Skip to main content

Posts

Showing posts from January 7, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Sare za Jwtz zamponza, afungwa Jela Miezi Sita

Mahakama ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza imemuhukumu kifungo cha miezi sita Rajabu Reli (22), mkazi wa Sengerema baada ya kukutwa na hatia ya  kuvaa sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) bila ruhusa. Hukumu hiyo imetolewa jana tarehe 07.01.2025 katika shauri la jinai namba 445 la mwaka 2025 na Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo Mhe. Evodius Kisoka mbele ya mwendesha mashtaka wa Serikali Nyamhanga Tissoro. Kwa mujibu wa hati ya mashtaka iliyosomwa na mwendesha mashtaka wa Serikali Nyamhanga Tissoro mbele ya hakimu Evodius Kisoka,  mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 05.12.2024 huko kijiji cha Kasisa, wilaya ya Sengerema kinyume na kifungu cha 178(1) cha sheria ya kanuni ya Adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022. Mshtakiwa alifikishwa mahakamani januari 07.2025 na kusomewa shitaka la kuvaa sare za Jeshi la wananchi wa Tanzania bila ruhusa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Baada ya kusikiliza pande zote za ushahidi hakimu Evodius Kisoka alijiridhi...

Tanzania na Uingereza Kushirikiana Katika Kuendeleza Madini Mkakati

▪️Waziri Mavunde ainisha Mkakati wa uongezaji thamani Madini ▪️Taasisi za Jiolojia na Utafiti Madini  za Tanzania na Uingereza kushirikiana ▪️Watanzania kujengewa uwezo kukuza ujuzi 📍Dar es Salaam Serikali ya Tanzania imeihakikishia Serikali ya Uingereza kuendeleza ushirikiano kwenye sekta ya madini hususani katika kujengea uwezo watu wake, kubadilishana uzoefu, uongezaji thamani madini na kuwekeza kwenye kufanya tafiti mbalimbali ili kukuza sekta ya madini na kupanua mnyororo wa thamani ili kuongeza ajira na kuchangia katika ukuaji wa pato la taifa. Hayo, yameelezwa Jana na Waziri wa Madini, *Mhe. Anthony Mavunde* katika ofisi ndogo za Wizara ya Madini jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, *Mhe. Marianne Young*. "Kwanza kabisa *Mhe. Balozi Young* amefika ofisini kujitambulisha kwakuwa ana muda mfupi nchini tangu awasili lakini pia tumezungumzia ushirikiano mkubwa uliopo kati ya Tanzania na Uingereza. Katika mazungumzo hayo...

Bashungwa awakutanisha Polisi na Latra kujadili Mikakati ya Kuzuia ajali za Barabarani

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ameongoza kikao kilichoikutanisha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Jeshi la Polisi Tanzania pamoja na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) kujadili na kuweka mikakati ya kuzuia ajali za barabarani nchini. Kikao hicho ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Jeshi la Polisi ya kuongeza mikakati ya kuzuia ajali zinazosababishwa na makosa ya uzembe. Pamoja na mambo mengine, wamejadili utaratibu wa utoaji wa leseni kwa madereva pamoja na kuweka mikakati ya pamoja kwa Jeshi la Polisi na LATRA ya kupambana na kuzuia ajali za barabarani. Kikao hicho kimefanyika Dodoma, leo Januari 06, 2025 ambapo kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Gugu, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Camillus Wambura na Mkurugenzi Udhibiti Usafiri wa barabara (LATRA), DCP Jo...

