Skip to main content

Posts

Showing posts from March 16, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CRJE kukabidhi majengo ya hostel za wanafunzi kwa Chuo cha NIT mwezi huu

  Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Kichina ya CRJE (East Africa) Limited imesema mradi wa ujenzi ambao upo kwenye hatua za mwisho kabisa wenye thamani ya Tsh10.8 bilioni katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) unatarajiwa kukabidhiwa rasmi kwa Taasisi hiyo iliyo chini ya Wizara ya Uchukuzi mwezi huu. Kampuni ya CRJE (East Africa) Limited imejenga majengo mawili katika Chuo hicho kupitia Mradi wa Eastern Africa Skills for Transformation and Regional Integration (EASTRIP) ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia wenye lengo la kuendeleza Kituo cha Umahiri katika Usafiri wa Anga. Akizungumza katika mahojiano jana jijini Dar es Salaam, Dai Yanwei, Msimamizi wa mradi huo kutoka CRJE (East Africa) Limited alisema: “Tumefanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi huu unakamilika mapema iwezekanavyo. Tuna Mshukuru Mungu tumekamilisha salama na hivi sasa tupo kwenye hatua ndogo ndogo za mwisho ili tuweze kukabidhi mradi huu kwa Chuo.” Mnamo Novemba 2022, NIT imeingia mkataba wa mwaka mmoj...

Rais Samia Aagana na Makamu Mwenyekiti wa Benki ya Dunia

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika Bi. Victoria Kwakwa, tarehe 17 Machi 2025, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma. Bi. Kwakwa alifika Ikulu kuaga rasmi baada ya kustaafu kufanya kazi Benki ya Dunia kwa muda wa miaka 35. Kwa upande wake Rais Dkt. Samia amemshukuru kwa ushirikiano aliouonyesha kwa Tanzania kwa muda wote wa uongozi wake.

Kamati ya Bunge Yakagua Mradi Wa Nyumba Nssf Mtoni Kijichi, Kikwete Asifu Ustahimilivu Nssf

  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii wametembelea na kukagua Mradi wa Nyumba za Mtoni Kijichi awamu ya Tatu unaomilikiwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) leo Machi 16, 2025 Jijini Dar es salaam. Akizungumza Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Fatma Toufiq amesema Kamati hiyo imeridhishwa na kupongeza uwekezaji huo wenye tija ambao utawezesha wakazi wa jijini Dar es Salaam kupata makazi bora yaliyopo katika mradi huo. Aidha, amehimiza uwepo Zahanati, Maduka na maeneo ya michezo kwa ajili ya watoto katika eneo hilo ili wapangaji waweze kupata huduma mbalimbali za kijamii kwa karibu. Awali akizungumza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesema NSSF imeendelea kuwa stahimilivu kwa kusajili idadi kubwa ya Wafanyakazi kwenye sekta binafsi.  Naye Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba amesema mradi wa Nyumba wa Mtoni Kijichi tayari umetoa makazi kwa familia 390 ambapo nyumba zimenunuliwa. P...

Serikali ya Kenya yapambana Kuokoa Raia wake Dhidi ya Hukumu ya Kifo Vietnam

  KATIBU Mkuu katika Wizara ya Masuala ya Nje Korir Sing’oei Jumapili aliandaa mazungumzo ya simu na mwenzake wa Vietnam kuhusiana na juhudi za kumwokoa Mkenya Margaret Nduta anayekabiliwa na hukumu ya kitanzi nchini humo. Bw Singóei alisema Naibu Waziri wa Masuala ya Kigeni Nguyen Minh Hang alimhakikishia kuwa  ombi la Kenya kuwa Nduta asinyongwe lilikuwa likitathmniwa. “Nilimwambia Bi  Hang kuhusu wasiwasi wa Wakenya kuhusiana na  kitanzi kilichokuwa kikinukia kwa raia wetu na kuomba hukumu hiyo isitekelezwe.  Hiyo itatoa muda kwa Kenya na Vietnam kusaka muafaka ya kupata suluhu kwa suala hili,” akasema Bw Singóei kupitia ukurasa wake wa X “Nashukuru sana kwamba Bi Hang alinihakikishia kuwa ombi letu linatathminiwa na utawala wa Vietnam,” akaongeza. Katibu huyo aliwahakikishia Wakenya kuwa ubalozi wa nchi kule Vietnam ulikuwa ukifuatilia kesi hiyo kwa lengo la kuhakikisha Nduta hakutani na kamba. Baada ya kilio kutoka kwa Wakenya kuhusiana na masaibu ya Nduta,...

Rais Museveni Aamuru Chama chake Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge

  Chama cha Siasa kinachotawala nchini Uganda National Resistance Movement – NRM kinaripotiwa kutoridhika na matokeo ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika eneo la Kawempe Kaskazini. Inaripotiwa kwamba kamati kuu ya chama hicho iliandaa mkutano  kujadili uchaguzi huo mdogo na matokeo yake. Wajumbe wa kamati hiyo wanaripotiwa pia kujadili kuhusu matukio ya uchaguzi huo kama vile madai ya udanganyifu na vurugu. Chama hicho kinachoongozwa na Rais Yoweri Museveni hakikuridhika na matokeo ya uchaguzi huo mdogo ambapo Erias Luyimbazi Nalukoola wa chama cha upinzani cha NUP cha kwake Robert Kyagulanyi Maarufu Boby Wine  aliibuka mshindi. Msimamizi mkuu wa uchaguzi katika eneo bunge la Kawempe Kaskazini Henru Makabayi alimtangaza Nalukoola mshindi baada ya kujipatia kura elfu 17, 764. Chama cha NRM kimetangaza nia ya kuelekea mahakamani kupinga matokeo hayo ambapo mwaniaji wake kwa jina Farida Nambi alijipatia kura 8,593. Katibu mkuu wa NRM Richard Todwong, alisoma taarifa ya baada y...

