ya Naibu Waziri wa sekta hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), na uongozi wa COSOTA, yaliyolenga kujibu kiu ya muda mrefu ya wasanii kuhusu malipo ya haki zao. Akizungumza katika mahojiano maalum, MwanaFA alisema kuwa Serikali imejipanga kufanya ugawaji huo kuwa tukio kubwa na kihistoria kutokana na kiwango kikubwa cha fedha kilichopokea. "Kama msanii kama Naibu Waziri, nilipokea maswali mengi kutoka kwa wasanii wenzangu wakitaka kujua hatma ya mirabaha yao. Nimefanya (discussion) nzuri na COSOTA na tumekubaliana kuwa Januari 23 mwakani, tunakwenda kutoa zaidi ya shilingi bilioni moja na ushee. Himekuwa ni kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kutokea nchini," alis...
Marato tv - Sauti ya Jamii