Mheshimiwa Simbachawene akabidhi Gari la Wagonjwa Mtera

   Mtera:  🗓️ 07/01/2025.     📍Ikiwa takribani siku  42 zimepita ambazo ni sawa na mwezi mmoja na siku kumi na mbili lilipofanyika zoezi la ufungaji wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwezi Novemba leo hii wananchi hao wa Kata ya Mtera wamefanikiwa kukabidhiwa gari hilo la kubebea wagonjwa  Akikabidhi gari hilo Mheshimiwa Waziri wa nchi Ofisi ya Rais menejment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Mb) wa Jimbo la Kibakwe Mheshimiwa George B.Simbachawene mbele ya viongozi wengne wa serikali Mheshimiwa Simbachawene amesisitiza kulitunza gari hilo ili liweze kuwa msaada kwa wananchi hao hasa akina mama wajawazito ambao wengi wamekuwa wakipoteza maisha kwa kutoweza kukimbizwa haraka katika kituo Cha afya kwaajili ya kupewa huduma ya kujifungua.   Naye diwani wa Kata hiyo Mheshimiwa Robert Maulya amemshukuru Mheshimiwa Simbachawene ambae kwa Umoja wake yeye na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano w Tanzania Dkt Samia Suluhu Hass...

Vijana Mnaotaka Kuoa Mc Pilipili atoa Ushauri Kwa Vijana

-Mc Pilipili: Usioe Mwanamke Mwenye Tamaa Mchekeshaji / Mchungaji maarufu  hapa Tanzania  na Afrika Mashariki nzima Mc pilipili amefunguka ukweli mzima kuwa yeye na Mama wa mtoto wake hawapo sawa kabisa na kuwapa ushauri vijana wanaotaka kuingia kwenye ndoa. "Nazani nilioa mwanamke asiyekuwa na upendo wa kweli na aliyejaa Tamaa sana za maisha mazuri  ndoa maana amekuwa akinisumbua sana. Ushauri  ni jambo la bure vijana wenzangu tutafute wanawake wasiokuwa na Tamaa"- Amezungumza Mc Pilipili.

Rais wa zamani wa Ufaransa afikishwa mahakamani akituhumiwa kupokea pesa kutoka kwa Gaddafi

Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy amefikishwa mahakamani siku ya Jumatatu, kwa tuhuma za kupokea mamilioni ya euro za ufadhili usio halali katika kampeni za kugombea urais 2007, kutoka kwa hayati Rais wa Libya Muammar Gadaffi. Sarkozy amekuwa akikana mashtaka hayo na kesi hiyo itaendelea kwa muda wa miezi mitatu. Kiongozi huyo wa zamani wa chama cha kihafidhina anakabiliwa na mashtaka ya "kuficha ubadhirifu wa fedha za umma, ufisadi, ufadhili haramu wa kampeni na njama ya kufanya uhalifu," imesema ofisi ya mwendesha mashtaka wa fedha. Waendesha mashitaka wanasema mwaka 2005, Sarkozy, aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa wakati huo, aliafikiana na Gaddafi, ili kupata ufadhili wa kampeni ili kuiunga mkono serikali yake katika uwanja wa kimataifa ambapo ilikuwa imetengwa. Gaddafi aliyeondolewa madarakani kisha kuuawa mwaka 2011. Wachunguzi wanadai alifanya mapatano ya kifisadi na serikali ya Libya, yaliyohusisha majasusi wa Libya, gaidi aliyepatikana na hatia...

Balozi wa Zambia nchini afrika Kusini afutwa kazi baada ya Kutaka wafanyakazi wa Kiume Kumnyoa Sehemu za Siri

   Rais wa Zambia Hakainde Hichilema amemfuta kazi Balozi wa nchi hiyo,Nchini Afrika Kusini Baalizi Mazuba Monze. Hichilema amechukua uamuzi huo baada ya Monze kuripotiwa kutaka wafanyakazi wake wa kiume kumnyoa sehemu za siri. Mwanadiplomasia huyo aliyekuwa akihudumu katika ubalozi wa Zambia mjini Pretoria ameripotiwa kuwataka wafanyakazi wa ubalozi kumnyoa sehemu za siri ambapo wafanyakazi hao walikataa,wakisema kuwa haikuwa sehemu ya majukumu yao kumnyoa Balozi sehemu za siri.  Balozi Monze alichukuliwa kitendo hicho kuwa ni kutotii na hivyo kupelekea kuwafuta kazi. Hata hivyo baada ya ukimya wa muda mrefu, wafanyakazi hao walikataa rufaa dhidi ya uamuzi huo na kulifikisha suala hilo kwa wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa.  Wakati madai hayo yaliyowashangaza wengi yalipothibitishwa,Rais Hakainde Hichilema alimfuta kazi mara moja Balozi huyo huku ripoti nyingine zikisema kuwa madai dhidi ya Monze yametiwa chumvi.  Gazeti la Maravi Post linaripi...

