Skip to main content

Posts

Showing posts from May 2, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali kuendelea kushirikiana na Taasisi za dini kuimarisha amani na maadili nchini

_▪︎ Asema dini ni nguzo muhimu ya malezi na mshikamano wa Taifa_ _▪︎ Asisitiza jamii kuendelea kuombea na kulinda amani ya nchi_ Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za dini nchini ili kuimarisha maadili, mshikamano wa kijamii na kudumisha amani ambayo ni msingi wa maendeleo endelevu ya Taifa. Amesema hayo leo Jumapili, Mei 3, 2026, aliposhiriki ibada katika Kanisa Kuu la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mufindi, lililopo Mafinga Mjini, mkoani Iringa. Akizungumza na waumini, Dkt. Nchemba amesema taasisi za dini zina mchango mkubwa katika kujenga jamii yenye maadili mema, inayozingatia misingi ya haki na uwajibikaji. “Serikali inaendelea kusisitiza Watanzania wote kuwa wadau wa kuombea na kusimamia amani ya nchi yetu,” amesema. Ameongeza kuwa mafanikio ya mipango ya maendeleo ya Taifa yanategemea uwepo wa amani. “Pasipokuwa na amani, hata malengo binafsi ya mtu mmoja mmoja ya Mtanzania mmoja mmoja h...

Dkt.Mwigulu aagiza ujenzi wa barabara Mufindi kusini, Asisitiza ahadi za Rais zinatekelezwa

_▪︎ Aagiza TANROADS kumpata mkandarasi ndani ya wiki mbili_ _▪︎ Aelekeza fedha za awali zitolewe mara moja kuanza ujenzi_ Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza kuanza mara moja ujenzi wa barabara za Nyololo–Mtwango (km 40) na Mafinga–Mgololo katika Jimbo la Mufindi Kusini, mkoani Iringa, akisisitiza kuwa ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ni maelekezo ya moja kwa moja yanayopaswa kutekelezwa bila kuchelewa. Ameyasema hayo leo Jumamosi, Mei 2, 2026, alipofanya ziara ya kikazi katika Jimbo hilo na kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Igowole, kata ya Igowole, ambapo pia alisikiliza kero na mahitaji mbalimbali ya wananchi. Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Nchemba amesema Serikali inaendelea kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa vitendo na kuleta matokeo kwa wananchi. “Mheshimiwa Rais amejitambulisha kwa kazi zake kwamba yeye ni mtu wa matokeo,” amesema. Katika hatua ya kuharakish...

Safari ya gridi ya Taifa ya maji imeanza, Wananchi tutunze vyanzo vya maji Kwa maendeleo

NA: DK. REUBENI LUMBAGALA Ni dhamira ya kweli ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kumtua mama ndoo kichwani yaani kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji katika makazi yao na kuepukana na kadhia ya kuchota maji umbali mrefu. Kwa lugha rahisi ni kwamba, Dk. Samia anataka wananchi wote wapate maji kwa asilimia mia moja. Kwa kuzingatia umuhimu wa maji, katika maisha na maendeleo ya binadamu, ni muhimu kuhakikisha huduma hiyo inawafikia wananchi wote. Tanzania imebarikiwa kuwa na vyanzo vingi vya maji ambavyo mikakati madhubuti ikiwekwa, vinaweza kumaliza changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi.  Rais Dk. Samia akiwa mdau muhimu wa sekta ya maji, huku akichukizwa na namna wananchi wakiwemo wanawake na watoto wakitembea umbali mrefu kutafuta maji, ameipa Wizara ya Maji jukumu la kuhakikisha inatekeleza mradi wa Gridi ya Taifa ya Maji. Rais Dk. Samia ametolea mfano Wizara ya Nishati ilivyo na Gridi ya Taifa ya Umeme, ndivyo Wizara ya Maji inapaswa kuwa na Gridi ya Taifa ya Maji....

Hifadhi ya Mikumi yapata hoteli ya kisasa

Na Josephat Lazaro  Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbas  akiwa na mwenyeji wake Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, CPA (T) Musa Nassoro Kuji wametembelea Hifadhi ya Taifa Mikumi kukagua uwekezaji mkubwa wa hoteli iitwayo Mikumi Wildlife Lodge iliyojengwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Mikumi. Uwekezaji huo wa hoteli ya kisasa ndani Hifadhi hiyo ni ishara ya kuwepo kwa mazingira bora ya utalii na uwekezaji nchini ambapo uzinduzi wa hoteli hiyo unatarajiwa kufanyika hivi karibuni utaiweka Tanzania hususani Hifadhi ya Mikumi katika nafasi kubwa ya utalii duniani. Hoteli ya Mikumi Wildlife Lodge ina zaidi ya vyumba 48 vya kisasa vya malazi vyenye uwezo wa kulaza wageni 96 kwa wakati mmoja, chumba cha mazoezi cha kisasa (gym), sehemu za michezo, ukumbi wa kisasa wa mikutano na mandhari ya kuvutia.