Skip to main content

Posts

Showing posts from July 9, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa Aitaka Tra Kuendelea Kuongeza Ufanisi Ukusanyaji Kodi

_▪️Awapongeza kuvuka lengo 2024- 2025._ _▪️TRA yarejesha Shilingi Trilioni 1.2 kwa walipa kodi kiwango kikubwa kuwahi kutokea._   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuongeza usimamizi wa ukusanyaji wa kodi kwa wafanyabiashara ikiwemo wa mataifa ya nje walioamua kuja kufanya shughuli zao nchini. Amesema kuwa TRA inapaswa kuongeza ufanisi zaidi kwenye kuwasimamia wafanyabiashara wote kuhakikisha wanatambua sheria za ulipaji kodi pamoja na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kuhakiki utekelezaji wake. Ametoa agizo hilo leo (Jumanne Julai 08, 2025) alipofungua kikao kazi cha Viongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kituo cha Mikutano cha Arusha (IACC). “Nendeni mkachunguze hawa wanaokuja kufanya biashara nchini, kama wanaondoka na mapato yetu kwa kutolipa kodi yetu, ni lazima tubane eneo hilo kama ambavyo sisi tunabanwa tunapokwenda kwao, yeyote aliyeamua kuja kufanya biashara Tanzania ni lazima ajue Tanzania ina sheria zake ikiwemo za ul...

Rais Samia Awapa Stamico Leseni Kubwa Ya Uchimbaji Madini Ya Nikeli Katika Eneo la Ntaka Nachingwea-Lindi

▪️Ni hatua ya kuiimarisha STAMICO kiuchumi ▪️Aelekeza Wachimbaji wadogo kupewa leseni za  uchimbaji na kurasimishwa ▪️Waziri Mavunde awataka STAMICO kuanza uchimbaji ndani ya miezi 18 ▪️Wachimbaji wadogo wamshukuru Rais Samia kwa kuwajali *Nachingwea,Lindi* Waziri wa Madini, *Mh. Anthony Mavunde (Mb)* amebainisha kuwa *Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan*, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameelekeza kutolewa kwa leseni ya uchimbaji madini ya nikeli kwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na kwa Wachimbaji wadogo waliokuwepo katika eneo la vilima vya Ntaka- Nachingwea,Mkoani Lindi. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo tarehe 08 Julai, 2025 katika mkutano wa hadhara wa wananchi na wachimbaji katika Kijiji cha Nditi punde tu baada ya kufanya ziara ya kutembelea maeneo na migodi ya wachimbaji wadogo chini ya Umoja wa Vikundi vya Wachimbaji Madini (UVIWAMA). "* Rais Dkt. Samia S. Hassan amesikia kilio chenu cha muda mrefu cha kutaka kupewa maeneo ya uchimbaji katika Leseni inayomilikiwa ...

Azania Bank Kinara Sabasaba 2025,Yashinda Tuzo Mbili

  Azania Bank imeibuka kidedea kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya maonesho hayo ya kimataifa jijini Dsm. Azania Bank imetwaa tuzo ya mshindi wa kwanza ya muoneshaji bora kwenye sekta ya fedha ikizishinda benki zote zilizoshiriki maonesho hayo kwa mwaka huu. Pia imeibuka mshindi wa pili wa jumla katika waoneshaji wote. Tuzo za washindi zilikabidhiwa na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi aliyekuwa mgeni rasmi siku ya ufunguzi. Akizungumza katika maonesho hayo wakati Mh. Rais wa Zanzibar alipotembelea banda la Benki hiyo, Mkurugenzi mtendaji wa Azania Bank Bi. Esther Mang’enya alisema kuwa kwa mwaka huu walijikita katika kutoa huduma za kidijitali na kuonesha ni jinsi gani zinaleta tija kwa mfanyabiashara sambamba na kauli mbiu ndogo ya maonesho ya Sabasaba mwaka huu inayosema ‘’Sabasaba 2025,Kidijitali zaidi’’. Itakumbukwa kuwa mwanzoni mwa mwaka huu Azania Bank ilizindua toleo jipya la huduma zake za kidijitali la Azania Digital linalobeba huduma zake kama ...

CBE na SWUFE ya China wasaini ushirkiano wa kitaaluma

Na Mwandishi Wetu CHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimesaini makubaliano na Chuo Kikuu cha Fedha na Uchumi cha Kusini Magharibi mwa China (SWUFE) kuimarisha ubadilishanaji wa ujuzi, utafiti wa pamoja, na fursa za mafunzo kwa wanafunzi na wafanyakazi wa pande zote mbili. Mkataba huo ulisainiwa jana jijini Dar es Salaam baina ya Mkuu wa chuo cha CBE, Profesa Edda Lwoga na Mwenyekiti wa Bodi y SWUFE,  Zhao Jian Jun. Akizungumza mara baada ya kusaini makubaliano hayo, Profesa Lwoga alisema wamesaini mkataba huo ambao utawawezesha watumishi wa chuo hicho kuendelea kufanya shahada za uzamivu nchini China. Alisema wanatarajia kuanza kutoa shahada ya kwanza kwenye uongozi wa biashara ambayo mwanafunzi atasoma miaka miwili akiwa CBE na miaka miwili atakwenda chuo cha SWUFE China kumalizia shahada yake. “Mwanafunzi huyo akihitimu atakuwa na shahada inayotambuliwa na CBE na SWUFE, program hii itakuwa na msaada kubwa sana hasa wale ambao wangependa kwenda kusoma China  wataanzia hapa CBE...