Skip to main content

Posts

Showing posts from January 5, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu aanza ziara Zanzibar kwa Kufungua Shule

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Januari 06, 2025 amefungua Skuli ya Sekondari ya Makoba iliyopo Mkoa wa Kaskazini Unguja, Zanzibar ikiwa ni sehemu ya shamrashamra kuelekea maadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Ujenzi wa Shule hiyo ambao umefikia asilimia 100 umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 6.1 ambazo zimetolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt Hussein Ali Mwinyi.

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Sadc-Organ kwa njia ya Mtandao

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Dharura wa Utatu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi hiyo kwa njia ya mtandao katika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Januari, 2025.

Kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mbele Ya Kaburi la Mwalimu Nyerere

  Mwanasheria mkuu wa serikali Mh Hamza Johari amewataka Watanzania kutembelea eneo alilozaliwa na kuzikwa Baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hatua ambayo akesema itawawezesha kujifunza mambo mbalimbali yalifanywa na kiongozi huyo kwa enzi za uhai wake. Akizungumza baada ya kutembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa eneo la Mwitongo, kijijini Butiama,Mwanasheria huyo mkuu wa serikali,amesema kufika eneo hilo ni darasa tosha la kufahamu vema historia ya nchi na Baba wa Taifa wa Taifa. "Tumeona nyumba aliyojengewa na jeshi la wananchi,tumeona vitu vingi vya kujifunza kuhusu Mwl Nyerere pia tumefika kwenye kaburi na kumwombea dua,nawaasa watanzania wengine wakipata nafasi kufika Mara, wafike Butiama ili kupata maelezo ya kazi zake alizowahi kuzifanya wakati wa uhui wake" alisema Mh Hamza Johari. Hata hivyo Mwanasheria mkuu wa serikali, amepata nafasi ya kupanda juu ya jiwe ulipo Mwenge wa Mwitongo ambao umeasisiwa na Baba wa taifa na kila mwaka wakati wa mbio...

Kila Kijiji Kuwa na Shule ya Msingi na Sekondari Jimbo la Musoma Vijijini

Na Shomari Binda-Musoma MBUNGE wa Jimbo la Musoma vijijini Profesa Sospeter Muhongo amesema lengo ni kuhakikisha kila Kijiji na Kitongoji kinakuwa na shule ya msingi na sekondari ndani ya jimbo. Kauli hiyo ameitoa mapema leo jumapili januari 5 akikusudia Musoma Vijijini ya leo na kesho katika suala la elimu na mengine. Amesema hayo yote hayawezi kukamilishwa kwa mwaka mmoja na kuishukuru serikali kwa kuunga mkono jitihada hizo. Muhongo amesema kila Kijiji kinapaswa kuwa na shule ya msingi zaidi ya moja kutokana na wingi wa watoto ambapo kwa sasa zipo shule 120 za serikali zikiwa 116 za binafsi 4. Amesema kila sekondari inapaswa kuwa na maabara tatu za masomo ya sayansi ambayo yatawawezesha wanafunzi kuingia kwenye soko la ushindani Licha ya mkazo kwenye elimu amezungumzia pia suala la afya na kudai kila Kijiji kuwa na zahanati itakayotoa huduma karibu na wananchi. "Ndugu zangu naendelea kuwathibitishia kwamba tunajua tunakoelekea hatufanyi kazi kwa kubahatisha wala kwa msimu Malen...