Wasira: Marufuku Kuwatoza Fedha Wanaokwenda Kujifungua Hospitalini

  Na Mwandishi Wetu CHAMA  Cha Mapinduzi (CCM) kimepiga marufuku wajawazito wanaokwenda kujifungua hospitalini kutozwa fedha kwani huduma ya kujifungua ni bure na maelekezo tayari yalishatolewa. Akizungumza mbele ya wananchi wa Mlowo katika Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe akiwa katika ziara yake ya kikazi Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Stephen Wasira amesema sera ya CCM inaeleza wazi huduma ya kujifungua pamoja na watoto wenye umri kuanzia mwaka 0-5 hawatatozwa fedha ,hivyo ni marufuku kuwatoza fedha. Akiwa katika eneo hilo Wasira alipokea kero za wananchi hao wakidai wanawake wajawazito wanapokwenda kujifungua wanatakiwa kulipa fedha Sh.300,000 ili kupata huduma ya kujifungua hali iliyomshangaza na kutoa maelekezo ya kupiga marufuku huduma ya kujifungua kutozwa fedha. “Sera ya CCM iko wazi kabisa kuwa hairuhusiwi mama mjamzito anapokwenda kujifungua kulipa fedha ili apate huduma,hivyo wale ambao wanapisha sera hii waache mara moja na hii ni kwa maeneo yote ambayo wanaendelea ...

Wasira Awahakikishia Wananchi Tunduma Kupatikana Ufumbuzi Kero ya Msongamano

  Makamu Mwenyekiti Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara,  Stephen  Wasira,  amewahakikishia wananchi Wasira Awahakikishia Wananchi Tunduma Kupatikana Ufumbuzi Kero ya Msongamano Tunduma na mkoa wa Songwe kwa ujumla kuwa serikali ina fhamira ya dhati kutatua changmoto zao hususan ya maji na upanuzi wa barabara. Wasira ameeleza hayo leo Machi 15, 2025 alipokuwa akiwahutubia wananchi mjini Tunduma, wilayani Momba Mkoa wa Songwe ambapo amesema kwa upande wa kero ya msongamano wa malori katika mji huo ufumbuzi utatokana na kupanuliwa kwa barabara ya Mbeya-Tunduma kuwa ya njia nne. Amesema atakutana na Waziri wa Miundombinu (Abdallah Ulega) na atamfikishia ombi la wananchi wa mkoa huo kutaka upanuzi wa barabara hiyo ambao tayari umeanza mkoani Mbeya uwe na wakandarasi wawili ambapo mwingine aanzie Tunduma kuelekea Mbeya na hatimaye wakutane katikati kwa lengo la kuongeza kasi ya ujenzi.

Kazi Kubwa Iliyofanywa Na Rais Samia Nchini, Ccm Itashinda Kwa Kura Nyingi-Wasira

 Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amezungumza na wanachana na viongozi wa Chama wilayani ileje mkoani Songwe akiwa katika siku ya tatu ya ziara yake mkoani humo. Akizungumza na wana CCM hao katika Ukumbi wa Seselembe, Ileje leo, Machi 16, 2025, Wasira amesema Chama kinaingia katika uchaguzi mkuu wa mwaka kikiwa hakina wawasi wa kushinda kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. "Chama Cha Mapinduzi kinaingia katika uchaguzi kikiwa na hakika ya ushindi kutokana na kazi kubwa ya kuleta maendeleo iliyofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, tunavisihi vyama viingie vya siasa viingie katika uchaguzi huu na wananchi endeleeni kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura," amesema Wasira. Awali baada ya kuwasili wilayani humo akiwa katika siku ya mwisho ya ziara yake kwa Mkoa wa Songwe, Wasira alipokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na hali ya siasa ya wilaya hiyo, k...

Mwenyekiti wa Taifa wa ACT anataka kurithi sera za Savimbi wa Angola-mbeto

 Mbeto :OMO akatae kurithi sera za Savimbi wa Angola   Na Mwandishi  Wetu , Zanzibar Kamati Maalum ya Nec Zanzibar, Idara ya Itikaadi, Uenezi na Mafunzo  imemuasa Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo  ,Othman Masoud Othman,  kuepuka fikra zozote za kutamani  kurithi  sera za Kiongozi wa zamani  wa  UNITA, Jonas  Savimbi. Aidha azma ya kufikia  uamuzi wa kutaka kuweka kando maridhiaono ya kisiasa Zanzibar na kuanzisha mapambano , anaweza kuitia hofu dunia na kuanza kumtazama kwa jicho lenye shaka  Hayo yameelezwa na  Katibu wa Idara  hiyo ya CCM  upande wa Zanzibar, Khamisi Mbeto Khamis,  aliyesema  fikra zozote za kutishia  kuvunja maridhiano ya kisiasa, inakusudia kuchochea fujo na ghasia kuelekea oktoba mwaka huu. Mbeto  alisema  ni wazi Othman ameshindwa kukiongoza ACT kwa siasa za kisasa, badala yake kauli  zake zinavunja misingi ya demokrasia kwa kutamani urithi wa ...