Skip to main content

Posts

Showing posts from May 29, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

JICA Yaahidi Kuendelea Kuishika Mkono Serikali ya Tanzania-Majaliwa

_▪️JICA, Benki ya Dunia na AFDB watoa Dola za Marekani mil 516 miradi ya kilimo_ _▪️Washauri elekezi wawili Mjapan na Mtanzaniia wawekwa TIC kurahisha uwekezaji_   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) limeihakikishia Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa itaendelea kushirikiana nayo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi. Hatua hiyo imetokana na namna ambavyo Serikali imekuwa ikisimamia kikamilifu matumizi ya fedha mbalimbali zinazotolewa na wadau wa maendeleo likiwemo shirika hilo. Waziri Mkuu amesema “Serikali itaendelea itaendelea kusimamia ipasavyo fedha zote za maendeleo zinazoletwa nchini na kuhakikisha zinatumika kama ilivyokusudiwa.” Ameyasema hayo juzi (Jumatano, Mei 28, 2025) alipokutana na Makamu wa Rais wa JICA, Miyazaki Katsura kwenye ukumbi wa Mikutano wa Tachibana uliopo katika hotel ya New Otani, Tokyo nchini Japan akiwa katika ziara yake ya ...

Jela Miaka 30 Kwa Kubaka Mtoto Wake

Mkazi wa Kijiji cha Mwakubilinga, Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza, Ndakama Pauline Kisabo (35), amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na mahakama ya wilaya ya Kwimba baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka binti yake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10 (jina linahifadhiwa kwa sababu za kisheria). Hukumu hiyo imesomwa leo Mei 29, 2025 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Ndeko Ndeko, katika kesi ya jinai namba 4924/2025, baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka. Kwa mujibu wa Mwendesha Mashtaka wa Serikali,  Juma Kiparo, tukio hilo lilitokea tarehe 9 Februari 2025 katika Kijiji cha Mwakubilinga, wakati bibi wa mtoto huyo alipowamuacha mtoto huyo kwa baba yake ambaye alishatengana na mama wa mtoto huyo ndipo mshatakiwa alimvuta mhanga na kumbaka kisha kumpatia elfu moja ili asilie. Mshtakiwa alifikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza tarehe 26 Februari 2025 na kusomewa shtaka la kuzini na maharimu, kinyume na Kifungu cha 158(1)(a) cha Kanuni ya Adhab...

Fanyeni ukaguzi kwa weledi bila ya kumwonea mchimbaji yoyote – Mhandisi Kamando

_Wapendekeza maboresho Kanuni za Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira pamoja na Sheria ya Baruti._ 📍*Mwanza* WAKAGUZI wa Migodi ya Madini  na Baruti wametakiwa kufanya kazi kwa weledi, kuongeza  ufanisi na kufuata  taratibu na sheria za nchi katika utoaji wa huduma. Hayo yamesemwa leo Fanyeni ukaguzi kwa weledi bila ya kumwonea mchimbaji yoyote – Mhandisi  Kamando na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Migodi na Mazingira, Mhandisi Hamisi  Kamando jijini Mwanza  wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili cha wakaguzi migodi na baruti ambacho kililenga kujengeana uwezo ikiwemo kufanya maboresho ya  Kanuni mbalimbali za madini na Sheria ya Baruti. ‘’Tusikubali kuyumba au kuyumbishwa na hatimaye kutolewa kwenye mstari, tuendelee kufuata misingi, weledi na maadili katika utendaji kazi kwa kuepuka rushwa na kushinda vishawishi   na tamaa nyinginezo,’’amesema Mhandisi Kamando na kuongeza, “Nitoe rai, tunatakiwa kuwajibika kwa kuzingatia nidhamu, uami...