Mkutano wa siku mbili wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umehitimishwa jijini Pretoria, Afrika Kusini Machi 13, 2026. Madhumuni ya mkutano huo yalikuwa ni kupanua kasi ya mtangamano wa kikanda kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ili kutengeneza ajira, kuimarisha usalama wa chakula na upatikanaji wa nishati kwa wananchi. Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo uliongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe ambaye aliambatana na Naibu Waziri wa Fedha. Mhe. Laurent Luswetula. Katika hotuba yake ya kufunga, Mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye ni Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Mhe. Ronald Lamola alisisitiza umuhimu wa nchi wanachama kuwa na umoja na mshikamano ili kutekeleza kwa ukamilifu yale yaliyojadiliwa katika mkutano huo. Katika majadiliano hayo, pamoja na mambo mengine, Mawaziri walisisitiza umuhimu wa kuharakisha utekelezaji wa miradi ya kikanda hasa ujenzi wa mi...
Marato tv - Sauti ya Jamii