Na Helena Magabe-Tarime Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Mara(BAWACHA) Mhe.Veronica Irecho ametoa Wito Kwa wanawake Mkoani Mara kujitojeza Kwa wingi kujiandisha Kupiga Kura pamoja na Kugombea Nafasi Mbalimbali za Uongozi na hivyo Kushiriki kikamilifu Katika shughuli za maendeleo. Akizungumza katika kikao cha 7 tangu aanze ziara ya kuhamasisha uhai wa Bawacha Majimboni kilichofanyika katika ofisi ya chadema Tarime mjini Amesema lengo ni kuhamasisha wanawake kujiandikisha kupiga kura,kugombea nafasi mbali mbali sambamba na kukemea vitendo vya rushwa ndani ya Chama hicho Ikiwa ni mara ya kwanza kukutana na Wajumbe wa Bawacha wa Tarime amekemea vikali vitendo vya rushwa ambapo amewataka wanawake kuepuka ushiriki Vitendo vya rushwa kwani ni mbaya na itapelekea kukosa nafasi mbali mbali kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 pamoja na Serikali kuu 2025. Irecho ambaye ni Diwani Mstaafu wa viti maalumu pia am...
Marato tv - Sauti ya Jamii