● Ni matokeo ya MoU kati ya GST na Taasisi ya KIGAM kutoka Korea ya Kusini, ● Utekelezaji wa mradi huo kugharimu Bilioni 40 za Kitanzania ● Wataalam kutoka GST kujengewa uwezo ● Wachimbaji wadogo kupatiwa Mafunzo malum *Wizara ya Madini - Mtumba* Ikiwa ni utekelezaji wa Madini Vision 2030, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewezesha kuanzishwa kwa mradi wa ujenzi wa Kituo cha kisasa na kikubwa cha Teknolojia ya Madini Mkakati na muhimu pamoja na ununuzi wa vifaa vya kisasa vya utafiti wa kina wa madini. Hayo yamesemwa leo tarehe 26 Januari, 2026 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* alipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe maalum wa Watu 6 kutoka nchini Korea ukiongozwa na *Bw. Seong-Jun Cho* ambaye ni Mtaalam kutoka Taasisi ya Jiosayansi na Rasilimali Madini ya Korea (KIGAM). "*Mheshimiwa Rais* ametuelekeza sisi Wizara ya Madini kuhakikisha tunaongeza eneo la utafiti hadi kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2030. Mradi huu na wenzetu wa Korea Kusini ...
Marato tv - Sauti ya Jamii