Dkt Nchemba aipongeza Tra Kuimarisha Mapato

Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA kwa kuongeza makusanyo ya kodi kutoka sh. trilioni 22.2 mwaka wa fedha 2021/22 hadi kufikia sh. tril. 27.6 mwaka wa fedha 2023/2024 na kuvunja rekodi ya kukusanya sh. trilioni 16.528 katika kipindi cha Nusu Mwaka wa Fedha 2024/2025 kinachoanzia Julai hadi Desemba Mwaka 2024. Dkt. Nchemba alitoa pongezi hizo, wakati akifungua Kikao Kazi cha siku 5 kinacho Tathmini Utendaji kazi wa Nusu Mwaka wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025, kinachofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Arusha (AICC), Jijini Arusha. Alisema kuwa fedha hizo zimeisaidia Serikali kutekeleza miradi ya kimkakati inayolenga kuboresha huduma za jamii kama vile Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere, Mradi wa Treni iendayo kasi (SGR), miundombinu ya barabara, huduma za jamii na mingine mengi Dkt. Nchemba aliitaka TRA kuimarisha zaidi mifumo ya kisasa ya kielektroniki ya kukusanya m...

Hotel ya Kitalii yazinduliwa Katika Kisiwa cha Bawe Zanzibar

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, *Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassani* akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt Hussein Ali Mwinyi,mwekezaji wa hotel ya kitalii ya Bawe Island the cocoon Collection Bw. Andrea azzola wakati wa ufunguzi wa hotel Bawe Island the Cocoon Collection iliyopo katika kisiwa Cha Bawe, Zanzibar tarehe 07 Januari 2025. Uwekezaji Huu Ambao umwezesha Vijana wazawa zaidi ya 400 Kupata Ajira Katika Hoteli Hiyo. Hii ni Moja ya Malengo ya Serikali Katika uwekezaji Kuhusu Manufaa Kwa Wananchi wanaozunguka Mazingra Hayo.

Balozi wa Zambia nchini afrika Kusini afutwa kazi baada ya Kutaka wafanyakazi wa Kiume Kumnyoa Sehemu za Siri

 Rais wa Zambia Hakainde Hichilema amemfuta kazi Balozi wa nchi hiyo,Nchini Afrika Kusini Baalizi Mazuba Monze. Hichilema amechukua uamuzi huo baada ya Monze kuripotiwa kutaka wafanyakazi wake wa kiume kumnyoa sehemu za siri. Mwanadiplomasia huyo aliyekuwa akihudumu katika ubalozi wa Zambia mjini Pretoria ameripotiwa kuwataka wafanyakazi wa ubalozi kumnyoa sehemu za siri ambapo wafanyakazi hao walikataa,wakisema kuwa haikuwa sehemu ya majukumu yao kumnyoa Balozi sehemu za siri.  Balozi Monze alichukuliwa kitendo hicho kuwa ni kutotii na hivyo kupelekea kuwafuta kazi. Hata hivyo baada ya ukimya wa muda mrefu, wafanyakazi hao walikataa rufaa dhidi ya uamuzi huo na kulifikisha suala hilo kwa wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa.  Wakati madai hayo yaliyowashangaza wengi yalipothibitishwa,Rais Hakainde Hichilema alimfuta kazi mara moja Balozi huyo huku ripoti nyingine zikisema kuwa madai dhidi ya Monze yametiwa chumvi.  Gazeti la Maravi Post linaripiti kuwa...