Skip to main content

Posts

Showing posts from September 20, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

John Bina apongezwa kwa kuleta mabadiliko makubwa sekta ya madini

Wachimbaji wadogo wa Madini wameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa ushirikiano mkubwa na Shirikisho la Wachimbaji wa madini FEMATA  ambao umewezesha kupatikana kwa zana mbalimbali za kisasa za uchimbaji wa madini.  Wakizungumza na GM TV baadhi ya wachimbaji hao wamesema hatua hiyo imetokana kazi nzuri zinazodanywa na FEMATA  chini ya Rais wake John Wambura Bina "Hongera sana sana Mh Rais wa Shirikisho la vyama vya wachimbaji Madini Tanzania Ndugu John Wambura Bina kwa namna unavyoweza kushauri Serikali na kukubaliana nao juu ya mambo mengi ya msingi yanayo kwenda kuleta matokeo kwa wachimbaji" walisema wachimbaji wadogo na kuongeza kuwa "Vifaa hivi vinavyoendelea kuletwa nchini kwa ajili ya uchorongaji na utafiti vimetokana na hamasa yako ya kuwaunga wachimbaji wadogo kote nchini na mchango wao katika Pato la Taifa na Taifa limeona" Wachimbaji hao pia wamempongeza kwa dhati Mkurugenzi wa Shirika la Madini Tanzania(Stamico)Dkt.Vernus Mwase kwa kazi kubwa ya kute...

Naibu Rais wa kenya Rigathi Gachagua afanyiwa umafia wa aina yake

Naibu Rais wa Jamhuri ya Kenya, Rigathi Gachagua amezungumza kuhusu sababu za kukosa baadhi ya matukio muhimu ya kitaifa ambayo yanahudhuriwa na maafisa wa serikali pamoja na Rais William Ruto. Akizungumza jana Ijumaa katika mahojiano na Citizen TV, Gachagua amefichua kwamba yeye na timu yake wameondolewa kwenye kundi la WhatsApp ambamo huwekwa ratiba ya rais, labda kwa lengo la kuwafanya washindwe kushiriki masuala ya kitaifa. Amedai kuwa Katibu binafsi wa Rais, Reuben Miayo, aliondoa timu yake kutoka kwenye ratiba ya Rais wiki moja iliyopita, na hivyo amekuwa hajui kinachoendelea na hawezi kuhudhuria hafla za mkuu wa nchi. "Takriban wiki moja iliyopita, tuliondolewa kwenye hiyo ratiba hivyo hatukuwa tunaweza kufuatilia kinachoendelea na kwa hivyo hatuwezi kujiunga. Ninapojua mahali Rais yupo, mimi huwa hapo. Nikikosa kujua, sina la kufanya," amesema Gachagua. "Ni katika kundi la WhatsApp tunajua ratiba za kila siku. Lakini niliondolewa mimi, katibu wangu binafsi na mku...

Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma(Udom) kampasi ya njombe kuinua uchumi wa njombe

Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika amesema kuwa ujenzi wa Chuo kikuu cha Dodoma(UDOM)Kampasi ya Njombe utaleta manufaa mengi ikiwemo kusogeza huduma ya elimu karibu na wananchi pamoja na kuinua uchumi wa Njombe.  Mwanyika ameyasema hayo Septemba 20, 2024 wakati Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda akikagua utekelezaji wa miradi mbalimbali katika jimbo la Njombe Mjini. Mwanyika amewataka wananjombe kujiandaa kwa ongezeko la fursa mbalimbali ambazo zitainua uchumi wakati na baada ya  kukamilika kwa ujenzi wa Chuo Kikuu  Njombe.  Pia amewaasa wananjombe kuanza kuboresha nyumba za makazi na mahitaji mengine ambayo ni hitaji kwa uwepo wa Chuo Kikuu Njombe ifikapo 2027. Aidha, Mhe. Mwanyika ameishukuru serikali kwa ujenzi wa barabara ya Mabatini - Ramadhani yenye urefu wa kilometa 1.46 kwa kiwango cha lami ambayo imegharimu zaidi ya shilingi milioni 600 na kiasi cha milioni 70 zimetengwa kwa ajili ya kufunga Taa katika barabara hiyo. Pamoja...

Tanzania na Saudia Arabia zaingia makubaliano kudhibiti uhalifu

Na Mwandishi Wetu,Riyadh Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini hati ya makubaliano na Serikali ya Saudi Arabia makubaliano ambayo yanaenda kugusa sekta mbili muhimu za usalama ikiwemo udhibiti wa makosa mbalimbali ya uhalifu kwa kutumia utaalamu na teknolojia ya hali ya juu kwa Jeshi la Polisi sambamba na udhibiti wa majanga mbalimbali ikiwemo moto,ajali za bararani,maporomoko kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Hati hiyo ya makubaliano kwa upande wa Tanzania imesainiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni na upande wa Serikali ya Saudi Arabia imesainiwa na Mwanamfalme Abdul Aziz Bin Saudi Al- Saudi huku pande zote mbili zikionyesha nia ya kubadilishana uzoefu na vifaa mbalimbali ikiwemo vifaa vinavyotumia teknolojia katika udhibiti wa matukio ya uhalifu. ‘Nachukua fursa hii kumshukuru Waziri wa Mambo ya Ndani wa Saudi Arabia, Mwanamfalme Abdul Aziz Bin Saudi Al -Saudi kwa kunipa ushirikiano mkubwa katika ziara hii ambayo leo hii imepelekea kukami...

