Na Mwandishi Wetu UONGOZI wa Shule ya Hazina Magomeni jijini Dar es Salaam umempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa miaka minne ya mafanikio kwenye sekta mbalimbali ikiwemo kuipasha sekta ya elimu. Kwa mujibu wa Mkuu wa shule hiyo, Omari Juma Rais Samia amefanya mambo makubwa hususan kwenye elimu ambapo amewezesha wanafunzi wengi kupata elimu ya msingi hadi sekondari. Shule ya Hazina imekuwa kinara kwa kuwa namba moja kwenye matokeo ya darasa la nne na lasaba kwenye Wilaya ya Kinondoni na Mkoa wa Dar es Salaam kwa miaka mingi. Alisema Rais Samia amefanikiwa kujenga shule za wasichana za sayansi zinazojulikana kwa jina la Mama Samia kwenye mikoa mbalimbali hivyo kuwapa fursa wasichana wa kitanzania kusomea masomo ya sayansi kwa wingi. “Hazina mdau mkubwa wa elimu tumekuwa tukiongoza Wilaya ya Kinondoni na Mkoa wa Dar es Salaam karibu kila mwaka kwa kuwa wakwanza kwenye matokeo ya darasa la saba kwa hiyo tunapoona sekta ya elimu inapewa kipaumbele inatutia moyo sana kamawadau ...
Marato tv - Sauti ya Jamii