Skip to main content

Posts

Showing posts from July 11, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Acheni kutumia dawa bila ushauri wa Daktari - Mwakabala

  Na Ada Ouko, GMTV, Musoma. JAMII imetakiwa kuacha kununua dawa za binadamu na kuzitumia kiholela bila kuzingatia matumizi sahihi ya dawa hizo kutoka kwa wataalamu, kwa kuwa hali hiyo inapelekea usugu wa vimelea vya magonjwa. Mwito huo umetolewa Julai 11, 2025 na Mfamasia mkuu wa Mkoa wa Mara Apolinary Mwakabala wakati akihitimisha mafunzo ya siku mbili kwa watoa huduma za dawa kwenye maduka ya dawa muhimu (ADO) ikiwa lengo ni kupunguza usugu wa vimelea kwenye dawa aina za Antibiotic, na dawa za kuzuia maumivu kwa mtumiaji. "Acheni kuuza dawa kiholela mgonjwa akifika dukani kwako kupata dawa kama anaumwa mnapaswa kumshauri kwenda kupima zahanati au Hospitali kwanza... Ili kubaini ugonjwa unaomsumbua ndipo utaweza kumpa dozi kamili ya dawa kama alivyoandikiwa na daktari, badala ya kumpa dozi nusu jambo ambalo ni hatari kwa afya yake"Anasema Apolinary. Aidha amewataka kuzingatia sheria kanuni, taratibu za uendeshaji wa huduma za maduka ya dawa muhimu (DLDM) sambamba na hilo k...

Rais Mwinyi:Sekta ya Uhandisi na Usanifu ni Kiungo Muhimu Kwa Maendeleo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa sekta ya Uhandisi na Usanifu wa Majengo ni kiungo muhimu katika kufanikisha maendeleo ya miundombinu, ustawi wa jamii, na ukuaji wa uchumi kwa nchi za Afrika Mashariki. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati akifungua Semina ya Wataalamu wa Usanifu wa Majengo wa Afrika Mashariki inayofanyika katika Hoteli ya Madinat Al Bahr, Mbweni, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 10 Julai, 2025. Ameeleza kuwa taaluma ya usanifu wa majengo ni nyenzo muhimu katika kukabiliana na changamoto ya ongezeko la idadi ya watu mijini, pamoja na kuimarisha haiba na mpangilio wa miji.  Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa usanifu unaozingatia na kulinda urithi wa utamaduni wa Afrika Mashariki, akieleza kuwa ushirikiano wa pamoja na ushauri wa kitaalamu miongoni mwa nchi za ukanda huu ni jambo la msingi ili kunufaika ipasav...

Mhe. Queen Sendiga azindua rasmi mradi wa usambazaji wa mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku mkoa wa Manyara

📌Mitungi 16,275 kusambazwa mkoa mzima. 📌Kila wilaya kupata mitungi 3,255. Mkuu wa  Mkoa  wa Manyara Mhe. Queen  Sendiga  leo Julai 11,2025 wilayani Hanang amezindua rasmi mradi wa usambazaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku mkoa wa Manyara.  uzinduzi huo umeongozwa na mkuu wa mkoa pamoja na viongozi wengine wa mkoa, wilaya, kata pamoja na vijiji na vitongoji vyake.  Mhe. Sendiga amesema lengo la uzinduzi  mradi ni kuutambulisha rasmi mradi kwa wananchi wa mkoa wa Manyara ambao ndio walengwa na wanufaika wa mradi. Mhe. Sendiga, amepongeza juhudi za Serikali na REA katika kufanikisha utekelezaji wa mradi na kuongeza kuwa lengo la Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia ni kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia, jambo ambalo litasaidia kutunza na kuhifadhi mazingira. “Serikali, imeweka ruzuku ya asilimia 50, kwa hiyo wakina Baba na kina Mama wa mkoa wa Manyara, wajiandae kutumia gesi, tuwapu...