Waziri Mkuu awasili New York Marekani kumwakilisha Rais Samia

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Septemba 20, 2024 amewasili nchini Marekani na kupokelewa na Balozi wa Tanzania Mjini New York, nchini Marekani na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, Balozi Hussein Othman Katanga. Mheshimiwa Majaliwa yupo nchini humo kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA79)

Mbunge Mavunde amuunga mkono Rais kwa vitendo

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule leo ameongoza hafla maalum ya ugawaji wa majiko ya gesi 1000 kwa wakina Mama na Baba Lishe,Shule,Vituo vya Afya pamoja na watoto yatima. Majiko hayo yametolewa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Rosemary Senyamule ambaye amempongeza Mavunde kwa jitihada mbalimbali anazofanya katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Dodoma  Senyamule ameeleza  kuwa mitungi hiyo ni sehemu ya utunzaji mazingira kwa kutumia nishati mbadala ili kuepukana na matumizi ya kuni na mkaa sanjari na kupunguza muda wa kupika. “Asante sana Mhe. Mbunge kwa kutuletea mitungi hiyo Rafiki kwa mazingira, sasa tutapika kwa wakati mfupi,Tunakushukuru kwa kuwajali wananchi kata zote za Jimbo la Dodoma pamoja na taasisi mbalimbali za umma. Nendeni mkatumie mitungi hii ya kisasa"alisema Senyamule na kuongeza kuwa "Kati ya wabunge wanaofanya kazi vizuri, Mavunde yumo. Mavunde ni kijana mchapakazi na msikivu sana, mlifanya maamuzi sahihi kumchagua mbunge huyu. Naomba tumuunge mk...

Waziri Bashe apiga marufuku ununuzi wa kahawa kwa kutumia kangomba

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe (mb) amepiga marufuku wafanyabiashara wanaonunua kahawa kwa njia ya Kangomba na kuagiza wakamatwe huku akisisitiza kuwa uwekezaji mkubwa unaofanywa katika zao hilo umelenga  kuteka soko la kahawa ya Tanzania kimataifa. Amesisitiza kuwa serikali kwa sasa inawekeza katika kahawa kwa kugawa miche na mbolea ya ruzuku hivyo, anatarajia kupigwa vita na wafanyabiashara kutokana na kukemea kangomba lakini hatarudi nyuma kwa maslahi ya zao hilo. Waziri Bashe amesema hayo wakati wa kutembelea mashamba, viwanda vya kuchakata kahawa  na skimu za umwagiliaji kwenye wilaya za Mbinga na Nyasa. “Najua haya maamuzi yatakuwa na maumivu na yatakuwa na kelele, mimi kelele nimezoea, kamateni wanaonunu kahawa kwa kangomba"alisema Bashe na kuongeza kuwa  “Tutegemee  kelele nyingi kutoka kwa wafanyabiashara lakini sipo tayari kuona kangomba katika kahawa.Kelele zitakuwa nyingi watapitishia kwa wakulima tujiandae lakini nasema ili kufikia soko la kimataifa hatu...

Wanao Hamasisha Mmomonyoko wa Maadili Kwenye Mitandao Kuchukuliwa Hatua-Dkt. Ndumbaro

Na Elizabeth Zaya WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk.Damas Ndumbaro, ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), kuwashughulikia wale wote wanaohamasisha mmonyoko wa maadili kupitia mitandao ya kijamii na kusigina mila na tamaduni za Kitanzania. Dk.Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua Tamasha la Kitaifa la Utamaduni mjini Songea mkoani Ruvuma. Amesema hakuna taifa lolote duniani lisiloheshimu na kuthamini mila, desturi na tamaduni zao na kwamba ni jukumu la TCRA kuwashughulikia ipasavyo wale wote wanaotumia vibaya mitandao hiyo. "TCRA mna jukumu kubwa la kuhahikisha wale wanaokiuka mila na desturi za Kitanzania, kuzisigina na kuhamasisha mambo yanayochangia kuleta mmonyoko wa maadili katika nchi yetu wanashughulikiwa ipasavyo,”amesema Dk.Ndumbaro. “Tusipokuwa na utamaduni wetu, hatuna utu na tusipouenzi hatutauendeleza na ili taifa liwe hai lazima kuenzi na kuendeleza utamaduni wake, lazima turithishe utamaduni kwa vijana pamoja na watoto,tuwafundishe mila na...

Wanawake na vijana wajasiriamali misungwi waaswa kujiepusha na mikopo umiza

  Mamia ya wajasiriamali wanawake na vijana kutoka kata ya Mabuki wilayani Misungwi Mkoani Mwanza wamenufaika na Mafunzo yanayolenga kuwajengea uwezo wa namna ya kujikwamua kiuchumi. Mafunzo hayo yametolewa na Benki ya CRDB kupitia Progam ya Imbeju inayolenga kuwawezesha akinamama na vijana kuweza kupata mitaji wezeshi.   Akizungumza katika mafunzo hayo,Msimamizi wa biashara wa Benki ya Crdb kanda ya ziwa May Mosi Ndunguru amesema kuwa program hiyo imebuniwa na benki hiyo kwa ajili ya kuwezesha wajasiriamali vijana na wanawake kuweza kupata mitaji wenzeshi ili kukuza biashara zao. Naye mhamasishaji na mwezeshaji wa Benki ya Crdb Misungwi Angela Palangyo amesema kuwa Program Imbeju inatoa uwezeshaji wa kati ya shilingi millioni moja na millioni 30.   Palangyo amesema kuwa vigezo vya kupata uwezeshaji huo ni pamoja na kuwa mtanzania mjasiriamali ambaye amefanyia kazi wazo lake ambapo Benki hiyo baada ya kuona uthubutu,mhusika hupatiwa uwezeshaji ili aweze kukuza na kuendele...