Skip to main content

Posts

Showing posts from January 18, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tume ya Madini Yashiriki Uzinduzi wa Miradi ya Csr Mkoa wa Tabora

📍 Igunga, Tabora Tume ya Madini Mkoa wa Tabora imeshiriki rasmi katika hafla ya uzinduzi wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) iliyofanyika Wilaya ya Igunga, Mkoa wa Tabora. Hafla hiyo ilifunguliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Mhe. Sauda S. Mtondoo, na kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali, wadau wa sekta ya madini pamoja na wananchi wa maeneo husika. Miradi iliyozinduliwa inajumuisha ujenzi wa darasa moja na ofisi ya walimu katika Shule ya Msingi Mkwabi, pamoja na ujenzi wa vizimba vya maji katika Kijiji cha Nanga. Utekelezaji wa miradi hiyo unalenga kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji shuleni, sambamba na kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi, hivyo kuchangia kuboresha ustawi wa jamii. Miradi hiyo imetekelezwa na Kampuni ya TAUR TANZANIA LTD kwa gharama ya Shilingi milioni 50 katika mwaka wa fedha 2024/2025, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa mujibu wa sheria na miongozo ya sekta ya madini nc...

Waziri Makonda Awasili Nchini Morocco Kuwasilisha Ujumbe wa Rais Samia

  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amewasili nchini Morocco kwa ziara maalum ya kikazi akiwa na jukumu la kuwasilisha ujumbe maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dk. Patrice Motsepe. Ziara hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika sekta ya michezo, hususan maendeleo ya mpira wa miguu barani Afrika na nafasi ya Tanzania katika michuano na programu mbalimbali zinazosimamiwa na CAF.

Waziri Aweso atakawatendaji watakaoleta matokeo

Na MASHAKA MHANDO, Mkinga WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kufanya tathmini ya kina ya watendaji ndani ya wizara na taasisi zake na kuwaondoa wale wote "wanaohudhuria" kazini bila kuleta matokeo chanya ya wananchi kunywa maji. Waziri Aweso alitoa kauli hiyo jana wilayani Mkinga wakati wa hafla ya kukagua na kupokea vifaa vya mabomba yenye thamani ya shilingi Bilioni 7.7, kwa ajili ya umaliziaji wa mradi wa maji wa Mkinga-Horohoro ambao sasa umefikia asilimia 65 ya utekelezaji wake. Akizungumza kwa msisitizo, Waziri Aweso alisema tangu kuteuliwa kwake tena kuongoza wizara hiyo, amekuwa haridhishwi na namna baadhi ya watendaji wanavyotekeleza majukumu yao, akibainisha kuwa wizara inahitaji watendaji wanaopambana kukamilisha miradi na si wale wanaokwamisha huduma. "Wizara ya maji hatutaki watu wanaohudhuria kazini, tunataka watendaji wanaoleta matokeo. Unakuwa mtendaji miaka mitano hujaenda hata kuzindua kisima kimoja? Haiwezekani. Lazima w...

Serikali Kung’arisha Elimu ya Fedha Tanga

📍Wiki ya Huduma za fedha Kitaifa kuanza viwanja vya Usagara Tanga Na MASHAKA MHANDO, Tanga  Wizara ya Fedha imetangaza rasmi kuanza kwa maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa mkoani Tanga, yenye lengo la kuwajengea wananchi uwezo wa kusimamia uchumi wao na kuongeza uelewa wa masuala ya fedha nchini. Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa leo,  Kaimu Kamishina wa Idara ya Uendelezaji wa sekta za fedha wa Wizara ya Fedha, Dionesia Mjema msemaji ameeleza kuwa maadhimisho hayo yatafanyika katika Viwanja vya Usagara kuanzia Januari 19 hadi Januari 26, 2026.  Tukio hilo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb). Alisema malengo ya Serikali kwa maadhimisho haya ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha (2020/21 – 2029/30).  Alisema serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imedhamiria kuhakikisha ifikapo mwaka 2025, asilimia 80 ya Watanzania wanakuwa na uelewa ...

Serikali Itaendelea Kushirikiana na Viongozi wa Dini-Dkt. Mwigulu

_Asema lengo ni kujenga Taifa lenye hofu ya Mungu, upendo, haki na uwajibikaji_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 18, 2026 ameshiriki Ibada ya Jumapili katika Kanisa Kuu Anglikana la Roho Mtakatifu Dodoma na amesisitiza kwamba Serikali itaendelea kushirikiana na viongozi wa dini kujenga Taifa lenye hofu ya Mungu, upendo, haki na uwajibikaji. “Sote tunatambua kwamba Taasisi za dini zina nafasi ya kipekee ya kuhubiri na kufundisha maadili ya upendo, uvumilivu na kuheshimiana, ambazo ni nguzo kuu za amani ya Taifa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua na kuthamini sana mchango mkubwa wa taasisi za dini ikiwemo Kanisa la Anglikana, katika kudumisha amani, maadili mema na mshikamano wa Kitaifa. Pia, Waziri Mkuu amesema kuwa ibada za Jumapili ni sehemu muhimu ya maisha ya Mkristo na ni muda wa kujitathmini, kuimarisha mahusiano yao na Mwenyezi Mungu, na kujifunza namna bora ya kuishi kwa mujibu wa mapenzi ya Mwenyezi Mungu katika familia, jamii na Taifa kwa ujumla...